Itashangaza Dunia kama Waziri wa Afya na Naibu wake hawatafukuzwa kazi ya uwaziri

Itashangaza Dunia kama Waziri wa Afya na Naibu wake hawatafukuzwa kazi ya uwaziri

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
8,734
Reaction score
5,750
Wana Jf kwa jinsi tulivyo katika kipindi kigumu ambacho kimezua hofu kwa kila mtu ni wazi kuwa Waziri wa afya na naibu wake hawastahili kuwepo kwenye hii nafasi mpaka sasa.

Mwaka jana bila kupepesa macho Dk Faustine Ndugulile alieleza ukweli umma wa Watanzania kuwa kujifukisha hakuwezi kuua wadudu wa Covid 19, hii ni sababu hawa virus wakiingia kwa binadamu huingia moja kwa moja kwenye mfumo wa kupumua( mapafu) hivyo hata ukijifukiza ni ngumu kuwaua huko ndani ya mapafu.

Mwaka huu baada ya dalili kuwa hili janga limerudi Tanzania kwa namna nyingine,maana inadaiwa sasa hivi kirusi cha korona kimejibadili. Tumeshuhudia madaktari wawili ambao wanasimamia wizara ya afya wakisisitiza watu kujifukiza. Je hawa watu kwa nini hawakutoa ushauri wa kitaalamu unaozingatia taaluma yao kama Faustine Ndugulile?

Leo hii toka watoe demostrantion namna ya kujifukiza hali inaonekana kuwa mbaya. Maana vifo vya vigogo mpaka makabwela vinazidi kupamba moto. Na tatizo ni hilo la kukosa uwezo wa kupumua.

Karne ya ishirini na moja kuongozwa na wasomi ambao hawezi kusimamia taaluma yao na kumshauri rais namna ya kukabiliana na magonjwa kisayansi ni aibu kubwa. Mawaziri hawa wawili wasisubiri vifo vya watanzania iwe sababu ya wao kujiuzulu.
 
Alietoa "ORDER YA KUTOKUWEPO COVID-19 TANZANIA" ni Rais, yeye ndio wa kulaumiwa kwanza kabla ya Waziri, halafu ndio hao watendaji wengine wote wafuatie mpaka Wakuu Wa Mikoa (Mfano Mama Anna). Wakifuatiwa na Ma Mayor (Yule aliowavua barakoa wenzake kwenye kikao na yule aliosema hakuna Corona ni vita ya kiuchumi pindi shule ya ISM ilipotangaza wanafunzi wake kukutwa na kirusi).

Ingekuwa nchi nyingine, basi Wabunge haraka wangempigia "KURA YA KUTOKUA NA IMANI NA RAIS" na angeng'olewa madarakani hata kabla ya maafa haya kutufika watanzania. Ila kwa nchi yetu yenye "MAZUZU NA WENDAWAZIMU NA VIUMBE WENYE TAMAA" bungeni ndio kwanza wabunge wanataka "AONGEZEWE MUDA".

Nchi yetu kila kitu kina kwenda kinyume nyume, cha ajabu watendaji wa serikali wanaona nchi inakwenda mbele.
 
Only kama wangekua wamepita kihalali wangekua na confidance za kufanya hvyo.. washawekwa wanawaza matumbo yao... imewachapa kidogo tu na bunge wanaakhirisha.... mama Anna nae chenga tu eti misiba ipo mingi lkn haitoki hapa inatoka kwingine... yaaani wanatufanya sisi kama hata hatujafika stndard I... yaani akili zao sijui wamezifungia wapi... [emoji57][emoji57][emoji57][emoji57]
 
Tusitegemee ushauri kutoka kwa Waziri na Naibu Waziri wa Afya kwenda kwa mkubwa wao.

Tusitegemee ushauri, mkakati na ujasiri wa kumshauri mkubwa.

Muda mwingi walikuwa wanazunguka kutafuta kiki kupitia vyombo vya habari.
 
Back
Top Bottom