Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nani huyu?

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nani huyu?

Sio raia wote wenye dini, kuna wengine ni wapagani pia.
Mh. Rais Samia ,

Naamini unafahamu kabisa kuwa, Mwaka 2020 wakati tunampigia kampeni Dr. Magufuli, tulikupigia kampeni na wewe ukiwa mgombea mwenza.

Tuliwaamini nyote wawili kwamba ni watu sahihi kuliongoza Taifa letu.

Sasa wewe ni Rais wetu, hakuna ubishi katika hilo.

Sasa Mh. Rais napata ukakasi kidogo kwa kauli zako , Kila unapotusalimia,

Huyu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unayemtaja ni nani hasa,

Maana ninavyofahamu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Nchi inayotokana na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Sasa hakuna mtu, kitu, watu, vitu kwa jina hilo.

Ingawa naelewa kwamba unataka usionekane kuwa unapendelea Dini yeyote,

Lakini Bado Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Haina hadhi ya kutajwa Kwa jina.

Sio sahihi kuipa hadhi hiyo.

Serikali Haina dini, lakini sisi raia tuna dini zetu, na hatumfahamu huyo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mh. Rais, salami hii, inatufikirisha mno sisi wengi,

Unaweza usiambiwe ILA Kuna haja ya kuachana nayo.

Wasalaaam,

Statesman,

Dar es Salaam.
 
Wasio na dini wasalimiajwe?
Unajua madhara ya kuambiwa ^Badilisha hiki, badili na kile pia. Ona, badilisha hapa. Badilisha kila kitu kabisa. Hakikisha the so-called legacy inasahaulika,^ ndiyo haya ya kusafiri bila kujua aendako.

Christians and people of faith must know that, kwa kuitikia salamu husika, basi ^mungu^ wao sasa ni JMT. Salamu ni kutakiana ama kukiri heri baada ya kukutana ama kutengana kwa muda. Na heri inatoka kwa Maulana, na wala siyo kwa JMT -- huyu ^mungu^ mpya wa Bi Mkubwa!!!
 
Ni jambo jema sana kutoingiza mambo ya dini katika serikali. Nchi yetu inapaswa kuwa secular kadri iwezekanvyo kama tunataka utangamano wa muda mrefu zaidi.
Tunakwepa kutamka “Tumsifu Yesu Kristu “ na “Bwana Yesu asifiwe “.
 
Ukisalimiwa salamu ya dini yako ndio unaona umeheshimiwa?
Una point hapo. Sasa Rais lazima kupenda na kuheshimu dini za wananchi wote. Basi anagalau abadilishe kidogo aseme ""Msifuni Yesu Kristu!"
 
Awasalamie watu hamjambo ndugu zangu/habari zenu/ habari za wakati huu n.k
Salamu za dini ziwekwe mbali kabisa na mambo ya serikali, ni ushamba.
Maelezo yako naona kama yana siasa kwa mbali ndani yake

Hii hoja ni kweli kama mtu ataweka siasa kando

Maana ya salamu ni kujuliana hali na/au kutakiana heri

Salamu mara nyingi ni lazima inakuwa na pande mbili, mtoa salamu kuamkia na watolewa salamu kuitikia

Kiukweli hatuwezi kuhesabu kuwa mtu amesalimu watu kwa kusema "...nawasalimia kwa jina la..."

Wala kusema "Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kazi iendelee" si salamu

Sasa kwa tafsiri nyepesi ni kwamba Mama hatoi salamu anaposimama kuhutubia bali anatumia kutamka kaulimbiu tu

Kuna vitu kama kibwagizo, kaulimbiu, misemo, methali na kadhalika ambazo nazo huwa na sehemu mbili hivyo hivyo lakini hatuiti kuwa ni salamu

Ni wazi inabidi ashauriwe aanze kusalimia watu sasa

Tukirudi kwa upande wa dini yake Mama mwenyewe (ya uislamu) ni dhahiri pia ni kosa kufanya chochote kwa jina tofauti na MwenyeziMungu (Allah)

Hii sijui imekaaje kwa upande wake ila kauli hiyo hutafsiriwa anakufuru

Naamini washauri wapo hadi (wanaohusika) kwenye maswala ya dini sasa sijui hawalioni hili!!?
 
Ni jambo jema sana kutoingiza mambo ya dini katika serikali. Nchi yetu inapaswa kuwa secular kadri iwezekanvyo kama tunataka utangamano wa muda mrefu zaidi.
1624047469120.jpeg

Ungeyatamka haya wakati huo
 
Kwenye kamusi pia hakuna salamu ya Bwana Yesu asifiwe au tumsifu Yesu Kristo
Hakuna mantiki yeyote kwenye hoja yako,

Hata kwenye kamusi ya kiswahili hakuna salamu ya namna hiyo.
 
Wasio na dini wasalimiajwe?
Ni jambo jema sana kutoingiza mambo ya dini katika serikali. Nchi yetu inapaswa kuwa secular kadri iwezekanvyo kama tunataka utangamano wa muda mrefu zaidi.

