Jana nilifanya mazungumzo na Yesu Kristo na kumwomba ufafanuzi kuhusu amri zake kuu mbili za upendo. Na hapa nakuletea mazungumzo hayo kwa ufupi

Kweli dunia ina mambo
America nao wameandaa Biblia mpya newest na inatoka 2025
Kuna mengi wameandika humu
Nasubiri nikisome kama kitabu
 
Unasoma maandiko kwa kukurupuka, matumizi ya neno “wote” kumaanisha kila aliyemtangulia, muktadha wa maandiko unaonyesha Yesu alikuwa akizungumzia manabii na torati waliotangulia kumshuhudia Yeye, si kwamba kila aliyemtangulia hakuwa na thamani.

Soma maandiko taratibu ,Mathayo 11:13 inasema,

“Kwa maana manabii wote na torati walitabiri mpaka wakati wa Yohana.” Hii inathibitisha kwamba torati na manabii walikuwa na jukumu la kumwandaa mtu kumpokea Kristo. Yesu mwenyewe alisema, “Msidhani kwamba nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kuitangua, bali kuitimiliza” (Mathayo 5:17).

Ikiwa Yesu hakuitangua torati, kwa nini wewe unadai kuwa haituhusu tena?

Kuhusu 2 Wakorintho 3:7, ambapo Paulo anaita torati "huduma ya mauti," muktadha ni muhimu. Paulo anasema kwamba torati bila neema ya Kristo huleta hukumu kwa sababu dhambi inaonyeshwa wazi kupitia torati. Hata hivyo, hiyo haimaanishi kuwa torati haikuwa na thamani.

Warumi 7:12 inasema, “Kwa hiyo torati ni takatifu, na ile amri ni takatifu, ya haki, na njema.” Huduma ya mauti inahusiana na jinsi torati inavyofanya dhambi ijulikane, lakini hilo linapaswa kuongoza kwa wokovu kupitia Kristo (Warumi 8:3-4).

Kwa hiyo, si sahihi kusema torati haifai tena, bali ni kwa neema tunatimiza haki ya torati.

Kuhusu Warumi 7:10-13, Paulo anaeleza wazi kwamba torati yenyewe si mbaya. Dhambi hutumia torati kudhihirisha hatia ndani ya wanadamu. Hii inamaanisha torati ni kama kioo kinachoonyesha hali yetu ya dhambi. Paulo hakusema kwamba torati imemwua bali dhambi kupitia torati ilimletea mauti. Torati inabaki kuwa "mwalimu" anayetupeleka kwa Kristo (Wagalatia 3:24). Kwa hivyo, si sahihi kusema kuwa tumefika kwa Kristo na basi torati haina umuhimu.

Nauliza tena

1. Ikiwa Yesu alisema hatakuja kuitangua torati bali kuitimiliza (Mathayo 5:17), unathibitishaje kwamba torati haina maana tena kwa waamini?


2. Warumi 7:12 inasema torati ni takatifu, ya haki, na njema. Je, ni wapi maandiko yanaposema kwamba jambo lililo takatifu, haki, na njema halifai tena?


3. Ikiwa torati ni “huduma ya mauti,” kwa nini Paulo aliihimiza bado kama mwalimu wa kutupeleka kwa Kristo (Wagalatia 3:24)? Je, unawezaje kuelezea jukumu lake baada ya wokovu?
 
Una uelewa mdogo kuhusu Amri za Mungu, amri za Musa , hili somo hamtaki kujifunza ndio maana mnachanganya kila kitu
Sheria za vyakula ni Amri za Mungu ama Musa?

Sadaka za dhambi ni Musa ama Mungu?

Zaka ni Musa ama Mungu?

Mavazi ni Musa/Mungu?

Jibu hapo ili tumalize mjadala.

Swali langu la Mwisho kabisa kwanini unashika Sheria?
 
Sheria za vyakula ni Amri za Mungu ama Musa?

Sadaka za dhambi ni Musa ama Mungu?

Zaka ni Musa ama Mungu?

Mavazi ni Musa/Mungu?

Jibu hapo ili tumalize mjadala.

Swali langu la Mwisho kabisa kwanini unashika Sheria?
Nitakujibu,lakini maswali yangu huko juu yamekushinda kujibu ??

