Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

Yesu anathibitisha umuhimu mkubwa wa kutekeleza mapenzi ya Mungu kama yalivyorekodiwa kwenye torati na manabii (yaani, vitabu 5 vya Agano la Kale na sehemu zingine za Maandiko).

Biblia inasema Yesu hakuja kuitangua torati bali kuitimiliza—ikiwa na maana kwamba aliyapa Maandiko maana yake kamili zaidi.

Alikuja kuonesha namna bora ya kufuata mapenzi ya Baba Yake.

Katika Mathayo 5, kwa mfano, Yesu anabainisha vipengele kadhaa vinavyoonesha undani hasa wa torati. Anasema, kumchukia mtu ni sawa na uuaji (Mat 5:21-26), kutamani ni kuzini (Mat 5:27-30; Mat 19), talaka haramu ni zinaa (Mat 19:8-9); anawasisitiza wanafunzi Wake kusema ukweli, kuepuka kisasi na kuwapenda maadui wao (Mat 5:33-48).

Katika kila mmoja ya mafundisho hayo hapo juu, Yesu anasema mmesikia kwamba imenenwa au mmesikia watu wa kale walivyoambiwa; kisha anasema bali Mimi nawaambieni.

Hii ndiyo kusema kwamba Kristu alionesha undani wa torati, namna ilivyoeleweka awali na namna anavyoifafanua sasa.

Kwa waandishi na Mafarisayo, Marabi na walimu wa sheria, ni bayana Yesu alikuwa ameivunja torati.

Ndiyo maana walimchukia sana na kujaribu mara nyingi kumpiga mawe.

Sababu ya mwitikio huo mkali dhidi ya Yesu ni kwa vile viongozi wa dini walikuwa makini sana katika kufuata sheria zote.

Walikuwa na masharti magumu na yenye uzingativu mkubwa katika masuala ya dini yao.

Jibu pekee la Yesu ambalo lingeweza kuwafikirisha viongozi hao wa dini waliokuwa na uhakika wa mwenendo wao katika torati ni pale alipowaambia, nendeni mkajifunze maana ya maneno haya, Nataka rehema, wala si kujitoa mhanga (Mathayo 9:13)!

Yesu alikuwa akiwatafakarisha waichunguze mioyo yao zaidi kuliko kuishia tu kutazama matendo yao ya nje na kujisifu kwa namna walivyotekeleza vipengele vya dini.

Hii hutuambia kwamba Yesu alidai kwao wawe na mwenendo wa kina zaidi kuliko kushika vipengele ama masharti tu ya nje.

Alienda mbali zaidi hadi kwenye kiini ama msingi kabisa wa nia ya moyo. Nia, mawazo, matendo, vyote vinahusika katika kutekeleza mapenzi ya Mungu.

Kwa mujibu wa Kristo, kinachofanyika moyoni ndicho kinachoibua matendo ya nje. Ndiyo maana alisema chuki ni sawa na uuaji, kutamani ni sawa na kutenda zinaa, nk.

Matendo yao ya nje yalikuwa na maana tu pale ambapo yangeambatana na utauwa au tohara ya moyo.

Hayo imewapasa kuyafanya, wala yale mengine msiyaache (Mathayo 23:23)! Haki yenu isipozidi hiyo haki ya Mafarisayo!

Yesu aliwafundisha mambo ambayo kwao yalionekana kuwa mageni na yanayopingana na torati, kadiri uelewa wao ulivyohusika.

Hata hivyo, mafundisho Yake yalipatana kikamilifu na mafunuo ya Mungu.

Je, Paulo alipingana na mafundisho ya Kristu?

Ni katika mantiki kama hiyo ya Yesu ndipo tunaweza kumwelewa vyema Mtume Paulo.

Alifundisha mambo ambayo watu wasio makini hudhani aliipinga torati au aliibatilisha sheria ya Mungu, kama ambavyo Yesu alidhaniwa anafundisha kinyume na torati.

