Yesu Ana misemo ya kindengereko 😂😂Yesu akasema "Ewaaa"
Unasoma maandiko kwa kukurupuka, matumizi ya neno “wote” kumaanisha kila aliyemtangulia, muktadha wa maandiko unaonyesha Yesu alikuwa akizungumzia manabii na torati waliotangulia kumshuhudia Yeye, si kwamba kila aliyemtangulia hakuwa na thamani.Mbona unapindisha kwa kusema alimaanisha viongozi wa Dini, aah siyo hivyo alimaanisha WOTE waliomtangulia. Elewa neno WOTE.
Kwanini unajizima data.
Anyway unasemaje kuhusu 2 kor 3 : 7, amri za Mungu paulo aliziita HUDUMA YA MAUTI...
Lakini warumi 7 mbona huendelei mpaka aya ya 13, au basi kwanini huanzi kusoma angalau Rum 7 :10-13
Huwenda ni kwa sababu hutaki kukubali ukweli kuwa Amri iliyo njema na haki ndio ilimuua paulo.
Sheria ilikuwa ya kiongozi kutuleta kwenye wokovu(Kristo) lakini kwa kuwa tumeshafika kwa Kristo hatuhitaji kiongozi tena.
Kama bado hujafika kwa Kristo basi endelea na Torati mpaka ikufikishe kwa Kristo ndipo uiache.
Umekosa hoja japokuwa nitarudi kujibu maswali yako
Sheria za vyakula ni Amri za Mungu ama Musa?Una uelewa mdogo kuhusu Amri za Mungu, amri za Musa , hili somo hamtaki kujifunza ndio maana mnachanganya kila kitu
Nitakujibu,lakini maswali yangu huko juu yamekushinda kujibu ??Sheria za vyakula ni Amri za Mungu ama Musa?
Sadaka za dhambi ni Musa ama Mungu?
Zaka ni Musa ama Mungu?
Mavazi ni Musa/Mungu?
Jibu hapo ili tumalize mjadala.
Swali langu la Mwisho kabisa kwanini unashika Sheria?
Mpaka yote Yatimie. Yapi? Mpaka yote yatimie maana yake alimaanisha yakishatimia inaondolewa.1. Ikiwa Sheria ni mbaya na kazi yake ni kuua, kwa nini Yesu alisema katika Mathayo 5:17-18 kwamba hakuja kuitangua bali kuitimiza, na hata chembe ndogo ya sheria haitaondolewa mpaka yote yatimie?
Watu wakishafika kwa Kristo wanafanyaje? Yaani wameshika Sabato/sheria wameona kumbe haiwezi kuwaokoa badala yake wanazidi kuivunja inabidi waende kwa Kristo wakishafika kwa Kristo wanafanyaje?1. Ikiwa Sheria inatufanya tuwe vipofu au tulaumiwe, kwa nini Yesu alisema hakuja kutangua Sheria bali kuitimiliza (Mathayo 5:17)? Je, hili halionyeshi kuwa Sheria ina nafasi muhimu katika kuelekeza watu kwa Kristo?
Sawa mwadventista msabato! hongera kwa ubunifu wako!Wakuu, kwa kuwa katika muda huu, sisi wenye mamlaka ya kusimamia na kuandaa wataalamu wa baadae (walimu) tupo likizo. Ninaitumia likizo hii kwa kwenda shambani ili kuzalisha chakula.
Wakuu, jana nilibahatika kukutana na Yesu ana kwa ana, nilikuwa natoka shambani narudi nyumbani majira ya mchana kwa ajili ya kupata la mwidebe (kula).
Ghafla, mbele yangu kwa juu nikashangaa wingu safi jeupe linashuka kwa kasi katika ueleko nilipo, punde si muda, likanifikia, lahaula kumbe ulikuwa ni usafiri uliomsafirisha Yesu kutoka mbinguni kuja kuonana na mimi.
Alinikuta njiani. Wakuu, kwa kuwa kuna mambo mengi huwa yananitatiza kila ninaposoma Biblia hasa vitabu vinavyoelezea utumishi wa Yesu Kristo akiwa hapa duniani, ilibidi niruke fasta sana na fursa adhimu kama ile kwa kuongea na kumuomba ufafanuzi kwa yale yanitatizayo.
Mazungumzo baina yangu na Yesu Kristo yalikuwa kama ifuatavyo.
Mimi: Shikamoo Bwana mkubwa Yesu Kristo mwana wa Mungu aliye hai.
Yesu: Marhaba mdogo wangu na rafiki yangu Barnabas Mashamba.
Mimi: Hee, unalijua hadi jina langu bila kukuambia.
Yesu: Siyo jina tu, najua hadi idadi ya nywele zako kichwani. By the way, kama wewe umefahamu jina langu pasipo kukutajia, kitu gani kinafanya mimi nisilijue jina lako?
Mimi: Eniwei hivi Yesu Kristo, kwanini ulianzisha amri mpya? Si baba yako kupitia Musa alikuwa ametupatia amri kumi tena akiwa ameziandika kwa kidole chake mwenyewe kwenye mbao mbili za mawe?
Yesu: Amri gani mpya ambayo nilileta?
Mimi: Siku ulipoulizwa swali kuhusu amri ipi ni kuu katika torati na manabii, si ulileta amri mpya wewe.
