Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

Haiitwi Uhuru wa wakaldayo inaitwa Uru wa wakaldayo au Ur of Chaldeans..
Hilo la kwanza..


unahisi Ishamael hakuwa na Nchi aliyopewa?
Ishmael aliishi Parani akiwinda Huko..
Hizo ahadi zote ulizotaja Ni ahadi sawa na alizoahidiwa Ishmael

Haya tusome mwanzo 17:20
View attachment 3021508

kwa lugha ya Anko charles Pale Uk

Mwanzo 17:20

"And as for Ishmael, I have heard thee: Behold, I have blessed him, and will make him fruitful, and will multiply him exceedingly; twelve princes shall he beget, and I will make him a great nation."


Kwanza Mungu amesema
  • Amembariki (Blessed Him)
  • Amemzidisha (Make Him fruitful)
  • Atamzidisha Uzao wake (Multiply Him Exceddingly)
  • Atazaa watawala 12 (12 Prince)
  • Naye atamfanya Awe Taifa kuu..

Hoja zako Nchi ya Kanaani
Isaka Alipewa kanaani ila Ishamael alipewa Beersheba, na Parani

We unahisi kwanini Watoto wengine wa Ibrahimu Hawatajwi sana au hawatajwi kabisa Kwa sababu waliobarikiwa Na kupewa Urithi ni wawili tu..

Ketura MKEWE MWINGINE WA IBRAHIMU ALIKUWA NA WATOTO 6 Ila sijaona mkiwajadili wengine wala hawajawahi kujadiliwa kabisa..


Kingine kuhusu Kwamba Isaka ni maarufu kuliko Ishmael...

kwa mfano nikikupa nafasi uandike Historia Ya ukoo wenu Je Utaweza kuniandikia Historia ya Kaka Yake na Babu yako?

waandishi wa Biblia wote ni Waebrani ana Wayahudi wote wametoka kwenye Uzao wa Watoto 12 wa Yakobo mtoto wa Isaka na ndo maana Hata Historia ya Esau (Edomu) pia huwezi kuipata..

Mkuu kwanza kwenye biblia au hata Quran sijawahi kusoma kuwa Ishmael alipewa nchi ya Harani. Sijawahi kwa kweli.

Umesema vizuri

Moja ya ishara kuwa aliyetimiza ahadi ni Isaka ni hilo la taifa lao kuwa mpaka hivi leo.

Mimi na wewe na hata jamii zingine nyingi hazijui Historia zao.

Huyo Muhammad mwenyewe hajui ni kwakivipi ametoka kwa Ibrahim.
Hao waarabu wanaojinasibisha na Ibrahim wenyewe hawaelewi na ushahidi uliowazi kuwa Baba yao ni Ibrahim.

Hata ikiulizwa uzao au taifa la waishmael ni lipi sasa hivi hakuna majibu.
 
Nimesikiliza "qari" yaani msomaji, kasoma Surat Saffat aya ya 100 mpaka aya ya 105. Nimesikiliza na aliyepewa kutafsiri, hapo ndipo alipoboronga. Na yeye kwa kuwa anajuwa anahokisema akamsukumia mtafsiri mwengine aitwae Ibn kathir, akasema huyo mtafsiri ndiye kasema huyo mtoto ni "Ismail". Hayo Yanabaki kuwa ni maneno ya mtafsiri (commentator) na siyo ya Qur'an.

Maana yake nini hiyo? Maana yake hakuna katika hizo aya zilizosomwa alipotajwa Ismail.

Ndiyo maana post ya juu huko nikasema yamepachikwa maneno kutoka nje ya Qur'an. Hata wewe ukiisikiliza aya inaposomwa hutosikia jina la Ismail, hilo utalisikia kutoka kwa "mtafsiri (commentator). Kayatowa wapi hayo aliyoongezea kama hayapo kwenye Qur'an? Hilo ndilo swali la kujiuliza.
Kwa hiyo aliyetaka kuchinjwa ni nani?
Hilo ndilo swali lipo mezani.
Tunaomba ulijibu.t
 
Kwa hoja za wengi humu zinaonyesha kuwa Quran haijaeleza habari za mtoto yupi wa Ibrahimu alitakiwa kutolewa kafara, lakini Bibilia imeweka wazi kuwa aliyetakiwa kutolewa kafara ni Isaka

