Japan yaitangaza Tanzania kuwa Kitovu cha Uwekezaji, viwanda. Honda kujengwa nchini

Japan yaitangaza Tanzania kuwa Kitovu cha Uwekezaji, viwanda. Honda kujengwa nchini

Tumeshawahi kupita "BARABARA" hii wakati wa "ALMASI,DHAHABU,GAS" na vingine vingi,kwa nini tuamini sasa hivi Tanzania itakuwa DUBAI.
Dubai liyosheheni masnipers na wamwaga tindikali!!!?.
Ngoja tusubiri na kuona nchi inayoendeleza na nchi nyingine baada ya yenyewe kushindwa kujiendeleza, nadhani tutakuwa wa kwanza na wa aina yake!
 
Uwekezaji Nchini Tz unahitaji Sayansi kubwa sana kwani Ubinafusishaji uliofanyika awamu ya tatu umepelekea baadhi ya Viwanda kufa na baadhi vipo taabani hivyo Kama tumeshindwa kuviendeleza viwanda vilivyokuwepo Tokea awamu ya kwanza iweje kwa hivyo viwanda vipya? Tatizo kubwa wanalopata Wawekezaji ni Ufisadi hususani ikitokea mwekezaji akatoa ajila kubwa kwa Wazawa ambapo hutengeneza umoja na kubuni mbinu ya kujinufaisha Binafsi huku Viwanda vikiyumba na kufirisika. Swali je?hao Wajapani wa Honda watakuja na uongozi full na Watafunga CCTV kila kona kwenye Viwanda vyao? Hii ni tahadhali kwani inafahamika moja ya changamoto kubwa kwenye uwekezaji ni udokozi na hata mwekezaji akiweka CCTV kisha akamweka mzawa pale lazima afanye manuva Vinginevyo CCTV akae Mzungu na asiwe anajulikana Tunawakaribisha Wajapani na wengineo wote Duniani waje wawekeze kokote lakini uwekezaji wa uhakika isije ikawa kama TAMKO na Scania pale kibaha.japani jipangeni vizuri leteni hata viwanda vya magari lakini mzingatie changamoto za uwekezaji Tz kwani kuna Vilema pendwa vingi sana
 
tumeambiwa tutakachopata watanzania ila bado hamjatuambia hao wajapan watachukua nini in return!

Tazama documentary hii hutadanganywa tena na vibaraka wa wakoloni
https://www.jamiiforums.com/habari-na-hoja-mchanganyiko/503251-documentary-ya-aljazeera-inayofichua-utumwa-wa-viongozi-wa-nchi-za-kiafrica.html
 
Guys, personally siipendi CCM, lakini kama tutatuliza akili zetu na kuwa positive na kutumia fursa hizi vizuri bila ubinafsi na rushwa, Tanzania ya miaka mitano mpaka kumi ijayo itakuwa yenye maendeleo na uchumi imara. Kuna watu hawaelewi ni kwa nini 5 Asian tigers kama Korea Kusini, Malaysia na nyinginezo zimeweza kutoka kimaendeleo?? Waliweza kutumia fursa za technolojia na misaada ya kimifumo na uwekezaji katika elimu vilivyo. Kwa kifupi walijitambua wana nini na wanataka nini.

Kwa sasa kuna mwamko mkubwa sana wa kujitambua kwa wa Tanzania, tupo pazuri tunahitaji kubadili attitude za watanzania, wapende kufanya kazi, rushwa idhibitiwe, uzalendo pia uongezeke na hili si jukumu la serikali pekee ni sisi wote.

Mwisho nimalizie, HAKUNA JINSI NI LAZIMA TANZANIA IWE SUPER POWER AFRIKA MASHARIKI NA KATI BY 2025, dalili zote zinaonyesha hivyo. TUACHE KUJIDHARAU JAMANI CHONDE CHONDE.........
https://www.jamiiforums.com/habari-na-hoja-mchanganyiko/503251-documentary-ya-aljazeera-inayofichua-utumwa-wa-viongozi-wa-nchi-za-kiafrica.html
 
Kwani hukusikia Mkulu anayoyaongea kila mara kuwa hii nchi ilikuwa inachezewa sana!
 
Wajapan walie tu maana Sehemu zote za kujengea viwanda BAKHRESA kesha pewa bure.. Inabidi wajapani waingie mkataba na Bakhresa wakitaka ardhi
 
Huu mwaka wa tatu sasa tangu mtuhabarishe kuhusu hii kitu. Naomba kujua kiwanda hiko kwa sasa hapa bongo kipo maeneo gani?
 
Back
Top Bottom