Iraq: Iran yashambulia kwa makombora kambi mbili za Jeshi za Marekani, Ain al-Asad na Erbil

Viongozi wa Iran wameomba wapewe target tu warushe makombora ili kuwapoza wananchi kuwa tumeweza lakini ukweli hawawezi hizi ni siasa tu viongozi wanajuwa vizuri wakipiga kweli basi na wao ndio mwisho wao.

hii yote na movie tu Iran hatapiga hata askari mmoja wa USA huo ndio ukweli. Na kama kweli wamepiga halafu hakuna majeruhi basi waache vita maana kama umeshindwa kuhit target Iraq jirani yako ujuwe mbali huwezi na vita huwezi.
 
Yaani Mimi Iran nilipoona amepandisha bendera nyekundu nilijua shambulizi la Kwanza litakuaa newyork city palepale,kumbe kaenda kupiga waarabu wenzie.....atakayeweza mtetemesha muamerika ni Yule atakayeweza piga bomu ndani ya ardhi ya amerika Siyo huko pembeni pembeni! Kaka Vita awamu hii hamuwez pigania ardhi yao basi hesabuni maumivu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi nadhan hakuna vita itakayotokea, na hakuna anaetaka vita sio US wala Iran.

Javad Zarif, Foreign Minister wa Iran kwnye twitter page yake anasema baada ya kuattack base za US wame "conclude" revenge yao and hawana mpango wa vita.

Iran wako under pressure kutoka ndani to respond lakini wamefanya shambulio calculated bila kusababisha casualties/vifo na kuplay diplomacy.

Kwa sasa nadhan balance kwny hii saga is restored, US walimuua general wakabaki na guilt, Iran amerespond somehow so guilt is written off suala hapa ni "what comes next", tusitegemee vita ila figisu zitaendelea.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapa ume andika utamu
Saafi bila Ushabiki maandazi
Vita hii itakuwa mbaya
 
Inamaana ile midude ya marekani ya kuzuia makombora sjui s300 na s400 zimeshindwa kuzuia grenades za Iran? Pro Us mbona tunaangushwa huku mtaani hatuna amani kama mashabiki wa Arsenal tu. Tunaiagiza marekani irestore heshima yake mara moja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi kuna kambi isiyo na mwanajeshi? baso hizo sio kambi ni Godown za kuhifadhia korosho! Unahani marekani atakubali kusema wanajeshi wake wameuawa??? Siasa nyingi usikute wameuawa ila wanaficha tu

Sent using Jamii Forums mobile app
Izo kambi zote uko zina bunkers (mahandaki) chini ya ardhi ya wanajeshi kuingia endapo watashambuliwa na mabomu kama leo na yana radar kudetect makombora mapema ili alarm ipigwe watu waingie kwenye bunkers wasipate madhara, na ndio kilichotokea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamani mpaka sasa hakuna jibu kutoka kwa marekani au amekubali yaishe ila Trump anaelekea pabaya sana Mara leo yuko kwenye trade war na china,mara ukuta Mexico ,mara north Korea halafu kimzaha mzaha anataka aanzishe WW3
 
Baada ya USA [emoji631] kufanya shambulizi ndani ya ardhi ya Iran [emoji1130] na Iran kujibu kwa kushambulia vituo viwili vya Kijeshi vya Marekani nchini Iraq [emoji1131], Rais wa Marekani Donald Trump ameahidi kutoa tamko kesho (kwa masaa ya Marekani). Tusubiri kuona mwanzo mpya wa Vita nyingine kali kabisa kati ya Iran na Marekani aka Vita ya Tatu ya Dunia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watabaki kutunguae ndege ambazo zinaongozwa kwa remote na drones tu....
mtu ambaye wamarekani wanamuogopa alikuwat ni panki tu....maana yule alisema atampiga mshirika wa marekani korea kusini at the same time ataipiga marekani.....
 
Taarifa niliyonayo dakika hii Iran wametungua ndege ya Ukraine kwa bahati mbaya
Speculation tu, haya ni matukio mawili tofauti labda kwa sababu yametokea same day. Ndege hyo ya Ukraine imeanguka muda mrefu umepita baada ya Iran kufanya attacks. Ndege imeanguka near Tehran, mashambulizi kwenda Iraq yamefanyika kutokea south....... it doesnt make sense Iran warushe kombora zao kuelekea mji mkuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…