Uchaguzi 2020 January Makamba asikitika kupitishwa bila kupingwa, atamani angechaguliwa na Wananchi wa Bumbuli

Uchaguzi 2020 January Makamba asikitika kupitishwa bila kupingwa, atamani angechaguliwa na Wananchi wa Bumbuli

Makamba yupo sahihi, ushindi wa mezani haunogi bana! Ni sawa tu na kununua mechi.
 
Kwahio wajumbe wachache wa Chama pamoja na Chama cha Siasa ndio kinachagulia kiongozi jamii nzima ?, Ni wakati muafaka kuleta mgombea binafsi na kuweka limit kwenye matumizi ya pesa kwenye kampeni...
Mgombea binafsi hawezi kuenguliwa? Labda atokee chama tawala awekwe kama zuga.
 
Mabeberu pia wanajisikia vibaya mno kwa vitendo vyao dhidi ya weusi! iko siku watatukabidhi Hazina ya Dunia. ili wawe huru.
 
January Makamba anasema mwaka 2015 kwenye kura za ubunge alifaulu kwa 84% na mwaka huu baada ya kufanya kazi kubwa jimboni alitegemea kufaulu kwa 90%.

Lakini kwa bahati mbaya kwa yale yaliyotokea amejikuta tayari amepitishwa kuwa mbunge jambo ambalo halimpi fahari yoyote kama mwanasiasa " hai".

January amesema hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter.

My take: January kupitishwa bila kupingwa ni ufaulu wa % ngapi?

Maendeleo hayana vyama!
Sasa sindo ufanye calculations mzee??
 
Mgombea binafsi hawezi kuenguliwa? Labda atokee chama tawala awekwe kama zuga.
utaengua wangapi ? wale wote ambao wengine huenda walikuwa kama ishirini wajumbe wakawapunguza huenda kila raia angefanya kazi ya wajumbe..., pia kuweka limit kwenye kiasi cha pesa cha kampeni kutaondoa hii advantage isiyo sawa ya chama tawala iliyochukua vyanzo vya mapato vya nchi, na wengine..., pia ili watu wajue nani anasema nini waweke midahalo ambayo itawapa platform wagombea wote (kwenye radio na TV ya taifa) TBC ili wananchi wapate kumsikia kila mgombea

Kama hayo hayawezekani tufute hizi sanaa za kujifanya tuna vyama vingi na kodi zetu kupotea bure kumbe ni maigizo tu....
 
Mwenyekiti wa chama na NEC wapi na wapi bwashee?!
Bwashee usisahau Mkurugenzi alishawahi kugombea na kugombea Ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama chetu..hivyo ni wa kwetu kabisa kabisaa..japo kisheria NEC hawana uhusiano na Mwenyekiti wetu..😛😛.
 
Back
Top Bottom