Ipi tathmini yako kuhusu siku 100 za Rais Samia madarakani?

Ipi tathmini yako kuhusu siku 100 za Rais Samia madarakani?

Mto mada na wewe umefeli kutuambia ugonjwa wa umeme wa moyo ndio kitu gani iko unazungumzia? huo ni mfumo wa moyo kufanya kazi sijaendelea tena kusoma.
 
Kama tunavyojua, kwa mujiba wa katiba yetu Mheshimiwa Rais halazimiki kufuata ushauri wa mtu yeyote yule.

Hivyo basi tunapokuwa na rais msikivu tena anayefanyia kazi maoni na malalamiko ya watu wake ni baraka kubwa kwa taifa

Kwasasa ukiangalia statement ya deni lako kwenye mfumo wa bodi ya mikopo ( olas.heslb.go.tz ) utaona kuwa wameondoa tozo zote za VRF, yaani hata zile walizotoza zamani (kabla ya agizo la rais) wameziondoa

Wanufaika wa mikopo tunamshukuru sana Mheshimiwa rais kwa kusikia na kuyafanyia kazi maombi yetu. Tulilalamika sana wakati wa mwendazake lakini tukajibiwa kuwa 'hapangiwi'.

Sasa ni muda wa kila mnufaika mwenye uwezo wa kulipa na alipe, tena wamerahisisha unaweza kulipa hata kwa m-pesa na malipo yako yanaonekana hapohapo kwenye mfumo.

Pia niwakumbushe wadau, twendeni vizuri na mama, naiona katiba mpya hususani wakati wa ungwe yake ya pili Mungu akimjaalia na wananchi wakampa ridhaa.
 
Hapa najua sitoeleweka.

Kwanza tukubaliane yote yaliyofangwa na waliopo madarakani ni SAWA NA KUFUTA VUMBI KINYAGO AMBACHO ULIKICHONGA WEWE NA KUKICHAFUA WEWE MWENYEWE.

Mfano kuwaachia wafungwa wa uhamsho, walikamatwa ukiwa wazir,ukushauri wafunguliwe,

Pili kusaini mikataba ya miradi ya kimkakati ni mwendelezo.

Hujaongeza mishahara,ujajenga kitu kipya,umetoa 500m kwa barabara za tarula,alie wanyima miaka yote ulikuwa miongoni,

Kumwachia mbowe na wenzake walikamatwa ukiwepo tena mkubwa.

Kuachia online tv bora ungefungulia magzet sio upupu huo wakat zinafungwa ulikuwepo.

Mimi sioni jipyaaaa nisindanganye siku 100 unafuta kinyago vumbi ulichokichafua mwenyewe.
 
Hao ndiyo CCM! Ni mabingwa wa kutengeneza matatizo, ili baadae waje kuyatatua na hivyo kupata sifa za kirahisi rahisi tu.
 
Mama anaupiga mwingi kama Ronaldinho Gaucho.

Watu flani wanateseka sana.

Chapa kazi mama... tuna imani kubwa sana na wewe.
 
Mama anaupiga mwingi kama Ronaldinho Gaucho...

Watu flani wanateseka sana...

Chapa kazi mama... tuna imani kubwa sana na wewe
Nafikiri wewe akili yako Kama ya panya! Una imani?????????????????!
 
Hakuna tena anaeogopa kukosoa.

Iwe Jf au hata ma group ya watsap.

Hakuna anaeogopa kutekwa wala kufatiliwa na Nissan nyeupe.

Kila mtu anajiona Yuko huru kutoa mawazo yake.

Wabunge wa CCM sasa wanaikosoa serikali.

Upinzan wanatembea nchi nzima kufanya siasa.

Mahakama zinafanya kazi bila maagizo ya wanasiasa.

Wanamuziki wanaimba bila kuogopa.

Asasi za kiraia zimeanza kufufuka.

Tra imeacha kenyanganya hela kibabe.

Siku 100 za neema tupu kwa waungwana na wenye akili...
Really? Unaota wewe
 
RAIS MAGUFULI ALIMWEKA "JELA" MAKAMU WAKE SAMIA SULUHU HASSAN

Na Bollen Ngetti

MWANAMUZIKI Ndanda Kosovo aliwahi kuimba, "Jela..jela ni mbaya, jela..jela ni mateso". Ndanda hakukosea. Aliimba uzoefu alioupata jela hapo Ukonga. Ninamuunga mkono Ndanda kwa uzoefu nilioupata nikiwa jela Keko na Segerea. Jela ni mbaya. Ukiwa jela umezungukwa kuta nene ndefu huwezi kuona nje kwa kifupi unakuwa umenyimwa uhuru wako.