Katika muktadha huo, tahadhari ya Petro ni muhimu sana:

^Katika nyaraka hizo yamo mambo ambayo ni vigumu kuelewa nayo; na mambo hayo watu wasio na elimu, wasio imara, huyapotoa, kama vile wayapotoavyo na maandiko mengine, kwa uvunjifu wao wenyewe.^ (2 Petro 3:16).

Kabla ya kuangalia baadhi ya mafundisho ya Paulo, hebu tuone yeye alikuwa ni mtu wa namna gani kabla hajakutana na Yesu na kuitwa kuwa mtume.

Wafilipi 3:3-4
^3 Maana sisi tu tohara, tumwabuduo Mungu kwa Roho, na kuona fahari juu ya Kristo Yesu, wala hatuutumainii mwili.

4 Walakini mimi ningeweza kuutumainia mwili. Mtu yeyote akijiona kuwa anayo sababu ya kuutumainia mwili, mimi zaidi.

5 Nalitahiriwa siku ya nane, ni mtu wa taifa la Israeli, wa kabila ya Benjamini, Mwebrania wa Waebrania, kwa habari ya kuishika torati, ni Farisayo, 6 kwa habari ya juhudi, mwenye kuliudhi Kanisa, kwa habari ya haki ipatikanayo kwa sheria sikuwa na hatia.

7 Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, naliyahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo.^

Mtume Paulo alikuwa Farisayo wa Mafarisayo! Paulo alijua namna ya kuishika sheria au torati, lakini kama Yesu asemavyo, lazima haki yake izidi ile ya waandishi na Mafarisayo ili aurithi ufalme.

Si ajabu Paulo anasema, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu; ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nimpate Kristo; tena nionekane katika Yeye, nisiwe na haki yangu mwenyewe ipatikanayo kwa sheria, bali ile ipatikanayo kwa imani iliyo katika Kristo, haki ile itokayo kwa Mungu, kwa imani (Wafilipi 3:8, 9).


ESV 1 Cor. 10:25
Eat whatever is sold in the meat market without raising any question on the ground of conscience.

Muktadha wa 1Kor 10:14-33 ni namna ya kuikabili ibada ya kipagani hasa kuhusu vyakula au nyama zilizotolewa sadaka kwa sanamu.

Hivi ni vyakula vya matambiko kwa miungu, ibada ya sanamu na ushirikina.

Paulo anaeleza namna 4 za kukabiliana na changamoto hiyo:

a) Ni kosa kwa mfuasi wa Kristu kwenda kwenye mahekalu ya wapagani na sehemu zao za matambiko ili kushiriki vyakula vilivyotolewa sadaka kwa sanamu. Kufanya hivyo ni sawa na kujihusisha na ushirikina na ibada ya mashetani (1Kor 10:18-21).

b) Iwapo chakula kinauzwa sokoni ama sehemu za umma, ni halali kula bila kuuliza maswali ili kujua iwapo au la kilitokana na matambiko (1Kor 10:25-26).

Paulo anasema si haramu kula chakula kilichonunuliwa mahali sahihi ambapo hakuna matambiko wala ibada za kipagani na iwapo mtu husika hafahamu kwamba chakula hicho kilitolewa sadaka kwa sanamu (kilitambikiwa).

c) Kufuatia mwaliko wa mtu asiyeamini—ni halali kula chakula chake bila kuuliza iwapo au la kilitambikiwa (1Kor 10:27).

d) Hupaswi kula chakula hicho iwapo umeambiwa kilitambikiwa. Paulo anabainisha sababu husika kwamba hilo hufanyika kwa faida ya mtu huyo asiyeamini (1Kor 10:27-28, 32-33).

Hitimisho: Paulo hazungumzii kula tu kitu chochote bila kubagua vyakula najisi na visivyo najisi, bali anaongelea vyakula—vitu ambavyo vimeainishwa kwamba vinapaswa kuliwa kwa mujibu wa Walawi 11 na Kumbukumbu la Torati 14.

