Jaji Elinaza Luvanda ajiondoa kuendesha kesi ya Mbowe na wenzake baada ya washtakiwa kudai hawana imani naye

Jaji Elinaza Luvanda ajiondoa kuendesha kesi ya Mbowe na wenzake baada ya washtakiwa kudai hawana imani naye

K
Nafahamu kuwa Jaji yeyote anaweza kujitoa kusikiliza kesi yoyote ile endapo tu tuhuma hizo zitathibitika kuwa ni za kweli na zitapelekea haki kutokutendeka.
Sasa tuhuma alizo zitoa Mbowe na Mawakili wake dhidi ya Jaji Luvabda eti kuwa amepewa maelekezo kutoka juu kuwa amfunge Mbowe, tuhuma hizi zilipaswa zithibitishwe kwanza kabla ya Jaji kujitoa kusikiliza kesi hiyo.
nasema hivyo kwa sababu zifuatazo;

1. Tuhuma zilizo tolewa dhidi ya Jaji ni tuhuma nzito ambazo sio tu kwamba zinamchafua yeye Jaji Luvanda bali zinawachafua Majaji wote wa Tanzania bara na Muhimili wa Mahakama kwa ujumla wake kuwa hawatendi haki.
Tuhuma hizo zilipaswa zithibitishwe kwanza, huko ni kuichafua Mahakama, na wananchi wa kawaida watapoteza IMANI na MAHAKAMA.
Kwa kitendo cha Jaji kuamua kujitoa bila hata tuhuma hizo kuthibitishwa kumewaabisha Majaji wote pamoja na Muhimili kuwa huwa hawatendi haki.
Wana usafi gani? Luvanda ni mchafu, kuna Mtu huko juu amesema mahakamani imewapa jamuhuri haki ya kurekebisha hati ya mashitaka ambayo hawa kuomba! Kwanini awape hiyo ‘zawadi’ kama ni msafi?
 
Kengeza la gaidi DJ haliwezi kumtisha jaji mpaka akubali kujitoa, gaidi ajiandae kula mvua za kutosha!. [emoji1787]
Hata babayako nikengeza alilogaidiwa bila ya kuwa na ushahidi wa hayo uliyoyasema juu yake.
 
Pole sana Mh Mbowe..

Ni vyema Mh Mbowe na team yake pamoja CDM ili suala mpambane zaidi kisheria kuliko kuleta siasa... tukijikita kwenye siasa tunaweza kusahau masuala muhimu ya kisheria na mwisho ukawa mbaya halafu bado tukaendeleza harakati za kisiasa za Free Mbowe....

Siasa ina mambo mengi, unaweza kuwekewa mtego na wewe ukajaa huku maadui zako wakiwa na malengo ya baadaye kukumaliza kwa wewe kuingia kwenye target yao bila kijua...mfano unaweza kuchokozwa baada ya watu kujua unahasira na wewe kupitia hasira zako ukaua kifupi utakuwa na kesi ya kuua...TUWE MAKINI....
Jaji amesema hati imekosewa kama imekosewa suluhisho lake kisheria ni lipi?
 
Ni kipindi gani hiyo hati ya Mashitaka hufanyiwa marekebisho? Ni baada ya Jaji kugundua mapungufu husika au Jamhuri kuomba kwa Jaji kurekebisha mapungufu hayo?????
Tena kwenye hili, siyo Jaji aliyegundua makosa, ni mawakili upande wa utetezi waliliona hilo na kuli address. Sasa badala ya Jaji ku deal nalo kisheria, yeye anawaelekeza upande wa jamhuri kufanyia amendment. Mawakili wa utetezi wakaleta kama pingamizi kwamba liko kinyume cha sheria kwa Jaji kuelekeza upande mmoja. Leo Jaji akaamua kutupilia mbali pingamizi hilo, ndipo upande wa utetezi wakaona hawana imani na Jaji Luvanda.
 
Hii haimanishi judge anaingilia mwenendo wa kesi..na anatoa maelekezo nini cha kufanya..ili iweje..hiyo ni kazi ya judge??kwakuwaambia wakairekebishe inamaana anakubali imekosewa..and what does the law say hati inapokosewa..na ombi la kina kibatala lilikuwa ni nini kuhusiana na hati??
Hati ya mashitaka inapokosewa sheria inatoa mamlaka kwa mahakama kutoa amri kwa upande wa serikali kurekebisha. Jaji alikuwa sahihi kabisa sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai inaruhusu.
 