Nikimnukuu FAIZFOX ameenda mbali na kusema Quran haijazungumza habari za mtoto yeyote wa Ibrahimu kuchinjwa, hilo si limeisha
 
Kwani urithi ulikuwa Ni nini ningependa Kujua..
Maana nikiangalia Biblia Nakuta kuwa Ishmael au Waishmael ndo wafanya Biashara wakubwa sana wa Agano la kale..
Urithi ni vitu vile unavyopewa na mzazi wako vilivyo halali yako kutoka kwake. Vinaweza kukubariki au kukulaani. Isaka alipewa urithi wa vitu vyote vya Ibrahim. Vikihusisha ardhi, Mungu( agano) la kuwa baba wa mataifa, Wafalme kutoka kwake, kubariki Kwa watakaombariki. Watoto wengine wa Ibrahim waliopewa zawadi hivyo hawakurithishwa chochote Cha baba yao.
Pia kulikua na zuio la kuoa aina za wanawake. Hakuruhusiwa kuoa mtu ambae sio wa uzao wa baba yake. Yeye alioa Mmisri. Na kama ahadi ingekua Kwa Ismael Kwa Nini hakuna nabii zaidi ya Mohamed aliyetoka kwenye viuno vyake?
 
Sijaona kwenye Qur'an kuwa Ibrahim alikuwa na mtoto anitwa Ismail, au hayo ni mafundisho nje ya Qur'an?
Suratul Maryam aya 54

وَٱذْكُرْ فِى ٱلْكِتَٰبِ إِسْمَٰعِيلَ ۚ إِنَّهُۥ كَانَ صَادِقَ ٱلْوَعْدِ وَكَانَ رَسُولًۭا نَّبِيًّۭا

TAFSIRI:

Na mtaje katika Kitabu Ismail. Bila ya shaka yeye alikuwa ni mkweli wa ahadi, na alikuwa Mtume, Nabii.
Aya ya pili
surat Ibrahim Aya ya 39

ٱلْحَمْدُ لِلَّهِ ٱلَّذِى وَهَبَ لِى عَلَى ٱلْكِبَرِ إِسْمَٰعِيلَ وَإِسْحَٰقَ ۚ إِنَّ رَبِّى لَسَمِيعُ ٱلدُّعَآءِ

TAfsiri..

"Alhamdulillahi! Himdi zote ni za Mwenyezi Mungu aliye nipa juu ya uzee wangu Ismail na Is-haq. Hakika Mola wangu Mlezi ni Mwenye kusikia maombi."


Aya ya Tatu


Suratul Baqarah aya ya 127

وَإِذْ يَرْفَعُ إِبْرَٰهِۦمُ ٱلْقَوَاعِدَ مِنَ ٱلْبَيْتِ وَإِسْمَٰعِيلُ رَبَّنَا تَقَبَّلْ مِنَّآ ۖ إِنَّكَ أَنتَ ٱلسَّمِيعُ ٱلْعَلِيمُ

Tafsiri:

"Na kumbukeni Ibrahim na Ismail walipo inyanyua misingi ya ile Nyumba wakaomba: Ewe Mola Mlezi wetu! Tutakabalie! Hakika Wewe ndiye Msikizi Mjuzi."


Aya Ya nne:

Suratul Baqarah aya ya 136

قُولُوٓا۟ ءَامَنَّا بِٱللَّهِ وَمَآ أُنزِلَ إِلَيْنَا وَمَآ أُنزِلَ إِلَىٰٓ إِبْرَٰهِۦمَ وَإِسْمَٰعِيلَ وَإِسْحَٰقَ وَيَعْقُوبَ وَٱلْأَسْبَاطِ وَمَآ أُوتِىَ مُوسَىٰ وَعِيسَىٰ وَمَآ أُوتِىَ ٱلنَّبِيُّونَ مِن رَّبِّهِمْ لَا نُفَرِّقُ بَيْنَ أَحَدٍۢ مِّنْهُمْ وَنَحْنُ لَهُۥ مُسْلِمُونَ


TAFSIRI:-

"Semeni nyinyi: Tumemuamini Mwenyezi Mungu na yale tuliyo teremshiwa sisi, na yaliyo teremshwa kwa Ibrahim na Ismail na Is-hak na Yaakub na wajukuu zake, na waliyo pewa Musa na Isa, na pia waliyo pewa Manabii wengine kutoka kwa Mola wao Mlezi; hatutafautishi baina ya yeyote katika hao, na sisi tumesilimu kwake."


