Huwez kuwaona wanafik
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Huwez kuwaona wanafik
Wadau mimi sina mengi ya kusema ila tu nikitafakari haya mauaji na ukatili huu unaoendelea dhidi ya raia najikuta nakumbuka historia ya aliyekuwa kiongozi wa ujerumani Adolf Hitler na kuanza kujiuliza kama hata hapa bongo amepatikana mtu kama yeye.
Hakuna hatua inayochukuliwa kwa wahusika kanakwamba wanayoyafanya yana baraka zote kutoka juu.
Kwakweli inauma sana na penginei kadri siku zinavyozidi kwenda tutapata jibu la swali hili.
Hivi huwa tuakwenda misikitini na makanisani kama fashion tu?
Wataficha ukweli wa mambo haya mpaka lini?
Tusuburi kwani ni vigumu sana kuficha ukweli.
Ni vigumu pia kuamini kama kweli haya matendo yanatokea hapa bongo.
Heri mzungu kuliko mkoloni mweusi.
Huyu baba na mkewe alikufa ,aisee baada ya kifo Cha mumewe hakuwa vzr tenaHii nchi ina laana nyingi.
Aiseee watoto wapo wapi?Huyu baba na mkewe alikufa ,aisee baada ya kifo Cha mumewe hakuwa vzr tena
Mawazo yalimmaliza
Watt wao wamekuwa ss,walipata msaada ,na Wana akili balaa
Iringa ndo wapo!Aiseee watoto wapo wapi?
Miaka 12 imepita na matukio yanazidi kuongezeka.Mwwenyekiti na Chama cha Waandishi wa habari mkoa wa Iringa na mwandishi wa habari wa Channel 10 amepigwa risasi na polisi kwenye mkutano wa CHADEMA Mufindi.
---
Mwandishi wa habari wa Channel Ten mkoa wa Iringa na Mwenyekiti wa chama chama cha waandishi wa habari mkoa wa Iringa Daud Mwangosi ameuwawa katika vurugu za Polisi na wafuasi wa Chadema katika kijiji cha Nyololo wilaya ya Mufindi mkoani Iringa leo.
Mwanahabari huyo Daud Mwangosi aliuwawa majira ya saa 10 jioni katika ofisi za Chadema Nyololo huku askari mmoja akijeruhiwa vibaya kwa risasi.
Kabla ya kuuwawa kwa mwanahabari huyo mabomu yaliweza kupigwa eneo hilo kuwatawanya wafuasi hao wa Chadema ambao walikuwa wakigoma kutawanyika eneo hilo na kuamua kukaa chini kuwa hawapo tayari kuondoka katika ofisi yao.
Chanzo cha mwanahabari Mwangosi kuuwawa kilitokana na kukamatwa kwa mwandishi wa habari wa gazeti la Nipashe mkoa wa Iringa, Godfrey Mushi na hivyo mwanahabari huyo kutaka kuhoji polisi sababu ya kukamatwa kwa mwanahabari huyo, ndipo askari hao walipoanza kumshambulia kwa kichapo na baadae mlio kama wa bomu ulisikika eneo hilo na mwandishi huyo na askari mmoja waliaguka chini.
Ndani ya dakika tano ilisikika sauti kutoka kwa askari huyo kuwa 'afande nimekufa' ndipo walipomchukua na kumpeleka Hospitali ya wilaya ya Mufindi huku mwili wa mwanahabari huyo ukipelekwa chumba cha kuhifadhia maiti.
Katika vurugu hizo zilizodumu kwa takribani dakika 30 kwa askari na wafuasi wa Chadema kurushiana mawe kwa mabomu zaidi ya magari matano ya Chadema na ya wananchi yameharibiwa huku watu kadhaa wamejeruhiwa na mwanahabari mmoja Godfrey Mushi akijeruhiwa vibaya.
PIA SOMA
- Ripoti ya Kifo cha Mwangosi
Viongozi na Wanasiasa wengine waliowahi kupigwa risasi
VISA DHIDI YA WANAHABARI WENGINE WA TANZANIA:
- Utata kifo cha hayati Abeid Karume
- DODOMA: Tundu Lissu ajeruhiwa kwa risasi, akimbizwa Hospitali
- Simulizi: Kisa na Mkasa wa Mauaji ya Jenerali Imran Kombe (Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Usalama wa Taifa-TISS)
- Kifo chenye utata cha Waziri Nicas Mahinda
- Wakili mtetezi wa ICTR Prof. Jwani Mwaikusa auawa Tanzania
- TANZIA - Waziri Salome Mbatia afariki dunia, maswali yaibuka!
- Maandamano ya CHADEMA: Aqulina Akwilini Mwanafunzi wa mwaka wa kwanza NIT apigwa risasi na kufariki; Polisi wakiri kuhusika
- Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka ashambuliwa kwa risasi na Watu wasiojulikana
- Askari polisi aliyepigwa risasi na majambazi Tanga afariki
- Mwanahabari Erick Kabendera akamatwa na Polisi nyumbani kwake; yadaiwa anaendelea na Mahojiano
- Mwandishi wa kampuni ya Mwananchi Communications (MCL), Azory Gwanda apotea siku 10 na hajulikani alipo
- Absalom Kibanda (Mwenyekiti wa Jukwa la Wahariri) avamiwa na watu wasiojulikana na kujeruhiwa
- Mwandishi Mwangosi auawa katika vurugu kati ya Polisi na CHADEMA
- Mhariri Mtendaji wa Gazeti la MwanaHALISI, Saed Kubenea avamiwa na kumwagiwa tindikali akiwa ofisini kwake
- Mwandishi wa Mwananchi Jesse Mikofu ashambuliwa na askari akitekeleza majukumu yake
- Mchora katuni Opptertus John Fwema ashikiliwa na Polisi kwa Makosa ya Mtandao
- Mwandishi wa Watetezi TV mbaroni kwa madai ya kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni juu ya watuhumiwa kulazimishwa kulawitiana Kituo cha Polisi
🙏🙏🙏 God Bless them 🙏🙏🙏Iringa ndo wapo!
Wakati nimeenda iringa 1 alikuwa chuo,2 secondary ,wa mwisho alikuwa mdogo km Drs la 2 hivi.
Wale wawili wote I think watakua wanamalizia chuo
Sshv yule mdogo atakuwa secondary Kuna msamaria mwema alimchukua.
Awamu ya Nne ndipo yalipoanzia na kuendelea kushika kasi !Miaka 12 imepita na matukio yanazidi kuongezeka.
God have mercy.