Kesi iendelee. Mawakili wa mbowe wanasumbua mahakama ili kupiga hela ya wafadhili kwamba wanamtetea mteja wao kibaraka wa wazungu.
Unamuona kuelgeza macho anapokwenda anatembea na hayo mabeberu unayoyaona wewe.
 
Nafahamu kuwa Jaji yeyote anaweza kujitoa kusikiliza kesi yoyote ile endapo tu tuhuma hizo zitathibitika kuwa ni za kweli na zitapelekea haki kutokutendeka.
Sasa tuhuma alizo zitoa Mbowe na Mawakili wake dhidi ya Jaji Luvabda eti kuwa amepewa maelekezo kutoka juu kuwa amfunge Mbowe, tuhuma hizi zilipaswa zithibitishwe kwanza kabla ya Jaji kujitoa kusikiliza kesi hiyo.
nasema hivyo kwa sababu zifuatazo;

1. Tuhuma zilizo tolewa dhidi ya Jaji ni tuhuma nzito ambazo sio tu kwamba zinamchafua yeye Jaji Luvanda bali zinawachafua Majaji wote wa Tanzania bara na Muhimili wa Mahakama kwa ujumla wake kuwa hawatendi haki.
Tuhuma hizo zilipaswa zithibitishwe kwanza, huko ni kuichafua Mahakama, na wananchi wa kawaida watapoteza IMANI na MAHAKAMA.
Kwa kitendo cha Jaji kuamua kujitoa bila hata tuhuma hizo kuthibitishwa kumewaabisha Majaji wote pamoja na Muhimili kuwa huwa hawatendi haki.

So ulitaka kuwe na kesi nyingine (ndani ya hii) ya kuthibitisha hizo tuhuma ndipo ajitoe ? Kwa utaratibu upi ?

By the way, ukisikiliza alivyoongea Mbowe wala hajatoa tuhuma zozote. Yeye amesema hana imani na Jaji (swala la kutokuwa na imani na mtu ni very personal na ni haki yake), pili kuongezea hilo la kutokuwa na imani naye kasema kuna maneno yanasemwa huko mitandaoni "Akaya-quate" na kuseme hatuwezi ku-ya-ignore na akamwombwa Judge ajiuzulu kwa heshima yake.

Sasa yeye katoa tuhuma zipi hapo ? Na ndio maana Judge ameelewa na amejitoa.
 
Jaji hana tatizo kama ni jambo la kurekebishika hatakiwi kufuta shitaka bali kutoa oda ya kurekebisha Mkuu. Athari ya kufuta ni kwamba shitaka halitaweza kurudishwa na Jamhuri/ itasababisha mchakato wa kuanza kumkamata tena na kuzua taharuki zaidi. Sio aibu Jaji kujitoa bali ni ujasiri na heshima. Mawakili wa mshitakiwa wao wanakomaa kutetea maslahi ya mteja wao kuna muda wanajua kabisa wanachoomba mahakama ikifanye sio sahihi ila ndio njia waliyobaki nayo, Jaji ukiingia mkenge unawasaidia kupindisha mambo.

Usishangae mawakili hao hao kwenye kesi za madai wakakomaa kuwa Jaji hawezi kufuta mashtaka kisa mlalamikaji kakosea kuandika hati ya madai bali anatakiwa kutoa oda tu yakufanya marekebisho mdai arudi tena mahakamani akiwa kakamilika.

Kitu ambacho huku wanakikataa 😂 😂 , haya yote ni mambo ya kwenye fani ya sheria. ndio maana haitoshi kuamini kila anachokisema wakili wa upande wowote kwenye media, jaribu kufahamu sheria nayo inatakajee?.
Samahani mkuu; ni wakati gani hati ya mashitaka hufutwa na mstakiwa kuachiwa? mimi niliwahi kuachiwa huru mara tano na hati ya mashitaka inafunguliwa upya.
Mwisho wa siku niliishinda Jamhuri baada ya kushindwa kuleta mashahidi mahakamani licha ya kupewa upendeleo na serikali zaidi ya mara tano.

Swali langu: Ni muda/wakati gani Jaji/Hakimu anatakiwa kufuta hati ya mashitaka?
 
Samahani mkuu; ni wakati gani hati ya mashitaka hufutwa na mstakiwa kuachiwa? mimi niliwahi kuachiwa huru mara tano na hati ya mashitaka inafunguliwa upya.
Mwisho wa siku niliishinda Jamhuri baada ya kushindwa kuleta mashahidi mahakamani licha ya kupewa upendeleo na serikali zaidi ya mara tano.

