January Makamba kuitwa Rais ajaye na ukaribu wa familia yake na Mange Kimambi kumemponza na kutumbuliwa nafasi yake ya Waziri wa Mambo ya Nje

Hoja ya kuwa karibu na Kikwete kumbeba haina mashiko January uwezo anao ingekuwa hana hasingeaminiwa nafasi kubwa kama Waziri wa Teknolojia, Nishati, kubwa zaidi wizard nyeti ya mambo ya nje

Ingekuwa anabebwa angepewa wizara ambazo sio mama (kubwa) kama wizara ya michezo na utamaduni

Kuhusu ufisadi na tamaa Takukuru si wapo kwa nini wasimkamate ili kuthibitisha ufisadi huo na kuwa ushahidi wa hizo tuhuma?
 
Czani kama hiyo ni sababu, kwani tenguzi/teuzi hizi ni kama sandakalawe tu, akiamua ni hivyo, sasa mfano kwenye ardhi kulikuwa kuna shida gani? Alijitahidi kiasi chake lakini yuko wapi?
Huwezi jua huko ardhi pamoja na mikwara yake pengine nyuma ya pazia kuna madudu kibao yanafanyika rais wa nchi ana macho mengi na mkono mrefu na kuambiwa (kujua) mengi tambua hilo
 
Alikuwa anapeleka udaku kuhusu Rais kwa Dada Kimavi kwani hukumsikia RC? Halafu kweli sisi tutawaliwe na ukoo wa Makamba!!?
 
Haya sasa huyo mwalimu kuna kitu gani anafanya huko zaidi ya uchawa tu, lakini ataendelea sana kuwepo!! Yaani hata huwezi kujua tunataka nini, ni sandakalawe tu
Ummmy yupo vizuri..ukimsema vibaya unachuki zako tu..na Sio kingine..Ila mnyonge mnyongeni..haki yake mpeni; Waziri Ummy ameiweza sana siasa na utendaji wa Wizara ya afya..Haya mengine ni porojo tu ambazo hazina mashiko
 
Sidhani kama kumuita mtu Rais ajaye inaweza kuwa sababu
Kuna uzembe wa kazi na hata uwezekano wa upigaji, maana upigaji upo kila kona
Kuna wengine wanapiga huku wamelala
Na kuna wengine kelele nyingi mara aweke ndani mtu, mara atengue kitu kumbe mpigaji mkubwa

Tunaweza kuwa wapiga ramli ila mengine ni kweli
 
Karibu viongozi wote wanafanya ufisadi hasa nchi zetu hizi masikini za dunia ya 3 mpaka marais wenyewe kwa nini wengine wasitumbuliwe? Kuna vita kubwa sana kwenye nafasi ya urais nje na ndani ya CCM na ndio sababu za tenguzi hizi za mara kwa mara watu wanapanga timu zao mapema
 
Vingine vya kusemwa, infact kwenye serikali si kila kitu utafaham
Najua hilo kuwa rais ana macho mengi lakini ukweli ni kwamba kuna vita kubwa kwenye urais mwakani ndani ya CCM kwa hiyo wakubwa hawa wanawindana kama madudu (ufisadi) viongozi wengu wanafanya mbona hawaguswi?
 
Majengo yake ya kenya sijui itakuwaje
 
Alikuwa anapeleka udaku kuhusu Rais kwa Dada Kimavi kwani hukumsikia RC? Halafu kweli sisi tutawaliwe na ukoo wa Makamba!!?
Huyo RC mwenyewe ni mdaku, kwani ukoo wa Makamba hawana haki kutawala nchi hii? Ukoo upi wenye haki?
 
Ameshindwa uwaziri uraisi atauweza acheni matusi,tangu awe waziri ni tija ipi au la maana kwa nchi kafanya.
Hawa wanabebwa na mkataba wa mwitongo tu
 
Watarogana sana
Yote hayo sio Uzalendo ila ni tamaa za nafasi serikalini tu
Ni kweli nchi masikini zimeoza kwa wizi na Rushwa
Halafu unakuta kila mmoja ana mganga wake anaeishi kijijini kwenye pagala la nyasi

Huwa sielewi kabisa
Wacha watoane roho
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…