Israel ilikuwa imewinda Gaza kwa zaidi ya mwaka mmoja ili kupata SinwarChanzo cha picha,Getty Images
Saa 1 iliyopita
Wanajeshi wa Israel walikuwa wamemuwinda kwa zaidi ya mwaka mmoja kiongozi wa Hamas, ambaye alitoweka huko Gaza mara tu baada ya kupanga mashambulizi ya tarehe 7 Oktoba.
Yahya Sinwar, 61, alisemekana alitumia muda wake mwingi kujificha kwenye vichuguu chini ya Ukanda huo, pamoja na kada ya walinzi na "ngao ya kibinadamu" ya mateka waliokamatwa kutoka Israeli.
Lakini hatimaye, inaonekana alikutana na mwisho wake katika kukutana na doria ya Israeli kusini mwa Gaza. Alikuwa na idadi ndogo ya walinzi. Hakuna mateka waliopatikana.
Bado taarifa zinaendelea kujitokeza, lakini hiki ndicho tunachokijua hadi sasa kuhusu mauaji ya Sinwar.