Namaanisha Uturuki sasa hivi imekuwa na tabia ambazo tume zoea kuziona kwa mataifa ya kibeberu.
Uturuki ukiiangalia kwa juujuu utaliona ni taifa la kawaida,lakini ukijaribu kuichimba kwa undani ni tofauti kabisa.
Uturuki siku hizi imekuwa mjunjaji mzuri wa sheria za kimataifa na mbabe kupita kiasi lakini hakuna anaye chukua hatua dhidi yake.
Uturuki inayakalia kwa nguvu maeneo ya Syria na Iraq lakini hakuna anaye thubutu kumchulia hatua.
Anaikalia kwa nguvu ardhi ya sypulas kusini na hakuna anaye dhubutu kumgusa.
Juzi juzi kaenda bahari ya Mediterranean kwenye maji yanayo milikiwa na Ugiriki kaanza kuchimba mafuta kibabe na wakati ni mwanachama mwenzake wa NATO.
Umoja wa mataifa umeweka vikwazo vya kuingiza silaa nchini Libya ,lakini uturuki kila kukicha meli za uturuki zina pereka silaha nchini Libya na hakuna anaye thubutu kuzigusa.
Hii kwakweli imekuwa ikinifikilisha sana.
Uturuki anafanya haya kulinda haki ya mipaka yake, hasa ardhi, ajira, usalama na fursa kwa kuhitaji kudhibiti wakimbizi toka Syria, Iraq na Libya. Uturuki ndio taifa pekee duniani lenye idadi kubwa ya wakimbizi, wakimbizi wanaoruhusiwa kuishi na jamii na sio katika kambi, wakimbizi wanaopatiwa fursa za ajira, afya na elimu sawa na raia.
Rasilimali ya taifa inahusika kufaidisha watu zaidi wasiokuwa wahusika, huku wenye chanzo hawapatwi na dhahma hii.
Uturuki kufanya haya pasi ya kuguswa ni kuwa wenye uwezo wa kumgusa wanaofahamu nini anafanya, ubabe wa baadhi ya mataifa katika Syria, Iraq na Libya ndio chanzo cha Uturuki kuingiliwa na wakimbizi hivyo Uturuki anapiga na hao wahusika indirectly.
Dunia ya sasa haitaji upole wala ukarimu uliozidi maana utaendeshwa tu, huku wengine (Marekani, Uingereza, Ufaransa, Ubelgiji, Ujerumani, Japan, Uchina na Uhindini) wakionekana ndio wenye haki ya kuvamia pasi ya sababu za msingi maeneo na mataifa ya watu.