Jaji Mustapha Mohamed Siyani aliyekabidhiwa kesi ya Ugaidi ya Mbowe ni nani?

Jaji Mustapha Mohamed Siyani aliyekabidhiwa kesi ya Ugaidi ya Mbowe ni nani?

Ni lazima ifahamike kwamba;
Kutenda HAKI sio LAZIMA iwe unavyo taka wewe.
Lazima tuelewe kuwa ikitokea;
AMEACHIWA ni HAKI lakini pia ikitokea KAFUNGWA ni HAKI pia.
tusichukulie kuwa Kutendewa HAKI ni kuachiwa huru tu la hasha! tufahamu pia Kufungwa ni sehemu ya kutendewa Haki.
Ushahidi ndio unaamua yote hayo mawili.
Jaji anaagalia ushahidi tu hakuna kingine.
Usemayo ni kweli. Kumfunga mshitakiwa wakati anatakiwa kuachiwa inakuwa haki haikutendeka na kutolewa, lakini pia ukimuachia mshitakiwa wakati anatakiwa kupatikana na hatia pia si haki na haki haikutolewa. Lakini makanda wanadhani haki ni kuachiwa mbowe. Kama ana hatia, haki ni kunfungwa.
 
Walipita huko na ndiyo maana katiba mpya ikapatikana, na siyo mwiko kujadili mwenendo wa jaji pia uteuzi wa majaji upo ktk hali ya uwazi na wanafanyiwa usaili ktk uwazi na umma mpana wanapata nafasi ya uelewa weledi, uzoefu, maadili na muegamio wa jaji upo wapi ktk masuala Kadhaa yenye manufaa kwa jamii kupata haki yao wanayostahili.

Katiba mpya sio solution ya shida za kweli za wananchi. Zipo nchi nyingi zilizoandika katiba zao upya, lakini shida zao zimebaki palepale. Angalia, kwa mfano, Wakenya na Wazambia. Katiba zao mpya zimewasaidiaje? Mivurugano ya kisiasa na economic hardships za mwananchi wa kawaida ziko palepale. Mabadiliko ya katiba mara nyingi huishia kutengeneza fursa fulani kwa ajili ya political entrepreneurs tu!

Namna ya kupata majaji ni swala la utaratibu tu. There’s no gold standard; it’s all a function of the governing system in place! Zipo political jurisdictions ambazo zina utaratibu wa judges kuchaguliwa na wananchi kwa ballot paper; zipo zenye utaratibu wa kuteua kama tunavyofanya sisi, lakini subject to confirmation by the legislative branch na pia zipo zenye utaratibu wa kutumia tume za utumishi wa mahakama.
 
Katiba haitaondoa matatizo yote. Bado hata tukipata katiba kuna cgamoto zingine, na hazitaepukika. Mfano huko Marekani kunakosifika kuwa na katiba nzuri, bado kuna changamoto za uteuzi wa majaji. Kama kutakuwa na raisi na awe nna chama chake kina maseneta wengi, basi hao masenata watahakikisha uteuzi wa majaji unapita bila shida. Sasa ile koti kuu ya USA ina majority ya majaji (7) ambao ni conservatives. TZ tukisema majaji wapendekezwe na raisi na kuteuliwa na bunge, matatizo yatakuwa palepale. Kama CCM ndiyo majority bungeni, itateua wale wenye mwelekeo wa CCM, na kama upinzani utakuwa na wabunge wengi na raisi pia uteuzi utakuwa ni wa wale wenye mwelekeo wa upinzani. Na hii itakuwa hata kwenye tume mbalimbali. Wajumbe, makamishina, na wakuu wa tume, kamisheni, na bodi mbali mbali watateuliwa na kupata support ya bunge kufuatana na ni nani mwenye majority bungeni.

Mkuu umeandika vyema sana:

"Bado hata tukipata katiba kuna cgamoto zingine, na hazitaepukika."

Bila shaka ukimaanisha changamoto tunazozipigia kelele sasa kama za mihimili iliyojichimbia zaidi, kubambikiziana kesi, kurundikiana kodi na tozo hali vigogo hawahusiki nk kwa maana ya utawala wa kidemokrasia tutakuwa tumeyapatia dawa.

Kama ilivyo kirusi cha Corona ambacho hujifunza kutokana na makosa na kujiboresha zaidi kuwa leo tunaongelea Delta, ndivyo ambavyo itakavyokuwa kwetu kwa maana kamili ya kusonga mbele.

Tunataka kusonga mbele si kulemaa kubovu tulipo ambapo hata haya hapa yana ukweli:

IMG_20210911_000004_180.jpg
 
Usemayo ni kweli. Kumfunga mshitakiwa wakati anatakiwa kuachiwa inakuwa haki haikutendeka na kutolewa, lakini pia ukimuachia mshitakiwa wakati anatakiwa kupatikana na hatia pia si haki na haki haikutolewa. Lakini makanda wanadhani haki ni kuachiwa mbowe. Kama ana hatia, haki ni kunfungwa.

Katika sheria ni afadhali kumweka huko mkosaji kuliko kumwadhibu asiye na kosa. Huo ndio msingi wa “ushahidi usiokuwa na mashaka”. Siwasemei makamanda lakini kesi aliyopeleka Mbowe kwa jaji Luvanda ilisema zawadi iwe i kuachiwa huru. Na kwa kuwa kumwachia Mbowe huru isingemaanisha hakutenda makosa, jamhuri ilikuwa na uwezo wa kumkamata tena nje ya mahakama na kumfungulia kwai upya. Kumbuka: kesi haikuwa Mbowe hakutenda makosa anayostakiwa. Kesi ilisema hati ya mashtaka sio sahihi kwa sababu makosa yamerudiwarudiwa na hati ya mashtaka haina taarifa kama tarehe na siku makosa yalitendwa.
 
