Jamiiforums GYM (mazoezi ) thread

Jamiiforums GYM (mazoezi ) thread

Nina urefu wa 172cm, niko na uzito wa 62kg. Nahitaji tips za kuongeza mwili na uzito ukilinganisha na urefu.
 
Nina urefu wa 172cm, niko na uzito wa 62kg. Nahitaji tips za kuongeza mwili na uzito ukilinganisha na urefu.
Quote Reply
 
Mzee zamani nilikuwa frexble sa hivi hata kupanda juu ya paa unaona uoga so why nataka kupunguza potelea mbali maneno ya watu.
Njia ya msosi nimefeli
Dah pole sana mkuu hiyo ni changamoto kama changamoto nyingine utaishinda tu
 
Anza kukimbia kwa week mara 2 km5 ...then punguza kula kwa siku kula mara mbili na ule kwa kiasi...ukiweza usiku unapiga vyakula vyepesi kama matunda na juice

Punguza kula punguza kula...ukishindwa kujizuia kula basi nenda mloganzila ukaweke puto.
Bro Kuna aina za appetite Ni ngumu sana Ku control, unaweza kuanguka kumbe energy imepungua sababu ya mahitaji ya mwili
 
Wakuu mambo vipi....Binafsi sio mkufunzi(gym trainer) ila napenda sana mazoezi na ninayajua mazoezi kuliko hata hawa wanaojiita ma-trainer,nimeanza kupenda mzoezi ya gym nikiwa form 3 (2013) so unaweza kuona nina experience ya miaka 11.

Mazoezi pia yanaambatana na aina ya vyakula tunavyokula ukiwa mwanamazoezi automatically kuna vyakula utaanza kuviepuka kama soda na vyakula vya mafuta.Binafsi nina mwaka wa 7 sijui soda na mwaka 4 sijui chips zikoje.Mimi nafanya mazoezi sili chipsi(mafuta food) wewe je nyama uzembe.Week inasiku 7 unahitaji siku tatu mfululizo za mazoezi na siku 4 unapumzika .anza leo after 6 monthes utaona matokeo.

Nitakuwepo hapa kuwapa-assistance kwa bigginer wote.hapa ni uwanja wa mazoezi ya aina zote both weight lift and cardio(mazoezi ya kukimbia na kucheza mziki,kupunguza mafuta na kutafuta pumzi)

Uzi huu ukawe wa kuhamasishana mazoezi na kupeana tips mbali mbali najua humu kuna wataalamu zaidi na wajuzi wa lishe wa kutosha.

Zifuatazo ni Faida za Mazoezi mwilini

1. Kuboresha Afya ya Moyo.
Mazoezi ya mara kwa mara husaidia kuimarisha moyo na kuboresha mzunguko wa damu, kupunguza hatari ya magonjwa ya moyo.

2.Kuongeza Nguvu na Uimara.
Mazoezi ya nguvu huongeza misuli na kuimarisha mifupa, huku mazoezi ya uvumilivu yakisaidia kuboresha uwezo wa mwili kustahimili uchovu.

3. Kupunguza Uzito.
Mazoezi husaidia kuchoma kalori na kupunguza mafuta mwilini, hivyo kusaidia katika kupunguza uzito.

4.Kuboresha Mvuto wa Mwili
Mazoezi ya mara kwa mara husaidia kuimarisha misuli na kufanya mwili kuwa na muonekano mzuri na wenye nguvu.

5.Kupunguza Stress na Kuboresha Hisia.
Mazoezi yanaweza kusaidia katika kupunguza viwango vya stress na kuboresha hisia kwa kuongeza uzalishaji wa endorphins, kemikali zinazofanya mtu ajihisi vizuri.

6.Kuboresha Usingizi.
Mazoezi yanaweza kusaidia kuboresha ubora wa usingizi, hivyo kukufanya uamke ukiwa na nguvu na mchangamfu.

Jinsi ya Kuanza Mazoezi
Najua wabongo wengi hatupendi mazoezi kutoka na mfumo wetu na ukuaji wetu wa maisha maana mazoezi ni sehemu ya maisha ni hii husaidia sana watu kuiishi umri ya miaka 70 mpaka 90.

1. Anza Kidogo Kidogo.
Usijaribu kufanya mazoezi mengi mara moja. Anza na mazoezi madogo na polepole ongeza muda na kiwango cha mazoezi.

2. Chagua Mazoezi Unayoyafurahia.
Tafuta aina ya mazoezi unayopenda, iwe ni kutembea, kukimbia, kuogelea, kucheza dansi, au hata mazoezi ya nyumbani. Kama unajifurahisha, utapata rahisi kuendelea.

3.Panga Ratiba.
Weka ratiba ya mazoezi na ujitahidi kuifuata. Hakikisha una muda maalum wa kufanya mazoezi kila siku au kila wiki.

4.Tumia Rafiki.
Kufanya mazoezi na rafiki kunaweza kufanya mazoezi yawe na furaha zaidi na kukuongezea motisha.

5.Lenga Malengo Madogo na Yanayowezekana.
Weka malengo madogo na yanayoweza kufikiwa. Kwa mfano, lengo la kutembea kwa dakika 20 kila siku kwa wiki moja.

6. Sikiliza Mwili Wako
Usijilazimishe kufanya mazoezi zaidi ya uwezo wako. Sikiliza mwili wako na pumzika unapohisi uchovu.
Itabidi nianze mazoezi hivi karibuni umetupa hamasa sana
 
Mi kwa wiki nafanya mazoezi ya strength siku Tatu na cardio siku mbili napumzika weekend.

Mazoezi nnayofanya zaidi ni calisthenics sifanyi na sitakuja kufanya mazoezi ya kunyanyua chuma.
 
Mkumbushe pia mazoezi lazima yaendane na nidhamu ya ulaji sio anachoma carolies jioni anaenda kufakamia viepe pale uhasibu karibu na liquid
Anza kukumbia kila siku km 4 week tu utakuwa ushakata mafuta ya kutosha na kupunguza kilo sio ch
 
Mazoezi hayachagui aina gani ya mwili muhimu ni kuwa physical fitness...ila inategemea wewe unataka mwili wa aina gani kama unataka kuwa na mwili mkubwa kama 50 cent lazima ule vizuri na uingie sana gym.
Aongezee na maprotini na creatine
 
Back
Top Bottom