Wanabodi,
Kama kawaida yangu, kila nipatapo fursa, huja na makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa" kuhusu jambo lolote lenye maslahi makubwa kwa taifa letu liwe ni la kisiasa, kiuchumi au kijamii.
Mada ya leo ni kuhusu Bunge letu tukufu, limeridhia makubaliano ya IGA kati ya Serikali ya UAE na Tanzania, kampuni ya DP World ya Mwarabu wa Dubai, kutuendeshea Bandari zetu.
Kuna watu wana support hatua hiyo kwa hoja za msingi, kuwa DP World ni kampuni kubwa na ina uwezo mkubwa, inaendesha Bandari nyingi duniani, hivyo itatusaidia sana kuboresha uendeshaji wa Bandari yetu ya Dar es Salaam. Na kuna wanaopinga wakiwaita DP World ni matapeli, kufuatia kesi na migogoro mingi mahali pengi ambapo DP World wana operates, hivyo kitendo cha Bunge letu kuridhia hiyo IGA ya DP World bila kuifanyia a due diligence report, kumewafanya wachoke na kudhani, it's over, it's the end of the road kwa suala hili,. naomba kuwapa faraja na kuwatia moyo kuwa it's not the end!, it's not over yet until it's over!.
Hiyo HGA ni makubaliano tuu na sio mkataba, yaani ni an agreement na sio contract. Kila mkataba ni agreement, lakini sio kila agreement ni mkataba, mfano mzuri ni muungano wa Tanganyika na Zanzibar kuunda Tanzania, ni makubaliano tuu na sio mkataba, mkifika mahali mkashindwa kuelewana, mnagawana tuu fito, kila mtu anasepa kivyake
Je, Wajua Kuwa Tanzania Hatuna Mkataba wa Muungano?. Kilichopo ni Makubaliano Tuu ya Muungano?!.
Hivyo kile Bunge letu lilichoridhia, ni agreement tuu, tukiithibitishia serikali yetu, hawa DP World, pamoja na uzuri wao wote, pamoja na uwezo wao mkubwa wa kuendesha Bandari kibao, lakini ni matapeli na wana matatizo lukuki, hivyo serikali yetu iwe makini sana kabla ya kusaini HGA, na utepeli wao, ukiwekwa wazi hadharani peupe, kila mwenye macho aone, tutaisaidia sana serikali yetu, tutamsaidia sana Rais wetu Samia na kulisaidia taifa letu Tanzania tusiingizwe tena mkenge na Mwarabu wa Dubai kama alivyofanywa Chief Mangungo, hivyo serikali yetu, viongozi wetu na Bunge letu kuridhia fasta fasta kwasababu tuu, Mwarabu wa Dubai ni mtu Rahim, mkarimu, amemkirimu Mama yetu kuipaisha bure Tanzania kwenye Expo Dubai, akawakirimu waserikali wetu, kwa trips za Dubai, akawakirimu waheshimiwa wabunge wetu kwa trips za Dubai, na kuwakirimu waandishi wetu wa habari na media zetu kwa trips za Dubai.
Japo Rais wetu, Mama Samia, ana nia njema ya kweli na ya dhati kulisaidia taifa letu, lakini anapokutana na matapeli wa kimataifa wakamuingiza mkenge, sisi watu wa Mhimili wa Nne, the media, tuna wajibu wa kulisaidia taifa letu kwa kuonyesha utepeli huo uko wapi, kisha serikali yetu ikiamua kuendelea na HGA ya Mwarabu wa Dubai, sisi watu wa media, tutakuwa na a clear conscious kuwa angalau tumetimiza wajibu wetu, tumeieleza serikali yetu inavyotaka kuingizwa mkenge na kutapeliwa, hivyo vipengele vya mkataba wa HGA viboreshwe na kazi, iendelee!.
Kwa vile mimi licha ya kuwa ni mwandishi tuu wa habari wa kujitegemea kwa kujitolea, mimi pia ni mwanasheria na wakili wa kujitegemea, kwa kujitolea kutetea bure haki kwa wasio na uwezo, hivyo nitawaletea makubaliano hayo na kuwachambulia kuwaonyesha jinsi tunavyotaka kutapeliwa mchana kweupe.
- Utapeli wa kwanza mkubwa, ni hakuna mtu yoyote kati yetu aliyefanya a due diligence report ya DP World, tunaelezwa ni Governmental Organisation, wakati sii kweli, it's a private company!. Kabla ya kuingia mkataba wowote, lazima kwanza kufanyike kitu kinachoitwa a due diligence process na kutolewa a due diligence report. Hili halikufanyika hivyo serikali yetu kujikuta inaingia mkataba wa kimataifa na parties to contract which has no capacity to contract hivyo ku vitiate makubaliano kugeuka void hivyo makubaliano hayo yanakuwa null and void ab initio!.
- Mkataba wa IGA na HGA inaingiwa kati ya serikali na serikali, hivyo ukisoma documents za makubaliano utaona ni kati ya serikali ya Tanzania na serikali ya UAE, lakini signatories kwa serikali ya Tanzania ni serikali kweli, lakini kwa serikali ya UAE, signatories ni Mwarabu wa Dubai wa DP World na sio serikali ya UAE, kwenye mkataba wameandika serikali ya Dubai, Dubai hivyo hapa tunatapeliwa!, serikali yetu inaingizwa mkenge kuingia mkataba na a private company disguised as a government of UAE kumbe ni kampuni binafsi!.
- Mkataba Kati ya serikali ya Tanzania na Dubai ni batili kwenye sheria za kimataifa. Maana Dubai sio nchi, a sovereign state kama ilivyo Tanzania, hivyo has no the capacity to transact an international IGA, haiwezi kuingia mikataba ya kimataifa na nchi, inaweza kuingia mkataba wa kimataifa na mamlaka ya Bandari, taasisi kwa taasisi, not a sovereign nation na nchi isiyo na sovereignty!.
- Mikataba ya kimataifa inaingiwa na Falme ya Kiarabu inayotambulika kwenye sheria za kimataifa na sio Dubai ambayo ni sehemu ya UAE, hivyo hapa kuna utapeli!. Due diligence ingefanyika, hili lingeonekana.
- Status ya Dubai kwe UAE ni sawa na status ya Zanzibar ndani ya JMT, Zanzibar has no capacity to transact an international treaty kwasababu Zanzibar sio sovereign. Dubai pia sio sovereign, hivyo mikataba yote ya kimataifa ya Zanzibar, inaingiwa na JMT kwaniaba ya Zanzibar, IGA na HGA inapaswa kuingiwa kati ya Tanzania na UAE na sio Tanzania na Dubai!.
- Jambo jingine, kuna kipengele cha kuizuia nchi isiendeleze Bandari nyingine, hivyo kuiweka mashakani Bandari ya Bagamoyo, hili halikubaliki hata kidogo!.
Kwavile saa hizi ni usiku mkubwa, Joni Mtembezi ananisisitiza nitembee tembee nae hivyo nitamalizia kesho.
Paskali.