Kama ilivyoelezwa awali, tatizo hapa lilikuwa vyakula vilivyotolewa sadaka kwa sanamu au kufanyiwa matambiko.

Kamwe, tatizo haukuwa mgogoro wa vyakula gani viliwe na vipi visiliwe. Ni vyema kuzingatia muktadha ili kuepuka upotoshaji.

^Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lolote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu,^ ndivyo Mtume Paulo anavyohitimisha kipengele hiki.


Paulo anafundisha vyema kwamba mtu anayefanya tohara kwa kusudi tu la kuhesabiwa haki, huyo ni sawasawa amejifunga nira ya utumwa, ametengwa na Kristu, ameanguka mbali na neema!

Ni wazi kwamba Paulo hajivunii tohara yake kama sifa ya kumpatia haki kwa Mungu.

Anadai tohara ya kweli ni kumwabudu Mungu kwa Roho na kujivunia Kristu (Wafilipi 3:3, 4).

Hivyo ndivyo hasa alivyofundisha Bwana aliposema lazima haki ya wanafunzi Wake na waumini wa kweli izidi ile ya waandishi na Mafarisayo, ambao japo walikuwa wamefanya tohara ya mwili, mioyo yao haikuwa imefanyiwa tohara—hawakuwa na uongofu halisi wala badiliko kamili la moyo.

Ni wazi Paulo anaonesha tofauti kati ya tohara, ambayo si sharti lenye mamlaka tena katika Agano Jipya, na sheria zingine za Mungu ambazo zenyewe hudumu milele.

Anasema, ^Kwa maana kutahiriwa kwafaa kama ukiwa mtendaji wa sheria, lakini ukiwa mvunjaji wa sheria kutahiriwa kwako kumekuwa kutokutahiriwa.

Basi ikiwa yeye asiyetahiriwa huyashika maagizo ya torati, hivi kutokutahiriwa kwake hakutahesabiwa kuwa kutahiriwa?^ (Warumi 2:25, 26).

Izingatiwe hapa kwamba kuhesabiwa haki, ambako hufanyika kwa neema kupitia imani katika Kristu (Waefeso 2:8-10) ni tofauti na mchakato wa utakaso, ambao wenyewe hufanyika kwa kuishi kwa hiyo neema—yaani, kuzitii amri.

Ndiyo maana Paulo anasema linapokuja suala la kuhesabiwa haki, basi imani yetu katika neema ya Kristu iokoayo ndiyo hasa inahusika, kisha matendo ya utii wa sheria hujaa kama matokeo ya kuishi kwa imani hiyo.

Basi, twaona ya kuwa mwanadamu huhesabiwa haki kwa imani pasipo matendo ya sheria. (Warumi 3:28).

Tunatii sheria kwa sababu tumeokolewa kwa neema kwa njia ya imani; hatuitii ili tuokolewe.

Yakobo anafafanua jambo hili zaidi anaposema: imani bila matendo imekufa (Yakobo 2:17).

Imani yetu katika Kristu itaoneshwa kwa matendo ya kuitii sheria, yaani kuyafanya mapenzi ya Mungu.

Je, Paulo anasema sheria haina mamlaka tena kwa sababu ya neema ya Kristu? Hapana.

Sheria ni takatifu, ya haki na njema. Sheria ni kama kioo kinachotusaidia kuitambua dhambi (Warumi 7:7, 12); bila sheria, mdhambi hawezi kuona kasoro yake na hivyo hawezi kumhitaji Kristu na neema Yake.

Kamwe Paulo haioni torati kuwa ni laana!!! Paulo anasema Mkristu muumini hahukumiwi na sheria kwa sababu kupitia Kristu hatekelezi tena tamaa za dhambi ziletazo mauti (Warumi 7:5).

Paulo anasema nini? Kwa upande mmoja anaonekana kuitetea torati, kwa upande mwingine anaonekana kuibatilisha.

Ndiyo maana Mtume Petro akatupatia onyo kuhusu kuwa makini tunapojaribu kuuelewa ujumbe thabiti ambao Paulo anauwasilisha katika kanisa la Kristu.