Ziko nyingi ila kwa leo Chukua Hizo.labda nyongeza ni 2:133
 
Urithi ni vitu vile unavyopewa na mzazi wako vilivyo halali yako kutoka kwake. Vinaweza kukubariki au kukulaani. Isaka alipewa urithi wa vitu vyote vya Ibrahim. Vikihusisha ardhi, Mungu( agano) la kuwa baba wa mataifa, Wafalme kutoka kwake, kubariki Kwa watakaombariki. Watoto wengine wa Ibrahim waliopewa zawadi hivyo hawakurithishwa chochote Cha baba yao.
Pia kulikua na zuio la kuoa aina za wanawake. Hakuruhusiwa kuoa mtu ambae sio wa uzao wa baba yake. Yeye alioa Mmisri. Na kama ahadi ingekua Kwa Ismael Kwa Nini hakuna nabii zaidi ya Mohamed aliyetoka kwenye viuno vyake?
Rudi kwenye Post Yangu comment namba #337
 
Vizuri kwa kuliweka hili Sawa.
FaizaFixy FaizaFoxy Quran unayotumia haina aya hii?

Turudi kwenye hoja.
Nani aliyetaka kutolewa dhabihu?

Quran kwa Ishmael ingawaje haijamtaja ila moja kwa moja mtu anayesoma Quran atajua ni Ishmael lakini Biblia na vitabu vya kiyahudi vinamtambua Isaka.

Kwa nini Ibrahim alimfukuza Hajiri na Ishmael huku akijua mtoto wa kwanza ndiye mrithi?
Sawa,..kwanza naomba tuweke biasness pembeni ili tupate jibu sahihi la mtoto yupi hasa aliyetaka kuchinjwa au kutolewa dhabihu kama ulivyosema........

Kwa nilivyofuatilia huu mjadala kuna hoja moja ambayo nadhani ndiyo ya wazi kabisa ameigusia DR Mambo Jambo ..... hoja ya umri wa wahusika pindi amri ya kuchinjwa ilivyotoka.....DR ameweka verses za Biblia ambazo zinaonyesha wazi kwamba wakati amri inatoka Ismail ndiyo mtoto pekee wa Ibrahim ambaye alikua ana :-
1. Uwezo wa kuongea (kama ilivyoonyeshwa kwenye biblia akijadiliana na Baba yake)
2. Uwezo wa kutembea zaidi ya Km 300,..kuelekea eneo ambalo tukio la kuchinjwa ilikua lifanyike.

NB: kwa mujibu wa hoja nilizopitia humu Ismail alikua na umri wa miaka 14,.wakati amri ya kuchinjwa inatoka........vipi kuhusu Ndugu yake alikua na umri gani? huenda alikua hajazaliwa au alizaliwa miezi michache baada ya tukio hilo.


So,. kimsingi kwenye hoja ya umri wa watoto husika... dadisi zinaonyesha Ismail ndiyo muhusika kwenye ishu ya kuchinjwa..endapo tukiondoa ushabiki nadhani tunaweza kukubaliana juu ya hili.
 
Haiitwi Uhuru wa wakaldayo inaitwa Uru wa wakaldayo au Ur of Chaldeans..
Hilo la kwanza..


unahisi Ishamael hakuwa na Nchi aliyopewa?
Ishmael aliishi Parani akiwinda Huko..
Hizo ahadi zote ulizotaja Ni ahadi sawa na alizoahidiwa Ishmael

Haya tusome mwanzo 17:20
View attachment 3021508

kwa lugha ya Anko charles Pale Uk

Mwanzo 17:20

"And as for Ishmael, I have heard thee: Behold, I have blessed him, and will make him fruitful, and will multiply him exceedingly; twelve princes shall he beget, and I will make him a great nation."


Kwanza Mungu amesema
  • Amembariki (Blessed Him)
  • Amemzidisha (Make Him fruitful)
  • Atamzidisha Uzao wake (Multiply Him Exceddingly)
  • Atazaa watawala 12 (12 Prince)
  • Naye atamfanya Awe Taifa kuu..

Hoja zako Nchi ya Kanaani
Isaka Alipewa kanaani ila Ishamael alipewa Beersheba, na Parani

We unahisi kwanini Watoto wengine wa Ibrahimu Hawatajwi sana au hawatajwi kabisa Kwa sababu waliobarikiwa Na kupewa Urithi ni wawili tu..

