Islam’s role in Tanzania’s freedom struggle


We Nguruvi3 kwanza naomba rukhsa ya kucheka!
Teh teh teh teh !

We kweli mbulula swahiba! Na hili usiseme ni tusi! La hii ni sifa ya yule anaeongea bila kufikiri!
Unasema wazungu hawaijui tanganyika kuliko watanganyika wenyewe!

Hivi wewe unakula ile hashish au?

Mzungu AMEKUTALAWA WEWE NA NA BABU YAKO NA HUYO BABA YAKO WA TAIFA wa karne nyingi mno!

Akikutumikisheni na kukuamrisheni kila alitakalo! Halafu wewe uliezaliwa juzi unasema unajua kuliko your MASTER!?
Je!
Una habari kuwa mpaka leo huyo mzungu bado ana influence kwenye maisha yako ya kitanganyika??

Na kesho huyo mzungu akiamua wewe Nguruvi3 ufunge ndoa na Mag3 utakuwa huna hiari? Au utasema haya pia matusi??

Lkn kumuita maalim mohamed said mjinga unaona sawa sio?

Huyo mzungu aliyekutawala wewe na akamfundisha mpaka babu kutumia choo badala ya kunya porini ndio huyohuyo anaemualika Mohamed Said ktk nchi yake aende akatoe elimu aliyonayo ili huyo COLONIAL MASTER WAKO APATE FAIDA!

Sasa wewe badala ya kumshukuru sheikh MS kukuwakilisha huku ughaibuni!
bado unamtukana na kumuona hana maana!

Basi mi nakutizama tu! Manake wanasema waungwana
" you can take the donkey to the river but you cant force him to drink"

And I guess we have lots of donkeys around!
I am not sure if you are a member of the donkey club!

Teh teh teh teh!
 
Last edited by a moderator:


Nakusoma sana Ulamaa Gombesugu kwa bayana zako,

SISI tupo kwenye jamvi hapa huku tukizid kutaradadi na kujinafasi,

Si unajua??popote pale alipo Moh Said sisi tunatandika jamvi na kushika adabu zetu na kufyonza maarifa,

Hapa na hatubanduki labda abanduke yeye,ilmu hii wengine wanaitolea jasho kuipata,sisi twaipata hapa bure bure tuh kwanin tusitandike jamvi??

Tupo hapa tumejaa telee...
 

Al habib al akhyi gombesugu salam za amani zigike kwako inshallah.
Sisi tupo hapa tukipata darsa safi kutoka kwa maulamaa wote! Kuanzia kwa MS na nyie nyote!
Tunaburudika pita kiasi!
Yaani hata ile mi salsa sitizami tena siku hizi!
Inshallah tuko pamoja.
 
Last edited by a moderator:


Kuna nyakati Nguruvi3 anaenda upogo sana,

Anakuwa so judgemental,yeye anadhan ya kwamba watu wanapomjibu yeye kwa lugha za kebehi kulingana lugha ambazo yeye hapo awali alishazitumia kwa muktadha tofaut basi hudhani vijana hao husukumwa na mafundisho ya iman wanayoiamin,na hapo ndipo anapokosea,

Kwanin akimbelie kuhukum ya kwamba bila shaka vijana watakuwa wanafanza hivo kwa mafundisho ya iman zao??na ana uhakika gan kama hao anaozungumza nao ni watu wa weledi huo ama vipi??

KWANN yeye anapotumia lugha zinazolandana na hizo watu hawakimbilii kumnyooshea kidole kwa mafundisho ya iman yake??

Besides,hapa hatupo kwenye mjadala wa kuangalia dini ipi ina mafunzo mazur na ya maadili kwa vijana wake,hoja inayozungumzwa iko waz sana,kupishana lugha wakati mwingine ni sehem ya mnakasha tuh,isiwe sababu kwa mwingine kuanza kusema ati kina fulani hawana maadili ya dini,ina husiana vipi na mada husika?

NYEKUNDU IWE NYEKUNDU,KIJANI IWE KIJANI FULL STOP...!!
 
Last edited by a moderator:
Dr. kahtaan.

Hata vitabu vya historia ya Tanganyika wametuandikia hao wazungu kupitia msaada wa wazee wetu wa Mzizima.

