Japhet Maganga wa CWT akamatwa kwa kufanya fujo

Japhet Maganga wa CWT akamatwa kwa kufanya fujo

Point yako imesimama kwa kunyooka. Kama hivyo ndivyo ingawa inahitaji uthibitisho wa asili ya mtu, kwa nini majina ya asili kama hayo ya kijaluo kwa watu wa mikoa ya magharibi hasa Kigoma yanatiliwa shaka na idara ya uhamiaji?
Kuyatilia shaka ni muhimu, watu wengi wanahamia kwa njia za panya toka nchi jirani. Nilisoma na mtu anaitwa Niyonziza, mwingine nilikutana naye mitaani jina lake Amatus Ndayishimye. Kiasili, haya si majina ya Kitanzania, ni Warundi.

Kuna wakati nilidate na bint mdogo alikua hata haongei Kiswahili vizuri. Siku ya kwanza kukutana naye tulikua na gari sehemu, nikamwita akaja. Tulipokuwa tunapiga story nikagundua hakuwa Mtanzania......mimi na yule mwezangu aliyekuwa dereva tukaanza kumhoji. Kwa kuonekano wetu, akaanza kutuogopa. Tulipomuuliza amesoma wapi shule ya msingi, akajichanganya akataja mkoa, wilaya na kata ambayo yule dereva ndio kwao. Tukagundua anatuongopea, ikabidi atueleze ukweli kuwa anaishi na dada yake ambaye yupo huku Tz miaka mingi ila kwao ni Burundi. Hana kibali wala chochote yupo yupo tu, na hapo ni Mwanza. Akikaa miaka 5 huyu si anapata hadi passport yetu.

Bint kanyooka Mtutsi mzuri sana. Nikachukua namba.

So we acha tu uhamiaji wafanye kazi yao.
 
KATIBU Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Japhet Maganga, na wenzake 10 wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani hapa kwa tuhuma za kufanya fujo kwenye mkutano wa Baraza Kuu la chama hicho wakati wakipitisha bajeti ya mwaka.

Tukio hilo lilitokea baada ya baraza hilo kuazimia kumsimamisha kazi Maganga kutokana na kupoteza sifa baada ya kufukuzwa kazi na mwajiri wake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Martin Otieno, amethibitisha kukumatwa kwa kiongozi huyo pamoja na wenzake wakati wa mkutano huo.

“Tulipata taarifa kuwa kuna watu wanafanya fujo tukaenda kudhibiti kabla hayajatokea madhara. Kwenye mkutano huo sisi hatufahamu ilikuwaje zikatokea fujo. Ukitaka kufahamu zaidi waulizwe CWT wenyewe,” amesema Kamanda Otieno.

Source - Nipashe
Huyu jama naye ni kichwa maji kabisa.Alikuwa haoni kinachotengenezwa dhidi yake?Alienda kufanya nini?Kujilemaza na kujitegemeza kwa vitu ambavyo hujazaliwa navyo ndiyo matokeo yake hayo.
 
Ndege mjanja hunasa kwenye tundu bovu
 
Huu ni mjadala mpana ambao tena ni wa kitaifa na bado umenajisiwa kwa muda mrefu, badala ya kuhoji ametanguliza matusi... Niambie kama Verified member hapataswi kujibu mapigo?.
Ukikosolewa kubali. Ulibugi stepu pale uliposema kwa sababu ana jina la Otieno basi ni mkenya. Hukufikiria sawasawa. Jina haliwezi kuonyesha utaifa wa mtu. Tuna watanzania wanaoitwa Mackenzie na siyo watu wa Ulaya. Otieno Tanzania wapo wengi.
 
CWT:-JOKA LINALOTUMIWA NA MAFISADI KUNYONYA MAISHA YA WALIMU NCHINI!!

Nitakuja kuifanya Cwt ilipe mishahara basic ya walimu Kwa mwaka mmoja mfululizo ikishindwa inafutwa rasmi!haiwezekani wakusanye fedha zote miaka yote hii Leo washindwe kuboresha maisha ya walimu wenzao!!
Kwa kisingizio eti "tunajenga ofisi Kila wilaya"
 
Huu ni mjadala mpana ambao tena ni wa kitaifa na bado umenajisiwa kwa muda mrefu, badala ya kuhoji ametanguliza matusi... Niambie kama Verified member hapataswi kujibu mapigo?.
Mjadala wako ni kuwa wajaluo wote waliopo Tanzania ni wageni? Punguza ujuaji mkuu.

 
KATIBU Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Japhet Maganga, na wenzake 10 wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani hapa kwa tuhuma za kufanya fujo kwenye mkutano wa Baraza Kuu la chama hicho wakati wakipitisha bajeti ya mwaka.

Tukio hilo lilitokea baada ya baraza hilo kuazimia kumsimamisha kazi Maganga kutokana na kupoteza sifa baada ya kufukuzwa kazi na mwajiri wake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Martin Otieno, amethibitisha kukumatwa kwa kiongozi huyo pamoja na wenzake wakati wa mkutano huo.

“Tulipata taarifa kuwa kuna watu wanafanya fujo tukaenda kudhibiti kabla hayajatokea madhara. Kwenye mkutano huo sisi hatufahamu ilikuwaje zikatokea fujo. Ukitaka kufahamu zaidi waulizwe CWT wenyewe,” amesema Kamanda Otieno.

Source - Nipashe
Alikataa UTEUZI huyu siyo?
 
Back
Top Bottom