Ketura MKEWE MWINGINE WA IBRAHIMU ALIKUWA NA WATOTO 6 Ila sijaona mkiwajadili wengine wala hawajawahi kujadiliwa kabisa..


Kingine kuhusu Kwamba Isaka ni maarufu kuliko Ishmael...

kwa mfano nikikupa nafasi uandike Historia Ya ukoo wenu Je Utaweza kuniandikia Historia ya Kaka Yake na Babu yako?

waandishi wa Biblia wote ni Waebrani ana Wayahudi wote wametoka kwenye Uzao wa Watoto 12 wa Yakobo mtoto wa Isaka na ndo maana Hata Historia ya Esau (Edomu) pia huwezi kuipata..
Sasa Ndugu.

Unaamini kulingana na biblia Ismael alibarikiwia, alizidishiwa na ahadi nyingi tu alipewa na nikweli hizi baraka alizipata

Kwanini usiiamini hio hio biblia iliosema, isaka ndio aliyetaka kutolewa kafara? Kwanini usiiamini hio hio biblia iliyosema mtoto wa ahadi ni isaka na upo ushaidi kwenye biblia.

Kama unaamini Qur'an, kwanini utetezi wako usijitenge na biblia ukaelezea kupitia Qur'an. Kama unaamini bible kwanini usitumie bible yenyewe

Mimi nachukia sana mtu anaeonganisha hivi vitabu viwili kwenye kuelezea point zake. Maana havina uhusiano wowote. Zaidi ya mgawanyo wake unaonzia kwa ibrahimu

Biblia imeshaelezea . Sasa tunasubr ushahidi kutoka kwenye Qur'an.
 
Kwa hiyo mtu akisema Ishmael aliishi Dar es salaam na akataka kutolewa kafara na Babake Ibrahim Quran haina Mamlaka wala ushahidi wa kupinga hilo?

Unajua muongozo ni pamoja m biography?
Kujua ni kwa nini Mungu alimtumia fulani, wapi, wakati gani.

Quran sio biography Kwa sababu imeandikwa wa wakati mmoja yaani zama moja. Hivyo haina full details za nyakati zilizopita.
Unahangaika na nini wewe,vitu muhimu vyote kwenye QUR'AN vipo,ibada,sheria,mahusiano ya kijani,tawhiid...haihangaiki na birthday za watu
 
Urithi ni vitu vile unavyopewa na mzazi wako vilivyo halali yako kutoka kwake. Vinaweza kukubariki au kukulaani. Isaka alipewa urithi wa vitu vyote vya Ibrahim. Vikihusisha ardhi, Mungu( agano) la kuwa baba wa mataifa, Wafalme kutoka kwake, kubariki Kwa watakaombariki. Watoto wengine wa Ibrahim waliopewa zawadi hivyo hawakurithishwa chochote Cha baba yao.
Pia kulikua na zuio la kuoa aina za wanawake. Hakuruhusiwa kuoa mtu ambae sio wa uzao wa baba yake. Yeye alioa Mmisri. Na kama ahadi ingekua Kwa Ismael Kwa Nini hakuna nabii zaidi ya Mohamed aliyetoka kwenye viuno vyake?
Hakuna Mtu anayejua Historia Ya Ishmael au waishmael zaidi ya Kutajwa kwenye Biblia na kwemye Historia mara kadhaa kama Wafanyabiashara maarufu..

Kuhusu baraka watoto waliobarikiwa wa Ibrahimu ni wawili.tu Ishmail na Isaka ila wengine 6 waliobali hawakubalikiwa Unafikiri kwanini?
 
Mkuu kwanza kwenye biblia au hata Quran sijawahi kusoma kuwa Ishmael alipewa nchi ya Harani. Sijawahi kwa kweli.

Umesema vizuri

Moja ya ishara kuwa aliyetimiza ahadi ni Isaka ni hilo la taifa lao kuwa mpaka hivi leo.

Mimi na wewe na hata jamii zingine nyingi hazijui Historia zao.

Huyo Muhammad mwenyewe hajui ni kwakivipi ametoka kwa Ibrahim.
Hao waarabu wanaojinasibisha na Ibrahim wenyewe hawaelewi na ushahidi uliowazi kuwa Baba yao ni Ibrahim.