Je, Mkristu analazimika kutoa dhabihu ya wanyama, wanakondoo, mbuzi, nk. madhabahuni kama zamani?

Vipi kuhusu sikukuu au miandamo ya mwezi, sherehe zingine walizoagizwa Waisraeli wazidhimishe?

Habari gani juu ya makuhani na wakuu wa makuhani katika huduma za hekaluni?

Haya mambo yalikuwa vielelezo ama ishara ya Kristu ambaye angekuja na kufa Msalabani.

Alipotamka Imekwisha, pazia la hekalu likachanika vipande viwili juu hata chini, ndiyo kusema kwamba huduma hizo nazo zikafikia utimizo wao.

Paulo anasisitiza: ^Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato; mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo.^ (Wakolosai 2).


Mwanadamu anapomwamini na kumpokea Kristu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake, akaacha maisha yake ya zamani ya anasa za dhambi, anakuwa kiumbe kipya.

Hapo anahesabika kwamba ameifia torati. Na ndiyo mantiki nzima ya kielelezo cha ubatizo wa kuzamishwa kwenye maji mengi kama ishara ya kuamini mauti na ufufuo wa Yesu Kristu (Warumi 6:4).

Mwamini huyo anahesabika ameifia torati kwa sababu torati haiwezi kumhukumu tena mtu aliye milki ya Kristu.

Umiliki wake umehama kutoka kwenye dhambi na kuwa kwa Yesu na Mwokozi wa maisha yake.

Kama ambavyo mwanamke yuko huru na wala hafungwi na sheria ya ndoa baada ya mumewe kufariki (1 Wakorintho 7:1-3), kadhalika Mkristu hahukumiwi na torati anapokuwa kwenye himaya ya wokovu katika Kristu.

^Kadhalika, ndugu zangu, ninyi pia mmeifia torati, kwa njia ya mwili wa Kristo, mpate kuwa mali ya mwingine, yeye aliyefufuka katika wafu, kusudi tumzalie Mungu matunda.^ (Warumi 7:4)

Paulo anaendelea kusema kwamba wakati tukiishi nje ya Kristu, tuliiasi torati, tulitenda dhambi na hivyo torati ikatuhukumia kifo (aya ya 5).

Lakini tulipompokea Yesu, tulifunguliwa katika torati. Maana yake ni kwamba torati haituhesabu tena kama waasi bali viumbe wapya katika Kristu.

Anasema, tumeifia hali ile iliyotupinga, yaani utawala wa zamani wa dhambi na mauti juu yetu tukingali waovu.

Baada ya Mtume Paulo kuzungumzia badiliko hilo ambalo limemtokea mdhambi aliyempokea Kristu kuwa Bwana na Mwokozi wake, sasa anazungumzia matokeo husika ama lengo tarajiwa la ^kufunguliwa katika torati^ na ^kuifia hali ile iliyotupinga.^

Anaandika jawabu hilo: ili sisi tupate kutumika katika hali mpya ya roho, si katika hali ya zamani, ya andiko. (aya ya 6).

Huku ni kumtumikia Mungu chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu, ambaye hutusaidia kuzaa matunda ya Roho (Wagalatia 5:22).

Kabla ya kuhitimisha kwa kufafanua anachomaanisha Paulo anaposema hali ya zamani, ya andiko, ni vyema kukariri kwa mara nyingine tena kuhusu udaima wa sheria, torati au amri za Mungu.

Hizi bado zina mamlaka na wala hazikubatilika msalabani (Mathayo 5:17).

^Basi, hivi twaibatilisha sheria kwa imani hiyo? Hasha! Kinyume cha hayo twaithibitisha sheria.^ (Warumi 3:31).

Ili kuelewa vilivyo maana ya hali ya zamani, ya andiko, hebu tujiulize ni sehemu ipi ya torati ambayo imefikia tamati kwa kifo cha Kristu msalabani?

