Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

Vizuri,..Biblia inaonyesha wakati amri ya kuchinjwa kwa mtoto inatoka....Mtoto aliyekusudiwa kuchinjwa alikua na umri wa kuweza kuongea na kutembea umbali wa zaidi ya km 300....

Je, Kati ya Ismail na Isihaka nani umri wake unaendana na sifa za matendo ya kiumri ambazo Biblia imezitoa hapo?

NB:- Kwa mujibu wa Biblia amri ya mtoto kuchinjwa wakati inatoka,..mtoto pekee wa Ibrahim ambae alikua ana umri wa kuelewa mambo ni Ismail ( Umri wa miaka 14).
 

Attachments

  • IMG_7303.png
    IMG_7303.png
    710.5 KB · Views: 2
Mimi najua hao watu wapo kwenye Quran,shida yangu ni wewe kusema kwenye Quran wametajwa Kama waebrania,ndiyo naomba hiyo aya

Quran nimekuambia haijitoshelezi sio ajabu kuwa haijui hata asili ya wahusika iliyokuwa inawaelezea.

Hapo ndipo Myahudi alipomzidi akili muarabu. Muarabu ni muafrika kiasili hivyo hayuko mbali na sisi wabongo.

Unaeleza kitu juujuu yaani kulipualipua
 
"What is the meaning of the word "Hebrew"? A definition" What Does The Word "Hebrew" Mean?
Muebrania/Hebrew ni muhamaji,ukihama ukonga ujaenda tandika wewe ni muebrania,Ibrahim aliitwa muebrania kwa kuwa alikua mhamiaji Tena wa kuvuka moto,bila shaka Euphrates na Tigris
Kwa lugha za Kisemitic Waebrania maana yake ni upande wa pili wa mto

Katika Safari ya Ibrahim walikuwa na kundi lililobaki Upande wa pili wa mto Jordan (Upande wa Kaanani) na upande wa Sodoma na Ghomora (Jordan ya Leo) waliokuwa upande wa Jordan waliwaita waliokuwa Kaanani Waebrania na hapo Ndio Asili na Tamaduni yao ikakua...
 
Quran bana nzuri story ya Yusuf ndo iko in detail
Hizi zingine mtihani
Wkt Biblia kama movie full details
Quran siyo biography,hata hivyo imeela in detail story ya Musa,Ibrahim,nuhu,lut...biblia ni kitabu Cha akaunti za watu juu ya matukio,ndiyo maana utakuta paulo anajielezea yeye mambo yake,yale siyo maneno ya Mungu Bali maelezo ya watu kuhusu matukio,ndiyo unaona Kama movie
 
Bro unafikiri sawasawa!?..nabii mission yake iwe kujenga safina tu!?..so nuhu alikua mpagani?

Mwanzo 6
1 Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wa kike walizaliwa kwao,
2wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.
3BWANA akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini.
4Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile; tena, baada ya hayo, wana wa Mungu walipoingia kwa binti za wanadamu, wakazaa nao wana; hao ndio waliokuwa watu hodari zamani, watu wenye sifa. 5BWANA akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote.
6BWANA akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyo.
7BWANA akasema, Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemwumba usoni pa nchi; mwanadamu na mnyama, na kitambaacho na ndege wa angani; kwa maana naghairi ya kwamba nimewafanya.
8Lakini Nuhu akapata neema machoni pa BWANA

unaelewaje Aya hiyo?
 
Habari zote za Ishimaili na Isaka zimeelezwa kikamilifu katika Biblia, na ndio rejea kuu na pekee. Hizo habari haziko popote kwenye Quran.
Na bila ubishi wowote iliyetakiwa kutolewa sadaka ni Isaka.

Waislamu wanaaminishwa uzushi wa Ishimaili kutakiwa kutolewa sadaka pasipo rejea ya Quran.

Tuache kuisingizia Quran mambo ya uzushi na uongo.
hateeb10
 
Umri umezungumzwa wakati wa tohara
Sio kuchinja mtoto
Ya mtoto ni mwanzo 22
Umri wao haujatajwa ktk Biblia
Hapana,..kilichofanyika ni hesabu tu Biblia inasema wakati Ismail anazaliwa Baba yake Ibrahim alikua na umri wa Miaka 86....so series of events mpaka anakuja kuzaliwa Isihaka ukifanya hesabu utajua umri wa wote watatu Ibrahim na wanae hao wawili.
 
Quran nimekuambia haijitoshelezi sio ajabu kuwa haijui hata asili ya wahusika iliyokuwa inawaelezea.