Mazungumzo yangu na Yesu kristo yalitokana na yale niliyosoma katika kitabu kile cha Mathayo sura ya 22
Mathayo 22:35-40
[35]Mmoja wao, mwana-sheria, akamwuliza, akimjaribu;
Then one of them, which was a lawyer, asked him a question, tempting him, and saying,
[36]Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu?
Master, which is the great commandment in the law?
[37]Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote.
Jesus said unto him, Thou shalt love the Lord thy God with all thy heart, and with all thy soul, and with all thy mind.
[38]Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.
This is the first and great commandment.
[39]Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako.
And the second is like unto it, Thou shalt love thy neighbour as thyself.
[40]Katika amri hizi mbili hutegemea torati yote na manabii.
On these two commandments hang all the law and the prophets.
Yesu: Umesema swali lilihusu amri ipi kuu katika torati na manabii, right?
Mimi: exactly.
Yesu: Wakati natoa jibu, nilisema naleta amri mpya, au nilitoa jibu moja kwa moja kwa swali nililoulizwa kuhusu amri kuu katika torati na manabii?
Mimi: Sijui
Yesu: Hujui kwa kuwa hupendi kusoma.
Mimi: Sasa hapo Yesu naona unanitukana bila kujua elimu yangu, hivi kwanza wewe Yesu ulisoma ukahitimu hata darasa la kwanza?
Yesu: Hapana, sikubahatika kusoma elimu rasmi ya darasani ila nilijua kusoma na kuandika.
Mimi: Umesema kweli maana hata ulifuata msemo wa ndege wafananao huruka pamoja.
Yesu: Kwa nini unasema hivyo.
Mimi: Si ulichagua mitume ambao hawakusoma kama wewe ulivyokuwa kilaza wa elimu ya darasani yenye kumpatia mtu cheti, cheki umenukuliwa hadi kwenye mistari watu wakikuponda kuwa hukusoma, si unaona mwanao wa ukweli kabisa Yohana alitunukulia hilo kwenye Yohana 7:15, na wanafunzi wako waliokuwa wanawaza uvuvi tu wakati watoto wenzao wanakwenda shule nao wakinukuliwa kwenye Matendo 4:13, hivyo tabulalasa aliwachagua matabulalasa wenzake.
Yesu: Turudi kwenye swali lako maana naona unaanza kukwesheni elimu yangu na hapohapo unahitaji ufafanuzi wangu.
Mimi: Nisamehe master, hebu nipe nondo za kiufafanuzi sasa.
Yesu: Swali lililoulizwa lilihusu amri kuu katika torati na manabii, ndiyo au siyo?
Mimi: Ndiyo.
Yesu: Na mimi nilikuwa nimeshafundisha kuwa sikuja kutengua torati na manabii, bali kuzitimiliza, ndiyo au siyo?
Mimi: Ndiyo, tena hiyo nimeisoma kwenye Mathayo 5:17.
Yesu: Ewaaaa, uko sawa. Sasa kama nilishasema sikuja kutangua torati, kwa nini unanisakizia kuwa nilileta amri mpya?
Mimi: Kwa hiyo unamaanisha zile amri zako mbili, ya kumpenda Mungu na kuwapenda wanadamu hazikuwa mpya?
Yesu: Ewaaaa, hebu tusogee hapo kwenye mti tukae kivulini nikupe ujuzi.
Mimi na Yesu tukatembea kukiendea kivuli cha mti kilichokuwa karibu na tukaketi na mazungumzo yetu yakaendelea.
Yesu: Umenieleza umesoma, ulishawahi kusoma hisabati hata kiwango cha kujumlisha na kutoa?
Mimi: Siyo hesabu za kujumlisha na kutoa tu, hadi ma intergration, differentiation, mpaka ma-topology na abstract Algebra, ulishawahi kuzisoma?
Yesu: Nimekuuliza swali na wewe unajibu na kuniuliza swali, unanileta utanzania.
Yesu: Una Biblia hapo?
Mimi: Hapana nina jembe na panga tu.
Yesu: Ukifika nyumbani soma kitabu cha Warumi 13 : 8 , 9, lakini hapa nanukuu toka kichwani kwa ajili yako.
Warumi 13:8-9
[8]Msiwiwe na mtu cho chote, isipokuwa kupendana; kwa maana ampendaye mwenzake ameitimiza sheria.
Owe no man any thing, but to love one another: for he that loveth another hath fulfilled the law.
[9]Maana kule kusema, Usizini, Usiue, Usiibe, Usitamani; na ikiwapo amri nyingine yo yote, inajumlishwa katika neno hili, ya kwamba, Mpende jirani yako kama nafsi yako.
For this, Thou shalt not commit adultery, Thou shalt not kill, Thou shalt not steal, Thou shalt not bear false witness, Thou shalt not covet; and if there be any other commandment, it is briefly comprehended in this saying, namely, Thou shalt love thy neighbour as thyself.
Yesu: Kwenye hiyo aya hasa ya 9, tukifuata hesabu za kujumlisha mwandishi ambaye ni mtume wangu msomi kabisa ambaye hadi aliambiwa na mfalme Agripa kuwa kusoma kwake kwingi kumemgeuza akili (Matendo 26 : 24), mtume Paulo alileta ikwesheni ya kiarithimetikisi kama ifuatavyo.
Usizini + Usiue + Usiibe + Usitami + Amri nyingine yoyote = Mpende jirani yako kama nafsi yako.
Yesu: Sasa, zamu yako kujibu maswali yangu.