Hata hivyo hakuna jela mbaya duniani kuliko hata Gwantanamo kama jela ya fikra. Yani jela ambapo huwezi kutoa mawazo yako hadharani. Hii ni jela mbaya inayojengwa na shetani tu.

Niliwahi kudokezwa huko nyuma lakini sikuandika maana nilikosa ushahidi kwamba kuna wakati Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan alitaka kujiuzulu nafasi ya Umakamu kujiondoa kwenye gereza la fikra lakini wenye hekma na busara walimshauri asifanye hivyo.

Kwa namna Rais Samia Suluhu Hassan alivyoongoza nchi hii kwa siku 100 ni dhahiri alikuwa jela la fikra. Ni ukweli kwamba hakukubaliana na mambo mengi ya Rais Magufuli hata kama leo anasema "Mimi na Magufuli ni kitu kimoja" lakini matendo ni tofauti.

Mama Samia hakukubaliana na uendeshaji wa demokrasia nchini. Alikuwa jela na ilimtesa ndio maana amechukua njia tofauti kuendesha dhana nzima ya demokrasia. Hakuwa na jinsi wala namna. Bila shaka alilia kimya kimya gerezani.

Mama yetu Samia hakupenda uminyaji wa Uhuru wa Habari. Ilimtesa ndio maana "Fundi" alipomwondoa duniani Pombe naye kuchukua hatamu waandishi wa habari wakashangweka. Akaruhusu Uhuru wa Habari na dunia imeshuhudia maana enzi hizo za jela hata andiko hili lisingetoka maana ningekwenda jela la majengo.

Mama Samia hakufurahishwa na kesi za kubumba. Ilimtesa, ilikuwa ni jela kwake ndio maana alipoingia madarakani akafyatua kesi 147 zilizobumbwa na TAKUKURU. Hali hii ilimtesa. Lakini kuachiwa kwa viongozi wa dini wa Uamsho waliosota kwa miaka 9 jela nayo ilimweka jela kisaikolojia Samia. Hakupenda uonevu.

Huyu mama ni swala 5. Ni Muislamu Safi. Hapendi mali za dhulma iwe ni kwa mtu binafsi au Serikali. Hakupenda fedha za dhulma zilizotokana na kesi za kubumba za uhujumu uchumi na ML ndio maana tunaendelea kushuhudia watuhumiwa wakichomolewa magerezani kwa makundi. Lilimuumiza lakini hakuwa na lakufanya maana hakuwa Mkuu wa Maamuzi, Rais. Kitendo cha Mahakama Kuu kuamuru Serikali kurudisha fedha za dhulma kwa kina Mbowe ni ishara nyingine ya kuwa mama yetu aliumia sana kwa matendo hayo. Alikuwa jela.

Makamu wa Rais Samia (sasa Rais) hakupenda watu kuishi kwa hofu na woga. Alitamani watu wawe huru ndani ya nchi yao ila waheshimu Sheria za nchi. Ndio maana leo hata mama lishe, bodaboda nakadhalika wanakwambia, "nchi inafunguka". Wanahisi uhuru walioukosa miaka 5 tuliyoipa kisogo.

Kumbe hata mradi wa Bandari ya Bagamoyo (BEZ) iliyopigwa vita na Pombe ilimkera. Ilimweka jela la kifikra. Hakupenda lakini leo ameamua tufanye mazungumzo mradi ufanyike.

Ndugu zangu, tumuunge mkono Samia kuondokana na gereza la kifikra ili tulisongeshe mbele gurudumu la maendeleo ya nchi.

Binafsi nimejitoa sadaka kumlinda na kumtetea Mama yetu Rais Samia Suluhu Hassan. Mniunge mkono.

Bollen@2021
#MguseMamaNinuke
 
She's doing well, hawezi kumfurahisha kila mtu Ila nadhani anataka kufungua nchi, how does she want to do it is another question.

Anataka fair share, freedom in almost everything..je, watanzania wanaweza kuishi kwa kupewa uhuru kiasi hicho? It's another question.

Mimi namtakia kila lenye heri coz her achievements is my success!!
 
RAIS MAGUFULI ALIMWEKA "JELA" MAKAMU WAKE SAMIA SULUHU HASSAN

Na Bollen Ngetti

MWANAMUZIKI Ndanda Kosovo aliwahi kuimba, "Jela..jela ni mbaya, jela..jela ni mateso". Ndanda hakukosea. Aliimba uzoefu alioupata jela hapo Ukonga. Ninamuunga mkono Ndanda kwa uzoefu nilioupata nikiwa jela Keko na Segerea. Jela ni mbaya. Ukiwa jela umezungukwa kuta nene ndefu huwezi kuona nje kwa kifupi unakuwa umenyimwa uhuru wako.