Swali langu: Ni muda/wakati gani Jaji/Hakimu anatakiwa kufuta hati ya mashitaka?
Kabla ya kukujibu naomba nikuulize swali hili. Umesema uliwahi kuachiwa huru mara tano, je katika hizo mara tano ulizoachiwa huko kuachiwa kwako kulitokana na mahakama kufuta kesi kwa uzembe wa jamhuri au kulitokana na maombi ya jamhuri kuondoa hati ya mashitaka?
 
Swali dogo tu ndugu Ni kwanini aliipa jamuhuri kulekebisha hati ya makosa walioikosea bila jamuhuri kuomba kufanya hivyo? Kama uamuzi ulikuwa Ni kukosa uhaalali wa hati ya mashitaka?. Hapo Ni tayari kaonyesha upendeleo wa wazi
Sheria inaruhusu mahakama kutoa amri kwa jamhuri kurekebisha hati ya mashitaka pale mahakama inapogundua hati hiyo inamakosa.
 
Kabla ya kukujibu naomba nikuulize swali hili. Umesema uliwahi kuachiwa huru mara tano, je katika hizo mara tano ulizoachiwa huko kuachiwa kwako kulitokana na mahakama kufuta kesi kwa uzembe wa jamhuri au kulitokana na maombi ya jamhuri kuondoa hati ya mashitaka?
Ni hakimu.kufuta kesi kwa uzembe wa jamhuri alafu wakawa wananikamata mlangoni na kunifungulia kesi upya.
 
Ni hakimu.kufuta kesi kwa uzembe wa jamhuri alafu wakawa wananikamata mlangoni na kunifungulia kesi upya.
Hapo walikuwa wanakosea mkuu. Mahakama ikifuta kesi kwa uzembe wa jamhuri, jamhuri haitakiwi kukukama tena na kukufungulia kesi inayotokana na kesi hiyo hiyo mpaka hiyo amri ya mahakama itenguliwe na mahakama ya juu yake.
 
Jaji asikubali upuuuzi na ushenzi huu wa Mawakili wa Mbowe na Mbowe mwenyewe.

Huko ni kumtusi Jaji na Mahakama,

Mbowe na mawakili wake hawana sababu ya msingi zaidi ya kutaka kumyumbisha Jaji, tuhuma wanazo zitoa dhidi ya Jaji ni za kipuuuzi na hazina uthibitisho wowote zaidi ya kudhania na kuhisia tu, hakuna hoja hapo, kwa hiyo anamtaka Jaji ambaye ni RAFIKI YAKE ili asikilize kesi yake.

kwa hiyo imefikia sasa Mtuhumiwa kuchagua Jaji wa kusikiliza kesi yake aisee! hata marekani hakuna kitu kama hicho.

ninacho sema Jaji angeweza kujitoa kama tuhuma zinazo tolewa na Mbowe zina uthibitisho la sivyo Jaji aendelee tu kungurumisha kesi.......asikubali kubabaishwa na hoja za kipuuzi na za kuokoteza na zenye lengo la kuchelewesha haki kutendeka.
Kesi yenyewe ni ya kudhaniwa na kuhisi kuhisi tu na haina uzito wowote hata kwa yule asiyejua sheria,tatizo siasa ya chama kimoja inapoingia kwenye sheria inafanya wataalamu wetu wa sheria kama Jaji Luvanda kupindisha sheria kwa maslahi ya chama tawala na serikali.
 
Jaji amekosea sana kujitoa ktk kesi.
Maana yake ni kwamba tuhuma alizo zitoa Mbowe dhidi ya Jaji ni za kweli.
Kabla ya kujitoa hizo tuhuma lazima kwanza zithibitishwe maaana sio tu kwamba zina mchafua Jaji/Majaji bali zinauchafua Muhimili wa Mahakama.
Mihimili ya Mahakama na Bunge yote haiko independent. Peleka ujinga wako kijijini kwenu huko.
 
