Jamani kitaa ni kigumu sana, ukikutana na watu wa namna hii usiache kutoa msaada

Jamani kitaa ni kigumu sana, ukikutana na watu wa namna hii usiache kutoa msaada

Mkuu mi nimeshakuwa kiongozi kanisani kwa awamu tofauti tofauti hivyo hadi nafikia kuacha na kukataa uongozi najua ninacho kifanya 100%.

Waumini wanaweza toa hela kwa umoja na upendo lakini itakayo nunuliwa vitu vya kupeleka kwa hitaji ni robo tu nyingine inapigwa juu kwa juu.

Yaani kama mmechanga 2000 basi wahitaji itawafikia 500 tu. Nimeshaambiwa mimi ni muasi na wameshasubri nipate tatizo wasilete huduma kwangu. Najua nachofanya na kila ninapo toa kwa wahusika huwa wanafurahi mno mbele yangu.

Huu hapa mfano mmoja tu

Niliwahi mpelekea maam mjane mmoja vitu kadhaa wa kadhaa pamoja na nguo nadhani wanaita JAVA kama sio wax Zilikuwa pair 3 kama sijasahau na nilinunua 35k kila pea

Baada ya kumpa yule mama alilia machozi mbele yangu akaniambia nichukue jogoo la kuku nikakataa sasa kipindi nampa alipiga yowee mama jirani akaja ndo akaniambia chukua huyo kuku.......nikachukua.

Kesho yake yule mama alienda kuwashukuru wazazi wangu ukumbuke ni wakijij jirani wala wazazi hawakujua nilichokifanya ndo wakaniambia nilijisikia furaha mno nilipopata taarifa kutoka kwa wazazi.



Yule mama wakati wa mavuno huwa anapeleka nyumbani karanga,mahindi au mpunga halafu wazazi wanani taarifu nafuata. Huwa ansema huyu ni mwanangu kabisa hata akipata wageni waheshima ataenda home kumfuata baba akale kuku pale.
Yaani ,umenigusa mno
 
Huu uzi wachangiaji wanajisifia kutoa misaada.

Kama ni kweli mbona huko mitaani hatuwaoni mkifanya hivyo.

Kuna watu wengi tu wanapata matatizo lukuki hakuna wakuwasaidia.
 
Ukikutana na watu wa namna hii basi fanya kununua kitu
View attachment 3218915

Hata ukiwa hauna njaa fanya kuwa sehemu ya furaha kwao. Kitaa ni kigumu sana wanandugu.
View attachment 3218916
Na Ikiwezekana mpe muda wakubadilishana mawili matatu,

na ukipata kujua malengo yake na dhamira yake juu ya kile anachokiamini, unaweza ukampiga tafu kulingana na uwezo wako.

Mtu aliechukua maamuzi hadi hatua hii ya kujichanganya, anakua na uthubutu ni courageous man kinachomkwamishi ni sapoti tu, hasa hasa mtaji na mazingira sahihi.
 
Na Ikiwezekana mpe muda wakubadilishana mawili matatu,

na ukipata kujua malengo yake na dhamira yake juu ya kile anachokiamini, unaweza ukampiga tafu kulingana na uwezo wako.

Mtu aliechukua maamuzi hadi hatua hii ya kujichanganya, anakua na uthubutu ni courageous man kinachomkwamishi ni sapoti tu, hasa hasa mtaji na mazingira sahihi.
Kabsa Mkuu
 
Nilipitia life moja hvi aiseeeee ile life ilikua hatareeee..
Daah nikikumbuka huwa natamani kulia
 
Mkuu mi nimeshakuwa kiongozi kanisani kwa awamu tofauti tofauti hivyo hadi nafikia kuacha na kukataa uongozi najua ninacho kifanya 100%.

Waumini wanaweza toa hela kwa umoja na upendo lakini itakayo nunuliwa vitu vya kupeleka kwa hitaji ni robo tu nyingine inapigwa juu kwa juu.

Yaani kama mmechanga 2000 basi wahitaji itawafikia 500 tu. Nimeshaambiwa mimi ni muasi na wameshasubri nipate tatizo wasilete huduma kwangu. Najua nachofanya na kila ninapo toa kwa wahusika huwa wanafurahi mno mbele yangu.

Huu hapa mfano mmoja tu

Niliwahi mpelekea maam mjane mmoja vitu kadhaa wa kadhaa pamoja na nguo nadhani wanaita JAVA kama sio wax Zilikuwa pair 3 kama sijasahau na nilinunua 35k kila pea

Baada ya kumpa yule mama alilia machozi mbele yangu akaniambia nichukue jogoo la kuku nikakataa sasa kipindi nampa alipiga yowee mama jirani akaja ndo akaniambia chukua huyo kuku.......nikachukua.

