Iwepo sheria laptops kwa wanafunzi wote vyuoni ziwe ni "Lenovo Thinkpad" kuwanusuru stress za matengenezo na kugharamika zaidi kununua laptops mpya

NetMaster

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2022
Posts
1,454
Reaction score
4,925


Nashauri laptops za wanafunzi ziwe LENOVO THINKPAD, nje ya hapo mwanafunzi awe ana uwezo wa kifedha, vitu kama matengenezo ama kununua laptops mpya visiwe stress kwake, wale watoto wa kishua wanaopewa pesa bila mawazo na walioajiriwa tayari wenye spare money

Linapokuja suala la wanafunzi kwenda vyuoni kuna maamuzi ya gharama kubwa huwa yanafanyika kuhusu kununua laptop ya kuwafikisha mpaka mwisho wa safari ya chuoni na hata maisha ya baada ya chuo.


Wanafunzi wengi vyuoni hupatwa na dilemna pale laptops zikianza kuzingua, mara laptop imeizngua keyboard, speaker, screen, n.k, na hapo ilikuwa inatunzwa fresh tu, wakifika huko kwa mafundi ni stress za ziada, tatizo kama keyboard tu fundi anaomba laki, hapa shughuli za laptop inabidi zisimame hata mwezi ama miezi hadi hio pesa itafutwe.

Kuna wale laptop zinakufa mother board kabisa, hawa ndio huwa nawaonea huruma, fundi nae unakuta anasema motherboard laki 4, inabidi laptop ifungiwe kabatini tu, hapo hadi laptop ije kununuliwa ni panapo majaliwa.

Kwanini wanafunzi vyuoni wapitie kero hizi wakati kuna solution yenye uwezekano mkubwa kuwafanya wasiumize vichwa kwenye masuala ya kuhangaishana na mafundi ama kununua kubadili laptops,

Well, me naona suluhisho liwe ni LENOVO THINKPADS, hizi ni laptops ngumu sana, ni kawaida kutumika hata miaka 6 bila kumjua fundi na hapo ni hizi za mtumba, kwa wachache wenye uwezo wa kununua zile mpya ngoma inagonga mzigo mpaka utaichoka mwenyewe labda uwe careless sana kwenye kutunza.

Pia suala la battery nazo huwa zina maisha marefu na overall ziko poa kwenye kutunza chaji.

Zimetengenezwa maalum kwajili ya kuwa durable.

Sidhani kama wanafunzi wetu wana haja ya kusumbuka na hizi hp, dell, n.k. ambazo zikitumika ni kawaida kukuta keyboard imefeli, touchpad imekufa, kidogo tu screen ina mstari, n.k.
 
Thinkpad zina bei sana ni laptop za biashara sio wanafunzi, ni vile tu huku kuna mitumba ya kutosha ndio maana tunaweza kuzi afford. Thinkpad zina bei kuliko Macbook, Xps, spectre na premium laptop nyengine,

Ila upo sahihi, Thinkpad ni ngumu sana kuharibika hivyo zinafaa kuwapa watu ambao ni careless kama wanafunzi.
 
Kwa Dar zinauzwa wapi hizi mashine?.
 
Asante kwa mchango chief

Kuhusu bei wala sio ishu, uhalisia wa hapa bongo ni kwamba watu wengi wakiwemo na wanafunzi, laptops tunazotumia ni za mtumba zilizotumika nje ambazo huuzwa kwa bei nafuu, hii ni mpaka kwenye magari, nguo, n.k.

Wengi bajet za laptop huwa hazizidi milioni 1 hivyo hupendelea kununua mitumba, sio kwa lenovo pekee bali hata kwa hp, dell, n.k.

so nimelenga mule mule.
 
Kwa Dar zinauzwa wapi hizi mashine?.
Ndo laptop ambazo zimejaa kushinda zote kkoo.

Source ya laptop/Desktop mtumba ni Biashara kubwa, Kampuni kama FB ikibadili hardware ni Maelfu ya Comouter yanaenda soko la mtumba na kuletwa kwetu.

Thinkpad ndio laptop za kuaminika zaidi kwa wafanyabiashara, ndio maana zipo nyingi kkoo.

Sababu hii pia inapelekea laptop nyingi used specs zake zipo kiofisi, kutafuta Gaming laptop ama Creative laptop ni ngumu sana kkoo.
 
Kwa lenovo nzuri na za bei rahisi, imara na zenye uhakika wasiliana nasi.

Call/Whatsapp 0714894798

Ofisi ; Machinga complex 3rd floor

Laptop zetu zina warranty





























 
Hiyo brand kuna model yake zinakufa sana mouse pad na keyboard...na spare zake ni ghali mostly...
 
Nauza laptop dell latitude 5289
Specs
Storage 256gb
Ram 16gb
Core i7
Condition good
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…