Hata ikiulizwa uzao au taifa la waishmael ni lipi sasa hivi hakuna majibu.
Ibrahim mwarabu wa Iraq toka mji wa ur,180km kaskazini mwa saudia
 
Mimi nimeshangaa sana kusikia Hivyo maana Kuna aya Zaidi ya 10 zikimtaja Ismili na kuna moja illnataka kuhusu dua yake nimesahau ilipo nilikunbuka nitaileta..
Faiza kiukweli Anateleza
yes,.sahihi kaka hapo ameteleza...........ila tatizo Madam sidhani kama atakubali kwamba ameteleza... maana akikubali nadhani binafsi itakua mara ya kwanza kumuona akikiri kuteleza hapa JF.... Madam ni mtata Hahh 🙌
 
Sasa Ndugu.

Unaamini kulingana na biblia Ismael alibarikiwia, alizidishiwa na ahadi nyingi tu alipewa na nikweli hizi baraka alizipata

Kwanini usiiamini hio hio biblia iliosema, isaka ndio aliyetaka kutolewa kafara? Kwanini usiiamini hio hio biblia iliyosema mtoto wa ahadi ni isaka na upo ushaidi kwenye biblia.

Kama unaamini Qur'an, kwanini utetezi wako usijitenge na biblia ukaelezea kupitia Qur'an. Kama unaamini bible kwanini usitumie bible yenyewe

Mimi nachukia sana mtu anaeonganisha hivi vitabu viwili kwenye kuelezea point zake. Maana havina uhusiano wowote. Zaidi ya mgawanyo wake unaonzia kwa ibrahimu

Biblia imeshaelezea . Sasa tunasubr ushahidi kutoka kwenye Qur'an.
Mkuu nahisi haunifahamu Vizuri!
I am the Factual comparison person..

Huwa siegemei upande kama Shabiki Eti kwa kuwa naamini Hiki basi nikitetee..

Wanaonifahamu Jf Siku nyingi wanafahamu hilo..
Na ndo maana Naweza nikatoa Facts hata Kwa kutumia Hinduism au Hata other mystery kama wako sawa..

Narudia tena Kuhusu Mtoto aliyetolewa Kafara kwa Quran Haikutaja Jina ila wachambuzi na watafsiri wengi husema ni Ishamael..

Na stori iliyopo kwenye Biblia imetaja na imeleeza But Ni unlogical na Ni factual wrong..

Inaeleza kuwa Kipindi Ibrahimu akiwa na miaka 100 ndo Kipindi Mungu anamjaribu..

Lakini Biblia Inasema Isaka amezaliwa Ibrahimu akiwa na Miaka 100 na Ishamaili amezaliwa ibrahim akiwa na miaka 86..

Kwahyo kipindi Ibrahim akiwa na miaka 100 Isaka alikuwa na miezi na Ishmaili alikwa na miaka 14..

Na ndo kipindi ameagizwa kumtoa mtoto kafara..

Its True kwamba story ipo na Inasomeka But its Logical fallacy na Ina alot of Contradiction..

How comes mtoto wa Miezi kadhaa atembee Km 250 kwenda Kufanya kafara na How comes Hajaifikisha hata miaka na aweze kuongea..?

Try To think dont Confuse Faith, Beleive and Facts...
And FYI try to Reason Kila kitu
 
Mtume Muhammad S .A.W alisema msibishane kuhusu dini pasipo kuwa na elimu ......

Bismillah arahmanni rakhim
 
Sinai Zamani ilikuwa saudia kabla ya Ugawaji wa Mipaka..
Ingawa kwa sasa Iko katika Sinai penisula ambayo ni Kati kati ya Saudia, Jordan na Misri

Kwahyi jibu ni yes iko Saudia
DK Mambo Jambo, binafsi nakushukuru kwa uchambuzi mzuri sana.
Uko vizuri na umedhihirisha usomi wako
Ila ukweli unasimama kama ukweli.
 
Kwanza wekeni hapa hiyo Quran inayosema Ismail ndiyo alitakiwa kutolewa dhabihu.

Kwa upande wa Biblia ipo wazi ni kitabu cha Mwanzo 22:1-19. Abrahamu anataka kumtoa mwana wake wa pekee.

Jua pia kupitia Isaka ndipo anakuja kupatikana Yesu, ambaye Mungu alimtoa Mwanae wake huyo wa pekee kuwa dhabihu.

