Iringa: Mahakama ya Wilaya yamwachia huru Abdul Nondo baada ya kutomkuta na hatia

Iringa: Mahakama ya Wilaya yamwachia huru Abdul Nondo baada ya kutomkuta na hatia

Hii ni aibu kubwa sana kwa serkali ya CCM na wafuasi wake. Tutasikia mengi sana mwaka huu na mpaka kufika 2025 nchi itakuwa imeoza kabisa.
 
Asiwe kama hakimu wa kesi ya sugu kapokea maagizo katoa hukumu kalala mbele

Hivi huyu hakimu si alikataa kujitoa dogo aliposema hana imani nae? Tutegemee hukumu ya namna gani?
Hakimu kukataa kujitoa kwenye kesi sio kujiandaa kulipa kisasi. Mahakimu weledi hutenda kulingana na sheria na kuuchambua ushahidi. Kesi nyingi za serikali zina madoa ya kisiasa na haziwapi shida mahakinu wanaojitambua.
 
Hivi ishu yake na uhamiaji iliishaje.
 
Nae analia nini sasa,kama uko sahihi ujatenda kosa ulie nini.
 
Eti ndiye Amiri jeshi wa vikosi vya ulinzi na usalama mkoa wa Dar es salaam. Jamani imekaaje watu wa Dar kila kukicha kamanda wenu mkuu ni vilio tuu hadharan? hamjisikii aibu?
Kamanda wa hivi anaweza kuona panya chumbani akapanda juu ya kabati kujificha.
Huyo ni bingwa sana wa kuchanganya dini na siasa. Unakumbuka wakati ule wa dawa za kulevya? siku hiyo alienda kusali makanisa matatu sasa umewahi kuona wapi mkristo anasali makanisa matatu kwa siku moja au mwisilam kuingia kuswali misikiti mitatu kwa sala ya ijumaa tu?
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa leo itasoma hukumu ya kesi inayomkabili Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi #Tanzania (TSNP), Abdul Nondo. Katika kesi ya msingi, Nondo anakabiliwa na makosa mawili ya kudanganya kuwa alitekwa, na kutoa taarifa za uongo, aliyoyatenda Machi 7, 2018.

Mliopo iringa update muwe mnatupa.

UPDATE

Mahakama ya Wilaya ya Iringa imemkuta Abdul Nondo hana hatia hivyo imemuachia huru

View attachment 921914
====

ABDUL NONDO ASHINDA KESI DHIDI YA JAMHURI KATIKA MAHAKAMA YA WILAYA IRINGA

Swali la Hakimu la msingi, ni Je, Jamhuri wameshindwa kueleza kuwa mshatikiwa alifikaje Mafinga?? Pili, mahakama imekosa ushahidi kuhusu alifikaje Mafinga.

Tatu, hakuna ushahidi toka jamhuri kuwa mshatikiwa alikuwa wapi wakati wa tukio. Hivyo mashahidi wa jamhuri wametoa ushahidi wa hisia.

Nne, Jamhuri wameshindwa kuthibitisha uongo wa mshatikiwa kwa kila namna na hata kielelezo kilicholetwa na Jamhuri kinatia mashaka sana, kwa mkanganyiko huu makahama imejizuia kuyaamini maelezo yaliyoletwa mahakamani.

Ifahamike siyo jukumu la mahakama kujua mshatikiwa alitekwa au hakutekwa, hilo ni jukumu la polisi.

Hivyo basi, mahakama imeamua Abdul Nondo aachiwe huru.

Mwisho kabisa, Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), unawashukuru mawakili wake waliosimamia kesi ya Abdul Nondo tangu mwanzo, lakini kipekee zaidi tunaishukuru mahakama kwa kutenda haki katika hukumu hiyo.

Imetolewa leo tarehe 5 Novemba 2018.
Na: THRDC
Hii hukumu ukiiangalia kwa makini unapata picha nani alimteka Nondo na pia nani ni mhusika mkuu wa utekaji wa watu wenye maoni kinzani na viongozi wa serikali.
 
Hivi serikali wamewahi shinda kesi? Niabu sana kwa serikali na kambuka waziri wa kipindi kile aliongea kwa dharau sana kuwa dogo alikuwa anamfata mpenzi wake. Daahh inaumiza sana
 
Wakuu nimefuatilia katika mitandao naona watu wanatoa pongezi kwa Mahakama kutoa dhamana kwa NH. Zitto na kumwachia huru Abdul Nondo.
Nimebaki na mawsali yasiyokuwa na majibu.
Ivi Mahakama kama chombo cha kutafsiri Sheria inapotimiza wajibu wake kuna sababu ya kupongeza?
Mfano mdogo Baba ukinunua nguo za watoto na mahitaji mengine je kuna sababu ya kukupongeza? Jibu ni HAPANA maana unakuwa unatimiza wajibu.
 
Kupongezwa ni ishara ya kuaminiwa, raia kupongeza mahakama ujue wana imani nazo. Na kupongeza si kosa kisheria.

Japo siku hizi tunashuhudia watu wakipongeza kinafiki.
 
Back
Top Bottom