Israel VS Gaza. Kosa dogo tu likifanyika kama halijapangwa nyumba ya pazia, tunaingia WWIII (Nuclear War)

Israel VS Gaza. Kosa dogo tu likifanyika kama halijapangwa nyumba ya pazia, tunaingia WWIII (Nuclear War)

Baada ya Marekani kupeleka meli zake za kivita zenye thamani ya matrillioni. China na yeye anapeleka karibu na Gaza meli zake za kisasa z kivita nne.

Baada ya israel kuharibu uwanja wa ndege wa Damascus na Allepo. Leo dege kubwa la Iran limetua Syria likiwa na shehena za silaha kutumia uwanja wa kambi ya jeshi la urusi. Ikitokea Israel ikashambulia huo uwanja vita haitakuwa ndogo.

Shehena za silaha zinazoshushwa israel, makumi ya madege ya kivita ya US hayakauki Tel aviv airport ni ushahidi kuwa mlengwa sio Hamas. Ni kitu kikubwa zaidi ya hicho.

Kuzidiwa mapema kwa Jeshi la israel siku ya kushambuliwa na Hamas maana baadhi ya vyanzo vinasema sio kweli jeshi lilichelewa lakini lilifika kwa wakati ila hamas waliwazidi nguvu hadi ilipofika mchana. Ukizingatia kauli ya Rais wa Israel leo kuwa Hamas wamejipanga kutumia silaha za kemikali, Ukilinganisha na biti alilotoa Netanyahu ikiwa Hesbullah wataingilia kati, kunauwezekano ili kufupisha vita israel kutumia silaha kubwa kubwa za hatari ikiwemo Nuclear kwa mahasimu wake Iran.

Mvuto mkubwa unaoongezeka kuihusisha Russia, China na US katika vita hivi kama busara isipotumika dunia iko kwenye hatari ya WW3.

Ni hayo tu.
Hao china mikwala tu ila wakitishwa na US akipeleka dege au manuari pwani yake kazi imeisha wanarudi nyuma
 
Tatizo UN amewekwa pembeni, maana hadi watu wake wanakula phosphorus tu huko gaza.
Tuombe amani. Vile vita sio vya kushabikia, vikipata mkolezaji tu, yatatukuta kama kichocheo cha Sarajevo.
Wakati UNSEC walikubaliana kuharibu silaha za nyuklia na Mandela akaharibu silaha za Nyuklia za SA kisha wao wakazihifadhi zao, hakuna sala itakayowaokoa kwa sababu usaliti na unafiki ni sehemu yao.

Wacha wairarue dunia na nyuklia ili tufitike wote yatakuja maisha mapya tena huko mbeleni
 
Tatizo UN amewekwa pembeni, maana hadi watu wake wanakula phosphorus tu huko gaza.
Tuombe amani. Vile vita sio vya kushabikia, vikipata mkolezaji tu, yatatukuta kama kichocheo cha Sarajevo.
Watu wanashabikia vita kama mpira wakati hata wenyewe huko raia waisrael hawaishi kwa amani Wamekimbia majumba yao vita sio nzuri haijalishi una nguvu kiasi gani sio ya kuombea.
 
Africa tupo tu tunausoma mchezo.. Wasipige tu madude yao huku barani kwetu
Huku tutapata matokeo tu. Ila hawa jamaa walivyo na akili mbovu, hata wasiporusha Nuclear wanarusha virus ili dunia nzima iwe bize.
 
Inakadiriwa Israel kuwa tactila nuclear warhead 80, huku kwa Iran ikiwa ni 0.

Ni ngumu nchi za kiarabu kumgusa Israel, kitu kinaitwa Nuclear ni kipengele kingine unless uwe na guts kama za magharibi walivyomtuliza Putin na nuclear zake.
Wamemtuliza russia au wao ndio wametulia maana ukraine majimbo zaidi ya matatu yamechukuliwa na watu wamepewa mpk pasport za russia
 
Bluebeam
construction software empowers AEC teams to collaborate in real time and manage projects from design to completion on any device - anywhere
 
Spika wa bunge la Marekani wa sasa anaitwa nani?
Kwa jina simfahamu, labda nikaibie google chapu, ila navofahamu alivotoka nancy akafata mchizi mmoja ambaye ndo amefurushwa kwa njama za kushirikiana na serikali kwa siri kaja mpya hivi sasa
 
Unajua mende hafi kwa maangamizi ya nuclear weapons
Waache watwangane tuone binadamu gani mgumu kama mende atakaesalia kwenye atomic bombs
Sisi.tutadunda kama mende wala msihofu sana
Halafu tukianza upya mshindwe kuitawala Dunia
 
Kwa jina simfahamu, labda nikaibie google chapu, ila navofahamu alivotoka nancy akafata mchizi mmoja ambaye ndo amefurushwa kwa njama za kushirikiana na serikali kwa siri kaja mpya hivi sasa
Bunge la Marekani halina spika mpaka sasa, ndio wanataka kugombea
 
Kabsa mkuu wauane huko huko na hatutaki wakimbizi wao maanaa watakuja na ugaidi wao watatusumbua bure. Africa tuna shida zetu hawazipigii kelele ila zao wanataka huruma ya dunia
Mkikimbilia kwao hadi uraia wanawapa kisa mnakimbia Vita Congo Drc, Somalia, Ethiopia, Sudan, Nigeria, etc mkifika Canada wanawapa uraia na kazi juu na malipo makubwa
 
Mkikimbilia kwao hadi uraia wanawapa kisa mnakimbia Vita Congo Drc, Somalia, Ethiopia, Sudan, Nigeria, etc mkifika Canada wanawapa uraia na kazi juu na malipo makubwa
Sawa nimemaanisha magaidi. Kuna nchi yoyote duniani yenye itikadi ile inayompenda na kumpokea mtu mweusi. Toa nchi za europe.
 
Back
Top Bottom