imetoa funzo kuwa waafrika huwa tunatumika tu kama tambala na kutupwa huko, swala la spika kujihuzuru kisa ametoa maoni yake ni udikteta wa hali ya juu sana.
Cha kushangaza si bbc, Dot welle ya ujerumani ,chadema, Act wazalendo wala Ulimwengu waliokemea udikteta huu!.
Kama ingekuwa ni kipindi cha Magufuli ungeona ambavyo mishipa imewatoka kukemea udikteta kisa tu alikuwa anawabananga kwelikweli kwenye ulaji wao, leo kwa kuwa rais Samia amewaachia wale jinsi wanavyotaka basi wako kimyaaa wanakenua meno kana kwamba hawaoni kuwa kama kiongozi wa mhimili kama bunge anaweza kufukuzwa kwa kutoa maoni je wewe kikaragosi wa Maswa ndani ndani itakuwaje?
Kipindi cha Magufuli hata kufukuza watumishi hewa waliita ni udikteta.