Mimi sijaona ubaya wa hii barua ya kuvikumbusha vyama vya siasa vyote HAKI na WAJIBU wao...
Labda hajatoa msisitizo mkubwa zaidi kwenye ishu ya "haki za vyama vya siasa" ikiwemo kufanya mikutano na makongamano. Lakini kusema kweli haya;
1. Kuheshimu sheria za nchi - NI SAHIHI NA INAKUBALIKA
2. Kuepuka lugha ya uchochoezi, dhihaka, dharau, vitisho na matusi
- HILI HAPANA, Msajili hawezi KUTUPA TAFSIRI YA LUGHA YA UCHOCHEZI, DHIHAKA, DHARAU, VITISHO na MATUSI...
- Kiukweli, hiki ndicho kimekuwa kichaka cha vyombo vya dola hususani police kukitumia kukamata kamata watu hovyo na kuwapotezea muda kwa kukaa nao kwenye vituo vya polisi...
- Hii ni kwa sababu kwao kila neno linalotoka midomoni mwa wanasiasa wa upande wa vyama visivyo na serikali, kama limewaudhi au linakera masikioni mwa wanasiasa wale waliomo serikalini, linaweza kugeuzwa kwa makusudi kuwa TUSI, DHARAU, DHIHAKA au KITISHO au UCHOCHEZI ili tu kupata sababu ya kuwaaumbua na kuwapotozea muda wapinzani wao...!!