Iringa na Njombe ilivyoshambuliwa na chawa

Iringa na Njombe ilivyoshambuliwa na chawa

inasikitisa lakini,
but hizo ndio indicator za nchi ya uchumi wa kati (sick)
5 tena oyeee
 
mimi chawa simjui na sijawahi kumuona ila kunguni balaa lake siyo la kitoto, wakikushambulia kwa muda mrefu unaweza ukaugua kiharusi.
kunguni nmemfahamu nikiwa secondary nakaa hostel
 
Hawa wadudu ni ishara njema kwetu hatujui tu. Ukiona mdudu ujue upo kwenye mazingira halisi (nachuro) kwa binadamu. Hawa wadudu wanakufa kirahisi sana sehemu yenye makemikali.
Kenya inaongoza EA kwa watu walioathirika na wanaokufa kutokana na funza hao. Kuna mashirika kabisa yanasaidia kupambana na hao funza na chawa jaribu kuingia youtube search "jigger in kenya" utajionea
 
Funza wanaingia ndani ya mguu inamaana?
Kiroboto kinapenya miguuni baadae kinanenepa kwa kunyonya damu. Linakuwa jeupe kama punje ya kunde. Ndani linakuwa na mayai kibao. Kama halijatolewa, hayo mayai yakitotolewa yanasambaa sehemu zingine za miguuni.
 
Ukweli mtupu! Nimetembelea maeneo ya Malangali, Ifunda, Nyololo, Makambaku, Ulayasi na Madaba chawa ndio kwao na mimi nimeondoka nao.

Nimerudi Same nimefua nguo kwa maji ya moto nikanyoa na mkulungu (kipara) angalau sasa nina ahueni.
Ukijipulizia na Marashi
 
Tatizo hawaogi, dawa ya chawa usafi (kwa uzoefu wangu)

halafu, hv funza ndo wapoje eti na wanasababishwa na nini? Nawasikia tu hawa wadudu.
 
Ubaridi unasingiziwa tu, issue ni uchafu.

Chawa wapo mikoa yote ila viunoni mwa wachafu tu.

Hao jamaa Wana tabia ya kutaga mayai kwenye "pindo" za nguo hasa viunoni.
Hata uache kuivaa hiyo nguo mwezi,siku ukiivaa tu lile joto la mwili linatotolesha mayai 😁 unaanza kupiga tena gitaa.
 
Ukweli mtupu! Nimetembelea maeneo ya Malangali, Ifunda, Nyololo, Makambaku, Ulayasi na Madaba chawa ndio kwao na mimi nimeondoka nao.

Nimerudi Same nimefua nguo kwa maji ya moto nikanyoa na mkulungu (kipara) angalau sasa nina ahueni.
Jamani! Jamani!,acheni kutudhalilisha,huo ulikuwa ni uchafu wako.
 
Kwa ambao hamjui chawa nawasihi mtembelee vijiji vya Iringa mjionee!

Kutokana na jiografia ya ubaridi, wadudu hawa wamekita kambi mkoa huu! Inahitajika tahadhari kubwa sana kukwepa chawa uwapo mkoa huu.

Hoteli na lodge nyingi wanatumia mablanket mazito ambayo siyo rahisi kufuliwa Mara kwa Mara kutokana na hali ya hewa, hali hiyo imechangia sana kuzagaa kwa chawa!

Ukifika mkoa huu usipokuwa makini unaweza ukasalimia mtoto mdogo shikamoo ukizani ni mzee mwenye nywele za Mvi kumbe ni mayai ya chawa yametanda kichwani!

Wabibi wa huku miongoni mwa starehe ni pamoja na ile ya kuua chawa kwa vidole ama ile ya kung'ata kwa meno.

Ukiwa kijijini kama unaendesha chombo unatakiwa kwenda pole pole la sivyo unaweza kugonga mtu aliyesimama barabarani akiua chawa kiunoni!

Ajabu kuliko yote! Ni vile chawa wakiwa kiunoni wanakuwa weupe, na wakihamia kichwani wanabadilika rangi wanakuwa weusi!

Usiombe umkute mtu ana chawa halafu miguu nayo iwe imetafunwa na funza mithili ya vidole kuwa kama Tangawizi! Unaweza kuondoka Iringa bila kuaga!

Chawa wa Iringa Kiboko!
Wewe jamaa itakuwa tu Wewe mwenyewe sio msafi.chawa na funza wapo kila sehemu,ishu hapo ni usafi.
 
Back
Top Bottom