Mimi: Yalete, yalete.
Swali la 1
Yesu: Ukizini na mke au mme wa mtu, atakayeumia kihisia na kiakili ni Mungu au mke au mme wa aliyezini.
Mimi: Mke au mme ndiye ataumia kiimoshono, kihisia na huenda hata kiakili. Wengine hufikia hatua ya kuua waliozini na baada ya hapo hujimaliza pia.
Swali la 2
Yesu: Unakubaliana nami kuwa kwenye amri kumi, kuanzia amri ya tano mpaka ya kumi, amri hizo zote zinahusu mapendano ya binadamu na binadamu?
Mimi: Kwani amri hizo ya tano hadi ya kumi zinasemaje?
Yesu: Ndiyo hizo alizonukuu mtume Paulo, sema yeye hakuanza na amri ya tano, kwa faida yako amri zenyewe tuzijumlishe kwenye ikwesheni ya kiarithimetikisi kama ifuatavyo.
Amri ya tano + Amri ya sita + Amri ya saba + Amri ya nane + Amri ya tisa + Amri ya kumi = Mpende jirani yako kama nafsi yako.
Ambazo ini samare.
Waheshimu baba na mama yako + Usiue + Usizini + Usiibe + Usishuhudie uongo + Usitamani mali ya jirani yako = Mpende jirani yako kama nafsi yako.
Yesu: Ukimweshimu mzazi wako, umempenda jirani yako, binadamu mwenzako mwenye cheo cha uzazi.
Yesu: Usipozini, utakuwa umempenda binadamu mwenzako anayemiliki mme au mke ambaye ungezini naye. Kwa kutozini unakuwa umeepusha mambo ya misongo na matatizo ya kiakili yawakumbayo walioziniwa.
Yesu: Usipoiba, umempenda mwenye mali ambayo ungeiiba. Fikiria mtu ameteseka miaka ya kutosha akitafuta mali, wewe kwa siku moja tu unataka uimiliki mali yake.
Yesu: Ni hivyo hivyo kwa zile amri nne za mwanzo, zenyewe zinahusu kumpenda Mungu kama nafsi yako.
Yesu: Kwenye hesabu zetu, tuki-recall from above
Amri ya kwanza + Amri ya pili + Amri ya tatu + Amri ya nne = Mpende Bwana Mungu wako, kwa moyo wako wote, kwa roho yako na kwa akili zako zote.
Yesu: Amri ya kwanza inakataza kuwa na miungu mingine. Kitendo cha kutafuta mungu mwingine na kumuacha Mungu muumbaji, umemwacha Mungu, umependa miungu.
Yesu: Amri ya pili inakataza kuchonga sanamu na kuliweka mahali pa Mungu.
Yesu: Amri ya tatu inakataza kutaja jina la Mungu pasipo sababu za msingi.
Yesu: Ya nne inakumbusha utunzaji wa sabato ambayo Mungu anasema ni mali yake na mimi Yesu Kristo niliwafundisha hata wanafunzi wangu kuwa mimi ndiye Bwana wa Sabato.
Hivyo kwa ikwesheni ya kiarithimetikisi
Usiwe na miungu mingine + Usijifanyie sanamu ya kuchonga + Usilitaje bure jina la Bwana Mungu wako + Ikumbuke siku ya sabato uitakase = Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako na kwa akili zako zote.
Mimi: Nisipozishika, kuna madhara yoyote nitapata.
Yesu: Chukulia mfano huu. Si unayafahamu yale maspika yaitwayo poromondo.
Mimi: Nayafahamu, si yale mara nyingi wanayatumia machinga kutangazia bidhaa zao mfano "Nanunua mabetri mabovu, ya gari, ya sola pamoja na ya pikipikiiiiiiiiii".
Yesu: Ewaaaa, hayohayo. Ukilichukua ukapita mfano karibu na kituo cha Polisi huku unamtukana Mungu kwa sauti inayosaidiwa na kusikika sehemu kubwa na hilo poromondo, Polisi watakukamata?
Mimi: Nadhani watanichukulia kama mwehu flani aliyetoroka matibabu.
Yesu: Vipi kwenye hicho hicho kituo ukapita unamtukana Rais wa nchi?
Mimi: Mhhh, nadhani Tanzania bara jeki, makofi, virungu, na kufunguliwa kesi ya kumtukana Rais vitanihusu.
Yesu: Ewaaa, ila hapo umechemka sehemu moja, ni Tanganyika jeki na siyo ulivyosema wewe.
Mimi: Ni kwa vile tu mfupa hauna ulimi.
Yesu: Kwa nini aliyetukana Mungu aachwe na aliyetukana Rais aadabishwe?
Mimi: Mungu anahitaji kupruviwa uwepo wake, sasa kwa mfano polisi anikamate namtukana Mungu, akifika mahakamani akaulizwa huyo Mungu niliyemtukana anakaa wapi, si atabaki anatoa macho kama kenge anayejifungua.
Yesu: Ewaaa, lakini kwa kuwa Rais ni binadamu anayeonekana, ndiyo maana utashughulikiwa papendikulale.
Yesu: Hapo nchini kwenu, mtu akiiba atafanywaje?
Mimi: Akiwa mwenye bahati, atakingiwa kifua na wakubwa, akiwa na bahati ya wastani atashitakiwa mahakamani, akiwa hana bahati akakutana na wenye hasira kali, atapigwa mawe, atavishwa tairi, mafuta yataletwa na kumwagwa kwenye tairi, moto utawashwa, na habari yake itaishia hapo.
