Uchaguzi 2020 January Makamba asikitika kupitishwa bila kupingwa, atamani angechaguliwa na Wananchi wa Bumbuli

Kama kweli yeye ni mwanasiasa hai.. ajitoe , mchakato uanze upya ili apate mshindani alafu aone kama ataweza kupata japo ticket ya chama chake.
 
Ajiondoe tu kufupisha maneno
 
Kama kweli yeye ni mwanasiasa hai.. ajitoe , mchakato uanze upya ili apate mshindani alafu aone kama ataweza kupata japo ticket ya chama chake.
Hahahaaaa...... January hajawahi kujiajiri labda yule mwamvita ndio anajua uswahilini kulivyo!
 
Kwani kukataa si kupo.au hana tu fake kama mzarendo
 
Nakumbuka Rais Magufuli aliwapongeza Mrema na Cheyo kwa kumuunga mkono na kuwataka wapinzani wengine wafuate nyayo zao ili kuokoa fedha za walipa.

Kwani kupiga kura za Ndio na Hapana hakuna gharama bwashee?!
Gharama za kura za ndio na zile za kushindanisha wagombea zaidi ya mmoja ziko Sawa, lkn bwana mkubwa aliongea vile sababu anajua anaongoza wafu hata akibaka katiba nothing can happen!
 
Endapo Tundu.angefanikiwa kuweka pingamizi lake kwa Magufuli je usingefulahi?
Lissu alikuwa na msingi thabiti wa pingamizi: kutohakiki fomu kwa Tume siku ya uteuzi. Alijua hawezi kufanikiwa, lakini alituwezesha kuona upendeleo wa Tume
 
Kapirishwa kwa asilimia 600%. Ila Jana niliuliza kuhusu Makamba na Nape kukubali viti maalum!
 
Endapo Tundu.angefanikiwa kuweka pingamizi lake kwa Magufuli je usingefulahi?
Lissu aliweka pingamizi lake kimkakati, maana mliwaandaa wa kumwekea pingamizi, mliposikia kaweka mkarudisha korodani ndani.
 
Apo ana 0% aina flan ya unafiki mkubwa wanadhani hatujui kinachofanyika mpaka wanapitishwa bila kupingwa ..kama haitoshi anakimbilia ku tweets et kaskitishwa ovyo sana.
 
Niliwahi kuandika mwaka 2015 kwama wabunge wanaopitishwa bila kupingwa wananyimwa nafasi zao za kuchaguliwa na wananchi.

Wangepitishwa hata kwa uchaguzi wa kura ya ndiyo au hapana.

Mbona Nyerere na Mwinyi tumewachagua kwa kura za "Ndiyo" au "Hapana" wakati walikuwa hawana mpinzani?

Kwa nini tusingesema Nyerere kapita bila kupingwa, au Mwinyi kapita bila kupingwa, hakuna haja ya uchaguzi?

Kwani haiwezekani January akakosa mpinzani wa chama tofauti, halafu wananchi wasimkubali?

Kwenye katiba hakuna ubunge wa kupita bila kupingwa, kuna ubunge wa kuchaguliwa na wananchi.

Sasa kama January anapitishwa bila kuchaguliwa na wananchi, atasemaje yeye ni mbunge wa kuchaguliwa na wananchi?
 

Ni viti maalumu WANAWAKE
 
Hypocrisy. Ni màandalizi ye team hacking.
 
Kwa sasa January ni mbunge wa viti maalumu na hilo ndio linalomsikitisha.

Yaani Ummy Mwalimu akishinda atakuwa na hadhi kubwa zaidi yake!
 
Ila huu utaratibu wa kupitisha watu bila kupingwa inabidi uangaliwe vzr maana ni kama kuwachagulia wananchi mbunge wao bila hata wao kutoa maamuzi.

anapaswa kupiga kampeni kama kawaida tusikilize mipango yake na tukiridhika tunampa kura za YES tusipolidhika nae tunampa kura za NO ..lakini kumpitisha tu wanatukosea sisis wananchi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…