Jana ilikuwa siku ya Furaha kukutana na Graduate anachoma mahindi Barabarani

Hahhahahahah....we jamaa huyo mchizi kakudanganya,IT hadi uuze mahindi ya kuchoma mchezo,kama kweli hana akili ya kujiongeza!....unashindwa hata kutengeneza simu,au ukafungua kaframe uwe unadesign card
 

Wewe jamaa unatundanganya
Muuza mahindi akijitahidi sana anaanza kazi saa 6 mchana, na wengi mwisho wao ni saa 2 jioni hapo masaa aliyotumia ni masaa 8 pekee.
Akifika aanze kuandaa jiko lake, kuandaa mahindi kuanza choma ishafika saa 7,
Jiko lake linachoma mahindi 10 kwa wakati mmoja na mahindi kusema kuwa kahudumia watu 400 kwa siku unatupeleka chaka kabisa ndugu. akijitahidi sana kwa siku ni watu 50-80.

Hakuna mtu anaefanya kazi masaa 24 dunia hii

Kubali unatupiga fix
 
Sasa umepata furaha gani hapo zaid ya kuona huruma?? Sometimes this world is not fair. Sometimes haimaanish the hard you struggle you will have happy ending.
Kuna siku MTU alinipigia mahesabu pesa wanayopata wauza mahindi kwa siku.Kwanza ukianza na mhindi mmoja mmoja anavyojumua mkaa anaotumia na faida.Aiseee wakitulia wanapata faida kubwa sana.Yupo sahihi.Na atafika mbali.Huruma tuwaonee ambao mpaka Leo watamsubilia Angela Kairuki amalize ukaguzi wa vyeti ambao hauna End .Viva Mchoma mahindi MPE salamu zangu na hata kamtaji kidogo naweza muongezea akuze mtaji.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe ndo hujui.Leo pita kijiweni wanakouza piga mahesabu.Utaniambiaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Somo kubwa la kujivunza hapa ni kutokuwa na uoga na aibu!!
Ila kukusanya mtaji kwa kuchoma mahindi, huduma zingine za kimaisha anaziendesha vipi na anasevu kiasi gani??!!
Kama anatokea nyumbani kwao je?kuna watu mnajua kukatisha watu tamaa kama mnajua.So upo tayari ashinde home kutizama TV na si kuchakarika??huyo keshaanza hatua.Baki mkimsubiri Anjela Kairuki

Sent using Jamii Forums mobile app
 
sio kweli. sio lazima uanze na kuflash smart phone.. angeanza na kutengeneza vitoch.. kwa hio laki hawezi kukosa desktop..hata angekuja hapa JF mimi ninngeweza kumpa hio desktop ya kuanzia.. afu badae angejiongeza mwenyewe ila kuchoma mahindi ni kuwa KIAZI
 
IT ameshindwa kujiongeza hata akaanza kutengeneza simu?
mkuu ndio maana jamaa kasema anakusanya mtaji nadhani kwa hesabu za haraka kunavifaa vya ofisini kuna pango na mengine mengi....so nampa big up huyo jamaa

UOGA WAKO NDIO UMASIKINI WAKO

I BLNG 2 JESUS CHRST
 
Kama anatokea nyumbani kwao je?kuna watu mnajua kukatisha watu tamaa kama mnajua.So upo tayari ashinde home kutizama TV na si kuchakarika??huyo keshaanza hatua.Baki mkimsubiri Anjela Kairuki

Sent using Jamii Forums mobile app

1. Nimekubali afanyacho,
2. Nimeuliza swali, sijui unajua maana ya "?"?
Acha povu dogo!
 
kama hivyo sawa.
kwa sababu tunaweza kumponda kumbe ndio safari yake inaanza hivyo
Yap maana wengne safar wanaazia
Mwishon badala ya mwanzao

[Color= yellow]Triple A[/color]
 
una maanisha kafungua kampuni ya kuchoma mahindi... akiwa na vijiwe kama mia hivi atakuwa na pesa nzuri... sana

waaaaoow hii ndio idea ya kisomi nimeipenda zaidii
 
Sasa unafikiri ni hicho ni kitu kizuri?
Kwahiyo hukuona huruma pia?
Sidhani kama mtoa mada amefurahia graduate kuchoma mahindi. Alichotaka kutueleza ni kwamba tusione aibu kufanya kazi au biashara ndogo ambayo baadae itakuza mtaji kufanya kitu ukipendacho.
Graduates wengi wapo mtaani wanasubiri ajira na mitaji. Bila uthubutu kama huyo mchoma mahindi watasubiri sana. Maisha ni magumu.
 
Angekuwa kafungua Bucha na anauza Nyama je? Ungesemaje?

Vipi angekuwa kaajiriwa kama mkuuwa walinzi pale KKGuard ungesema pia?

Au shida mahindi?

Angekuwa anashinda home je? poa tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza kabisa mie nimecheka sana kwa mleta post kumsifia huyo Graduate kwa kuchoma mahindi, baada ya kusoma nikaona eti kasoma IT, hapo ndio nikazidi kushangaa, bora angekuwa amesoma mambo ya kilimo na biashara anagalau tungesema anafanya research ili aje na bonge la project

Mie nashangaa kwa nini kama unasema lengo ni kuanzia chini, basi asianze hata na kakibanda ka kurekebisha software katika simu, kuistall apps mbali mbali, kutengeneza laptops, Computer nk, yaani kuna watu ni darasa la saba wanapiga hela kwa kujifany amafundi simu na simu zetu zinapona tukiwapelekea, sasa huyo IT wa degree hili limemshinda, si angeenda kwa fundi simu akajifanya mjinga akafundishwa utundu wa kutengeneza halafu akaongeza na elimu yake baada ya mwaka huenda atakuwa mbali.

Mie ninachokiona hapo ni kuwa degree zetu ni za vyeti lakini kichwani hamna kitu, mtu aliyesoma IT lazima atakuwa anamiliki laptop, lazim anajuana na watoto wa mjini wanaouza laptop used, fursa zote hizo hajaziona akaenda kuchoma mahindi, this is a shame for real

Wasomi wengi wa kibongo wakimaliza hutaka kuajiriwa kwa kuwa hawana skills, hivyo wanakimbilia kuajiriwa ili wakafundishwe kazi huko maofisini na watu wenye uzoefu lakini wao huja kwenye ajira vichwa tupu, we fuatilia tu, tafuta Mhasibu aliyegraduate mwambie akufungie mahesabu hawezi, tafuta engineer wa umeme aliyegraduate mwambie akakague mradi wa umeme wa TANESCO utaona madudu tu, hao ndio wasomi wa bongo

Sasa badala ya kusifiana ujinga tuambiane ukweli kuna haja gani ya kumaliza zaidi ya Tsh 10 MIL kwa miaka mitatu aliyotumia kusoma IT halafu anakuja kuchoma mahindi, hiyo 10 mIL si angeanza biashara ya kuuza mahindi jumla na reja reja mapema tu akaachana na huko alikoenda kusoma halafu hawezi hata kutengeneza simu.

THIS IS A SHAME FOR OUR COUNTRY
 
Mind set unafikiri kufanyaje?.Usha wahi some histori za makumpuni makubwa yalivyo anza?

Hayo mahindi hujui anawez siku moja kupack na ku export?.

Mind set gani wak wewe hapo uko kazin kwa watu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…