Jamii inayonizunguka inanipa mawazo sana ndugu zangu

Jamii inayonizunguka inanipa mawazo sana ndugu zangu

Sikushauri uachane na huyo demu,Ila fanya Kama ume bet,ni wasichana wachache Sana wanao weza kukwepa mishale ya chuo,
Demu akikoswa na lectures atapigwa na vipanga wa class,akikoswa na hao atapigwa na mabishoo wa chuo.
 
kamwe usifanye kitu kwa kuangalia shinikizo la ndugu/jamii inayokuzunguka, hayo mashinikizo yachukulie kama changamoto coz changamoto ni sehem ya maisha, umenifurahisha kuona haubagui kazi, kwa huu uthubutu wako soon mungu atakubarikia na kila kitu kitakua sawia.

huyo dada we msubirie kwa sababu ameonesha nia coz anaijua hali yako vyema
 
Nimeona kama wewe ndio tatizo....

Kuna tatizo labda unalo ile kwavile sisi wanadamu ni bias hua tunaamini sisi hatuna matatixo,wenye matatizo ni wale wengine wanaotuzengua
 
umesema kutoka umerudi ukweni mapenzi yameongezeka niwazi wazazi wake wamekukubali kubwa ondoa hofu na mawazo yako yaelekeze kwenye kutafuta kz au pesa km ulivyoeleza jinsi ulivyosoma kwa tabu bila kukata tamaa basi na kwenye maisha pia usikate tamaa mtangulize Mungu wako.
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Mkuu komaa kutafuta mtaji kama ulivyokomaa kutafuta ada yachuo..... Kwasasa ukiwekeza nguvu nyingi kutafuta kazi utajichosha bure namuda haukusubiri
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
MKUU nenda kijijini kwenu msimu huu wa maoteo muombe mtu utamsaidia kumsafishia shamba lake naimani utafanikiwa fanya hivo mkuu
 
Nimesoma uzi wako mpaka roho imeniuma umeandika kiunyonge sana mkuu.

Ushauri wangu.
1. Endelea kupambania kombe upate hela mzee.
2. Hakuna umri sahii wa kuoa usiteseke na mafanikio ya wenzako kuna waliofanikiwa na umri wa 25 na wakafilisika na umri wa 35. Na kuna waliofanikiwa at their 60's.
3. Binti lazima aende kusoma wakati ndio huu kuhusu hali ya chuo tumuachie maulana chochote kitatokea. Ila usipunguze uaminifu kwa kuwa yupo chuo. Big mistake.

I am at my mid 30's sijaoa ingawa nina watoto. Sijui naoa lini but kila nikitaka kuoa mambo yangu yanaharibika[emoji848][emoji848][emoji848].... So pambana
 
Huyo binti mwingine utamuoa bila kua na hela? Yaan wewe unahisi maisha ni sherehe ya harusi tu ambayo pesa yake huna hufikirii maisha halisi ya wewe na mtoto wa watu mtakayoanzisha,

Shida yako ni binti kwenda chuo unahisi utapoteza muda wa wewe kuoa na kuzaa kama ambavyo jamii yako inataka au shida ni binti kutaka sherehe?
 
Hahaaa halafu eti binti anamwambia haitaji pesa kwake ila apambane waishi maisha mazuri. Hivi hayo maisha mazuri yapo kweli bila pesa?
Haitaji pesa kwa sasa ndio maana hampigi mizinga ila anamshauri apambane atafute pesa sababu wana ndoto za kuanzisha familia, hao watoto wakija kuwaleta wataishi vipi kama wazazi wao hawana pesa?

Huyo Manzi ana akili sana, alipaswa amuoe huyo tena kabla hajaenda chuo, yaani yupo chuo tayari ni mke wake.
 
NGOSWE PENZI KITOVU CHA UZEMBE. HTOFANIKIWA KIMAISHA KAMA UTAENDEKEZA MAPENZI.