Yesu: Mtu akizini.
Mimi: Mwenye bahati (asiyekamatwa au hata kuhisiwa au akiwa na mme au mke zumbukuku) atapeta tu, mwenye bahati ya wastani ataendewa kwa mafundi na kupewa mimba hata kama ni mwanamme, asiye na bahati (hasa mwanamme) atageuzwa malindalesi, dushe kukatwa na kubanikwa kama mshikaki na watu kulila mbele yake.
Yesu: Hivyo, ukimtukana Mungu, au hata ukitoa kufuru lolote kwa kusema mambo kama vile Mungu hayupo, chonga sanamu liabudu, na vitu vyote kinyume cha zile amri kumi, no wani wili kea, hakuna kesi utafunguliwa mahakamani kwamba umemtukana Mungu, du yu no whai.
Mimi: Sijui
Yesu: Ni kwa sababu, hizo amri zinamhusu Mungu mwenyewe, hivyo hakuna binadamu mwenye mamlaka ya kumuwajibisha mwenzake kisa amemtukana Mungu, hashiki sabato, kajifanyia sanamu n.k, hizo mtoa adhabu ni Mungu. Hivyo amri nne zenye summary ya "mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote... " mtoa adhabu ni Mungu mwenyewe.
Yesu: Lakini ni tofauti na amri zile za upendano wa kibinadamu, zinawahusu binadamu ambao wanaonana, hakuna haja ya kutafuta prufu ya kuthibitisha kama mme au mke wa mtu anaegizisti, hivyo ukimkosea binadamu mwenzako lazima utawajibishwa, utawajibishwa kwa kupelekwa mahakamani au hata kuuliwa papo kwa papo.
Yesu: Kwa ufupi, amri nne za kumhusu Mungu, adhabu za kuzikiuka zitatolewa na Mungu mwenyewe, amri sita zinazohusu mapendano ya wanadamu adhabu ya kwanza mnamalizana ama kibabe au mahakamani hapa hapa duniani na baadaye Mungu pia atatoa adhabu yake.
Mimi: Kwa sentensi yenye maneno yasiyozidi matano, unanishaurije, yaani nipe code ya kuziishi hizo amri maana nimeona kuna pande mbili, kumkosea Mungu au binadamu, bora kwa Mungu kwenyewe hakuna adhabu ya papo kwa papo mpaka wakati ulioamriwa, ila binadamu nimeona wanatoa adhabu za papo kwa papo tena zingine za kikatili sana mpaka najiuliza hao ni binadamu?
Yesu: Shika amri hutaona neno baya.
Mimi: Kama kawaida yako kunukuu toka kwenye maandiko, maana hapo naona umenukuu toka kitabu cha Muhubiri 8:5.
Yesu: Ulikuwa wakati mzuri baina yetu kwa siku ya leo, nitakutembelea tena wiki ijayo, siku, muda na mahali hapa hapa kama ilivyokuwa leo, wahi nyumbani usije kuta chakula kimepoa.
Mimi: Karibu sana Yesu Kristo nyumbani kwangu.
Yesu: Asante sana.
Baada ya mazungumzo hayo, Yesu alipanda chombo chake cha usafiri (wingu), na kwa spidi ya mwanga akatoweka machoni pangu.
Wakuu, kwa kuwa Bwana Yesu Kristo ameniahidi kunitembelea tena wiki ijayo, nitawaletea kitakachojiri kwenye mazungumzo kati yetu hapa hapa JamiiForums saa mbili kamili asubuhi siku ya jumamosi.
Hata hivo ni utunzi, Yesu mwenye kujua idadi ya nywele za muhusika hawezi kushindwa kutambua amri mpya anayozungumzia mtumishi ni ipi!,.eti mpaka amfafanulie ....... Lugha ,eti eti ulikuwa kilaza ndio mana ukachagua vilaza wenzio😆😆😆😆hata hivo utunzi mzuri,umefanikiwa saana kuwasilisha Nini maana ya UPENDO , kwa mtazamo wa kimaboresho kumuelekea Yesu, ,,,,,, ila punguza masikhara, yesu siyo Ali Kamwe !!Isije ikawa ni utungaji tu maana wenye akili pevu inayopembua na kutafsi mambo tusoma between lines kubaini uhalisia au filosofia ya theolojia tu. Tuna roho ya kumbambanua mambo ya kiroho kwa usahihi bila kuingiza dogma za nje
Ni utungaji wa nje na mawazo ya kichwani mwake!Isije ikawa ni utungaji tu maana wenye akili pevu inayopembua na kutafsi mambo tusoma between lines kubaini uhalisia au filosofia ya theolojia tu. Tuna roho ya kumbambanua mambo ya kiroho kwa usahihi bila kuingiza dogma za nje
Kama sikosei Mapenzi ya Mungu ni wote tuwe na Uzima.Majibu yangu ni haya ,Sababu ya kushika sheria ni kutii mapenzi ya Mungu.
Barnabas Ameamua Kuwa Tapeli Kwa Kutumia Jina La Babu Yake YesuYesu Ana misemo ya kindengereko 😂😂
Hapa Mungu alifuta nini?Nitakujibu,lakini maswali yangu huko juu yamekushinda kujibu ??
Nalujibu kwa mujibu wa maandiko matakatifu
Unauliza Sheria za vyakula ni Amri za Mungu au Musa?
