Gombesugu,
mimi nadhani content ya article yako ni bora nikabaki kama a very neutral by-stander nayo. Kwa sababu naamini masuala ulioibua especially mazazi ya Julius na witchcraft nayaona yananipa shida kuchangia. kwa vile nayaona kama ni too intrusive into a personal life ya mtu binafsi.
With regards
wickama
Wickama,
Salaam,nimependa umeandika
sincerely.
Napenda pia kuchukua fursa hii kiduchu,kukutoa
mashaka ati yakuwa mimi nimekasirika au naandika kwa hamaki
...hasha,abadan asilan!
Labda nikubali "
makosa" yangu kiduchu, yakuwa natumia exclamation mark/s
excessively!? Kwa hili nakuomba radhi mno!...lakini hata hivyo najaribu mno kukuwekea na
vicheko kwenye mangi ninenayo!?
Wewe ni kati ya watu wachache mno walobaki humu
Jf,ninaowaheshimu...ndo maana sikirihiki kukupa majibu
mwanana pale inapojiri.
Nisingependa asilan kutumia neno
mzandiki/hypocrite dhidi yako,lakini lazim nikubali yakuwa ndugu yangu wakti mwingine
unanistaajabisha mno!?
Hivi hayo mambo ya "
matambiko"/witchcraft wakti huyo
Nguruvi3,anayaanzisha na kujisifia hapa jamvini,tena huku akifanza
istizahi na kutuhimiza kumjibu ili amwage huo
"mtama" wake...wewe binafsi hukuona hiyo ilikua ni
intrusive kubwa mno tena ilovuka mipaka na hata kuingilia mambo ya ndani/mazito ya kidini aka
Tawhid!?...ambayo nina hakika huyo
Nguruvi3 na hata wewe binafsi itakuwa hizo si anga zenu asilan na wala hamna ujuzi wa
kunyambua yayo!?
Pia hukuona kabisa yakuwa ni
intrusive dhidi ya
personal lives za
Wazee Wetu/Masheikh wetu,au
Iman yetu...wakti wewe binafsi ukijaribu kunyambua na kumsaidia
Nguruvi3 kwa yayo mliyoita ati ni
"matambiko"!?
Hukuona ni
intrusive na pia ni
attack kubwa mno kwa mtu kama
Nguruvi3,pale anapoona ati ni "hoja" kuanza ku-
question Uislam wa wale
Wazee Wetu waliotangulia mbele ya Haki!?....
Inna Lillahi Wa Inna Illahi Raj'uun!
Wewe binafsi huoni yakuwa hapo nyinyi mlikua mnatoka
nje ya
mada!?
Pitia
post/s uone ni mara ngapi mimi binafsi nimemwambia/nimemstaajabu huyo
Nguruvi3,yakuwa kama kweli yeye ni msomi na pia ni "
mstaarabu" kama anavyodai,basi ilikua hakuna hata haja ya yeye kujinasib yakuwa ati ana
"mtama" from the start!?
Huoni hiyo
situation/scenario ndo ilotufanza wengi kuwa na
curiosity hapa jamvini
!?
Kwa kifupi ndugu yangu,nyinyi binafsi ndo mlokua mna-tread on a very thin
balancing act!
Embu rejea nyuma kiduchu tafadhali,uchungulie ni
post/s ngapi huyo
Nguruvi3 analazimisha sisi tumjibu hizo
karaha zake ambazo mwenyewe anaita ni "hoja",kuhusu hayo
"matambiko"...tena huku sisi
tukistahamili na kukaa kimya,yeye hurejea tena kwa
istizahi zaidi na kudai ati tumelikimbia jamvi!? Kwi! Kwi! Kwi!
Technically, huyo
Nguruvi3 anadai ati
Wazee Wetu hawakuwa
Waislam kwa sababu walifanza visomo/tawasul na "matambiko"!? Duh! Kwi! Kwi! Kwi!
Ndo maana kwenye ile post/s yangu ya jana nikakuwekea ile
code,yakuwa itakuwaje
Najsi ku-
qualify na kufikia hata kutoa
Fatwa yakuwa kipi ni
Halal na kipi ni
Haram!?
Sasa kwenye hayo maoni yako,ati unadai sasa hivi unapata shida ya kuchangia haya mauchawi/"matambiko" kwa sababu yamegeukia upande wa
Nyerere aka "Baba wa Taifa"!?
Mbona awali ndugu yangu hukupata hiyo
dhiki/shida kuchangia ule upande mwingine wa shilingi hiyo hiyo!?
Wakti mkinyumbulisha hayo mauchawi/"matambiko" na kuwachafua
Wazee Wetu!?....
Tena huku mki-question
Uislam wa hao
Wazee Wetu na nafikiri mliwatoa kabisa kwenye
Uislam...mpaka pale nadhani Shariff
Ritz na Ayatollah
Chamviga maskini ilipowalazim kutoa
Fatwa hapa jamvini ya kuwarejesha!? kwi! Kwi! Kwi!
