Janga la Corona limempaisha Rais Magufuli kisiasa

Janga la Corona limempaisha Rais Magufuli kisiasa

🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣Wa mujini wanasema ULIKURUPUKA!
Namna ambavyo Rais magufuri amejipambanua kukabiliana na janga la corona ni dhahiri amekonga nyoyo za walio wengi na hii imepelekea kupata uungwaji mkono na maelfu ya watanzania wakiwemo wa vyama vya upinzani.

Kitendo cha Rais Magufuli kutokubaliana na agenda ya kujifungia (LOCK DOWN) ambayo ndio ilikuwa agenda kuu ya upinzani, wananchi wamekipokea kama maamuzi sahihi ya kuwavusha katika kipindi hiki cha janga la corona dhidi ya baa la njaa na matatizo mengine ya kiuchumi.

Leo Rais Magufuli ametoa tamko la kufungua vyuo na shule kwa wanafunzi wa form six hili pia wananchi wamelipokea kama uamuzi wa busara kwa sababu linasaidia kulinda ajira za walimu wa shule na vyuo binafsi ambao walikuwa wanaishi katika kipindi kigumu kutokana na kusitishiwa mishahara yao. Hali kadhalika uamuzi huu unasaidia kulinda usalama wa wanafunzi dhidi ya vishawishi mitaani na hatari ya mimba za utotoni.

Kwa namna Rais Magufuli amejitoa na hatua alizochukua kukabiliana na corona hakika amepata wafuasi wengi hasa katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi mkuu. kwahivyo vyama vya upinzani vijipange kisawa sawa kwa sababu uchaguzi ujao utakuwa ni mgumu kwa upande wao baada ya kupoteza wafuasi wake kutokana na agenda zilizokosa credibility katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa corona.

Sambamba na hatua nzuri anazochukua Rais Magufuli kupambana na corona ni vema sasa akaangalia areas of weakness ambazo bado zinahitaji utatuzi mathalani suala la ajira kwa vijana, azitatue ili kufikia October wananchi wawe na kazi moja pekee ya kuchukua na kuweka waaa.
 
Hakika janga la corona limewazamisha sana wapinzani na hoja yao ya kulazimisha lockdown, kulazimisha habari za uongo kwamba hali ni mbaya saana wakati watanzania wao wanadunda na maisha kama kawa.

Lockdown waliyoishabibia sana;

1. Imekosa kabisa uhalisia wa utekelezaji kwa nchi kama zetu. Madhara ya kukataa lockdown yameeleweka na yanaimbwa na wananchi wa kawaida kabisa.

2. Hata nchi za Ulaya/US zimekuja kuacha a na lockdown.

3. Faida zilizokuwa zinapigiwa upatu zimekuja kuonekana si halisia. Badala yake kuna consensus ya kwamba lockdown ina madhara na haifai kufuatwa

4. Mifano ya wananchi kuigomea lockdown iko wazi nchi nyingi wananchi wa kawaida wanaoandamana ikiwemo majirani zetu Kenya, Zambia, Afrika ya kusini.

Hata hivyo nawasifu viongozi wa upinzani kwa mshipa wa ung'ang'anizi! Wamejua lockdown haikubaliki na watanzania, haina faida za kiafya kama wanavyosema, kuna madhara makubwa zaidi ya lockdown, siyo mbinu inayopendwa tena! Lakini bado wameshindwa kukiri!
Ni kweli mku issue ya Lockdown kwa Chadema ilileta maafa na anguko. Wabunge wa Chadema walitaka tujifungie huku wakijua sisi kipato chetu hata week hakiwezi kumaliza. Walikuwa na pesa zao za kutosha kufanya Shopping hata ya miezi 3 na zaidi. Sasa walitaka sisi tukifungiwa tule nini katika kipindi cha Lockdown? Kweli walitusaliti!!!!
 
Ni kweli mku issue ya Lockdown kwa Chadema ilileta maafa na anguko. Wabunge wa Chadema walitaka tujifungie huku wakijua sisi kipato chetu hata week hakiwezi kumaliza. Walikuwa na pesa zao za kutosha kufanya Shopping hata ya miezi 3 na zaidi. Sasa walitaka sisi tukifungiwa tule nini katika kipindi cha Lockdown? Kweli walitusaliti!!!!

Sawa. Lakini msimpuuze Uhuru Kenyatta aliyesema: uchumi twaweza ufufua lakini sisi hawezi fufua mtu.
 
Huyu mzee anajua sana ndio maana kila kukicha mabeberu wanatafuta mbinu za kumuua ili wafanye biashara yao haramu ya chanjo za mRNA,barakoa,na vipimo hivi vipya vya kuchokonolea makalioni
 
Kweli covid imempaisha Magufuli mpaka hatumwoni wiki ya tatu sasa
 
Huyu mzee anajua sana ndio maana kila kukicha mabeberu wanatafuta mbinu za kumuua ili wafanye biashara yao haramu ya chanjo za mRNA,barakoa,na vipimo hivi vipya vya kuchokonolea makalioni
Kwa hiyo kwetu ndo kuna zaidi!!0 Subiri kidogo atakuja kukushika mkono
 
Back
Top Bottom