Kitabu cha mwanzo 24:5-6, Abrahamu anamrithisha Isaka Mali zake zote, ila watoto wake walizaliwa na Masuria wake walipewa Zawadi na kutakiwa kwenda mbali na Isaka huko Mashariki ya Kati.

So uzao wa Masuria haukuwa na mipango endelevu ya Mungu.
 
Mkuu nahisi haunifahamu Vizuri!
I am the Factual comparison person..

Huwa siegemei upande kama Shabiki Eti kwa kuwa naamini Hiki basi nikitetee..

Wanaonifahamu Jf Siku nyingi wanafahamu hilo..
Na ndo maana Naweza nikatoa Facts hata Kwa kutumia Hinduism au Hata other mystery kama wako sawa..

Narudia tena Kuhusu Mtoto aliyetolewa Kafara kwa Quran Haikutaja Jina ila wachambuzi na watafsiri wengi husema ni Ishamael..

Na stori iliyopo kwenye Biblia imetaja na imeleeza But Ni unlogical na Ni factual wrong..

Inaeleza kuwa Kipindi Ibrahimu akiwa na miaka 100 ndo Kipindi Mungu anamjaribu..

Lakini Biblia Inasema Isaka amezaliwa Ibrahimu akiwa na Miaka 100 na Ishamaili amezaliwa ibrahim akiwa na miaka 86..

Kwahyo kipindi Ibrahim akiwa na miaka 100 Isaka alikuwa na miezi na Ishmaili alikwa na miaka 14..

Na ndo kipindi ameagizwa kumtoa mtoto kafara..

Its True kwamba story ipo na Inasomeka But its Logical fallacy na Ina alot of Contradiction..

How comes mtoto wa Miezi kadhaa atembee Km 250 kwenda Kufanya kafara na How comes Hajaifikisha hata miaka na aweze kuongea..?

Try To think dont Confuse Faith, Beleive and Facts...
And FYI try to Reason Kila kitu

Unajua Ndugu.

Kwenye umri wa Isaka na Ibrahimu, inaweza kuwa changamoto kama isaka alikua bdo mchanga wakati wa kutolewa kafara.

Ukisoma Mwanzo sura 21.
21:8 inaonesha mtoto alikua akaachishwa kunyonya. Hii inadhihirisha mtoto alikua sio mchanga.

21:14 Ismael na mama yake wanatoka ili isaka asiwe mrithi pamoja na isaka.

21:34 Ibrahimu akakaa kwenye nchi ya wafilisti miaka mingi.

Sura 22.
Mungu anakuja kumjaribu Ibrahimu kuhusu kafara.
mwanz 22:1 tena inasema ikiwa baada ya mambo hayo yaan mambo ya Mwanzo 21 kupita.


Swali langu, Nini au kipi kinakuthibitishia wakati isaka anatolewa kafara alikua bdo mchanga?

Kama ibrahimu alikaa kwenye nchi ya wafilisti miaka mingi kwenye mwanz 21:34, ilikua ni baada ya kumzaa isaka au isaka alikua bdo ajazaliwa?
 
Ni hiari yako kusikiliza chanzo cha habari au masimulizi mengine ya baadae.

Biblia iliyoanza kuripoti hilo tukio inasema Isaka ndiye aliyetolewa sadaka.

Waislamu wapambane na dini yao ambayo ina aya za mkato mkato na hazina mtiririko wa matukio.

Waislamu na qurani yao wameambiwa ishamaeli ndiye aliyetolewa sadaka wala hupaswi kuuliza.

Mungu wa kwenye Biblia alisha sema mara nyingi tu kuwa yeye ni Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo ambaye ndiye Israeli.

Na ametoa family tree ya mtiririko wa Manabii na watu aliowatumia katika mpango wake wa kumwabudu, na Ishamael hayupo kwenye hiyo family.