Jaji Mustapher Mohamed Siyami

Je Media wameshindwa kuingia ndani ya Mahakamani Maalum ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi ?

Mheshimiwa Jaji wa Mahakama Kuu anaweza kusaidia kuondoa mkwamo wa Waandishi kuzuiwa kuingia ndani ya Mahakama.



Source : Mubashara Studio
 
Hawa watu
1.Ni wateule wa Rais.
2.HAWALIPI KODI.
3.Wanapata ulinzi bure wa serikali
4.wanahudumiwa na serikali kwa Kila aina ya huduma.

Kwa muktadha huo tumuomba M/Mungu amjaaliye jaji kuweza kutenda haki kwa mujibu wa SHERIA za nchi yetu.

Jaji Kama ataamua kufuata maelekezo ya bosi wake aliyemteua Wala tusihuzunike,Mbowe Ni sehemu ya raia mwenye haki ya kukaa gerezani, hospital,mahabusu,na hata kufariki.

Sisi na wale watakaokuwa mtaani waendeleze Moto wa KATIBA MPYA mpaka ipatikane.
Tusikumbushane yaliyompata JAJI JOSEPH KAPINGA.
 
Kauli alizowahi kuzitoa Mh. Jaji Mustapher Mohamed Siyani kusisitiza haki na weledi ili Mahakama zijijengee imani kwa umma mpana.



Jumatatu, 31 Agosti 2020​

MASHAURI YA UCHAGUZI YASIATHIRI IMANI YA WANANCHI KWA MAHAKAMA – JAJI SIYANI​

Na Innocent Kansha – Mahakama Dodoma.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Dodoma Mhe. Mustapher Siyani amewataka Mahakimu Wakazi Wafawidhi wa Mahakama ya Tanzania kusikiliza mashauri uchaguzi kwa kuzingatia weledi na kutenda haki ili wasiathiri Imani ya wananchi kwa Mhimili wa Mahakama.

Akifungua awamu ya tatu ya mafunzo ya namna bora ya uendeshaji wa Mashauri ya uchanguzi kwa Waheshimiwa Mahakimu Wakazi Wafawidhi wa Mahakama za Hakimu Mkazi Tanzania, Jaji Siyani amewataka Mahakimu hao wafawidhi kusimamia masjala kwa karibu zaidi, ili mashauri yanayofunguliwa yaweze kushughulikiwa ndani ya muda stahiki.

Jaji Mfawidhi aliwakumbusha Mahakimu hao kutilia mkazo matumizi ya Teknologia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) ili mashauri yanayofunguliwa kwa njia ya mtandao (E-Filing) yaweze kusikilizwa na kumalizika kwa wakati.

“Mafunzo haya ni muhimu kwenu binafsi na Mahakama kama taasisi, umuhimu wake hauelezeki kwa maneno mepesi, kwa wale ambao wamewahi kusikiliza mashauri ya uchaguzi wanaelewa nini ninachozungumzia hapa”, alisistiza Jaji Siyani.

Alisema, katika kuyashughulikia mashauri yatokanayo na uchaguzi, suala la muda ni jambo la muhimu kwani viongozi wa ngazi za juu wa Mahakama pia wameelekeza mashauri hayo kutodumu Mahakamani kwa zaidi ya miezi minne tu na si vinginevyo, hivyo amewataka Mahakimu hao kujiandaa kutekeleza majukumu maelekezo hayo muhimu.

Jaji Mfawidhi alisema Mahakama haiwezi kujitenga na mchakato wa kidemokrasia wa nchi yetu,hivyo ushiriki wa muhimili uko katika hatua zote ikiwemo kabla ya kuanza kwa uchaguzi na hata baada ya matokeo kutangazwa. Aliongeza kuwa Ibara ya 107 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka dhahiri kuwa Mahakama ndicho chombo chenye kauli ya mwisho katika kutoa haki. Source : MASHAURI YA UCHAGUZI YASIATHIRI IMANI YA WANANCHI KWA MAHAKAMA – JAJI SIYANI

16 September 2021
Dar es Salaam, Tanzania

BENSON KIGAILA AWALIPUA JESHI LA POLISI KUZUIA WATU MAHAKAMANI

Kongole mheshimiwa jaji Mustapher M. Siyani kwa kukataa Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi kuwa mateka wa jeshi la Polisi
 

Kwa ufupi sana Jaji huyu Mustapha Mohamed Siyani aliapishwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu kanda ya Dodoma siku ya Ijumaa tarehe 20 April 2018, na Aliyekuwa Rais wa Tanzania wa awamu ya 5 Dr John Magufuli, Baada ya kuteuliwa kushika nafasi hiyo tarehe 15 April 2018 .

Pia amewahi kuwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma.

NOTE : Jaji wa Mahakama Kuu ni mtumishi wa Umma, kumfahamu haijawahi kuwa kosa kisheria

Tuanzie hapa kwanza halafu tuendelee
 
16 September 2021
Dar es Salaam, Tanzania

BENSON KIGAILA AWALIPUA JESHI LA POLISI KUZUIA WATU MAHAKAMANI

Kongole mheshimiwa jaji Mustapher M. Siyani kwa kukataa Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi kuwa mateka wa jeshi la Polisi
Shukrani sana mkuu
 
Back
Top Bottom