Hapo walikuwa wanakosea mkuu. Mahakama ikifuta kesi kwa uzembe wa jamhuri, jamhuri haitakiwi kukukama tena na kukufungulia kesi inayotokana na kesi hiyo hiyo mpaka hiyo amri ya mahakama itenguliwe na mahakama ya juu yake.
Hapo nimekuelewa; je na hii ya Mbowe hayo marekebisho anayoyapendekeza jaji ni nani angeyatetea kisheria? Mimi ninachojua ni kua jaji alitakiwa kufuta hati ya mashitaka kwani inapelekea kesi kua batili alafu jamhuri iweze kufungua kesi upya.
Watu wengine wanasema umuhimu wa kesi bila kujua pia kesi muhimu inahitaji umakini zaidi.
Kwangu mimi ninaamini kua 90% ya waendesha mashitaka kwa upande wa jamhuri ni corrupted.
 
So ulitaka kuwe na kesi nyingine (ndani ya hii) ya kuthibitisha hizo tuhuma ndipo ajitoe ? Kwa utaratibu upi ?

By the way, ukisikiliza alivyoongea Mbowe wala hajatoa tuhuma zozote. Yeye amesema hana imani na Jaji (swala la kutokuwa na imani na mtu ni very personal na ni haki yake), pili kuongezea hilo la kutokuwa na imani naye kasema kuna maneno yanasemwa huko mitandaoni "Akaya-quate" na kuseme hatuwezi ku-ya-ignore na akamwombwa Judge ajiuzulu kwa heshima yake.

Sasa yeye katoa tuhuma zipi hapo ? Na ndio maana Judge ameelewa na amejitoa.
Nimejifunza kitu, kumbe kama unaona huyu Jaji ama hakimu haelewekia ama hasomeki kumbe naweza kumkataa tu kisha nikachagua Jaji au Hakimu ninaye mtaka na akasikiliza kesi yangu.
Kumbe siku hizi unaweza kuchagua Jaji ama Hakimu wa kusikiliza kesi yangu. aise!!
 
Sheria inaruhusu mahakama kutoa amri kwa jamhuri kurekebisha hati ya mashitaka pale mahakama inapogundua hati hiyo inamakosa.
Unasema pale mahakama inapogundua hati hiyo ina makosa, je katika hii kesi mahakama iligunduaje kwamba kesi ina makosa? Kumbuka Jaji hakuwa na tatizo na hati iliyowakilishwa na jamhuri mpaka pale alipopewa somo na upande wa utetezi kwamba hati hiyo ni batili.

Jaji alikuwa tayari kuendelea na kesi kwa msingi kuwa hakuona tatizo na hati hadi pale utetezi ulipompiga stop kuendelea na kesi kwa kutoa ushahidi kuwa hati ni batili. Na kweli Jaji baada ya kusikiliza hoja ya utetezi na kukubaliana nao alitakiwa kufuta ile kesi mara moja.
 
Kweli ktk hii nchi kuna mhimili uliojichimbia chin zaidi
Baada ya Jaji Luvanda kutupa mapingamizi yote yaliyotolewa na Mawakili wanaomtetea Mbowe na wenzake, Mbowe amesimama na kumtaka Jaji Luvanda ajiondoe kuendesha kesi hiyo kwani ameonyesha upendeleo na taarifa zinasema ana maelekezo ya kupindisha sheria ili amfunge Mbowe na wenzake.

Jaji Luvanda amesema hati ya mashtaka ni batili amewashauri Mawakili wa serikali wakaibadilishe, Mawakili upande wa utetezi wamegoma wamemwambia kama hati ya mashtaka ni batili basi futa kesi Jaji akakataa ila amekubali kujiondoa kuendesha kesi.

====

Jaji Elinaza Luvanda wa Mahakama Kuu Divisheni ya Uhujumu Uchumi na Makosa ya Rushwa na aliyekuwa anaisikiliza kesi ya Uhujumu Uchumi namba 16/2021 yenye mashtaka sita yakiwemo ya Ugaidi, amejitoa kusikikiza kesi hiyo.

Sababu ya kujitoa katika kesi hiyo ni kutokana na mshtakiwa wa nne katika kesi hiyo, Freeman Mbowe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema Taifa, kuieleza mahakama hiyo kuwa yeye na washtakiwa wenzake watatu hawana imani na Jaji huyo katika kutenda haki dhidi ya kesi yao.

Kesi imehairishwa mpaka jaji mwingine atakapopatikana. Pia awali Jaji Elinaza Benjamin Luvanda alikataa kutoa uamuzi wake leo juu ya mapingamizi ya upande wa utetetezi mpaka atapopata hansard / kumbukumbu za majadiliano ya Bunge kuhusu sheria ya ugaidi.

Wote walikubaliana kuwa kesi hii ina masilahi mapana kwa umma wote waliopo ndani ya Mahakama na nje.

