Jambo TV: Wakazi wa Dar wamshukuru Rais kwa huduma ua umeme kurejea!

Jambo TV: Wakazi wa Dar wamshukuru Rais kwa huduma ua umeme kurejea!

Precious Diamond

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2023
Posts
593
Reaction score
1,376
Yaani kuzungumza na watu wawili ndio imekuwa "Wakazi wa Dar"? Jambo mmeanza kuzingua.

=====

1711974164784.png

Wakazi wa jiji la Dar es Salaam wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kutokana na huduma ya umeme kurejea baada ya kuwapo kwa hitilafu katika gridi ya Taifa iliyodumu kwa saa kadhaa.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wakazi hao wamesema walikuwa na hofu ya bidhaa walizoziacha kwenye jokofu kuharibika kwa joto kali lakini hatua ya kurejea kwa umeme imeleta ahueni kwao

“Watu wengi sana ikiwamo mimi bado wapo kwenye sikukuu na walitumaini kwamba bidhaa zao zingekuwa salama kutokana na kutokukatika kwa umeme kwa siku nyingi, sasa usiku umeme umekatika ghafla sijui ingelikuaje kama usingerejea mapema” Amezungumza Amina Rajab mkazi wa Magomeni Kota.

Naye, Ramadhani Mubaarak ambaye amejiajiri kupitia mtandaoni amesema yeye amefika kazini akiwa hajui kama umeme utarudi ama la lakini kabla ya kupata athari zaidi katika kazi yake, umeme ulirejea.
 
Yaani kuzungumza na watu wawili ndio imekuwa "Wakazi wa Dar"? Jambo mmeanza kuzingua.

=====


Wakazi wa jiji la Dar es Salaam wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kutokana na huduma ya umeme kurejea baada ya kuwapo kwa hitilafu katika gridi ya Taifa iliyodumu kwa saa kadhaa.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wakazi hao wamesema walikuwa na hofu ya bidhaa walizoziacha kwenye jokofu kuharibika kwa joto kali lakini hatua ya kurejea kwa umeme imeleta ahueni kwao

“Watu wengi sana ikiwamo mimi bado wapo kwenye sikukuu na walitumaini kwamba bidhaa zao zingekuwa salama kutokana na kutokukatika kwa umeme kwa siku nyingi, sasa usiku umeme umekatika ghafla sijui ingelikuaje kama usingerejea mapema” Amezungumza Amina Rajab mkazi wa Magomeni Kota.

Naye, Ramadhani Mubaarak ambaye amejiajiri kupitia mtandaoni amesema yeye amefika kazini akiwa hajui kama umeme utarudi ama la lakini kabla ya kupata athari zaidi katika kazi yake, umeme ulirejea.
Kwanza kabisa namshukuru Mheshimiwa Rais Dakta Samia..

Kwa kuwezesha Wizara ya ahabari na technolojia kufanya vizuri na mimi nimeweza kutumia Bamdo langu pasipo na shida..

Pili Namshukur Kwa kuwa sasa hivi Nipo na nitakuwepo kwa sababu yake 😅
 
Wakazi wa jiji la Dar es Salaam wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kutokana na huduma ya umeme kurejea baada ya kuwapo kwa hitilafu katika gridi ya Taifa iliyodumu kwa saa kadhaa.
Pia tunamshukuru sa100 kwa mvua kunyesha leo kusindikiza Pasaka
 
Wakazi wa jiji la Dar es Salaam wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kutokana na huduma ya umeme kurejea baada ya kuwapo kwa hitilafu katika gridi ya Taifa iliyodumu kwa saa kadhaa.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wakazi hao wamesema walikuwa na hofu ya bidhaa walizoziacha kwenye jokofu kuharibika kwa joto kali lakini hatua ya kurejea kwa umeme imeleta ahueni kwao

“Watu wengi sana ikiwamo mimi bado wapo kwenye sikukuu na walitumaini kwamba bidhaa zao zingekuwa salama kutokana na kutokukatika kwa umeme kwa siku nyingi, sasa usiku umeme umekatika ghafla sijui ingelikuaje kama usingerejea mapema” Amezungumza Amina Rajab mkazi wa Magomeni Kota.

Naye, Ramadhani Mubaarak ambaye amejiajiri kupitia mtandaoni amesema yeye amefika kazini akiwa hajui kama umeme utarudi ama la lakini kabla ya kupata athari zaidi katika kazi yake, umeme ulirejea.

Usiku wa leo Aprili 1, 2024 wakazi wa maeneo mengi nchini walishikwa na bumbuwazi baada ya umeme kukata ghafla ambapo mapema asubuhi Shirika la umeme Tanzania TANESCO likarejesha huduma hiyo na kueleza kuwa kulikuwa na hitilafu kwenye gridi ya taifa iliyosababishwa na kiwango kikubwa cha maji kwenye mitambo ya kufua umeme ya Kidatu kilichopelekea mitambo kujizima kwa ghafla ili kujilinda.
20240401_144632.jpg
 
Kwamba yeye ndio Fundi aliyerekebisha ?

Nadhani alaumiwa kama ukikatika (sababu karne hii ya Sayansi na Teknolojia Kukatika kwa Umeme na kukosekana plan B ni uzembe na lack of planning) Na kama ikitokea sio apongezwe bali watu wapewe onyo kwamba isitokee tena

Tofauti ya hapo ni kukumbatia Mediocrity...
 
Umeme hauko stable unarudi na kukatika, hao wanaosema umerejea nenda kawaulize tena usikie majibu yao.
 
Kwamba yeye ndio Fundi aliyerekebisha ?

Nadhani alaumiwa kama ukikatika (sababu karne hii ya Sayansi na Teknolojia Kukatika kwa Umeme na kukosekana plan B ni uzembe na lack of planning) Na kama ikitokea sio apongezwe bali watu wapewe onyo kwamba isitokee tena

Tofauti ya hapo ni kukumbatia Mediocrity...
Hahahaha 🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Wakazi wa jiji la Dar es Salaam wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kutokana na huduma ya umeme kurejea baada ya kuwapo kwa hitilafu katika gridi ya Taifa iliyodumu kwa saa kadhaa.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wakazi hao wamesema walikuwa na hofu ya bidhaa walizoziacha kwenye jokofu kuharibika kwa joto kali lakini hatua ya kurejea kwa umeme imeleta ahueni kwao

“Watu wengi sana ikiwamo mimi bado wapo kwenye sikukuu na walitumaini kwamba bidhaa zao zingekuwa salama kutokana na kutokukatika kwa umeme kwa siku nyingi, sasa usiku umeme umekatika ghafla sijui ingelikuaje kama usingerejea mapema” Amezungumza Amina Rajab mkazi wa Magomeni Kota.

Naye, Ramadhani Mubaarak ambaye amejiajiri kupitia mtandaoni amesema yeye amefika kazini akiwa hajui kama umeme utarudi ama la lakini kabla ya kupata athari zaidi katika kazi yake, umeme ulirejea.

Usiku wa leo Aprili 1, 2024 wakazi wa maeneo mengi nchini walishikwa na bumbuwazi baada ya umeme kukata ghafla ambapo mapema asubuhi Shirika la umeme Tanzania TANESCO likarejesha huduma hiyo na kueleza kuwa kulikuwa na hitilafu kwenye gridi ya taifa iliyosababishwa na kiwango kikubwa cha maji kwenye mitambo ya kufua umeme ya Kidatu kilichopelekea mitambo kujizima kwa ghafla ili kujilinda.View attachment 2950819

Inasikitisha mno!
 
Back
Top Bottom