Hatinaye mashine ya kwanza kuanza kuzalisha umeme,
Mambo tayari huko [emoji91][emoji91][emoji91]
Hongera Serikali, Hongera Rais na Hongera Waziri Makamba
---
WAZIRI wa Nishati, January Makamba ameliambia Bunge kuwa kwa muda wa wiki moja kuanzia leo (Mei 31, 2023), Bwawa la kufua umeme la Mwalimu Nyerere litafikisha kiwango cha ujazo wa maji utakaowezesha kuanza uzalishaji wa umeme.
Waziri huyo wa Nishati amesema hayo wakati akiwasilisha hotuba ya bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka 2023/ 2024 bungeni mjini Dodoma leo.
“Ninayo furaha kulitaarifu Bunge lako Tukufu kwamba katika kipindi cha wiki moja kuanzia leo, bwawa letu litafikisha kiwango cha ujazo wa maji (yaani mita 163 kutoka usawa wa bahari) kinachowezesha kuanza uzalishaji wa umeme” amesema Makamba.
Chanzo: Habari Leo