Nalujibu kwa mujibu wa maandiko matakatifu

Unauliza Sheria za vyakula ni Amri za Mungu au Musa?
Sheria za vyakula zinatoka kwa Mungu. Kumbukumbu la Torati 14:3-21 na Mambo ya Walawi 11 zinaonyesha kuwa Mungu mwenyewe alitoa sheria hizi kwa Waisraeli kupitia Musa. Katika Mambo ya Walawi 11:44-45, Mungu anasema:
"Kwa kuwa mimi ndimi Bwana Mungu wenu; takaseni nafsi zenu, mwe watakatifu; kwa kuwa mimi ni mtakatifu..."
Hii inaonyesha kuwa sheria hizi zilitolewa kwa kusudi la kutofautisha watu wa Mungu na mataifa mengine, na zilikuwa sehemu ya utakatifu.

Umeuliza pia Sadaka za dhambi ni za Musa au Mungu?
Sadaka za dhambi zilianzishwa na Mungu mwenyewe. Soma Mambo ya Walawi 4:1-35, ambapo Mungu anatoa maagizo ya moja kwa moja kuhusu sadaka za dhambi kwa Waisraeli. Musa alihusika tu kama mpokezi na mpitishaji wa sheria hizi, lakini chanzo chake ni Mungu. Sadaka hizi zilikuwa za muda, zikielekeza kwa sadaka ya Yesu Kristo kama upatanisho wa dhambi zetu zote (Waebrania 10:1-10).

Unauliza Tena Zaka ni za Musa au Mungu?, Tena hapa nyie mnaojifanya hamfati Sheria ndio mnanichekeshaga sana ,maana mnasisitizaga fungu la kumi kwa kutumia Torati na vitabu kama vya Malaki,

Zaka zinatoka kwa Mungu. Katika Mambo ya Walawi 27:30, inasema:
"Kila zaka ya nchi, kama ni mbegu ya nchi, au kama ni matunda ya nchi, ni ya Bwana; ni takatifu kwa Bwana."
Hili linaonyesha wazi kuwa agizo la kutoa zaka lilitoka kwa Mungu. Musa aliweka sheria hizi katika mfumo wa taifa la Israeli, lakini msingi wa sheria ni wa kimungu.

Umeuliza Kuhusu Mavazi ni Musa au Mungu?
Sheria za mavazi pia zilikuwa za Mungu, zilizotolewa kupitia Musa. Katika Kumbukumbu la Torati 22:11-12, Mungu alitoa maagizo maalum kuhusu mavazi, kama vile kutovaa mavazi yaliyotengenezwa kwa mchanganyiko wa nyuzi mbili tofauti. Agizo hili lilikuwa sehemu ya utaratibu wa kuwaweka Waisraeli tofauti na mataifa mengine.


Unauliza Kwanini unashika Sheria?

Majibu yangu ni haya ,Sababu ya kushika sheria ni kutii mapenzi ya Mungu.

Yesu alisema:

"Kama mnanipenda, mtazishika amri zangu" (Yohana 14:15).

Labda wenzetu hamumpendi Yesu ....


Hata hivyo, tunapaswa kuelewa kuwa sheria za Agano la Kale zilizokuwa kivuli cha mambo bora zaidi yajayo, ambayo yametimia ndani ya Kristo zimeelezwa vizuri kabisa na maandiko, ila Shida yenu mkisikia Amri,Sheria mnakimbilia Hadi Amri kumi, (Waebrania 10:1).

Sijui hata kama Unajua Yohana alioneshwa Sanduku la Agano lenye amri kumi huko mbinguni, Soma Ufunuo 10
 
1. Ikiwa Sheria ni mbaya na kazi yake ni kuua, kwa nini Yesu alisema katika Mathayo 5:17-18 kwamba hakuja kuitangua bali kuitimiza, na hata chembe ndogo ya sheria haitaondolewa mpaka yote yatimie?
Mpaka yote Yatimie. Yapi? Mpaka yote yatimie maana yake alimaanisha yakishatimia inaondolewa.

Ukiyajua hayo yaliyotakiwa kutimia, kama yalitimia maana yake Torati iliondoka kwa sababu ilikuwepo tu mpaka yote yatimie.

Tunarudi palepale... Yale yaliyotakiwa kutumia ni sisi kufika kwa Imani/Kristo kama tumefika basi yametimia torati inaondoka kwa kuwa yametimia.