Kesho yake yule mama alienda kuwashukuru wazazi wangu ukumbuke ni wakijij jirani wala wazazi hawakujua nilichokifanya ndo wakaniambia nilijisikia furaha mno nilipopata taarifa kutoka kwa wazazi.



Yule mama wakati wa mavuno huwa anapeleka nyumbani karanga,mahindi au mpunga halafu wazazi wanani taarifu nafuata. Huwa ansema huyu ni mwanangu kabisa hata akipata wageni waheshima ataenda home kumfuata baba akale kuku pale.
Namna hii inapendeza sana, mkuu umeshare kitu kizito sana... Hii ni nguvu chanya, ENERGY ⚡ umetuambukiza binadamu wenzio na nimeipokea pia nitaifanyia kazi pale inapobidi🤝🏿

(Imagine mood na emotions iliyoripuka siku hiyo na huyo mama imeamka tena leo na kwangu kupitia huu ujumbe wa maneno)

🤝🏿🤝🏿🤝🏿
 
Miezi ya mwisho wa mwaka nilikuwa sehemu semina
Kuna mother anauza vitafunwa/vitumbua
Mama mtu mzima umri wa mama yangu.
Day one 2,3 nikapita namsalimia. Day 4 roho ikanituma nitoe chochote kununua.
Nikatoa buku nikamwambia nitapita kuchukua baadaye.. kiukweli si mpenzi wa vitumbua.
Nilinunua kumsapoti tu, isitoshe nilikokuwa naenda kulikuwa na chakula kuanzia asbh hadi muda tunaondoka tumeshiba ndiii.

Nafsi ikawa inanisuta kwamba mbona umempa kidogo?
Umepewa Bure toa Bure...
Kiukweli I did nothing ni neema ya Bwana kupata zile pesa.

Kesho yake nilipita tena nikatoa hela yote niliyopata jana yake, nikampa yule mama. .haikuwa kubwa sana ila ndipo uwezo wangu ulipoishia.
Mama akiweka kila kitu chini akanyoosha mikono kunikumbatia.
Nikachuchumaa kumkumbatia pia kama dakika 2 amenikumbatia yule mama.

Alitamka maneno ya Dua za Baraka
Sikuyaelewa maana sijui kiarabu ila nadhani ni Aya za kwenye Quran.

Nikamwambia ukweli kwamba sitaweza kuchukua vitumbua maana tunakokwenda wanatuandalia chakula kuanzia muda tunaingia hadi tunatoka.

Alinibariki
Niliondoka nikiwa na amani na furaha sana.

.........
Jiwekeeni hazina Mbinguni ambapo hakuna wezi Wala kutu.
🤝🏿🤝🏿🤝🏿Jambo jema sana...

Kuna mambo sio hata ya kufuata mkumbo bali kutenda kile kinachokusukuma moyoni

Kuna msemo unasema kutoa ni Moyo ni sio utajiri... Kwa hiyo nafasi uliyonayo na kwa kile kidogo ulichonacho basi inatupaswa tufanye kwa nafsi/upande wetu(kucheza nafasi yake) kulingana na uwezo, na si kuangalia wengine au kusema mbona kuna matajiri basi matajiri watamsaidia.
 
Namna hii inapendeza sana, mkuu umeshare kitu kizito sana... Hii ni nguvu chanya, ENERGY ⚡ umetuambukiza binadamu wenzio na nimeipokea pia nitaifanyia kazi pale inapobidi🤝🏿

(Imagine mood na emotions iliyoripuka siku hiyo na huyo mama imeamka tena leo na kwangu kupitia huu ujumbe wa maneno)

🤝🏿🤝🏿🤝🏿
Mkuu ni maamzi kuna watu huwa wanajitoa sana kwenye michango hadi wanajinyima hata kula vizuri ama kuvaa vizuri kwa ajiri ya kutoa lakini hela isipofika kama ilivyochangwa inauma sana.Haya huwezi elewa kama wewe sio kiongozi na ukiwa kiongozi mla hela utaona kawaida tu kunyonya waumini wenzao.
 
Wanasiasa hawamuachii Mungu wanajipa madaraka, Nyumba za ibada hazimuachii kukusanya SADAKA ..na mimi niko vitani kipande Cha keki yangu nataka" ...
 
Back
Top Bottom