Kitabu cha Judith Listowel, kimeandikwa mwaka 1965 " The Making of Tanganyika.

Kingine kitabu cha John Iliffe, kimeandikwa mwaka 1977 "A Modern History of Tanganyika.

Tanzania wameandika kitabu cha historia ya TANU pale Kivukoni uchafu mtupu.
 
Last edited by a moderator:

issue ni majina. kleist sykes alikuwa ni dini gani
 

Ndugu yangu al shariff Ritz haya yako wazi! Tatizo ni hawa watu kama huyu Nguruvi3 kwa kutokuwa na weledi huo!

Lkn tutafanya nini zaidi ya kuwakumbusha?
Manake kama bara letu lingekuwa bado halina matatizo ya sheria za uhamiaji!
Basi watu kama hawa tungeenda watupa Sierra Leone! Mbaali kabisa na sisi!
Teh teh teh teh!
Tupe darsa shariff! Tuburudike zaidi.
 
Last edited by a moderator:
Dr. kahtaan.

Hawa wazungu tunaoambiwa hawaijuhi Tanganyika wapo toka mwaka 1880 Wajerumani, mwaka 1914 wakachuwa Waingereza, leo tunaambiwa wazungu hawawezi kuijua Tanganyika kutuzidi sisi.
 
Last edited by a moderator:
Upo hapa kuita watu "Stupid" Ukirsto wako ndiyo umekufundisha haya.
Yani wewe jamaa IQ yako ilivyo ilivyondogo hata mdogo wangu wa mwsho form one maua seminary huwezi ku'argue nae.
 
Nimeuliza kuwa nionyeshwe wapi nimesema Mohamed ni STUPID. Endapo hakuna kipande kama hicho basi sina hiari bali kuwaachia ku promote hilo neno kwake.

Nadhani upande wa hoja hakuna sasa mnazua mada za kuchafua watu hilo halina tatizo kwangu kwasababu sitegemei kuwa ninaposimamia ukweli kila mtu ataupenda. Kazi ya elimu kwa umma si rahisi haya ni sehemu ya changamoto.

Ninaposema Mohamed Siad ni mentor wenu huu ndio ushahidi kwasababu yeye hajalalamika kama kuna tusi.
Hakuna aliyeonyesha wapi neno stupid lilipo! Mimi najikita katika maudhui endeleeni na spinning,
 
Kwahiyo mzee MS siku hizi kwako ni 'STUPID'
Please omyesha wapi neno hilo nimelitumia kwa Mohamed. Vinginevyo kumzulia mtu jambo si sehemu ya maadili au uadilifu kibinadamu na kwa dini the least to say. Hivi mbona mimi mumeniita kila aina ya neno na mara zote nimekuwa nawasihi kuhusu ndimi zenu iweje muzue jambo ambalo halipo?
 
Ni hivi kwa miaka mingi Mohamed Said amewaaminisha watu wa Ulaya na Marekani kuwa mwanzilishi wa AA ni K.Sykes. Si kweli ni mwalimu Cecil Matola.

Amewaaminisha watu kuwa Nyerere aliingia siasa baada ya kukutana na Abdul Sykes, si kweli na imethibitishwa.
Ameanisha watu kuwa hakuwahi kukutana na wajumbe wa AA kabla ya kukutana na Sykes mwaka 1952. SI kweli, alikutana na Dosa mwaka 1948.

Ameaminisha watu kuwa Sheikh Amir alinyimwa fursa katika serikali ya Nyerere baada ya kuongoza harakati za uhuru. Si kweli alipewa nafasi ya uwaziri akaikataa.

Mifano ni mingi sana ambayo Mohamed amekubali kuwa ni matatizo ya uandishi. Kilichopelekea yote kujulikana ni kutokana na Watanganyika wenyewe kuelewa undani na kushindwa kuunganisha dot.

Watu walijiuliza hivi inawezekana mwanzilishi wa chama akawa katibu mkuu bila kuwa na rais au mwenyekiti.
Ndipo waungwana wakasema no way baada ya kufukua wakaona Cecil Matola ndiye mwanzilishi wa wazo.
Kibaya zaidi hata akina Ramadhani Ally hawakuelezewa kwasababu tu wangefunika taswira ya mkusudiwa.
Leo tunajua AA ilikuwa na makamu wa rais.