Sheria za vyakula zinatoka kwa Mungu. Kumbukumbu la Torati 14:3-21 na Mambo ya Walawi 11 zinaonyesha kuwa Mungu mwenyewe alitoa sheria hizi kwa Waisraeli kupitia Musa. Katika Mambo ya Walawi 11:44-45, Mungu anasema:
"Kwa kuwa mimi ndimi Bwana Mungu wenu; takaseni nafsi zenu, mwe watakatifu; kwa kuwa mimi ni mtakatifu..."
Hii inaonyesha kuwa sheria hizi zilitolewa kwa kusudi la kutofautisha watu wa Mungu na mataifa mengine, na zilikuwa sehemu ya utakatifu.
Umeuliza pia Sadaka za dhambi ni za Musa au Mungu?
Sadaka za dhambi zilianzishwa na Mungu mwenyewe. Soma Mambo ya Walawi 4:1-35, ambapo Mungu anatoa maagizo ya moja kwa moja kuhusu sadaka za dhambi kwa Waisraeli. Musa alihusika tu kama mpokezi na mpitishaji wa sheria hizi, lakini chanzo chake ni Mungu. Sadaka hizi zilikuwa za muda, zikielekeza kwa sadaka ya Yesu Kristo kama upatanisho wa dhambi zetu zote (Waebrania 10:1-10).
Unauliza Tena Zaka ni za Musa au Mungu?, Tena hapa nyie mnaojifanya hamfati Sheria ndio mnanichekeshaga sana ,maana mnasisitizaga fungu la kumi kwa kutumia Torati na vitabu kama vya Malaki,
Zaka zinatoka kwa Mungu. Katika Mambo ya Walawi 27:30, inasema:
"Kila zaka ya nchi, kama ni mbegu ya nchi, au kama ni matunda ya nchi, ni ya Bwana; ni takatifu kwa Bwana."
Hili linaonyesha wazi kuwa agizo la kutoa zaka lilitoka kwa Mungu. Musa aliweka sheria hizi katika mfumo wa taifa la Israeli, lakini msingi wa sheria ni wa kimungu.
Umeuliza Kuhusu Mavazi ni Musa au Mungu?
Sheria za mavazi pia zilikuwa za Mungu, zilizotolewa kupitia Musa. Katika Kumbukumbu la Torati 22:11-12, Mungu alitoa maagizo maalum kuhusu mavazi, kama vile kutovaa mavazi yaliyotengenezwa kwa mchanganyiko wa nyuzi mbili tofauti. Agizo hili lilikuwa sehemu ya utaratibu wa kuwaweka Waisraeli tofauti na mataifa mengine.
Unauliza Kwanini unashika Sheria?
Majibu yangu ni haya ,Sababu ya kushika sheria ni kutii mapenzi ya Mungu.
Yesu alisema:
"Kama mnanipenda, mtazishika amri zangu" (Yohana 14:15).
Labda wenzetu hamumpendi Yesu ....
Hata hivyo, tunapaswa kuelewa kuwa sheria za Agano la Kale zilizokuwa kivuli cha mambo bora zaidi yajayo, ambayo yametimia ndani ya Kristo zimeelezwa vizuri kabisa na maandiko, ila Shida yenu mkisikia Amri,Sheria mnakimbilia Hadi Amri kumi, (Waebrania 10:1).
Sijui hata kama Unajua Yohana alioneshwa Sanduku la Agano lenye amri kumi huko mbinguni, Soma Ufunuo 10
Jambo lililo takatifu na jema kwanini liwe njia ya Mauti? Kwa nini lihusishwe na mauti?2. Warumi 7:12 inasema torati ni takatifu, ya haki, na njema. Je, ni wapi maandiko yanaposema kwamba jambo lililo takatifu, haki, na njema halifai tena?
Paulo hakuhimiza torati badala yake aliwaambia wale waliochini ya Torati wako chini ya laana (Gal 3 : 10)3. Ikiwa torati ni “huduma ya mauti,” kwa nini Paulo aliihimiza bado kama mwalimu wa kutupeleka kwa Kristo (Wagalatia 3:24)? Je, unawezaje kuelezea jukumu lake baada ya wokovu?
ULOKOLE NI UKAFIRI TU KAMA UHISIHARAMU TU HAKUNA JIPYAIsije ikawa ni utungaji tu maana wenye akili pevu inayopembua na kutafsi mambo tusoma between lines kubaini uhalisia au filosofia ya theolojia tu. Tuna roho ya kumbambanua mambo ya kiroho kwa usahihi bila kuingiza dogma za nje
Nitaondokaje duniani sasa wakati ndiyo kwanza kunazidi kuchangamka.Kwanini hukumuambia muondoke naye uachane na hizi hekaheka hapa duniani...
Nakushauri uachane kabisa na bangi za Njombe, rudi kwenye bangi za Gezaulole sio kali kama za Njombe!Wakuu, kwa kuwa katika muda huu, sisi wenye mamlaka ya kusimamia na kuandaa wataalamu wa baadae (walimu) tupo likizo. Ninaitumia likizo hii kwa kwenda shambani ili kuzalisha chakula.
Wakuu, jana nilibahatika kukutana na Yesu ana kwa ana, nilikuwa natoka shambani narudi nyumbani majira ya mchana kwa ajili ya kupata la mwidebe (kula).
