JUAN MANUEL
JF-Expert Member
- Nov 26, 2010
- 7,808
- 16,972
Wabongo wamefanywa mazombi hatari, kwani hitilafu na ubovu wa MIUNDOmbinu, ulisabsbishwa na Rwanda au Kenya! ?Wakazi wa jiji la Dar es Salaam wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kutokana na huduma ya umeme kurejea baada ya kuwapo kwa hitilafu katika gridi ya Taifa iliyodumu kwa saa kadhaa.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wakazi hao wamesema walikuwa na hofu ya bidhaa walizoziacha kwenye jokofu kuharibika kwa joto kali lakini hatua ya kurejea kwa umeme imeleta ahueni kwao
“Watu wengi sana ikiwamo mimi bado wapo kwenye sikukuu na walitumaini kwamba bidhaa zao zingekuwa salama kutokana na kutokukatika kwa umeme kwa siku nyingi, sasa usiku umeme umekatika ghafla sijui ingelikuaje kama usingerejea mapema” Amezungumza Amina Rajab mkazi wa Magomeni Kota.
Naye, Ramadhani Mubaarak ambaye amejiajiri kupitia mtandaoni amesema yeye amefika kazini akiwa hajui kama umeme utarudi ama la lakini kabla ya kupata athari zaidi katika kazi yake, umeme ulirejea.
Usiku wa leo Aprili 1, 2024 wakazi wa maeneo mengi nchini walishikwa na bumbuwazi baada ya umeme kukata ghafla ambapo mapema asubuhi Shirika la umeme Tanzania TANESCO likarejesha huduma hiyo na kueleza kuwa kulikuwa na hitilafu kwenye gridi ya taifa iliyosababishwa na kiwango kikubwa cha maji kwenye mitambo ya kufua umeme ya Kidatu kilichopelekea mitambo kujizima kwa ghafla ili kujilinda.View attachment 2950819
Uchawa kila sehemu,unamshukuru house girl kwa kuhakikisha nguo zimetakata! Kwani cha ajabu nini! Analipwa mshahara ili atakatishe nguo! Nguo zikitakata, ndio kazi, yake,na stahili yake ni salary tu,
Ingetokea jambo LA kipekee, kama vile nyumba imeshika moto kwa hitilafu ya umeme! House girl yupo peke yake na watoto,kwanza akatoa watoto nje, pili akafanikiwa kuingia chumba cha boss wake, akaokoa nyaraka nyeti za kampuni, na pesa,tatu, akaweza kukata umeme, na kupanda dalini na kuzima moto, nyumba ikapona, hasara ikawa ndogo! Hapo lazima umshukuru!
Sasa samia kafanya nini cha upekee!! Kuteua majambazi!?
So patheitic