1. Ikiwa Sheria inatufanya tuwe vipofu au tulaumiwe, kwa nini Yesu alisema hakuja kutangua Sheria bali kuitimiliza (Mathayo 5:17)? Je, hili halionyeshi kuwa Sheria ina nafasi muhimu katika kuelekeza watu kwa Kristo?
Watu wakishafika kwa Kristo wanafanyaje? Yaani wameshika Sabato/sheria wameona kumbe haiwezi kuwaokoa badala yake wanazidi kuivunja inabidi waende kwa Kristo wakishafika kwa Kristo wanafanyaje?

Kwamba Kristo atawaambia nendeni mkajikaze muendelee kushika🤣 Unachekesha.
 
Saw
Sawa mwadventista msabato! hongera kwa ubunifu wako!
 
Isije ikawa ni utungaji tu maana wenye akili pevu inayopembua na kutafsi mambo tusoma between lines kubaini uhalisia au filosofia ya theolojia tu. Tuna roho ya kumbambanua mambo ya kiroho kwa usahihi bila kuingiza dogma za nje
Hata hivo ni utunzi, Yesu mwenye kujua idadi ya nywele za muhusika hawezi kushindwa kutambua amri mpya anayozungumzia mtumishi ni ipi!,.eti mpaka amfafanulie ....... Lugha ,eti eti ulikuwa kilaza ndio mana ukachagua vilaza wenzio😆😆😆😆hata hivo utunzi mzuri,umefanikiwa saana kuwasilisha Nini maana ya UPENDO , kwa mtazamo wa kimaboresho kumuelekea Yesu, ,,,,,, ila punguza masikhara, yesu siyo Ali Kamwe !!
 
N
Isije ikawa ni utungaji tu maana wenye akili pevu inayopembua na kutafsi mambo tusoma between lines kubaini uhalisia au filosofia ya theolojia tu. Tuna roho ya kumbambanua mambo ya kiroho kwa usahihi bila kuingiza dogma za nje
Ni utungaji wa nje na mawazo ya kichwani mwake!
 
Hapa Mungu alifuta nini?

Kol 2:13-14 SUV
[13] Na ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutokutahiriwa kwa mwili wenu, aliwafanya hai pamoja naye, akiisha kutusamehe makosa yote; [14] akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutushitaki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani;

Kama mtu asituhukumu kwa vyakula, ama sabato. Inamaana hata Mungu mwenyewe hatuhukumu kwa mambo hayo sababu kuna kitu alifuta hapo juu...

Kol 2:16 SUV
[16] Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;
 
2. Warumi 7:12 inasema torati ni takatifu, ya haki, na njema. Je, ni wapi maandiko yanaposema kwamba jambo lililo takatifu, haki, na njema halifai tena?
Jambo lililo takatifu na jema kwanini liwe njia ya Mauti? Kwa nini lihusishwe na mauti?

Sheria ➡️ Dhambi ➡️ Mauti

3. Ikiwa torati ni “huduma ya mauti,” kwa nini Paulo aliihimiza bado kama mwalimu wa kutupeleka kwa Kristo (Wagalatia 3:24)? Je, unawezaje kuelezea jukumu lake baada ya wokovu?
Paulo hakuhimiza torati badala yake aliwaambia wale waliochini ya Torati wako chini ya laana (Gal 3 : 10)

Baada ya Kugundua kweli, kumjua Yesu Paulo aliyaona mambo yote aliyokuwa anafanya ya sheria ni kama MAVI (flp 3:2-9)

Paulo kujadiliana na wazee waliokuwa na imani kama yako (mdo 15:1-21) utajua paulo alikuwa anahubiri nini
 
Isije ikawa ni utungaji tu maana wenye akili pevu inayopembua na kutafsi mambo tusoma between lines kubaini uhalisia au filosofia ya theolojia tu. Tuna roho ya kumbambanua mambo ya kiroho kwa usahihi bila kuingiza dogma za nje
ULOKOLE NI UKAFIRI TU KAMA UHISIHARAMU TU HAKUNA JIPYA
 
Nakushauri uachane kabisa na bangi za Njombe, rudi kwenye bangi za Gezaulole sio kali kama za Njombe!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…