Ghafla, mbele yangu kwa juu nikashangaa wingu safi jeupe linashuka kwa kasi katika ueleko nilipo, punde si muda, likanifikia, lahaula kumbe ulikuwa ni usafiri uliomsafirisha Yesu kutoka mbinguni kuja kuonana na mimi.
Alinikuta njiani. Wakuu, kwa kuwa kuna mambo mengi huwa yananitatiza kila ninaposoma Biblia hasa vitabu vinavyoelezea utumishi wa Yesu Kristo akiwa hapa duniani, ilibidi niruke fasta sana na fursa adhimu kama ile kwa kuongea na kumuomba ufafanuzi kwa yale yanitatizayo.
Mazungumzo baina yangu na Yesu Kristo yalikuwa kama ifuatavyo.
Mimi: Shikamoo Bwana mkubwa Yesu Kristo mwana wa Mungu aliye hai.
Yesu: Marhaba mdogo wangu na rafiki yangu Barnabas Mashamba.
Mimi: Hee, unalijua hadi jina langu bila kukuambia.
Yesu: Siyo jina tu, najua hadi idadi ya nywele zako kichwani. By the way, kama wewe umefahamu jina langu pasipo kukutajia, kitu gani kinafanya mimi nisilijue jina lako?
Mimi: Eniwei hivi Yesu Kristo, kwanini ulianzisha amri mpya? Si baba yako kupitia Musa alikuwa ametupatia amri kumi tena akiwa ameziandika kwa kidole chake mwenyewe kwenye mbao mbili za mawe?
Yesu: Amri gani mpya ambayo nilileta?
Mimi: Siku ulipoulizwa swali kuhusu amri ipi ni kuu katika torati na manabii, si ulileta amri mpya wewe.
Mazungumzo yangu na Yesu kristo yalitokana na yale niliyosoma katika kitabu kile cha Mathayo sura ya 22
Mathayo 22:35-40
[35]Mmoja wao, mwana-sheria, akamwuliza, akimjaribu;
Then one of them, which was a lawyer, asked him a question, tempting him, and saying,
[36]Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu?
Master, which is the great commandment in the law?
[37]Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote.
Jesus said unto him, Thou shalt love the Lord thy God with all thy heart, and with all thy soul, and with all thy mind.
[38]Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.
This is the first and great commandment.
[39]Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako.
And the second is like unto it, Thou shalt love thy neighbour as thyself.
[40]Katika amri hizi mbili hutegemea torati yote na manabii.
On these two commandments hang all the law and the prophets.
Yesu: Umesema swali lilihusu amri ipi kuu katika torati na manabii, right?
Mimi: exactly.
Yesu: Wakati natoa jibu, nilisema naleta amri mpya, au nilitoa jibu moja kwa moja kwa swali nililoulizwa kuhusu amri kuu katika torati na manabii?
Mimi: Sijui
Yesu: Hujui kwa kuwa hupendi kusoma.
Mimi: Sasa hapo Yesu naona unanitukana bila kujua elimu yangu, hivi kwanza wewe Yesu ulisoma ukahitimu hata darasa la kwanza?
Yesu: Hapana, sikubahatika kusoma elimu rasmi ya darasani ila nilijua kusoma na kuandika.
Mimi: Umesema kweli maana hata ulifuata msemo wa ndege wafananao huruka pamoja.
Yesu: Kwa nini unasema hivyo.
Mimi: Si ulichagua mitume ambao hawakusoma kama wewe ulivyokuwa kilaza wa elimu ya darasani yenye kumpatia mtu cheti, cheki umenukuliwa hadi kwenye mistari watu wakikuponda kuwa hukusoma, si unaona mwanao wa ukweli kabisa Yohana alitunukulia hilo kwenye Yohana 7:15, na wanafunzi wako waliokuwa wanawaza uvuvi tu wakati watoto wenzao wanakwenda shule nao wakinukuliwa kwenye Matendo 4:13, hivyo tabulalasa aliwachagua matabulalasa wenzake.
Yesu: Turudi kwenye swali lako maana naona unaanza kukwesheni elimu yangu na hapohapo unahitaji ufafanuzi wangu.
Mimi: Nisamehe master, hebu nipe nondo za kiufafanuzi sasa.
Yesu: Swali lililoulizwa lilihusu amri kuu katika torati na manabii, ndiyo au siyo?
Mimi: Ndiyo.
Yesu: Na mimi nilikuwa nimeshafundisha kuwa sikuja kutengua torati na manabii, bali kuzitimiliza, ndiyo au siyo?
Mimi: Ndiyo, tena hiyo nimeisoma kwenye Mathayo 5:17.
Yesu: Ewaaaa, uko sawa. Sasa kama nilishasema sikuja kutangua torati, kwa nini unanisakizia kuwa nilileta amri mpya?
Mimi: Kwa hiyo unamaanisha zile amri zako mbili, ya kumpenda Mungu na kuwapenda wanadamu hazikuwa mpya?
Yesu: Ewaaaa, hebu tusogee hapo kwenye mti tukae kivulini nikupe ujuzi.
Mimi na Yesu tukatembea kukiendea kivuli cha mti kilichokuwa karibu na tukaketi na mazungumzo yetu yakaendelea.
Yesu: Umenieleza umesoma, ulishawahi kusoma hisabati hata kiwango cha kujumlisha na kutoa?
Mimi: Siyo hesabu za kujumlisha na kutoa tu, hadi ma intergration, differentiation, mpaka ma-topology na abstract Algebra, ulishawahi kuzisoma?
