Jaji Warioba: Miaka yote watu wanaelewa kujaza fomu, lakini 2020 ghafla hawajui. Siasa inataka kuingia kwenye Dini

"Miaka yote watu wanaelewa na wanajaza fomu vizuri lakini Mwaka 2020, ghafla watu hawajui kujaza fomu (wanaenguliwa). Hapa lazima kuna namna" - Jaji Warioba.

Amesema hayo wakati akichangia kwenye mkutano wa TCD leo Dodoma.
Alikuwa wapi kusema huyu Mzee nae?
 
Kwanini hawakuenda mahakamani?
Kubaki unalialia umeonewa wakati hakuna kesi hata moja mahakamani ya kupinga uchaguzi ni upuuzi na kupoteza muda.
Mtu anazurura mahala kote na hakimu halafu upeleke kesi kwake huyo basi utakuwa mjinga tu kutaraji kushindwa kama sio ndio unaharalisha eti utawala wa Sheria unafuatwa
 
Nchi ilipitia kwenye mateso makubwa .

Pichani huyo alikua ni mgombea aliyekua akirejesha fomu ili kuepuka kutekwa na makuwadi wa dikteta ilibidi jamaa avae ushungi.

Udikteta ulitembea kwenye kivuli cha uzalendo uchwara.
 
Kwanini hawakuenda mahakamani?
Kubaki unalialia umeonewa wakati hakuna kesi hata moja mahakamani ya kupinga uchaguzi ni upuuzi na kupoteza muda.
Kama waliokukata ndiyo Wana ushawishi mkubwa kwa mahakama unategemea haki iapatikane?!
Ndiyo maana ufumbuzi wa madudu haya ni Katiba Mpya!
 
Hoja mufilisi hii. Wewe ni mahaba niue tu. Ina maana wapinzani tu ndio walikuwa vilaza wa kujaza fomu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…