Hoja 3 za upande za upande wa utetezi zilikuwa zinashambulia madhaifu na kasoro ya hati ya mashtaka. Hoja ya kwanza ilikubaliwa na jaji wakati hoja ya pili ilikubaliwa kwa nusu yake na jaji wakati hoja ya tatu ya kutupiliwa mbali au kufutwa kesi, jaji aliikataa.

Na kwa msingi huo mtuhumiwa Freeman Mbowe kwa niaba ya wenzake akasimama na kusema hawana imani na Jaji Elinaza Benjamin Luvanda kuendelea kusikiliza kesi hiyo, na mheshimiwa Jaji E.B Luvanda akaafiki ombi hilo na kujiengua kusikiliza kesi hii.

Source : Mwananchi Digital


UPDATE: Jaji Luvanda akubali
Jaji Elinaza Luvanda aliyekuwa anaisikiliza kesi ya Uhujumu Uchumi nyenye mashtaka 6 yakiwemo ya ugaidi, amejitoa kusikiliza kesi hiyo, sababu ya kujitoa kwake, ni kutokana na mshtakiwa wa nne katika kesi hiyo, Mhe. Freeman Mbowe na wenzake kuwa hawana imani na Jaji huyo.

Pia soma >
Mahakama ya Uhujumu Uchumi: Mvutano mkali kesi ya Mbowe na wenzake. Hatma ya kesi kujulikana Septemba 6
. "Jaji Mwenzangu Luvanda" Machozi ya samaki majini hayatakufikia wewe na kizazi chako mpaka cha nne, tekeleza maagizo
. CHADEMA tusimpe vitisho Jaji Luvanda, mpaka sasa hajapendelea pande yoyote. Kibatala na jopo lake walichemka
 
Pole bi.mjane wa mwendazake
Jaji asikubali upuuuzi na ushenzi huu wa Mawakili wa Mbowe na Mbowe mwenyewe.

Huko ni kumtusi Jaji na Mahakama,

Mbowe na mawakili wake hawana sababu ya msingi zaidi ya kutaka kumyumbisha Jaji, tuhuma wanazo zitoa dhidi ya Jaji ni za kipuuuzi na hazina uthibitisho wowote zaidi ya kudhania na kuhisia tu, hakuna hoja hapo, kwa hiyo anamtaka Jaji ambaye ni RAFIKI YAKE ili asikilize kesi yake.

kwa hiyo imefikia sasa Mtuhumiwa kuchagua Jaji wa kusikiliza kesi yake aisee! hata marekani hakuna kitu kama hicho.

ninacho sema Jaji angeweza kujitoa kama tuhuma zinazo tolewa na Mbowe zina uthibitisho la sivyo Jaji aendelee tu kungurumisha kesi.......asikubali kubabaishwa na hoja za kipuuzi na za kuokoteza na zenye lengo la kuchelewesha haki kutendeka.
 
Hapo nimekuelewa; je na hii ya Mbowe hayo marekebisho anayoyapendekeza jaji ni nani angeyatetea kisheria? Mimi ninachojua ni kua jaji alitakiwa kufuta hati ya mashitaka kwani inapelekea kesi kua batili alafu jamhuri iweze kufungua kesi upya.
Watu wengine wanasema umuhimu wa kesi bila kujua pia kesi muhimu inahitaji umakini zaidi.
Kwangu mimi ninaamini kua 90% ya waendesha mashitaka kwa upande wa jamhuri ni corrupted.
Ngoja nikutoe tongotongo. Hati ya mashitaka inapokuwa batili kuna njia mbili za kuitibu. Moja, serikali iamue kuiondoa mahakamani na kuleta hati mpya isiyo na makosa au kuomba amri ya mahakama kuirekebisha bila kuiondoa na kesi iendelee. Pia mahakama pale inapoona kuwa hati ya mashitaka inamakosa, sheria inaipa nguvu mahakama kutoa amri kwa upande wa serikali kurekebisha hati ya mashitaka na kesi iendelee.


Alichokifanya jaji ni kutumia hiyo njia ya mwisho ambayo imepewa mahakama na sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai ambayo ni , pale mahakama inapoona hati ya mashitaka inamapungufu, mahakama inaweza kutoa amri kwa upande wa serikali kurekebisha hayo mapungufu na kesi iendee bila kuifuta kesi yenyewe. Kwa mlengo huu jaji yupo sahihi kabisa.
 
Back
Top Bottom