MUDA AMBAO AKILI YAKO INABIDI IFIKIRIE KUTAFUTA HELA NA KUBUNI MRADI WEWE UTAKUWA UNAWAZA MAPENZI TU.

UKIPENDA KUPITILIZA HATA UWEZO WAKO WA KUFIKIRI UNAPUNGUA SANA.

huyo binti akimaliza chuo na wewe ukiwa bado huna direction atakuacha, huyo ni mtu wa kaskazini anahitaji mtu mpambanaji.

Sent from my Infinix Zero 3 using JamiiForums mobile app
 
Akienda chuo msahau tu huna chako hapo , kwanini uwe unapata shida tafuta binti wa level yako mbona wanawake ni wengi tu,hatukuletwa duniani kuteseka furahia maisha uliekuwa nayo sasa
 
Habarini ndugu zangu, naombeni niwape mkasa wangu kidogo ili walio nizidi umri na wenye busara wanishauri kwenye ili ninalopitia, maana nina ongozwa na mawazo sana na nashindwa kuiona kesho yangu ilio bora

Kwanza kabisa umri wangu ni miaka 30 kwa sasaivi, nimetokea katika familia ya ufukara mkubwa (ata elimu yangu ya o-level nilisomeshwa na wilaya kitengo cha elimu), nina mpenzi ambaye nimekaa nae kwenye mahusino miaka 5 sasaivi (nimetangulia kusema ivyo vitu viwili ili nielezee kinaga ubaga kinachonisibu)

Mpaka muda huu wa miaka iyo 30 sina familia (sina mtoto), rafiki zangu wengi wameoa, wana watoto na familia zao ila kwa upande wangu imekuwa tofauti kidogo, kwa huu umri nilionao napata ujumbe mwingi sana kutoka kwa marafiki na baadhi ya ndugu kuniuliza vipi nafikilia nini kuhusu kuwa na famili (nabaki na mawazo ndugu zangu)

Ndugu zangu muda mwingi katika maisha yangu nimeutumia shuleni, nilipomaliza form-four sikubahatika kuchafaulu kwenda advance level, ilinibidi kufanya vibarua vya hapa na pale na kuweza kufanikisha kupata pesa ya kusoma level ya certificate, baada ya kumaliza certificate nikaanza kupambana tena na vibarua vya hapa na pale kwa mwaka mzima na kupata pesa ya kusoma diploma, baada ya kumaliza diploma katumia tena mwaka mzima kupambana kufanya vibarua na kupata pesa ya kusoma degree (nashukuru mungu kwa level ya degree nilipata mkopo wa asilimia 96%) na zile pesa zilinsaidie kwenye mambo yangu mengine

Nilimaliza chuo level ya degree mwaka 2018 (mpaka ivi sasa bado natafuta ajira bila mafanikio yeyote yale)

Kwa sasa najifanyia vibarua vyovyote vinavyokuja mbele yangu, iwe ni kuchimba misingi ya nyuma, kukusanya kuni na kuuza kwa wakaanga samaki, kuchotea watu maji, na kadhalika (nk).

Nimeishia kupata ela ya kula tu, jamii, marafiki, ndugu wakiniambia kuhusu kuoa uwa wananiweka kwenye wakati mgumu sana nashindwa la kufanya.

MAHUSIANO.
Nina girfriend wangu nilikutana nae kipindi nasoma diploma mwaka wa mwisho yeye akiwa anasoma form 5 (PCB), akuweza kuendelea hakuweza kubahatika kwenda levele ya degree alienda kusoma diploma baada ya kumaliza from six, na alimaliza diploma mwaka jana mwezi wa 10.