Kuhusu wazungu nashukuru umekiri kuwa wana uwezo mkubwa na ni kwa uwezo huo kumwalika Mohamed ni sehemu ya kutaka kujua mengine nje ya historia. Utashangaa siku yanapotoka maandishi kuhusu 'extremist' wa East Africa au kuhusu udini Tanzania n.k. kwahiyo usifanye conclusion kuwa wanataka kujua sana kuhusu mzee Kiyate, wana zaidi ya hapo.

 
Nadhani ungesoma kuhusu Mohamed na tambo zake halafu ungeuliza swali la endapo tupo katika mjadala au kutambiana. Nilichofanya nikumjibu tu mzee wetu sikuwa na la ziada.

Kuhusu chuki na Mohamed Said, mimi sina sababu za kuwa na chuki naye.
Kitu kimoja ambacho anapaswa kuelewa ni kuwa heshima ni two way traffic.

Ama kwanini namuongelea sana hilo ni wazi maandishi ni yake na sijui ni vibaya nikimpa credit na wakati huo huo nikibaki na haki ya ku-critic kwa maana hii ' person who judges the merits of literary or artistic works, especially one who does so professionally'

Mimi sina mapenzi wakati wa kulisha akili yangu, na wala sipendi kulishwa hata kama ni hisani.
Kama hilo ni chuki nimeridhia niwe nalo kwasababu naiheshimu sana akili yangu na siwezi kuiweka rehani.

Ahsante
 
Inshallaha, ukipata nafasi tafadhali rejea. Natumaini utatumia wakti ulio nao kuweka lugha yako katika muktadha mzuri ili hoja zako zieleweke.

Mie nipo katika mjadala sikujua kuna kudondoshana, hata hivyo muhimu kwangu ni kufikisha ujumbe niliokusudia. Kwamba, mimi ni mahanatha, fataani n.k. hizo ni changamoto za kazi hasa elimu ya umma.

Inshallah wasalaimie hapo numbani ahli na vijana.
 
Elimu ni gharama na huapatikana kwa gharama ukiona ni ya bure jiulize sana.
 
Naam nyuzi ya Mohamed kama ile ya paper ya Nairobi hivi karibuni ilipata wafuasi wengi sana tena wakiwa wazoefu wa matusi. Nyuzi ile kaisome uniambie umepata nini!

Kuhusu vikongwe ah !hilo ni muhimu sana kwasasa. Huwezi jua kuwa matatizo ya vikongwe yanaweza kuwa ukumbini mwako au kwangu au hapa jamvini. Ni kitu kigumu sana kukielewa ndio maana nikasema nikiweka hapa itakuwa white elephant maana mzee au viajana watasoma kila mstari kama mtihani, mwisho wa paper watakuwa katika hali itakayonihitaji zaidi. Sitaki tufike huko
.
 
Mkuu THE BIG SHOW,
Haiwezekani watu wakaanza kujadili uwepo wa Bakwata bila kufikiri kwanini ilianzishwa.
Kuna kuficha sehemu muhimu ya kisa cha Bakwata ili kukidhi haja za watu na si ukweli.

Nikutanabaishe kidogo hali tuliyo nayo sasa. Unaona ambavyo Mshume Kiyate anapewa hadhi kuliko rais wa TAA marehemu mzee V.Kyaruzi. K.Sykes akipewa sifa na wala si cecil Matola . Jitihada za kumdhalilisha Nyerere kwa mavazi hadi chakula zikiendelea n.k. Hata ni makusudi kabisa kwa mtazamo wa Imani

Jitihada hizi ni mwendelezo wa majaribio ya miaka ya 1957-60+ kutaka kumuondoa Nyerere madarakani kwasababu ni mkristo.Jitihada hizo zilipozimwa zikahamishiwa katika EAMWS na kuendeleza chuki ile ile.

Nyerere na baraza la TANU wajumbe asilimia 98 waislam waliwaalika ‘waasi’ wawe sehemu ya serikali.
Sheikh Amir akakataa uwaziri na kuenedeleza siasa za mitaani zenye lengo la kumuondoa Nyerere kwa imani yake kama ilivyokuwa miaka kabla ya hapo

Hadi 1967 majaribio ya kumuondoa Nyerere kwasababu tu ya imani yake yalikuwa mengi.
Nyerere kwa uungwana akamuondoa Sheikh Amir na kumrejesha Zanzibar. Inaonekana weird eh!!