Bila shaka hayo ni maagizo ya torati yaliyohusu taratibu za kiibada (ceremonial laws) kama vile tohara, kafara au dhabihu za wanyama, sikukuu mbalimbali, miandamo ya mwezi, nk. (Walawi 23).

Mambo haya, ambayo ni hali ya zamani ya andiko, yalilenga wakati ujao kwenye kazi na kafara ya Kristu, nayo yalikoma alipokufa msalabani.

Inavutia kuona kwamba Paulo aliyekuwa akijivunia ufarisayo wake na tohara ya nje tu, sasa baada ya uongofu wake na kuwa kiumbe kipya anamshangilia Bwana Yesu Kristu.

Anasema, 14 Lakini mimi, hasha, nisione fahari juu ya kitu chochote ila msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambao kwa huo ulimwengu umesulibishwa kwangu, na mimi kwa ulimwengu.

15 Kwa sababu kutahiriwa si kitu, wala kutokutahiriwa, bali kiumbe kipya. 16 Na wote watakaoenenda kwa kanuni hiyo, amani na iwe kwao na rehema, naam, kwa Israeli wa Mungu.^ (Warumi 6:14-16)

Mafunzo ya Paulo yalileta mzozano na ubishi mkubwa tangu pale mwanzo katika historia ya Kanisa baina ya kikundi chake cha Wakristo waliomfuata kutoka upagani, na wale Wakristo wa asili ya Kiyahudi.

Wao walipinga moja kwa moja ile shauri ya kwenda kupelekewa mafunzo ya Ukristo mataifa waliokuwa hawakutahiriwa, wala hawaikubali sharia ya Taurati. Baadhi ya wanafunzi wa Yesu walikuwa hawakubali hata kula nao wale "wasiotahiriwa".

Wao walikuwa wanajua vyema kuwa Yesu aliwakataza wasiende kuwahubiria mataifa mengine isipokuwa Mayahudi tu, kwani ni wao ndio walikuwa wanaamini Mungu Mmoja na wao ndio wakiifuata sharia ya Mungu.

Mwishowe ulifanywa mkutano na yakawapo baadhi ya masikilizano kuwa yafaa kuhubiriwa Ukristo kwa mataifa yasiokuwa ya Kiyahudi, na wao wasilazimishwe kubeba mizigo mizito katika dini kama vile wenye asli ya Kiyahudi.

Walitumwa Paulo na Barnaba kuwaendea hao mataifa, nao ni Wazungu wa Kirumi na Kigiriki, na wakachukua barua iliomalizikia maneno haya muhimu:

Kwa maana ilimpendeza Roho Mtakatifu na sisi, tusiwatwike mzigo ila hayo yaliyo lazima, yaani, mjiepushe na vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na damu, na nyama zilizosongolewa na uasherati. Mkijizuia na hayo mtafanya vema. Wasalamu.

Matendo 15.28-29

Nyama zilizosongolewa, yaani nyama za kunyonga, zisiochinjwa. Yazingatieni haya si maamrisho ya Yesu, lakini ni masikilizano baina akina Paulo na wanafunzi wake Yesu, (kwa ridhaa ya Roho Mtakatifu) baada ya kuwa Yesu mwenyewe hayupo tena. Ikiwa hayo ndiyo waliokubaliana ilikuwaje Paulo tena kuwaandikia Wakorintho:

"Kila kitu kiuzwacho sokoni kuleni bila ya kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri" (?)

Lakini Paulo ni Paulo.

Mtakatifu Paulo anadai kuwa yeye aliteuliwa mahsusi kuwa ni mtume wa Yesu katika ufunuo (Wahyi), na kuwa bado yeye anaendelea kupata amri moja kwa moja kutokana na mwenyewe Bwana Yesu, ijapokuwa amri hizo na mafunzo hayo yanapingana kabisa na yale waliyoyapata wale wanafunzi wake Yesu waliokuwa naye mwenyewe alipokuwa hai.