mimi na uyu bnti tumepitia up and down nyingi sana, mwaka jana niliisi mwenzangu amebadilika baada ya kuona mawasiliano yetu hayapo kama kipindi cha nyuma, na nilikuwa nikimuuliza mwenzangu anakuwa mkali sana, ilinilazimu nimuache uku nikiwa na uchungu sana moyoni maana ni binti niliyempenda sana sana (kumbuka wakati nipo nae uyu binti muda wote huo ndugu zake nilikuwa nawaona kwenye picha tu akiwa-post), ila rafiki zake baadhi nilikuwa nawafahau, baada ya kuaamua kukaa pembeni (nilifuta mawasilino yake kabisa) baada week 3 alikuja kunitafuta, aliniomba msamaa kwa yaliotokea na nikamsamehe kabisa tukaendelea na mahusiano mpaka ivi sasa

mwaka huu mwezi wa saba aliniomba niende kwao nikaonanae na ndugu zake, nikamuone baba yake na mama yake (ndugu zangu nilipata kama woga flani ivi, maana sikutegemea awe na ughafla wa kuniambia vile) ni kweli nampenda aswaaa, alianza kunipa simu niongee na mzazi wake wa kike (mama yake) alisema ameshamuambia mama yake kuwa mimi ni rafiki yake

Kuna siku mama yake aliniambia ni lini nitakwenda kuwasalimia (maana wazazi wake wanakaa mkoa wa kaskazini), nilimpanga tarehe ya kwenda kuwasalimia, tarehe ikafika nikafika kwao, nilipokelewa vizuri sana sana sana, nilitambulishwa kwa ndugu zake wengi tu. sikuwahi kufika kwa yule binti ila baada ya kufika nikajionea mwenyewe, kwao ni watu wenye uwezo kifedha, kifupi wanajimuda aswaa, nikaanza kama kukosa confidence ivi.

Mwezi huu uyu binti anakwenda kusoma chuo kikuu, matokeo bado hayajatoka ya chuo (selection),

uyu binti tangu nimeenda kwao ni mtu ambaye ametokea sana kunipenda zaidi ya kipindi cha nyuma kabisaaa, kila ninachosema kwake anakuwa yupo tayari, ila issue inakuja kwenye mambo yafuatayo.

anakwenda kusoma chuo (hapa pananiogopesha kama penzi letu litaendelea kudumu)
kuhusu kumuoa yupo tayari kabisaa ila tatizo linakuja upande wangu sina kazi kabisa kwa sasa (nabagaiza sana sana) kwenye miangaiko yangu kupata ela ya kula
ila pia anaonyesha kuitaji japo sana sana sherehe, hapa napo pananipa mawazo

Mpaka sasaivi ni binti amekuwa akiniheshimu, akinisikiliza tunahishi vizuri sana pasipo shida yeyote ile, ni binti amabaye uwa ananitamkia maneno haya "Siitaji pesa wala kitu chochote kutoka kwako, ila nahitaji tuje kuishi maisha mazuri, pambana unavyojua ki-alali kikubwa tuje kuishi maisha mazuri" aya maneno yake uwa yanazunguka sana kichwani mwangu.

Kuna muda pia nawaza, nimuache nikatafute binti mwingine uko nyumbani kwetu nianze nae maisha kwa kuoana kwa kutoa maali tu kwao, nianzishe familia kuliko kuanza kusubiliana na uyu ambaye kwanza anataka sherehe (ananisikiliza kote ila kwenye kufunga ndoa ambayo sherehe akuna anaonekana kutokuwa tayari).

nampenda sana sana, ila kuna muda nakosa amani binafsi, umri unakimbia sana ndio kitu kinanipa mawazo pia.

samaani kwa uzi mrefu, mbarikiwe
Mkuu usiwe na shaka, kikubwa zidisha ukaribu kwa kipindi chote atachokuwa chuoni, usitangulize hisia za fedha bali tanguliza hisia za kuushika moyo wake zaidi! Huyo anaonekana amekupenda kutoka moyoni.

