Israel kupitia Waziri Mkuu, Benjamin Netanyahu imetangaza kukubali kusitisha mapigano dhidi ya kundi la Hezbollah la Lebanon, hatua inayodhaniwa kumaliza vita hivyo vilivyodumu ndani ya mwaka mmoja na kuua takriban watu 3,800.
Rais Joe Biden ametangaza kuwa Marekani imesaidia kufanikisha makubaliano ya kusitisha mapigano nchini Lebanon, ambayo yatamaliza vita kati ya Israeli na kundi hilo linaloungwa mkono na Iran.