Yeye Paulo hakupata kuonana na Yesu, bali yeye alikuwa ni mpinzani mkubwa wa Ukristo na akawa ni sababu ya kuteswa na kuuwawa Wakristo kadhaa wa kadhaa, mmoja wao ni Mtakatifu Stefano, shahidi wa mwanzo katika Wakristo.

Paulo alikuwa na asli ya Kiyahudi, na dini yake rasmi ilikuwa ya Kiyahudi.

Kwa kuwa alizaliwa nje ya Palastina katika mamlaka ya Kirumi alikuwa na uraia kamili wa Kirumi, na huko alipata fursa ya kusoma ilimu na falsafa za Kiyunani.

Mazingara yake yote ya Kigiriki na Kirumi yalikuwa ya kikafiri, kipagani.

Kwani Magiriki na Warumi walikuwa washirikina wenye kuamini chungu ya miungu, kama ilivyokuwa ada ya karibu mataifa yote ya wakati ule isipokuwa Mayahudi.

Yalipozuka mafunzo ya Yesu Kristo, ambayo kwa asli yake hayakuwa ila ni kuendeleza ile ile imani ya Kiyahudi ya Mungu Mmoja na kufuata sharia ya Taurati na kuongeza uchamngu, na ikawa mafunzo hayo yanaendelea juu ya kupingwa,

Paulo aliona anaweza kuipa nguvu hiyo dini au kwa hakika madhehebu mpya kwa kuwatia wale Warumi na Magiriki kwa kuchanganya imani zao na falsafa zao pamoja na imani ya Kiyahudi. Mayahudi wanaamini Mungu Mmoja, ndio.
Ukristo unaamini Mungu Mmoja.

Magiriki na Warumi wanaamini miungu mingi, si chini ya watatu, ndio na Ukristo nao unaamini hivyo.

Jee, si pana mgongano hapo?

La, katika Ukristo imani ni ya Mungu Mmoja katika Utatu Mtakatifu: Mungu Mmoja, mwenye nafsi tatu, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu.

Mapagani wa Kigiriki na Kirumi wakiamini mungu aliyekufa, akafufuka na akapaa mbinguni.

Hilo si kitu wanaweza kuendelea na imani hiyo katika Ukristo.

Wazungu magovi hawataki kutahiriwa.

Hapana kitu, kutahiriwa si kitu wala kutotahiriwa.

Hoja ipatikane tahara ya roho.

Wazungu wamezoea kula kila kitu, nguruwe, damu, kilichochinjwa na kisichochinjwa. Hilo si tatizo, mtaendelea vivyo hivyo, kwani dhambi ni kitokacho mdomoni, sio kiingiacho.

Kuleni kila kiuzwacho sokoni.

Hapana halali wala haramu.

Huo ndio Ukristo mpya wa Paulo, na hiyo ndio Thiolojia yake ambayo, inasikitisha Wakristo wameifuata, wakayaacha mafunzo mepesi na yaliyonyooka ya mwenyewe Yesu Kristo.
 
Mungu atake sadaka ya damu ya mtu imsaidie nini?

Huyo Mungu mwenye kutaka kafara ya damu hafai kabisa.

Qur'an watafsiri wamepachika pachika yao lakini hakuna upuuzi huo kwenye Qur'an. Allah hahitaji kafara yoyote.

Naahidi, In shaa Allah kaa nipo hai nitakuja na kisa cha Ibrahim na Ismail vya kwenye Qur'an bila kuongezea wala kusherehesha, Qur'an inajitisheleza, nitachafanya mimi ni kufa "tafsil" tu.

Sasa hivi nimeanza uzi wa kisa cha Yesu wa kwenye Qur'an na nimeazia kwa John na Zacharia.

Ulikuwa unafahamu kuwa John baba'ke ni Zakaria? Ukitaka kufahamu wameongelewa vipi kwenye Qur'an, bofya chini hapo:

Thanks for this
P
 
Sasa hivi nimeanza uzi wa kisa cha Yesu wa kwenye Qur'an na nimeazia kwa John na Zacharia.