Kwa kifupi,pamoja na yoote, nyinyi mlichokua mnakifanza labda bila kujua au kwa
makusudi;ni kuwa potray wale
Wazee Wetu ni kama vile ati ni watu dhalili,duni/
primitives,na yule
Nyerere wenu ati ndo
"msomi","mstaarabu"/"westernized"...na ati yeye ndo alokua anafuata
maadili ya dini yake ya
Ukatoliki kwa adabu na utuvu!?
Ndo pale iliponilazim kuingilia kati na kukupa
"khabar Al yaumy" kiduchu.
Na yale nilokwambia ni
kiduchu mno,hayafiki hata
thuluthi ya yale niyajuayo tena kwa undani mno,mangine hayafai hata kuthubutu kuyaweka humu mitandaoni au kumwambia yeyote!
La muhimu,nakusihi ndugu yangu,turejeeni tena kwenye
mada na kubadilishana mawazo bila ya kujali utafauti wa
opinions zetu na
itikadi zinavyotafautiana.
Pia nachukua fursa hii kumshukuru tena Sheikh
Mohamed Said,kwa upambanuzi wake uso shaka.
Nafurahika mno kila nikusomapo,na nimefurahi umenitajia
Pangani kwenye mojawapo ya
posts zako hapa.
Kama ni kweli uko
Pangani,basi kagonge hodi nyumbani kwa
Bwana Ali Masomaso,ni mfanyibiashara maaruf mno pale na kitambo aliwahi kuwa Mwenyekiti wa
CCM wa Wilaya.
Wewe jaribu kumuuliza je wamtambua
Shariff Nganganga ambaye ni mjukuu wa Shariff Simba wa
Mauya aka
Gombesugu!? Kwi! Kwi! Kwi!
Khalaf,muulize huyu jamaa anafanza jitihada zipi hapa
wilayani na kwingineko,na Wazee wake walifanza nini kabla huyo
Mjarumani hajatia maguu yake
Tanganyika hii!?
Pia muulize akukhadith
kiundani,mambo,harakati,muhanga uso kifani na fadhila kwa yule
Nyerere binafsi,alivyofanziwa na
Wazee wetu!?
Khalaf,muulize akukhadith ni vipi huyo
Nyerere alivyowafanzia
Wazee Wetu baada ya kupata
madaraka!?...mwambie pia akukhadith kiundani kuanzia zile
nakma zoote aka
"Azimio la Arusha","Sera ya Vijiji vya Ujamaa" na kumalizia na ile
"Uhujumu wa Uchumi" jinsi zilivyoadhibu,kudhulumu na kutesa
Wazee Wetu!
Mwambie pia akukhadith kwa
utuvu pia,jinisi gani
Nyerere huyo huyo,baada ya kumchokoza yule
Idd Amin na kuanzisha vita...ni magari mangapi
lorries/buses alikuja kutupora pale
Pangani peke yake,ili kwenda kumsaidia ati kupigana na
Idd Amin!? Kwi! Kwi! Kwi!
Yaani haiingii akilini asilan,watu walewale unaowapiga vita miaka yoote na kuwapora mali zao zoote,tena waliokusaidia kwa hali na mali kupata hayo madaraka...khalaf umechokoza/umeanzisha vita pahala,unapigwa,khalaf unarejea tena kuzidi kuwapora tena mali zao ili kuzidisha
dhulma zako!? Duh!
Nyerere sina hamu nae!
Kuna mangi yakunena,wala sikutaka asilan kwenda mbali,lakini naona ulinipachikia kwenye mojawapo ya
post/s zako yakuwa niache
"uvivu" na nende
Pangani nikajenge Shule/Skuli!? kwi! Kwi! Kwi!
Khalaf pia humu humu
Jf,niliwahi kupitia baadhi ya
thread/s nikaona
Nguruvi3,akisifia ati watu wa
kanda ya ziwa walivyojitolea kwa hali na mali kumsaidia
Nyerere na ile vita yake!?...sikuona asilan ni wapi alitaja michango kama hiyo pia iliyotoka hata mikoa yoote ya
Pwani/Mwambao na Zanzibar!? Kunani!? Kwi! Kwi! Kwi!
Marehemu
Babu yangu wakti wa uhai wake maskini,akitembelea mkoa wowote wa
Pwani/Mwambao...basi hata kama alikua hajawahi kufika huko/hiyo sehemu,lakini akikutana na mtu yeyote njiani,yeye atakua ndo wa mwanzo
kumsaili yule mtu hata kama ndo
mwenyeji na amezaliwa pale!? Na
suali lake kubwa itakua,je wewe ni nani mwenzangu,maana kama itakua si
ndugu yangu basi utakuwa ni
mtumwa wangu!? Kwi! Kwi! Kwi!
Inna Lillahi, bila hata tone ya shaka,tunajua kwa yakini yakuwa,
Wazee Wetu walikua ni wakarim mno,wasomi,wenye maarifa,waungwana,majasiri na wenye bashasha mwanana maskini!
Shukran kwa kunisikiza huo uchechefu wangu japo kiduchu,niwie radhi kwa huo urefu wa mazungumzo.
Lakini kama usemavyo...tuko
pamoja Mkuu!
Ahsanta.