Evelyn Salt
JF-Expert Member
- Jan 5, 2012
- 70,916
- 141,437
- Thread starter
- #61
Mi kuna siku bwana nimebaki ndani ya gari ya mtu, akashuka kuchukua chipsi funga. Nikamuambia nnataka kubreak ze wind mi nabaki garini. Full kipupwe, afu tinted ya maana. Tukawa tumeblock gari, nikawaona jamaa wanahangaika nikahamia kwa driver ili nilisogeze. Jamaa wakanigongea kioo kwa abiria nikashusha kioo. Dah, harufu ya ze wind hapo na kumbe ni mshkaji namjua. Yaani hatujawahi kuiongelea hiyo embarrassment manake dah! Im sure mshkaji aliskia harufu yaani. Na sijui why sikushusha kioo kwanza harufu ikatoka. Mtu akinitania about this ntaua aisee.
he he he hii kali.....pole!
mi nakumbuka nilipokuwa msichana mbichi kuna vibrazamen vilikuwa vinakaaga kona fulani mtaani, kila nikipita they sing praises mi bichwa hiloo sasa si kujipitisha uko.
Sasa kuna kipindi mvua ilinyesha na kuacha madimbwi ya maji, wenye maarifa yao wakawa wanaweka vitofali watu wakanyagie. Siku hiyo mwenyewe na madoido yangu napita kona ya wale mabishololo nikakutana na dimbwi la maji nikakanyaga kitofali cha kwanza cha pili yarabi tobaa! kumbe kuna wahuni wametegesha kipande cha kigodoro, niliingia dimbwini mzima mzima......niliwasikia wale mabishoo wakicheka, si aibu hiyo! sikugeuka nyuma na pozi lote lilikata
Nikabadilishaga na njia
ha ha ha aibu yangu ni ndogo sana kwa hii!pole