Guys, personally siipendi CCM, lakini kama tutatuliza akili zetu na kuwa positive na kutumia fursa hizi vizuri bila ubinafsi na rushwa, Tanzania ya miaka mitano mpaka kumi ijayo itakuwa yenye maendeleo na uchumi imara. Kuna watu hawaelewi ni kwa nini 5 Asian tigers kama Korea Kusini, Malaysia na nyinginezo zimeweza kutoka kimaendeleo?? Waliweza kutumia fursa za technolojia na misaada ya kimifumo na uwekezaji katika elimu vilivyo. Kwa kifupi walijitambua wana nini na wanataka nini.
Kwa sasa kuna mwamko mkubwa sana wa kujitambua kwa wa Tanzania, tupo pazuri tunahitaji kubadili attitude za watanzania, wapende kufanya kazi, rushwa idhibitiwe, uzalendo pia uongezeke na hili si jukumu la serikali pekee ni sisi wote.
Mwisho nimalizie, HAKUNA JINSI NI LAZIMA TANZANIA IWE SUPER POWER AFRIKA MASHARIKI NA KATI BY 2025, dalili zote zinaonyesha hivyo. TUACHE KUJIDHARAU JAMANI CHONDE CHONDE.........