sosssy
JF-Expert Member
- Nov 17, 2017
- 668
- 537
Wadai kinachostahili kwa njia ya VITA??? Hakuna namna nyingine ya kutafuta haki bila machafuko???
ndio manaake
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wadai kinachostahili kwa njia ya VITA??? Hakuna namna nyingine ya kutafuta haki bila machafuko???
Una uhakika gani kuwa baada ya hiyo VITA wewe au familia yako mtakuwa salama???
Rais wa CCM na CCM yake, na polisi wake na wateule wake na vyombo vingine vya kisheria na dola, hawaamini katika demokrasia. Wao wakisikia Chadema wanachukulia kama ni waasi au magaidi. Kwa hiyo wanapambana kwa njia zote zisizo za kidemokrasia, bila kujali dhuluma wanayofanya kwa wananchi wanaotumia muda wao mwingi kwenye kwenye mikutano ya kampeni na kwenye foleni, wakisubiri kupiga kura. Mbaya zaidi, CCM wako tayari kufanya mauaji kwa viongozi na wafuasi wa Chadema, tena wakishirikiana na vyombo vya dola na viongozi wa serikali ya CCM.
Jambo wanalopaswa kufahamu Chadema, ni kwamba muda wa kufanya siasa za kistaarabu umekwisha.
Sikuwahi kukubaliana na wanaosema Watanzania hatuwezi kuheshimiana kwa sababu hatukuwahi kumwaga damu wenyewe kwa wenyewe, lakini sasa nakubaliana nawo. Sihamasishi kumwaga damu, lakini nakubali kwamba dhuluma inafanyika kwa sababu hatuheshimiani, na hatuheshimiani kwa sababu hatujatoana damu.
Dhuluma wanayofanyiwa Chadema itaendelea, kama wao wataendelea kusubiri siku ambayo CCM watakubali kukaa mezani, hiyo siku haiwezi kutokea. Hakuna mazungumzo kati ya mtu anayepoteza (looser) na mtu anayefaidika (beneficiary). Mazungumzo na suluhu vitakuja vyenyewe ikiwa wote mnapoteza.
Kila kukicha tunasikia kiongozi wa CDM amechinjwa, mara amepotea, mara amekatwa katwa mapanga na kutupwa mtaroni, mwingine ametiwa ndani kwa amri ya mkuu wa wilaya, wengine wanachomwa visu....hatusikii wa CCM wakifanyiwa hayo. Kwa hali hiyo, hakuna suluhu, kwa sababu anayepoteza (CDM) analialia, mnufaika (CCM) anafurahi. Lakini kama wote watalia, suluhu itakuja bila kuitwa.
Jambo wanalopaswa kufanya Chadema ni kujiandaa kifedha na kiintelijensia kabla ya 2020, la sivyo hawatapata jimbo hata moja.
Kujiandaa kifedha ni rahisi kuliko kujiandaa kiintelijensia. CCM hawana intelijensia zaidi ya kutegemea vyombo vya kiserikali. Lakini kama Chadema itawekeza kiuhakika kwenye intelijensia, ni Jeshi la wananchi pekee ndio litaweza kuidhibiti. "Jeshi" tu ndio chombo cha kogopa, na kuheshimu kiasi.
Idara ya usalama imejaa 'corrupts' na 'ignorant'. Wachache wanaojitambua hawawezi kufanya ujinga wa CCM, na hata wakirubuniwa hawawezi kufanya ujinga wa CCM kwa ufanisi wa kutosha. "Mtu anayefanya kazi kwa kurubuniwa au kulazimishwa hawezi kuifanya kwa ufanisi wa kutosha".
Zaidi wanaojitambua ndani ya vyombo vya dola, watakuwa radhi kutoa ushirikiano kwa Chadema kuliko CCM.
Na kwa hiyo, Chadema ikitaka kuunda intelijensia imara, itahitaji watu wa kujitolea. Ogopa mtu anayejitolea kupambana. Lakini pia anayejitolea anaweza kuwa 'ametumwa'.
