Japan: Waziri Mkuu wa zamani, Shinzo Abe afariki dunia baada ya kushambuliwa kwa risasi

Japan: Waziri Mkuu wa zamani, Shinzo Abe afariki dunia baada ya kushambuliwa kwa risasi

Hasa hasa ni misimamo yake ambayo ilionekana kuanza kwenda kinyume na sera za marekani
Mtwa Mkulu hakuna mwenye hitimisho kamili ni nani hasa alihusika na kifo cha Kennedy, ripoti rasmi ya serikali nadhani ya Bwana Warren ni kuwa Lee H Oswald ni muhusika pekee, baadhi ya wengi Marekani hawakubaliani nayo, hapo ndipo milango ya conspiracies kibao zimezaliwa! Wengine wakisema CIA, MAFIA, Jeshi la Marekani nk, au Urusi baada ya Marekani kuiwekea ngumu na kuilazimisha Urusi kuondoa Makombora yake Cuba.Hivyo Mkulu kila anayesoma habari za Kennedy huwa anatoa hitimisho yake.Mimi mwenyewe nimebadili mtizamo wangu Mara nyingi, nimepita mahali alipouawa mwezi uliopita nikiwatembeza jamaa zangu toka Tanzania, naanza kuamini risasi iloyomuua Kennedy haikutoka pale juu dirishani, maybe upande wa kichaka kile cha Grass Knoll, Lee Oswald angle aliyokaa ilikuwa ngumu mno kumpata Kennedy akiwa ndani ya gari ikitembea, anyway mauaji ya Kennedy yanabaki kuwashangaza wamarekani wengi kwa kukosa hitimisho wanalolitaka na kuikataa report ya Warren.
 
Suala hapa ni ulinzi, yaani hata kama mtu alindwe vipi anapotokea mtu, mtu asiyejali kitu, mtu anayesema; "na liwalo liwe"---hapo mtu huyo anaweza kuua anayelindwa kabla ya yeye kuuawa au kukamatwa na walinzi wa anayelindwa.

Kuhusu Anwar Sadat, yeye aliuawa na askari waliopita mbele yake kutoa heshima katika gwaride kwenye sherehe za uhuru na sio kwamba aliuawa na mlinzi wake, walinzi wake wakati huo walikuwepo kando yake.
Asante kwa ufafanuzi, Sadat hakuliwa na walinzi wake, Bali na askari wa jeshi wakitoa heshima zao, walinzi walishindwa kabisa kuzuia, kiongozi aliyeuawa na walinzi wake nadhani ni Indira Ghandi.
 
One of the best Pm Rest in peace shinzo Abe tutakumbukuka miradi iliyojengwa na serekali yako mchapakaz na muungwana Sana
 
Mtwa Mkulu hakuna mwenye hitimisho kamili ni nani hasa alihusika na kifo cha Kennedy, ripoti rasmi ya serikali nadhani ya Bwana Warren ni kuwa Lee H Oswald ni muhusika pekee, baadhi ya wengi Marekani hawakubaliani nayo, hapo ndipo milango ya conspiracies kibao zimezaliwa! Wengine wakisema CIA, MAFIA, Jeshi la Marekani nk, au Urusi baada ya Marekani kuiwekea ngumu na kuilazimisha Urusi kuondoa Makombora yake Cuba.Hivyo Mkulu kila anayesoma habari za Kennedy huwa anatoa hitimisho yake.Mimi mwenyewe nimebadili mtizamo wangu Mara nyingi, nimepita mahali alipouawa mwezi uliopita nikiwatembeza jamaa zangu toka Tanzania, naanza kuamini risasi iloyomuua Kennedy haikutoka pale juu dirishani, maybe upande wa kichaka kile cha Grass Knoll, Lee Oswald angle aliyokaa ilikuwa ngumu mno kumpata Kennedy akiwa ndani ya gari ikitembea, anyway mauaji ya Kennedy yanabaki kuwashangaza wamarekani wengi kwa kukosa hitimisho wanalolitaka na kuikataa report ya Warren.
Lakini ukitazama ile video mbona ni kama ghorofani...kuna theory nyingi dhidi ya mauaji yake ila naamini aliuawa na watu wa ndani ya mfumo.. umechambua vizuri nimepata radha ya ile jf ya zamani
 
Kuna FFU aliniambia Risasi hainaga jasiri.. nimeona hapo walinzi knowledge ya kwanza ilikuwa kujitetea wao.. tena Inaonesha walau Abe alielewa kinachoendelea.. wanakuja kukumbuka ameshaanguka.
 
Lakini ukitazama ile video mbona ni kama ghorofani...kuna theory nyingi dhidi ya mauaji yake ila naamini aliuawa na watu wa ndani ya mfumo.. umechambua vizuri nimepata radha ya ile jf ya zamani
Ni kweli Lee Harvey Oswald alikuwa ghorofani, na Alipiga risasi,ila alikua ni kama kanyaboya tu! Ukiona picha za mwili wa Kennedy,risasi ilimfumua kisogoni,maanake iliingilia mbele ikatokea nyuma! Risasi ya Lee Oswald ilitakiwa iingilie kisogoni, maana gari ilikuwa imeeisha mpita! Na ukiangalia vizuri utashangaa jinsi alivyomwangukia Jackie! Inaonyesha kuna risasi nyingine mkuu, na Kitendo cha Jack Ruby kumuua Lee Oswald kesho yake, tena kwenye kituo cha polisi, inaonyesha he was just a fall guy, au ningesema mbuzi wa kafara! Huwa naangalia trajectory ya risasi, hasa risasi ya kwanza na ya pili, na utalamu wangu mdogo wa bunduki, naona Oswald aliwekwa pale aonyeshe wazi kuwa ndiye muuaji, lakini real killers bundling, kule Kennedy alipokuwa anaelekea! Kwenye kile kichaka cha majani.Anyway labda na mimi nimekumbwa na hii conspiracy ya kuwa Lee Harvey Oswald was not a real killer.
 
Back
Top Bottom