Hata hivyo hakuna jela mbaya duniani kuliko hata Gwantanamo kama jela ya fikra. Yani jela ambapo huwezi kutoa mawazo yako hadharani. Hii ni jela mbaya inayojengwa na shetani tu.

Niliwahi kudokezwa huko nyuma lakini sikuandika maana nilikosa ushahidi kwamba kuna wakati Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan alitaka kujiuzulu nafasi ya Umakamu kujiondoa kwenye gereza la fikra lakini wenye hekma na busara walimshauri asifanye hivyo.

Kwa namna Rais Samia Suluhu Hassan alivyoongoza nchi hii kwa siku 100 ni dhahiri alikuwa jela la fikra. Ni ukweli kwamba hakukubaliana na mambo mengi ya Rais Magufuli hata kama leo anasema "Mimi na Magufuli ni kitu kimoja" lakini matendo ni tofauti.

Mama Samia hakukubaliana na uendeshaji wa demokrasia nchini. Alikuwa jela na ilimtesa ndio maana amechukua njia tofauti kuendesha dhana nzima ya demokrasia. Hakuwa na jinsi wala namna. Bila shaka alilia kimya kimya gerezani.

Mama yetu Samia hakupenda uminyaji wa Uhuru wa Habari. Ilimtesa ndio maana "Fundi" alipomwondoa duniani Pombe naye kuchukua hatamu waandishi wa habari wakashangweka. Akaruhusu Uhuru wa Habari na dunia imeshuhudia maana enzi hizo za jela hata andiko hili lisingetoka maana ningekwenda jela la majengo.

Mama Samia hakufurahishwa na kesi za kubumba. Ilimtesa, ilikuwa ni jela kwake ndio maana alipoingia madarakani akafyatua kesi 147 zilizobumbwa na TAKUKURU. Hali hii ilimtesa. Lakini kuachiwa kwa viongozi wa dini wa Uamsho waliosota kwa miaka 9 jela nayo ilimweka jela kisaikolojia Samia. Hakupenda uonevu.

Huyu mama ni swala 5. Ni Muislamu Safi. Hapendi mali za dhulma iwe ni kwa mtu binafsi au Serikali. Hakupenda fedha za dhulma zilizotokana na kesi za kubumba za uhujumu uchumi na ML ndio maana tunaendelea kushuhudia watuhumiwa wakichomolewa magerezani kwa makundi. Lilimuumiza lakini hakuwa na lakufanya maana hakuwa Mkuu wa Maamuzi, Rais. Kitendo cha Mahakama Kuu kuamuru Serikali kurudisha fedha za dhulma kwa kina Mbowe ni ishara nyingine ya kuwa mama yetu aliumia sana kwa matendo hayo. Alikuwa jela.

Makamu wa Rais Samia (sasa Rais) hakupenda watu kuishi kwa hofu na woga. Alitamani watu wawe huru ndani ya nchi yao ila waheshimu Sheria za nchi. Ndio maana leo hata mama lishe, bodaboda nakadhalika wanakwambia, "nchi inafunguka". Wanahisi uhuru walioukosa miaka 5 tuliyoipa kisogo.

Kumbe hata mradi wa Bandari ya Bagamoyo (BEZ) iliyopigwa vita na Pombe ilimkera. Ilimweka jela la kifikra. Hakupenda lakini leo ameamua tufanye mazungumzo mradi ufanyike.

Ndugu zangu, tumuunge mkono Samia kuondokana na gereza la kifikra ili tulisongeshe mbele gurudumu la maendeleo ya nchi.

Binafsi nimejitoa sadaka kumlinda na kumtetea Mama yetu Rais Samia Suluhu Hassan. Mniunge mkono.

Bollen@2021
#MguseMamaNinuke
Hapa ndipo mnapokera watu, kama kweli Samia alikuwa opposite na mkuu wake, the best decision kwake ingekuwa kujiuzulu na tungeona ukomavu wake kisiasa, angekuwa kinyume na mkuu wake angekataa kuongeza mda katika kipindi cha pili cha utawala wa JPM.

Msitake kumfanya Samia malaika kwamba hakupenda the way JPM anatawala wakati she was part of his "dictatorial regime" kama mnavumyosema.

Kama angekuwa mtu wa haki, angekataa utawala wa JPM na angejuondoa, ref. Lowassa in 2007. Otherwise tuendelee kuimba mapambio ya CCM coz wametukamata masikio bila kujielewa.
 
Hapa ndipo mnapokera watu, kama kweli Samia alikuwa opposite na mkuu wake, the best decision kwake ingekuwa kujiuzulu na tungeona ukomavu wake kisiasa, angekuwa kinyume na mkuu wake angekataa kuongeza mda katika kipindi cha pili cha utawala wa JPM.