NB: vyuoni kuna mambo mengi, jitahidi uwe unamtembelea mara kwa mara asipate upweke
 
Habarini ndugu zangu, naombeni niwape mkasa wangu kidogo ili walio nizidi umri na wenye busara wanishauri kwenye ili ninalopitia, maana nina ongozwa na mawazo sana na nashindwa kuiona kesho yangu ilio bora

Kwanza kabisa umri wangu ni miaka 30 kwa sasaivi, nimetokea katika familia ya ufukara mkubwa (ata elimu yangu ya o-level nilisomeshwa na wilaya kitengo cha elimu), nina mpenzi ambaye nimekaa nae kwenye mahusino miaka 5 sasaivi (nimetangulia kusema ivyo vitu viwili ili nielezee kinaga ubaga kinachonisibu)

Mpaka muda huu wa miaka iyo 30 sina familia (sina mtoto), rafiki zangu wengi wameoa, wana watoto na familia zao ila kwa upande wangu imekuwa tofauti kidogo, kwa huu umri nilionao napata ujumbe mwingi sana kutoka kwa marafiki na baadhi ya ndugu kuniuliza vipi nafikilia nini kuhusu kuwa na famili (nabaki na mawazo ndugu zangu)

Ndugu zangu muda mwingi katika maisha yangu nimeutumia shuleni, nilipomaliza form-four sikubahatika kuchafaulu kwenda advance level, ilinibidi kufanya vibarua vya hapa na pale na kuweza kufanikisha kupata pesa ya kusoma level ya certificate, baada ya kumaliza certificate nikaanza kupambana tena na vibarua vya hapa na pale kwa mwaka mzima na kupata pesa ya kusoma diploma, baada ya kumaliza diploma katumia tena mwaka mzima kupambana kufanya vibarua na kupata pesa ya kusoma degree (nashukuru mungu kwa level ya degree nilipata mkopo wa asilimia 96%) na zile pesa zilinsaidie kwenye mambo yangu mengine

Nilimaliza chuo level ya degree mwaka 2018 (mpaka ivi sasa bado natafuta ajira bila mafanikio yeyote yale)

Kwa sasa najifanyia vibarua vyovyote vinavyokuja mbele yangu, iwe ni kuchimba misingi ya nyuma, kukusanya kuni na kuuza kwa wakaanga samaki, kuchotea watu maji, na kadhalika (nk).

Nimeishia kupata ela ya kula tu, jamii, marafiki, ndugu wakiniambia kuhusu kuoa uwa wananiweka kwenye wakati mgumu sana nashindwa la kufanya.

MAHUSIANO.
Nina girfriend wangu nilikutana nae kipindi nasoma diploma mwaka wa mwisho yeye akiwa anasoma form 5 (PCB), akuweza kuendelea hakuweza kubahatika kwenda levele ya degree alienda kusoma diploma baada ya kumaliza from six, na alimaliza diploma mwaka jana mwezi wa 10.

mimi na uyu bnti tumepitia up and down nyingi sana, mwaka jana niliisi mwenzangu amebadilika baada ya kuona mawasiliano yetu hayapo kama kipindi cha nyuma, na nilikuwa nikimuuliza mwenzangu anakuwa mkali sana, ilinilazimu nimuache uku nikiwa na uchungu sana moyoni maana ni binti niliyempenda sana sana (kumbuka wakati nipo nae uyu binti muda wote huo ndugu zake nilikuwa nawaona kwenye picha tu akiwa-post), ila rafiki zake baadhi nilikuwa nawafahau, baada ya kuaamua kukaa pembeni (nilifuta mawasilino yake kabisa) baada week 3 alikuja kunitafuta, aliniomba msamaa kwa yaliotokea na nikamsamehe kabisa tukaendelea na mahusiano mpaka ivi sasa

mwaka huu mwezi wa saba aliniomba niende kwao nikaonanae na ndugu zake, nikamuone baba yake na mama yake (ndugu zangu nilipata kama woga flani ivi, maana sikutegemea awe na ughafla wa kuniambia vile) ni kweli nampenda aswaaa, alianza kunipa simu niongee na mzazi wake wa kike (mama yake) alisema ameshamuambia mama yake kuwa mimi ni rafiki yake

Kuna siku mama yake aliniambia ni lini nitakwenda kuwasalimia (maana wazazi wake wanakaa mkoa wa kaskazini), nilimpanga tarehe ya kwenda kuwasalimia, tarehe ikafika nikafika kwao, nilipokelewa vizuri sana sana sana, nilitambulishwa kwa ndugu zake wengi tu. sikuwahi kufika kwa yule binti ila baada ya kufika nikajionea mwenyewe, kwao ni watu wenye uwezo kifedha, kifupi wanajimuda aswaa, nikaanza kama kukosa confidence ivi.

