..hata Magufuli alikosea kuweka picha ktk fomu yake lakini Tume ikamhurumia.
..Juma Duni Haji ambaye amegombea chaguzi nyingi alienguliwa ktk uchaguzi wa 2020.
NB:
..Mwaka 2020 Tume ya uchaguzi iliengua wagombea wengi wa upinzani kuliko ilivyofanya mwaka 1995.
Mzee Warioba aliwahi kusema kazi ya tume si kuengua wagombea, kukosea kujaza fomu si sababu ya kumuengua mgombea, akauliza sheria hiyo ipo wapi?
Tume inapata wapi muongozo huo?
Pili, kuna matatizo mengi.
Wakurugenzi kukimbia ofisi mgombea achelewe kurudisha Fomu . Wanaochelewa ni Wapinzani tu
Tatu, kuna uhuni wa watu kunyang'anywa fomu na ni Wapinzani tu, haijawahi kutokea Polisi ikakamata watu hao ambao kisheria ni wahalifu kama wahalifu wa uporaji tu
Ukimsikiliza Mahera lazima tumbo litakukata, tuna watu wa ajabu sana
Mahera anasema kama kuna kuenguliwa tume haihusiki kwasababu haifiki huko vijijini.
Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi Tanzani Dr Mahera anadhani tume ipo makao makuu tu ikisubiri kujumlisha matokeo. Huyu ni Dr hajui wigo wa Tume, unabaki kujiuliza sana!
Ni kama niliyosikia Dr Kitila akisema kwanini Wapinzani hawakwenda Mahakamani.
Mkumbo anajua Jaji mkuu aliambiwa kuna mhimili uliojichimbia tangu hapo tukaanza kumuona kila hafla ya kuapishwa hata Wenyeviti wa Bodi.
Mahakama iliyosema Wakurugenzi wakiapa basi ni waadilifu kwasababu ya kiapo
Hii ndiyo unapeleka kesi ya kushindwa tena wakati wa mwendazake utegemee haki
Mkumbo bado ana kumbu kumbu za akina Nyalali, Kisanga, Samatta!
Sijui ni kuvimbiwa asali au ni kitu gani.