Yesu: Nimekuuliza swali na wewe unajibu na kuniuliza swali, unanileta utanzania.
Yesu: Una Biblia hapo?
Mimi: Hapana nina jembe na panga tu.
Yesu: Ukifika nyumbani soma kitabu cha Warumi 13 : 8 , 9, lakini hapa nanukuu toka kichwani kwa ajili yako.
Warumi 13:8-9
[8]Msiwiwe na mtu cho chote, isipokuwa kupendana; kwa maana ampendaye mwenzake ameitimiza sheria.
Owe no man any thing, but to love one another: for he that loveth another hath fulfilled the law.
[9]Maana kule kusema, Usizini, Usiue, Usiibe, Usitamani; na ikiwapo amri nyingine yo yote, inajumlishwa katika neno hili, ya kwamba, Mpende jirani yako kama nafsi yako.
For this, Thou shalt not commit adultery, Thou shalt not kill, Thou shalt not steal, Thou shalt not bear false witness, Thou shalt not covet; and if there be any other commandment, it is briefly comprehended in this saying, namely, Thou shalt love thy neighbour as thyself.
Yesu: Kwenye hiyo aya hasa ya 9, tukifuata hesabu za kujumlisha mwandishi ambaye ni mtume wangu msomi kabisa ambaye hadi aliambiwa na mfalme Agripa kuwa kusoma kwake kwingi kumemgeuza akili (Matendo 26 : 24), mtume Paulo alileta ikwesheni ya kiarithimetikisi kama ifuatavyo.
Usizini + Usiue + Usiibe + Usitami + Amri nyingine yoyote = Mpende jirani yako kama nafsi yako.
Yesu: Sasa, zamu yako kujibu maswali yangu.
Mimi: Yalete, yalete.
Swali la 1
Yesu: Ukizini na mke au mme wa mtu, atakayeumia kihisia na kiakili ni Mungu au mke au mme wa aliyezini.
Mimi: Mke au mme ndiye ataumia kiimoshono, kihisia na huenda hata kiakili. Wengine hufikia hatua ya kuua waliozini na baada ya hapo hujimaliza pia.
Swali la 2
Yesu: Unakubaliana nami kuwa kwenye amri kumi, kuanzia amri ya tano mpaka ya kumi, amri hizo zote zinahusu mapendano ya binadamu na binadamu?
Mimi: Kwani amri hizo ya tano hadi ya kumi zinasemaje?
Yesu: Ndiyo hizo alizonukuu mtume Paulo, sema yeye hakuanza na amri ya tano, kwa faida yako amri zenyewe tuzijumlishe kwenye ikwesheni ya kiarithimetikisi kama ifuatavyo.
Amri ya tano + Amri ya sita + Amri ya saba + Amri ya nane + Amri ya tisa + Amri ya kumi = Mpende jirani yako kama nafsi yako.
Ambazo ini samare.
Waheshimu baba na mama yako + Usiue + Usizini + Usiibe + Usishuhudie uongo + Usitamani mali ya jirani yako = Mpende jirani yako kama nafsi yako.
Yesu: Ukimweshimu mzazi wako, umempenda jirani yako, binadamu mwenzako mwenye cheo cha uzazi.
Yesu: Usipozini, utakuwa umempenda binadamu mwenzako anayemiliki mme au mke ambaye ungezini naye. Kwa kutozini unakuwa umeepusha mambo ya misongo na matatizo ya kiakili yawakumbayo walioziniwa.
Yesu: Usipoiba, umempenda mwenye mali ambayo ungeiiba. Fikiria mtu ameteseka miaka ya kutosha akitafuta mali, wewe kwa siku moja tu unataka uimiliki mali yake.
Yesu: Ni hivyo hivyo kwa zile amri nne za mwanzo, zenyewe zinahusu kumpenda Mungu kama nafsi yako.
Yesu: Kwenye hesabu zetu, tuki-recall from above
Amri ya kwanza + Amri ya pili + Amri ya tatu + Amri ya nne = Mpende Bwana Mungu wako, kwa moyo wako wote, kwa roho yako na kwa akili zako zote.
Yesu: Amri ya kwanza inakataza kuwa na miungu mingine. Kitendo cha kutafuta mungu mwingine na kumuacha Mungu muumbaji, umemwacha Mungu, umependa miungu.
Yesu: Amri ya pili inakataza kuchonga sanamu na kuliweka mahali pa Mungu.
Yesu: Amri ya tatu inakataza kutaja jina la Mungu pasipo sababu za msingi.
Yesu: Ya nne inakumbusha utunzaji wa sabato ambayo Mungu anasema ni mali yake na mimi Yesu Kristo niliwafundisha hata wanafunzi wangu kuwa mimi ndiye Bwana wa Sabato.
Hivyo kwa ikwesheni ya kiarithimetikisi
Usiwe na miungu mingine + Usijifanyie sanamu ya kuchonga + Usilitaje bure jina la Bwana Mungu wako + Ikumbuke siku ya sabato uitakase = Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako na kwa akili zako zote.
Mimi: Nisipozishika, kuna madhara yoyote nitapata.
Yesu: Chukulia mfano huu. Si unayafahamu yale maspika yaitwayo poromondo.
Mimi: Nayafahamu, si yale mara nyingi wanayatumia machinga kutangazia bidhaa zao mfano "Nanunua mabetri mabovu, ya gari, ya sola pamoja na ya pikipikiiiiiiiiii".
