JamiiForums ya Maxence Melo imenipatia mume. Clepatina naolewa

JamiiForums ya Maxence Melo imenipatia mume. Clepatina naolewa

I have already move on sina kinyongo na yeye...Namtakia baraka na ndoa ikatimie🤣🤣
Brother kuwa muwazi jana tu you already moved on😬 au basi
Screenshot_20230531_003032_Google.jpg
 
Kanuni kuu ya kuoana ni moja tu upendo

Oa au olewa na mtu kwa kuwa unampenda sio ohh naoa au au namhurumia au sababu nina stress au nataka kumpunlguzia stress wewe sio ofisa wa ustawi wa jamii au mshauri nasaha wa wenye stress

Upendo pekee ndio unatakiwa kuwa mwamuzu na upendo na mtu unayemjua vizuri

Hizi ndoa za matchmaking za mitandaoni nyingi future huwa hazina future nzuri

Anyway ulichofanya mleta mada ni trial and error lakini sio best way ya kupata mke au mume unless una malengo ya mafupi ya kuchumchuna au kupata fursa fulani toka kwake yakikamilika kuwa hata mkibwagana it doesn't matter to you mission accomplished
 
"Apataye mke apata kitu chema; Naye ajipatia kibali kwa Bwana."
MITHALI 18:22.

Wapendwa nilitaka nipotee kimya kimya, ila kwa namna hii ID yangu ilikaribishwa kwa upendo na kwa upendo nilionao kwa marafiki na ndugu zangu zangu niliojipatia hapa JF nimeona sio ubinadamu nikaitelekeza hii ID bila kuwaaga halafu niwaache wapendwa wangu wakijiukiza Clepatina kapatwa na nini mbona kapotea jukwaani.

Wapendwa, Mungu akitoa kibali November ninaolewa na mchumba niliyempatia hapa JF.[emoji1787][emoji3590].

Huyu jamaa hajanikuta single. Alinikuta nikiwa kwenye uhusiano na jamaa ambae hata hapa jukwaani nishawahi kumtaja kama Mgweno.

Kwa huyu mgweno ndiko moyo wangu uliko. Nilimpenda sio kwa moyo wangu wote bali kwa vyote vilivyotumika kuniumba. Nilimpenda sana huyu mwanaume kiasi cha kuwaona wanaume wengine wote walionitongoza kama wachumba tu[emoji1787].

Baadae nikagundua ninampenda Mgweno zaidi ya anavyonipenda na nikawa mtu wa kulalamika kila siku.

Hata hivyo Mgweno ndio aliyesababisha huyu shemeji yenu mpya atangaze ndoa fasta fasta.

Ni hivi,wakati nakutana na Mgweno nilikua na stress sanaa kiasi kwamba nilikua naonekana kama nina mara mbili ya umri wangu. Nilikua nimechoka sana. Nilikua kibibi[emoji1787] lakini mahaba na faraja alizonipa Mgweno zikarudisha peace of mind na stress zikaisha na Clepatina nikawa pisi kali tena[emoji1787].

Amini usiamini, mwanamke akipendwa na mwanaume anayempenda uzuri wake unarudi[emoji1787]. Ndio maana mtu ukiwa single hufatwi ila ukipata tu wa kukupenda utashangaa kila mwanaume anakutaka[emoji1787].

Sasa baada ya kuona Mgweno haeleweki/kabadilika nikapambania penzi haijasaidia, ndio kajitokeza huyu shemeji yenu mpya na japo hatuna muda mrefu na siwezi kusema namjua vizuri ila nafsini mwangu nahisi amani juu yake.

Kwa hatua alizochukua na gharama alizoingia juu yangu nina imani yuko serious katika kutaka kunioa.

Yeye na familia yake yote ni walokole kama mimi na ninajihisi salama kuwa mikononi mwa mwanaume amchae Mungu.


Ndugu zangu, mwanaume Mcha Mungu, msomi, mwenye ofisi zake kubwa kubwa, handsome, mpole ila mkali kwenye upuuzi, asiyependa wanawake wengi na mwenye mapenzi kama kapewa limbwata, hatoki kokote zaidi ya Mbinguni kwa baba Mungu, Mungu wa ishara na miujiza. Mgweno anisamehe ila naamini huyu ndie niliumbwa toka ubavuni mwake[emoji3590].

Hii itakua ni post yangu ya mwisho hapa. Kwa sasa najikita zaidi kusoma biblia kama alivyoniomba mume wangu mtarajiwa na pia kutumia free time yangu kujifunza kupika. Sijui kupika ndugu zangu[emoji24] na shemu wenu kasema kutojua kwangu kupika ni tatizo na mpaka siku ananioa niwe nimeshajua kupika.

Najua ndoa zina changamoto, najua mume wangu mtarajiwa atakuwa na madhaifu yake, najua kuna siku za kulia na siku za kucheka najua kuna siku tutapata na kuna siku tutakosa najua kuna mengi mazuri na mabaya yatajitokeza ila hata itokee nini kamwe sitafanya yafuatayo;

1) Sitamcheat hata akipoteza dushe yake.

2) Sitamdharau hata akikosa uwezo wa kunipa jero.

3) Kamwe sitajiona nina akili kumshinda.

4) Kamwe sitapaza sauti yangu ninapoongea nae.

5) Kamwe sitonyanyasa watoto wake ambao mama yao amefariki, kwani tayari nawapenda na wao wananipenda kama nimewazaa mimi.

Kwa mnaonipenda naombeni mniage kwa neno zuri la ushauri.

Joannah Half american Gily
I CAME, I SAW, I CONQUERED
Kila kitu kikitumika vizuri kinaleta matokeo chanya na kikitumika vibaya kinaleta matokeo hasi. Kuna msemo unaotumika katika computer inasema "Garbage in Garbage out"

Nasema hivi kutokana na baadhi ya wanawake humu wanajiheshumu,wanapenda kuolewa na kutulia, wanamaanisha na pia kutokana na changamoto ya maisha ya kimapenz,wamedharauliwa,kunyanyaswa,na hata kuvunjika moyo kutokana na mateso ya mapenzi na manyanyaso na hivyo wanapenda kuwa na wapenzi wa chaguo lao na kufaidi mapenzi matamu.

Shangaa Sasa wapo wanawake na wanaume walioko serious, wengine na malaya tu humu ndani, utashangaa mwanamke anataka kuolewa ila ukimtafuta basi dk chache hana hela ya kula,kafiwa,hana hela ya saluni,nyumba anayokaa anadaiwa Kodi,hana vocha, ana shida binafsi anataka hela,mara akutumie picha za nusu utupu,mara anataka nguo aende kwenye harusi,mara anaumwa. Hivyo vyote hata siku haijaisha. Ukimtumia hela tu anakublock. Hao ndo wanaharibu taswira ya wengine wanawake walioko serious.

Kwa upande wa wanaume utasikia maneno mengi Sana,mara ooooh, huna mwanaume, hujawahi kuwa na mwanaume, kwenu huko hakuna wanaume,una chura,piga picha sura yako tuione, wewe unataka mwanaume basi ni malaya tu nk.

Anyway humu kuna walioko serious na walioko na utani na ujinga mwingi, nk. Yaani kwenye msafara wa mamba na kenge wamo.

Cha msingi ni kutambua walioko serious na walio choko ndo ugumu uliopo. Otherwise humu pangekuwa na sehemu salama kwa wale wasio na wanaume au wanawake kutafuta wenza wao hapa.
 
Back
Top Bottom