Achana na stori za kuunga unga, familia ya Wayahudi ni hii hapa.
Mathayo 1
2 Ibrahimu alimzaa Isaka; Isaka akamzaa Yakobo; Yakobo akamzaa Yuda na ndugu zake;

3 Yuda akamzaa Peresi na Zera kwa Tamari; Peresi akamzaa Esromu; Esromu akamzaa Aramu;

4 Aramu akamzaa Aminadabu; Aminadabu akamzaa Nashoni; Nashoni akamzaa Salmoni;

5 Salmoni akamzaa Boazi kwa Rahabu; Boazi akamzaa Obedi kwa Ruthu; Obedi akamzaa Yese;

6 Yese akamzaa mfalme Daudi; Daudi akamzaa Suleimani kwa yule mke wa uria;

7 Sulemani akamzaa Rehoboamu; Rehoboamu akamzaa Abiya; Abiya akamzaa Asa;

8 Asa akamzaa Yehoshafati; Yehoshafati akamzaa Yoramu; Yoramu akamzaa Uzia;

9 Uzia akamzaa Yothamu; Yothamu akamzaa Ahazi; Ahazi akamzaa Hezekia;

10 Hezekia akamzaa Manase; Manase akamzaa Amoni; Amoni akamzaa Yosia;

11 Yosia akamzaa Yekonia na ndugu zake, wakati wa ule uhamisho wa Babeli.

12 Na baada ya ule uhamisho wa Babeli, Yekonia akamzaa Shealtieli; Shealtieli akamzaa Zerubabeli;

13 Zerubabeli akamzaa Abihudi; Abihudi akamzaa Eliakimu; Eliakimu akamzaa Azori;

14 Azori akamzaa Sadoki; Sadoki akamzaa Akimu; Akimu akamzaa Eliudi;

15 Eliudi akamzaa Eleazari; Eleazari akamzaa Matani; Matani akamzaa Yakobo;

16 Yakobo akamzaa Yusufu mumewe Mariamu aliyemzaa YESU aitwaye Kristo.
..............
Na nyie mnao mwona Ishmaeli kama ndio baba wa Uislamu naomba mnipe family tree yake hadi kuzaliwa Muhammadi.
Maana Mungu anatunza kumbukumbu za Manabii wake hadi wa mwisho.

Maswali mengine hayana mantiki, kweli ya mtu ni ile anayoiamini.

Kweli ya Wayahudi na Wakristo ni Isaka.

Kweli ya Waislamu ni Ishmaeli ambaye hawajui hata family tree yake.

Kila mtu ana kweli yake kutikana na kukiamini chanzo cha hiyo kweli.

Wayahudi na Wakristo tunamchukulia Muhammadi kama mtu mpotoshaji tu na kamwe hatumwamini kwa chochote anacho ongea
Ni naona thread ifungwe maana imejibu kila kitu hapa..
 
Ndugu yangu mwandishi mahiri. Kama sehemu ya jibu lako nakuzawadia kitabu kitabu hiki, kisome utafaidika sana.
Kitabu kimeandikwa na waislamu lazima wajipe promo wao.. siwezi kusoma maandiko yeyote yaliyoandikwa na waislamu yanaimpure ukweli
BIBLIA INASEMA Ibrahim aliambiwa amtoe sadaka mwanawe wa PEKEE (only son)...Je ni nani kati ya Ismael na isaka alikuwa mwana wa pekee wa ibrahim? Kumbuka Ibrahim alimpata Ismael akiwa na miaka 86 na kwa miaka 14 ,Ismael aliendelea kuwa ndio mtoto wa pekee wa Ibrahim mpaka pale alipokuja mpata Isaka akiwa na miaka 14. Baada ya hapo Isaka hawezi kuwa mtoto wa pekee maana tayari alishamkuta kaka yake ambaye ni Ismael akiwa na miaka 14.

Pia mtihani wa kumtoa mtoto wa pili (ambaye sie wa pekee) hauwezi kuwa sawa na mtihani wa kumchinja mtoto wa kwanza ilihali alishatafuta mtoto kwa zaidi ya miaka 60 bila ya mafanikio...mpaka alipompata ismael akiwa na miaka 86


Mwanzo 22:1-2

Sasa baada ya mambo hayo Mungu wa kweli akamjaribu+ Abrahamu, akamwambia: “Abrahamu!” akajibu: “Mimi hapa!” 2 Kisha Mungu akamwambia: “Tafadhali, mchukue mwana wako, mwana wako wa pekee unayempenda sana,+ Isaka,+ usafiri kwenda katika nchi ya Moria+ nawe umtoe kuwa dhabihu ya kuteketezwa juu ya mlima mmoja nitakaokuonyesha.”
Mtoto wa pekee ni mtoto halali wa kwenye ndoa (Sarah na Ibrahim)
 
Back
Top Bottom