Hapo ndipo Myahudi alipomzidi akili muarabu. Muarabu ni muafrika kiasili hivyo hayuko mbali na sisi wabongo.

Unaeleza kitu juujuu yaani kulipualipua
Nilikuambia mapema QUR'AN siyo biography,ndiyo maana bible ni tabu kubwa la story za watu wakati QUR'AN imeja tawhiid,sheria na maelekezo,ni muongozo siyo kitabu Cha story
 
Quran siyo biography,hata hivyo imeela in detail story ya Musa,Ibrahim,nuhu,lut...biblia ni kitabu Cha akaunti za watu juu ya matukio,ndiyo maana utakuta paulo anajielezea yeye mambo yake,yale siyo maneno ya Mungu Bali maelezo ya watu kuhusu matukio,ndiyo unaona Kama movie
Ya Ibrahim sio full
Huoni hata mama yake Ismael hajatajwa?
Wala mtoto tunayejadili hapa kwenye Quran hajatajwa
Ila kwenye Biblia iko bayana
 
Hapana,..kilichofanyika ni hesabu tu Biblia inasema wakati Ismail anazaliwa Baba yake Ibrahim alikua na umri wa Miaka 86....so series of events mpaka anakuja kuzaliwa Isihaka ukifanya hesabu utajua umri wa wote watatu Ibrahim na wanae hao wawili.

Umri huo hauhusiani na Kafara isipokuwa tohara.
Ishmael alifanyiwa tohara akiwa na miaka 13 kwenda kumi na nne. Ibrahim akiwa na miaka 100, Isaka akiwa na siku nane.

Sio tukio la Kafara
 
Nimeona hayo ni mawazo yake,..cha msingi ni kuweka hoja zenye mantiki ili athibitishe madai yake..

Kwa mfano,.. muulize Je, Isihaka ashawahi kuwa mtoto wa pekee wa Ibrahim?

Na, Je, Kati ya Ismail na Isihaka yupi alipitia kipindi ambacho alikua ndiyo mtoto pekee wa Ibrahim?

Hizo ndiyo hoja za msingi.
 
Hapana,..kilichofanyika ni hesabu tu Biblia inasema wakati Ismail anazaliwa Baba yake Ibrahim alikua na umri wa Miaka 86....so series of events mpaka anakuja kuzaliwa Isihaka ukifanya hesabu utajua umri wa wote watatu Ibrahim na wanae hao wawili.
Biblia inasema Isaka alipozaliwa
Ismael na mama yake walifukuzwa hapo nyumbani kwa Ibrahimu kwenda Jangwani
Hapakua na amani baada ya Isaka kuzaliwa hivyo familia hiyo ilitengana
Akabaki Isaka na Sara na Ibrahim
Isaka akakua ndo badae likaja jaribu la mtoto kuchinjwa
Hapo Ismail na mamaye kitambo washapewa chemchem ya Zamzam jangwani huko
 
Mwanzo 6
1 Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wa kike walizaliwa kwao,
2wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.
3BWANA akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini.
4Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile; tena, baada ya hayo, wana wa Mungu walipoingia kwa binti za wanadamu, wakazaa nao wana; hao ndio waliokuwa watu hodari zamani, watu wenye sifa. 5BWANA akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote.
6BWANA akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyo.
7BWANA akasema, Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemwumba usoni pa nchi; mwanadamu na mnyama, na kitambaacho na ndege wa angani; kwa maana naghairi ya kwamba nimewafanya.
8Lakini Nuhu akapata neema machoni pa BWANA

unaelewaje Aya hiyo?
Huu si ugwadu tu,Wana wa Mungu!!?..Mungu Hana watoto,Wala Aya haisemi mission ya nuhu ni kujenga safina tu,nabii wa kujenga safina tu!!?..be serious babu
 
Nimeona hayo ni mawazo yake,..cha msingi ni kuweka hoja zenye mantiki ili athibitishe madai yake..

Kwa mfano,.. muulize Je, Isihaka ashawahi kuwa mtoto wa pekee wa Ibrahim?

Na, Je, Kati ya Ismail na Isihaka yupi alipitia kipindi ambacho alikua ndiyo mtoto pekee wa Ibrahim?

Hizo ndiyo hoja za msingi.
Issue is kwani Quran imemtaja Ismail kwenye jaribu la kuchinja mtoto?
Biblia iko bayana ni Isaka
 

Attachments

  • IMG_7303.png
    IMG_7303.png
    710.5 KB · Views: 3
  • IMG_7304.png
    IMG_7304.png
    2.2 MB · Views: 2
Back
Top Bottom