Ni uungwana kwasababu ingekuwa leo sheikh Amir angepelekwa mabwepande kufanyiwa ‘dental hygiene na pedicure’ kama Yule aliyedai mishara mzuri.

Kama si uungwana tutasemaje kwa yanayotokea sasa ya kung'oana meno na kucha? Je, ni sahihi akitokea 'mwanahistoria' na kusema haya yalifanywa dhidi ya kundi fulani.

Hakuna kiongozi duniani anayeweza kuvumilia tishio la kuangusha serikali yake kwa njia haramu.
EAMWS ilikuwa chombo huru, tatizo ikawa ni chaka la waliotaka kumuondoa Myerere kwa imani yake
EAMWS ikavunjwa na kuundwa BAKWATA kwa muktadha wa kudhibiti chaka hilo.

Je BAKWATA ni chombo cha serikali, absolutely! Nimewahi kuhoji mambo mengi tu kuhusu suala hili.
Je ilianzishwa kudhibiti waislam No . Bakwata ilianzishwa kudhibiti kundi la waislam waliokuwa na lengo la kumuondoa Nyerere madarakani, kuigawa nchi katika udini kama tunavyoshuhudia akina mzee n.k..

Tatizo ni Bakawata kama chombo au ni zaidi? jibu ni hapana, kwasababu kuna umuhimu wa kuwa na chombo cha pamoja cha kuwaunganisha watu. Tatizo ni viongozi wa Bakwata wenye masilahi mbele badala ya dini. Wanapotofautiana kimasilahi hujiondoa na kuunda makundi yanayoipinga Bakwata

Asilimia 98 ya makundi ya sasa(akiwemo Mohamed Said) walikuwa Bakwata.
Viongozi hao hawakutoka kwasababu wanaipinga Bakwata, walitoka kwa kupingana na viongozi wa Bakwata katika masuala ya masilahi.

Ni kwa muktadha huo kila anayejiuengua anatengeneza chombo chake na ndicho chanzo makundi dahari ambayo kiutendaji hayana tofauti na Bakwata kwani masilahi mbele.

Hadi hapa utaona kuwa Bakwata haikuundwa makusudi kwa sababu ya kukudhibiti Big show ukiwa Kadewele, Ligula au Naliendele.Iliundwa kudhibiti makundi ya waasi ambao watoto na wajukuu wapo bize kuendeleza harakati za watangulizi hadi leo tena wakiwa wamejificha katika magunia ya kitaaluma, kiharakati n.k.

Rais Mwinyi, Mkapa na Kikwete wote wameikumbatia Bakwata. Tafsiriyake ni kuwa kuna umuhimu wa kufanya hivyo na wala si kudhibiti waislam, vinginevyo Julius yupo kaburini miaka 10 na nje ya utawala miaka 28 nini kinawashinda kuacha waislam waunde chombo chao?

Endapo ingekuwa kudhibiti waislam basi kusingekuwa na tofauti ya waislam wa Machame na Mkuranga, wa Bukoba na Mlimba. n.k.

Kwanini Bakwata ina nguvu, jibu ni kuwa inaungwa mkono na waislam.
Iwe ni sahihi au la ukweli unabaki kuwa serikali isingeweza ku-side na Bakwata ya watu 20 Kinondoni.
Nsni stsksye wekeza kwa soko la watu 20 na si milioni zaidi ya 15

Kwa kumalizia niseme Nyerere alikuwa analinda utawala wake dhidi ya waasi waliokuwa wamejificha katika kivuli cha dini. Bahati mbaya katika kufanya hivyo lazima wapo wahanga kama wanavyolalamika sasa hivi.
Hata hivyo usahihi wa Nyerere unathibitishwa na miaka 10 ya Mwinyi na 8 ya Kikwete.

Kuseme kirahisi Nyerere lifanya hivyo kuukandamiza uilsam si kweli! lakini ni ukweli kuwa Bakwata imekuwa katika udhibiti wa serikali na nimeeleza mara nyingi kuhusu hili.

 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…