Nakubaliana na wewe 100% kwamba religion and politics must be separated. Kosa analofanya Bi Mkubwa kwenye salamu hii ni kuondoa mamlaka ya Mungu kwenye mahali husika pa msingi (^Nakusalimieni kwa jina la Yesu^) na kuweka ile nyingine ya kibinadamu -- JMT, huku akitegemea raia anaowaongoza ambao wana imani zao wakubaliane nayo.

Ukishaanza kutumia mstari huo tu (^Nakusalimieni kwa jina la ...^), kwa MKristo yeyote yule huwa inaprovoke feelings za kumsabihi Muumba ama Mola. Sasa kinapopachikwa kipande kingine (JMT), ni wazi Wakristo huamini kwamba wanalazimishwa mchwaha (indirectly) kuabudu mungu sanamu yaani, JMT.
 
Wakae kimya, sio lazima kuitikia, Halafu wajue mama ni muislamu safi, hawezi kumkana Allah wake kwa mungu mwingine ambao hao Wakristo wanaamini ni JMT.
Nakubaliana na wewe 100% kwamba religion and politics must be separated. Kosa analofanya Bi Mkubwa kwenye salamu hii ni kuondoa mamlaka ya Mungu kwenye mahali husika pa msingi (^Nakusalimieni kwa jina la Yesu^) na kuweka ile nyingine ya kibinadamu -- JMT, huku akitegemea raia anaowaongoza ambao wana imani zao wakubaliane nayo.

Ukishaanza kutumia mstari huo tu (^Nakusalimieni kwa jina la ...^), kwa MKristo yeyote yule huwa inaprovoke feelings za kumsabihi Muumba ama Mola. Sasa kinapopachikwa kipande kingine (JMT), ni wazi Wakristo huamini kwamba wanalazimishwa mchwaa (indirectly) kuabudu mungu sanamu yaani, JMT.
 
Mmeanza chokochoko wanaume wazima mnakuja humu na mada za kitoto.au mmetumwa? Hapo tatizo lipo wapi au ilimradi karaha tu mtafute pakuhemea? Shame on you!!
 
Ni jambo jema sana kutoingiza mambo ya dini katika serikali. Nchi yetu inapaswa kuwa secular kadri iwezekanvyo kama tunataka utangamano wa muda mrefu zaidi.
Ungeileta hii hoja wakati huo.
View attachment 1823101
Ungeyatamka haya wakati huo
Actually, tunaposema serikali haina dini maana yake ni kwamba mtawala yeyote aliyepewa dhamana ya uongozi, mathalani Rais wa Nchi, hatatumia nafasi yake ya Urais KUSHURUTISHA dini yoyote kwenda kinyume na misingi ya imani ya dini husika ambayo haipingani na kanuni za haki, usawa, utu na ubinadamu zilizowekwa kwa mujibu wa sheria.

Lakini pia ni wajibu wa viongozi hawahawa kuwafuata wananchi kule waliko -- yaani, kwa muktadha huu, kuwasiliana nao katika ^lugha wanazofahamu na imani wanazoshikilia.^ Mbona wakati wa kampeni za uchaguzi huwa hakuna mtu anayewafundisha hawa viongozi namna ya kuenenda, kuzungumza na hata kutenda wanapohitaji kuwasiliana na raia!??? Na huwa wanafanya vizuri sana!!!

Hitimisho: It's the leaders who should be flexible not their subjects, with regard to the mode of conversation and communication.
 
When you go places, go places with style. Mama amebuni Salamu na akatuelekeza jinsi yakuijibu. Hiyo ni maalum kwa ajili yake baada ya hapo endelea na utamaduni wako, tatizo lipo wapi?
 
Mmeanza chokochoko wanaume wazima mnakuja humu na mada za kitoto.au mmetumwa? Hapo tatizo lipo wapi au ilimradi karaha tu mtafute pakuhemea? Shame on you!!
Wewe mwenzao unaona kuwa ni ^mada za kitoto,^ lakini wenzangu na mie tunaona ni ^mada za moto^ Umeelewa sasa, au umelewa na kuelemewa!???
 
Mbona sioni watu wengi masokoni na sehemu nyingine mitaani wakisalimiana Tumsifu Yesu Kristu au Asalamaleku
Actually, tunaposema serikali haina dini maana yake ni kwamba mtawala yeyote aliyepewa dhamana ya uongozi, mathalani Rais wa Nchi, hatatumia nafasi yake ya Urais KUSHURUTISHA dini yoyote kwenda kinyume na misingi ya imani ya dini husika ambayo haipingani na kanuni za haki, usawa, utu na ubinadamu zilizowekwa kwa mujibu wa sheria.

Lakini pia ni wajibu wa viongozi hawahawa kuwafuata wananchi kule waliko -- yaani kuwasiliana nao katika ^lugha wanazofahamu na imani wanazoshikilia.^ Mbona wakati wa kampeni za uchaguzi huwa hakuna mtu anayewafundisha hawa viongozi namna ya kuenenda, kuzungumza na hata kutenda wanapohitaji kuwasiliana na raia!??? Na huwa wanafanya vizuri sana!!!

Hitimisho: It's the leaders who should be flexible not their subjects, with regard to the mode of conversation and communication.
 
Back
Top Bottom