Jaji Warioba: Miaka yote watu wanaelewa kujaza fomu, lakini 2020 ghafla hawajui. Siasa inataka kuingia kwenye Dini

Jaji Warioba: Miaka yote watu wanaelewa kujaza fomu, lakini 2020 ghafla hawajui. Siasa inataka kuingia kwenye Dini

"Miaka yote watu wanaelewa na wanajaza fomu vizuri lakini Mwaka 2020, ghafla watu hawajui kujaza fomu (wanaenguliwa). Hapa lazima kuna namna" - Jaji Warioba.

Amesema hayo wakati akichangia kwenye mkutano wa TCD leo Dodoma.
Alikuwa wapi kusema huyu Mzee nae?
 
Nchi ilipitia kwenye mateso makubwa .

Pichani huyo alikua ni mgombea aliyekua akirejesha fomu ili kuepuka kutekwa na makuwadi wa dikteta ilibidi jamaa avae ushungi.

Udikteta ulitembea kwenye kivuli cha uzalendo uchwara.
IMG_20200829_122313.jpg
IMG_20200829_122313.jpg
IMG_20200829_122311.jpg
 
Kwanini hawakuenda mahakamani?
Kubaki unalialia umeonewa wakati hakuna kesi hata moja mahakamani ya kupinga uchaguzi ni upuuzi na kupoteza muda.
Kama waliokukata ndiyo Wana ushawishi mkubwa kwa mahakama unategemea haki iapatikane?!
Ndiyo maana ufumbuzi wa madudu haya ni Katiba Mpya!
 
Hoja mufilisi hii. Wewe ni mahaba niue tu. Ina maana wapinzani tu ndio walikuwa vilaza wa kujaza fomu?
Possibility kubwa ni kuwa, miaka yote fomu zilikuwa zinajazwa hovyo hovyo bila kuzingatia kanuni, sheria na taratibu, lakini watu wakawa wanafumbia macho au kuangalia pembeni na kuzipitisha kiujumla jumla. Mwaka 2020 watu wakaamua ku-enforce sheria kwa ku-scrutinize fomu ili kuhakikisha kama zipo sawa, kwakuwa watu waliweka mazoea ya ilimradi fomu imejazwa, matokeo ndiyo yakawa yale tuliyoona.

Tatizo bongo yetu ni unafiki.
 
Back
Top Bottom