Mwezi huu uyu binti anakwenda kusoma chuo kikuu, matokeo bado hayajatoka ya chuo (selection),

uyu binti tangu nimeenda kwao ni mtu ambaye ametokea sana kunipenda zaidi ya kipindi cha nyuma kabisaaa, kila ninachosema kwake anakuwa yupo tayari, ila issue inakuja kwenye mambo yafuatayo.

anakwenda kusoma chuo (hapa pananiogopesha kama penzi letu litaendelea kudumu)
kuhusu kumuoa yupo tayari kabisaa ila tatizo linakuja upande wangu sina kazi kabisa kwa sasa (nabagaiza sana sana) kwenye miangaiko yangu kupata ela ya kula
ila pia anaonyesha kuitaji japo sana sana sherehe, hapa napo pananipa mawazo

Mpaka sasaivi ni binti amekuwa akiniheshimu, akinisikiliza tunahishi vizuri sana pasipo shida yeyote ile, ni binti amabaye uwa ananitamkia maneno haya "Siitaji pesa wala kitu chochote kutoka kwako, ila nahitaji tuje kuishi maisha mazuri, pambana unavyojua ki-alali kikubwa tuje kuishi maisha mazuri" aya maneno yake uwa yanazunguka sana kichwani mwangu.

Kuna muda pia nawaza, nimuache nikatafute binti mwingine uko nyumbani kwetu nianze nae maisha kwa kuoana kwa kutoa maali tu kwao, nianzishe familia kuliko kuanza kusubiliana na uyu ambaye kwanza anataka sherehe (ananisikiliza kote ila kwenye kufunga ndoa ambayo sherehe akuna anaonekana kutokuwa tayari).

nampenda sana sana, ila kuna muda nakosa amani binafsi, umri unakimbia sana ndio kitu kinanipa mawazo pia.

samaani kwa uzi mrefu, mbarikiwe
😂😂😂 Brother pole bhan maana stori yako inafurahisha ingawa we unasema unakosa amani, ila chanzo kikuu cha ww kukosa amani ni umasikini tu wa kukosa pesa wala si mahusiano yako, yani ww stress zako zinasababishwa na kukosa pesa tu na wala si mahusiano yako wala umri wako, dat's all 🙂🙂🙂, we binti ameshakaa poa kabisa yuko tiari kuishi na ww sasa sijui we unakwama wapi, tena umesema mwaka huu anaenda chuo kuchukua degree ambapo atatumia miaka si chini ya mitatu na huu muda wa miaka mitatu unatosha kabisa we kutafta pesa broo ili akimaliza tu unamweka ndani, nashindwa kuelewa unafeli wapi ww stress zingine unaendekeza mwenyewe alafu ukizingatia ww ni mtoto wa kiume hupaswi kuwa ivo broo.... Vijana kibao tuna degree tupo mtaani na hali halisi ishajulikana ajira hamna lakini sasa kama hajira hamna isikufanye ww uchanganyikiwe kiakili, umri n namba tu tafta pesa broo, we mtoto wa kiume unashindwa kabisa kutafta hata million moja kwa mwaka mpaka miaka mitatu dem wako anamaliza chuo unakuwa hata n million 3 unaanzisha kibiashara chako hapo huwezi lala njaa na dem wako broo.... Amka kifkra aisee usiisubiri serikali ikuamshe, hakuna ajira serikalin saiv, tena bora utafte pesa hata dem ukaja kumkosa badae ( maana madem wakiendaga chuo hubadilikia huko huko) ingawa ni probability ila sasa kuliko kukosa pesa alafu na dem ukamkosa ni hatari sana
 
Back
Top Bottom