Anyway! Jambo la msingi ndio hilo, kujiandaa. La sivyo, hakuna jimbo litaenda Chadema mwaka 2020. Kwanza hakutakuwa na uchaguzi zaidi ya vituko, na kama kweli Chadema wanataka kuirudisha nchi kwenye mstari, ni vema kujiandaa na vituko hivyo. Haipaswi hata kidogo kusubiri "Rais Mstaarabu" ili kupambana, hapana. Anayestahili "kupigwa" ni mtu asiye na ustaarabu. Mwaka 2020 unapaswa kuwa mwaka wa kukomesha vitendo visivyo vya kistaarabu tunavyofanyiana watanzania wenyewe kwa wenyewe. Na njia pekee iliyobaki ya kukomesha vitendo visivyo vya kistaarabu, ni kuwafanyia hao wahusika, vitendo visivyo vya kistaarabu.
Msimamizi anayetangaza matokeo ya uongo, halafu akaendelea kuishi kwa raha mustarehe, atarudia tena.
Mkuu wa polisi anayetuma polisi kutishia watu, kupiga raia na kusaidia CCM, akiachwa aendelee kula maisha kwa raha mustarehe, atarudia tena.
Kila kiumbe kinachofanya ujinga, kikaachwa kiendelee kuishi kwa raha mustarehe, kitarudia ujinga wake.
Kiongozi wa tume ya uchaguzi anayetumiwa na CCM kudhulumu demokrasia akiachwa aendelee kula maisha, atarudia tena.
Hao, wanatakiwa kukomeshwa, ili iwe funzo kwao na kwa wengine wenye tabia kama zao, na iwe funzo kwa anayewatuma.
Ukitaka kuua Nyoka, kata kichwa, ukishindwa, kata hata mkia, uwezekano ni kuwa atakimbia lakini tayari umempumguzia nguvu.
Nani mwenye uwezo wa kuwakomesha, bila kujiingiza katika mgogoro wa kisheria? Ndio hapo pa kuandaa intelijensia imara. Lawama ni bora kuliko fedheha, na katika hili anayestahili lawama ni CCM, na fedheha ni kwa Chadema. Mwaka 2020, Chadema ni vema walaumiwe kuliko kufedheheka.
Hata hivyo viongozi wakubwa wa Chadema hawapaswi kujiingiza katika hayo, kwasababu watakamatwa na kufungwa mara moja.
Na sisi wengine, tu waumini wa ubinadamu, ni rahisi zaidi kuachana na siasa kuliko kufanya hayo, hatuwezi hayo.
mr mkiki.
Ndiyo.Hata ugaidi ni matokeo ya ukandamizaji wa tabaka fulani la watu ndani ya jamii.Leo mpinzani anaonekana ni raia wa daraja la pili ndani ya nchi yake.Njia halali ya kuonyesha kutoridhika na mfumo ni kupitia uchaguzi,nao umegubikwa na dhulma.Sasa nini kimebakia zaidi ya Violence in whatever form?Wadai kinachostahili kwa njia ya VITA??? Hakuna namna nyingine ya kutafuta haki bila machafuko???
Ndugu zangu, tusifike huko
Mkuu vita unaijua au unaisikia tu kwa wenzako?? Haya mambo siyo ya kushabikia shabikia tu kama mpira vile. Ukitaka kuijua vita au harufu ya vita hebu safiri mpaka Syria ukaone kinachotokea kisha ndio utajua vita ni nini.mimi nadhan hili ndo litakua solution,
nchi zenye vita sio kwamba hawapendi amani ni kutokana na watu kuchoka uonevu!!
bora vita tu itokee.
Suala la muda tu.Madaraka hulevya sana.Huyu LOFA anasema hatuwezi kuheshimiana hadi tumwage damu. Ndiyo maana Mzee Ben aliwaita malofa na wapumbavu,
Sijui anaandika tu bila fikilio, haya mwaga hiyo damu kama wanaume kweli, Ukuta mlishindwa maandamano ya fesibuku mmeshindwa alafu unaongea kumwaga damu.
Hili taifa tulikuwa tunataka maeendeleo tu na si siasa hata Chadema walikuwa wakihubili maendeleo ya nchi yetu tulianza kuwaamini tukashangaa baadaye wanapinga kilakitu hata Elimu bule ambayo ilikuwa sera yao wanaipinga.
Naomba vyombo vya usalama vimkamate huyu jamaa aunganishwe na akina Freeman mboye ktk kesi yao maana Mboe alisema lazima wafe watu 100 au 200 sasa yupo ktk kesi hili apate kujifunza.
