Jamaa aliyeniibia kuku mwaka jana leo amefariki, mtaa unahisi nimemroga

Kwa maelezo yako haya huyo mzee wako ni kweli kuna dawa anayo ila wewe anakuficha ila utakuja kuujua ukweli mwaka atakaofariki utaitwa ili urithishwe hiyo dawa.
Haiwezekani matukio zaidi ya mara mbili itokee hapohapo kwenu.
Sina hakika na hilo aliwahi ugua sana namimi ndo nilikuwa karibu nae zaidi akitoka mama. Alikuwa ananimbia mambo kadhaa wa kadhaa tu lakini hili hata hana hakujaribu kuliongelea kamwe.

Wala mzee si mtu wa kwa waganga angekuwa mama ningesema kanunua au alipewa hii dawa maana yeye ndo kahusika kutupeleka kwa waganga sana udogo wetu wote hasa kwa kumtoroka mzee maana mzee alikuwa hapendi na hapendi hadi leo
 
Mzee wako kuna Zindiko alifanya si bure
 
Amefariki kwenye mazingira gani?(kuumwa au ajali)..Ameiba vipi kuku wako?alivunja banda au ilikuaje?
 
Ha
Hama hiyo sehemu, Fanya sana maombi ya ulinzi. Nenda katoe sadaka na mshirikishe mtu Mungu muwe mnaomba pamoja
 
Mzee wako kuna Zindiko alifanya si bure
Kwasababu mleta uzi kanikumbusha basi nitaenda tena kwa mzee shida hanywi pombe muda wote yupo active hivyo ni ngumu sana kunambia. Hlafu kwanini anifiche kitu cha faida na tuna share nae vitu vingi? Ila awamu hii namuuliza ikiwa kweli anayo nitafurahi mno
 
eeeh[emoji17] pole sana mkuu, but relax, najua ndio wataongea sanaa kwa muda kiasi, ila baada ya muda watasahau , mi nikushauri ujipe likizo fupi uende ubadirishe mazingira then urudi, utarefresh mind sana, but pole, ndo binadamu walivo, wanaamini upumbavu.
 
🤓 🤓 🤓, Kabisa mkuu, kuna jamaa alienda kuiba kuku usiku, Sasa baadala ya kuwanyonga shingo ili asipige kelele, yeye akakosea akanyonga mguu 😂😂. Wacha kuku apige makelele ya kiwango cha lami.

Mpaka leo ni R. I. P
Nimeshuhudia matukio mawili ya watu kufa, sababu ya kuku,...mmoja aliiba kuku vizuri kabisa,sasa wakati anakimbia akaingia kwenye shimo lililochimbwa kwa ajili ya kupanda mgomba, akavunjika mgongo, akakutwa asubuhi akiwa mzima, ila watu wakagoma kumsaidia mpaka akafa , maana walisema alikuwa msumbufu sana, na huwezi amini alikuwa na wake wawili,.....

wengine ilikuwa pale mbeya karibu na shule ya iyunga boys, walienda kuiba kuku, jirani wa mwenye kuku alikuwa katoka kupiga masanga akawaona wakiwa wanatoboa ukuta, akawashtua wengine kwa simu, wezi wakajaa kwenye kumi na nane... wawili wakala kiberiti,..mmoja tu ndo alipokonyoka,......

Kuku..🙌🙌🙌
 
Umemroga live bila chenga.. Hapa unatupa tu taarifa tukuogope😂
 
Ingawa sijasoma content ila ushauri wa hao wapuuzi unaoishi nao kitaa anzisha biashara ya uganga nadhani utawapata (Kama na wewe ni walewale wa Imani hizo za kale... )
 
Maana halisi ya "wanaokwenda jela sio wote wenye hatia....!" Mtafute huyo sheikh, mama aliyenunua kuku, ndugu wa marehem na baadhi ya watu wenye ushawishi mkae muyajenge! ndugu wa marehemu tu ndio wanaweza kukuondolea hizo hisia au kufanya zidumu!
 
Bonge moja la fursa mkuu, kama ulikuwa unawafungia kwenye banda waachie wawe wanazurura. Hakuna mtu atawagusa...
Tena atengeneze na mahirizi ya mchongo, awafunge kuku shingoni au miguuni, hapo atakuwa amemmaliza adui mmoja mkubwa sana wa maendeleo,...MWIZI....😂😂🤣
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…