Msitake kumfanya Samia malaika kwamba hakupenda the way JPM anatawala wakati she was part of his "dictatorial regime" kama mnavumyosema.

Kama angekuwa mtu wa haki, angekataa utawala wa JPM na angejuondoa, ref. Lowassa in 2007. Otherwise tuendelee kuimba mapambio ya CCM coz wametukamata masikio bila kujielewa.
Ni mtazamo wa Bollen Ngeti
 
Hakuna tena anaeogopa kukosoa.

Iwe Jf au hata ma group ya watsap.

Hakuna anaeogopa kutekwa wala kufatiliwa na Nissan nyeupe.

Kila mtu anajiona Yuko huru kutoa mawazo yake.

Wabunge wa CCM sasa wanaikosoa serikali.

Upinzan wanatembea nchi nzima kufanya siasa.

Mahakama zinafanya kazi bila maagizo ya wanasiasa.

Wanamuziki wanaimba bila kuogopa.

Asasi za kiraia zimeanza kufufuka.

Tra imeacha kenyanganya hela kibabe.

Siku 100 za neema tupu kwa waungwana na wenye akili...
Na wala hatugombani.Yule dingi alikuwa anakula ganja.😝😝😝😝
 
Ogopa sana kuwa na Rais ambaye hata wapinzani kama CHADEMA na ACT wanamsifia kila kukicha kwenye mitandao.

Rais anayesifiwa na kupongezwa na "wapinzani" ni Rais asiyejua majukumu yake.

Mfano, akitokea Rais Marekani akiwa ni kutoka Republican halafu Democrats wakawa wanamsifia kila siku na kumpongeza basi huo utakuwa ndiyo mwisho au kifo cha siasa Marekani.

Hilo linatokea Tanzania, siasa ndiyo zinakufa sasa. Wapinzani wote wana mahaba na mama.
Mjinga weye.Kama mtu anafanya jambo jema ataachaje kusifiwa?Wote ni Watanzania.Usiwe unakariri visentensi vya lipuuzi.😝😝😝😝😝
 
Ogopa sana kuwa na Rais ambaye hata wapinzani kama CHADEMA na ACT wanamsifia kila kukicha kwenye mitandao.

Rais anayesifiwa na kupongezwa na "wapinzani" ni Rais asiyejua majukumu yake.

Mfano, akitokea Rais Marekani akiwa ni kutoka Republican halafu Democrats wakawa wanamsifia kila siku na kumpongeza basi huo utakuwa ndiyo mwisho au kifo cha siasa Marekani.

Hilo linatokea Tanzania, siasa ndiyo zinakufa sasa. Wapinzani wote wana mahaba na mama.
Akiamka Leo bwana yule atajishangaa sana sana atajua watu walikuwa wana mpuuza tuu
1)wapinzani wameshinda kesi kurudishiwa 350mi
2)barakoa mpaka vyumba vya ikulu
3)bodi ya mikopo imeondoa VRF
4) ATC hasara tupu interm of billions
5) kufundisha uzalendo kwa kiswahil...NO
6) Mpaka wa Kenya uko wazi bidhaa zinauzika
7)Bando za internet zimeshuka ( yeye) alitaka zipande na zikspanda
8) waliokuwa wanamwabudu akina sabaya wapo jela " wanashikishwa ukuta"
9)Manji karudi
10) wafanyabiashara hawaporwi tena pesa
10) vyombo vya habari vipo huru online TV zipo free
11) Aliokuwa akiwabeba kwa ukabila waliobdolewa katika nafasi MF Bashiru Dotto nk!!! Heri James yeye aliomba msamaha kabisa
12)bandari ya bagamoyo inajengwa na ndugai aliyeiponda anausifoa
Kwa kifupi tusichague kiongozi aliyetoka katika umasikin ni hatari sana tumejifunza
 
Ndani ya muda mfupi wa utawala wa Mama yetu kipenzi SSH tumeshuhudia yafuatayo;
  1. Ushetani unatoweka
  2. Uonevu, uharamia na ujambazi wa kisiasa unakosa nguvu.
  3. Demokrasia inaanza kutamalaki.
  4. Ukabila na ukanda unakwenda kupungua.
  5. Sifa, majigambo, umimi umetoweka
  6. Ubinafsi nao unakosa nguvu
  7. Kupotea na kuuawa nako kunakuwa historia.
Mama SSH ni chaguo la Mungu, huyu ni 'Easter' ktk Biblia takatifu.
Mimi nimejifunza kitu tusichague mgombea alietokea katika umasikin ukampa uongozi ni hatari sana
 
She is doing fine. Baadhi ya hofu zetu hata kama yeye si Rais hakuna wa kubadili. Asimamie maono yake asisikilize matapeli wa kisiasa.
 
Back
Top Bottom