Mkuu hakuna furaha Kama kufa, hebu fikiria kama ungekuwa umekufa ungekuwa unasumbuka humu jamii forum.Huyu LOFA anasema hatuwezi kuheshimiana hadi tumwage damu. Ndiyo maana Mzee Ben aliwaita malofa na wapumbavu,
Sijui anaandika tu bila fikilio, haya mwaga hiyo damu kama wanaume kweli, Ukuta mlishindwa maandamano ya fesibuku mmeshindwa alafu unaongea kumwaga damu.
Hili taifa tulikuwa tunataka maeendeleo tu na si siasa hata Chadema walikuwa wakihubili maendeleo ya nchi yetu tulianza kuwaamini tukashangaa baadaye wanapinga kilakitu hata Elimu bule ambayo ilikuwa sera yao wanaipinga.
Naomba vyombo vya usalama vimkamate huyu jamaa aunganishwe na akina Freeman mboye ktk kesi yao maana Mboe alisema lazima wafe watu 100 au 200 sasa yupo ktk kesi hili apate kujifunza.
Kumbe huyo jamaa alichinjwa jana?
Kwa hiyo wewe unataka kufanya UGAIDI ndani ya nchi hii kwa kisingizio cha kudai haki??Ndiyo.Hata ugaidi ni matokeo ya ukandamizaji wa tabaka fulani la watu ndani ya jamii.Leo mpinzani anaonekana ni raia wa daraja la pili ndani ya nchi yake.Njia halali ya kuonyesha kutoridhika na mfumo ni kupitia uchaguzi,nao umegubikwa na dhulma.Sasa nini kimebakia zaidi ya Violence in whatever form?
Mkuu vita unaijua au unaisikia tu kwa wenzako?? Haya mambo siyo ya kushabikia shabikia tu kama mpira vile. Ukitaka kuijua vita au harufu ya vita hebu safiri mpaka Syria ukaone kinachotokea kisha ndio utajua vita ni nini.
Mimi naamini kuna namna zingine za kupata solution kwenye mitafaruku lakini siyo vita, vita iacheni tu kwa majirani lakini siyo hapa kwetu.
Dogo yaonekana kama unawahusudu sana watu wa pande za mlimani eeh! Au umechumbiwa pande za Hai? Yaani kijana mwelewa wa calibre yako hustahili kushabikia ukabila hata mara moja kwani hauna maendeleo! Kemea mgawanyiko wa taifa kwanza ili lirejee hali yake ya umoja!
Uwe unasoma japo historia ya darasa la tano c basi kujua madhara ya ukabila na ukanda! Halafu wewe ndiye kinara wa kuutangaza sana ukabila na ukanda hapa jf as if unataka kurejea kwenu Burundi!
Siyo lazima niwepo mie.Je Mkwawa,Mirambo,Kimweri,Bushiri,Kinjekitile waliopambana na mkoloni walikuwepo wakati wa Uhuru?.Askari wanaoenda vitani nani mwenye uhakika wa kurudi hai?Una uhakika gani kuwa baada ya hiyo VITA wewe au familia yako mtakuwa salama???
Machafuko ni mabaya, tutakimbiakimbia hovyo tuache nyumba, watoto, wazee wetu, wengine tunafamilia, tusiombee hayo yatokee, kikubwa tuidai katiba katiba mpya basi.nipe sababu za msingi!!
Call it whatever you like.Hata Mandela aliitwa Gaidi na Makaburu na ANC ilikuwa ipo kundi moja na Alkaida nchini Marekani.Sisi tuliita Anc chama cha Ukombozi na Mandela mpigania haki.Kwa hiyo wewe unataka kufanya UGAIDI ndani ya nchi hii kwa kisingizio cha kudai haki??
CCM nayo iwashughulikie lowassa sumaye na nyalandu eti!..CHADEMA inatakiwa kuanzisha kitengo ‘maalum’ cha ‘kuwashughulika’ na mijitu misaliti kama waitara, mtatiro
Machafuko ni mabaya, tutakimbiakimbia hovyo tuache nyumba, watoto, wazee wetu, wengine tunafamilia, tusiombee hayo yatokee, kikubwa tuidai katiba katiba mpya basi.