Iringa: Mwanafunzi wa Mwaka wa pili amnyonga mpenziwe wa mwaka wa pili na kutuma ujumbe kwa Wazazi wa Marehemu

Iringa: Mwanafunzi wa Mwaka wa pili amnyonga mpenziwe wa mwaka wa pili na kutuma ujumbe kwa Wazazi wa Marehemu

"enyi vijana sikilizeni mnapokuwa masomoni acheni mchezo na mapenzi mnawapa shida wazazi wenu"
Mapenzi hayakwepeki ila tunakuwa makini. Yani unatoka chuo hujawahi kuwa na hisia na mtu? Ndoa si utajinyonga ukikosewa kidogo tu. Wanaotakiwa kuyaepuka ni walokole na masheikh washika dini sana. Sisi wa kawaida tunapenda kwa kiasi, na mikasa ipo ila sio ukichaa wa mtu mmoja ufanye ionekane ni kosa kupenda. Hata kwenye ndoa wana magunia ya mkaa wengine.
 
Hili neno, "mapenzi", linakosewa sana matumizi yake. Mapenzi ni kati ya wanandoa tu, nje ya hapo siyo mapenzi bali ni, "zinaa na uasherati".

Jamii yetu inapaswa kubadilika, mfano, kichwa cha habari hii kilipaswa kusomeka hivi; "MWANAFUNZI WA MWAKA WA PILI AMNYONGA MWASHERATI MWENZAKE".


Kumbe ukisema:

^JPM alikuwa na mapenzi mema na nchi yake,^ ni kosa la jinai!???

Halafu, siku hizi neno moja haliwezi kuwa na maana zaidi ya moja tena!???
 
Daah!!! hivi kumbe wivu wa mapenzi kupelekea mpaka kuuana bado upo??
 
Mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Chuo Kikuu Cha Iringa Bi Petronel Mwanisawa (21) ameuawa kwa kunyongwa na Mpenzi wake ambaye pia ni Mwanafunzi wa mwaka wa pili Chuoni hapo

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa Juma Bwire amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba wanamshikilia mtuhumiwa Mr Prudence Patrick (22)

Tukio hilo la kusikitisha limetokea maeneo ya Kihesa Iringa na mtuhumiwa alikamatwa njia ya Dodoma akijaribu kutoroka

MCL
hua mna maana gani vile???
 
Kumbe ukisema:

^JPM alikuwa na mapenzi mema na nchi yake,^ ni kosa la jinai!???

Halafu, siku hizi neno moja haliwezi kuwa na maana zaidi ya moja tena!???
Inategemea hilo neno "mapenzi" unalitumia katika muktadha upi. Mimi nimemaanisha matumizi ya hilo neno katika mahusiano. Wenye akili zao kichwani wamenielewa.
 
Hawa vijana wapewe elimu ya kujithamini wao kama wao, kuliko kufikiri yupo mtu mwingine wa kukupa thamani, people are always there to disappoint you...
 
Mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika Chuo Kikuu cha Iringa, Petronel Mwanisawa (22) amefariki dunia kwa kunyongwa na mpenzi wake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Juma Bwire amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba wanamshikilia mtuhumiwa, Prudence Patrick (21), ambaye pia ni mwanafunzi wa mwaka wa pili katika chuo hicho.

Akizungumza na Mwananchi, Kamanda Bwire amesema tukio hilo limetokea Juni 1, mwaka huu maeneo ya Kihesa.

Amesema siku ya tukio marehemu hakurudi nyumbani kwao jambo ambalo si kawaida yake, hivyo wazazi wake waliingiwa na hofu na kuanza kumtafuta.

"Marehemu alikuwa anaishi na wazazi wake, na huyu mtuhumiwa yeye alikuwa amepanga. Kwa hiyo siku ya tukio alitoka kwenda chuo, lakini mpaka usiku akawa hajarudi, ndipo wazazi walianza kupata wasiwasi, wakampigia simu rafiki yake lakini hawakufanikiwa," amesema Kamanda Bwire na kuongeza

"Kwa hiyo jana ndo tukampata, na hiyo ni baada ya mtuhumiwa mwenyewe kutuma ujumbe mfupi wa maneno kwa mzazi wa marehemu akisema alikuwa na Petronel na kwamba amefariki. Baada ya hapo hakupatikana tena," alisema.

Amesema baada ya wazazi kupata taarifa hizo waliripoti kituo cha polisi, ndipo askari walikwenda katika nyumba ya mtuhumiwa na kuukuta mwili wa marehemu.

Bwire amefafanua kuwa, taarifa za awali zinaonyesha binti huyo alinyongwa na mpenzi wake na chanzo ni wivu wa mapenzi.

"Mtuhumiwa tulimkamata njia ya kuelekea Dodoma alipokuwa akijaribu kutoroka na upelelezi wa tukio hilo unaendelea," amesema Kamanda Bwire.

Chanzo: Mwananchi
Mapenzi haya yanatesa wanachuo mnoo😡😡
 
Mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Chuo Kikuu Cha Iringa Bi Petronel Mwanisawa (21) ameuawa kwa kunyongwa na Mpenzi wake ambaye pia ni Mwanafunzi wa mwaka wa pili Chuoni hapo

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa Juma Bwire amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba wanamshikilia mtuhumiwa Mr Prudence Patrick (22)

Tukio hilo la kusikitisha limetokea maeneo ya Kihesa Iringa na mtuhumiwa alikamatwa njia ya Dodoma akijaribu kutoroka

MCL
Kwahyo umerudia uzi wa mtu kwenye comment..hiv mkoje
 
Dogo apelekwe gereza la Pawaga au Mafinga akalime huku akiwa ameolewa na nyapara ndio akili zake zikae sawa.
 
Back
Top Bottom