Yesu: Ewaaaa, hayohayo. Ukilichukua ukapita mfano karibu na kituo cha Polisi huku unamtukana Mungu kwa sauti inayosaidiwa na kusikika sehemu kubwa na hilo poromondo, Polisi watakukamata?
Mimi: Nadhani watanichukulia kama mwehu flani aliyetoroka matibabu.
Yesu: Vipi kwenye hicho hicho kituo ukapita unamtukana Rais wa nchi?
Mimi: Mhhh, nadhani Tanzania bara jeki, makofi, virungu, na kufunguliwa kesi ya kumtukana Rais vitanihusu.
Yesu: Ewaaa, ila hapo umechemka sehemu moja, ni Tanganyika jeki na siyo ulivyosema wewe.
Mimi: Ni kwa vile tu mfupa hauna ulimi.
Yesu: Kwa nini aliyetukana Mungu aachwe na aliyetukana Rais aadabishwe?
Mimi: Mungu anahitaji kupruviwa uwepo wake, sasa kwa mfano polisi anikamate namtukana Mungu, akifika mahakamani akaulizwa huyo Mungu niliyemtukana anakaa wapi, si atabaki anatoa macho kama kenge anayejifungua.
Yesu: Ewaaa, lakini kwa kuwa Rais ni binadamu anayeonekana, ndiyo maana utashughulikiwa papendikulale.
Yesu: Hapo nchini kwenu, mtu akiiba atafanywaje?
Mimi: Akiwa mwenye bahati, atakingiwa kifua na wakubwa, akiwa na bahati ya wastani atashitakiwa mahakamani, akiwa hana bahati akakutana na wenye hasira kali, atapigwa mawe, atavishwa tairi, mafuta yataletwa na kumwagwa kwenye tairi, moto utawashwa, na habari yake itaishia hapo.
Yesu: Mtu akizini.
Mimi: Mwenye bahati (asiyekamatwa au hata kuhisiwa au akiwa na mme au mke zumbukuku) atapeta tu, mwenye bahati ya wastani ataendewa kwa mafundi na kupewa mimba hata kama ni mwanamme, asiye na bahati (hasa mwanamme) atageuzwa malindalesi, dushe kukatwa na kubanikwa kama mshikaki na watu kulila mbele yake.
Yesu: Hivyo, ukimtukana Mungu, au hata ukitoa kufuru lolote kwa kusema mambo kama vile Mungu hayupo, chonga sanamu liabudu, na vitu vyote kinyume cha zile amri kumi, no wani wili kea, hakuna kesi utafunguliwa mahakamani kwamba umemtukana Mungu, du yu no whai.
Mimi: Sijui
Yesu: Ni kwa sababu, hizo amri zinamhusu Mungu mwenyewe, hivyo hakuna binadamu mwenye mamlaka ya kumuwajibisha mwenzake kisa amemtukana Mungu, hashiki sabato, kajifanyia sanamu n.k, hizo mtoa adhabu ni Mungu. Hivyo amri nne zenye summary ya "mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote... " mtoa adhabu ni Mungu mwenyewe.
Yesu: Lakini ni tofauti na amri zile za upendano wa kibinadamu, zinawahusu binadamu ambao wanaonana, hakuna haja ya kutafuta prufu ya kuthibitisha kama mme au mke wa mtu anaegizisti, hivyo ukimkosea binadamu mwenzako lazima utawajibishwa, utawajibishwa kwa kupelekwa mahakamani au hata kuuliwa papo kwa papo.
Yesu: Kwa ufupi, amri nne za kumhusu Mungu, adhabu za kuzikiuka zitatolewa na Mungu mwenyewe, amri sita zinazohusu mapendano ya wanadamu adhabu ya kwanza mnamalizana ama kibabe au mahakamani hapa hapa duniani na baadaye Mungu pia atatoa adhabu yake.
Mimi: Kwa sentensi yenye maneno yasiyozidi matano, unanishaurije, yaani nipe code ya kuziishi hizo amri maana nimeona kuna pande mbili, kumkosea Mungu au binadamu, bora kwa Mungu kwenyewe hakuna adhabu ya papo kwa papo mpaka wakati ulioamriwa, ila binadamu nimeona wanatoa adhabu za papo kwa papo tena zingine za kikatili sana mpaka najiuliza hao ni binadamu?
Yesu: Shika amri hutaona neno baya.
Mimi: Kama kawaida yako kunukuu toka kwenye maandiko, maana hapo naona umenukuu toka kitabu cha Muhubiri 8:5.
Yesu: Ulikuwa wakati mzuri baina yetu kwa siku ya leo, nitakutembelea tena wiki ijayo, siku, muda na mahali hapa hapa kama ilivyokuwa leo, wahi nyumbani usije kuta chakula kimepoa.
Mimi: Karibu sana Yesu Kristo nyumbani kwangu.
Yesu: Asante sana.
Baada ya mazungumzo hayo, Yesu alipanda chombo chake cha usafiri (wingu), na kwa spidi ya mwanga akatoweka machoni pangu.
Wakuu, kwa kuwa Bwana Yesu Kristo ameniahidi kunitembelea tena wiki ijayo, nitawaletea kitakachojiri kwenye mazungumzo kati yetu hapa hapa JamiiForums saa mbili kamili asubuhi siku ya jumamosi.