Ulikuwa unafahamu kuwa John baba'ke ni Zakaria? Ukitaka kufahamu wameongelewa vipi kwenye Qur'an, bofya chini hapo:

uki follows the links unakutana na ujumbe huu
" Kumradhi! Kuna changamoto kidogo"
"You do not have permission to view this page or perform this action".

P
 
Mungu atake sadaka ya damu ya mtu imsaidie nini?

Huyo Mungu mwenye kutaka kafara ya damu hafai kabisa.

Qur'an watafsiri wamepachika pachika yao lakini hakuna upuuzi huo kwenye Qur'an. Allah hahitaji kafara yoyote.

Naahidi, In shaa Allah kaa nipo hai nitakuja na kisa cha Ibrahim na Ismail vya kwenye Qur'an bila kuongezea wala kusherehesha, Qur'an inajitisheleza, nitachafanya mimi ni kufa "tafsil" tu.

Sasa hivi nimeanza uzi wa kisa cha Yesu wa kwenye Qur'an na nimeazia kwa John na Zacharia.

Ulikuwa unafahamu kuwa John baba'ke ni Zakaria? Ukitaka kufahamu wameongelewa vipi kwenye Qur'an, bofya chini hapo:



Tatizo kubwa la Quran na history yake it is very hard to prove authentic ya hizo Hadithi historically na pia watafsiri wa Quran they tried so much kufanya Biblia ambayo was already there 2000 years before Quran ionekane ni uongo at the end they have to go back to Bible kupata certain references au parallel to their teachings.

Mfano Jina la Yesu, Waislam wamehangaika sana kutafsiri neno Iēso and at the end they Used Isa na wakatunga mtu mpya kabisa

Jesus (/ˈdʒiːzəs/) is a masculine given name derived from Iēsous (Ἰησοῦς; Iesus in Classical Latin)
 
Tatizo kubwa la Quran na history yake it is very hard to prove authentic ya hizo Hadithi historically na pia watafsiri wa Quran they tried so much kufanya Biblia ambayo was already there 2000 years before Quran ionekane ni uongo at the end they have to go back to Bible kupata certain references au parallel to their teachings.

Mfano Jina la Yesu, Waislam wamehangaika sana kutafsiri neno Iēso and at the end they Used Isa na wakatunga mtu mpya kabisa

Jesus (/ˈdʒiːzəs/) is a masculine given name derived from Iēsous (Ἰησοῦς; Iesus in Classical Latin)
Hayo unayosema hayana ukweli wowote, kama u mkweli weka nukuu japo ya Qur'an ilipoingilia kisa chochote cha Biblia. Usifate watafsiri au washereheshaji kwani una uhakika gani kuwa wote ni Waislam?

Unataka kufananisha mkusanyiko wa vitabu vilivyotiwa mikono ya watu na kitabu kimoja kisochokuwa na mfano wake diuniani?

Isome Qur'an kijana ipo kwa ajili yako pia.

Mfano mzuri ni mimi nakwambia hakuna hata jina Sarah kwenye Qur'an, prove me wrong, uweke nukuu ya Qur'an yenye Sarah.
 
Tatizo kubwa la Quran na history yake it is very hard to prove authentic ya hizo Hadithi historically na pia watafsiri wa Quran they tried so much kufanya Biblia ambayo was already there 2000 years before Quran ionekane ni uongo at the end they have to go back to Bible kupata certain references au parallel to their teachings.

Mfano Jina la Yesu, Waislam wamehangaika sana kutafsiri neno Iēso and at the end they Used Isa na wakatunga mtu mpya kabisa

Jesus (/ˈdʒiːzəs/) is a masculine given name derived from Iēsous (Ἰησοῦς; Iesus in Classical Latin)
Unapoongea kuhusu biblia unakusudia biblia ipi ? KJV, QJV, RSV, AV Mormon Bible au maelfu ya Biblia tofauti?
 
King James or anything ni translation. But all of the Bibles are older than Quran

Mimi sijakuuliza ipi older , nilikuuliza hiyo Quran inachukuwa reference kutoka biblia ipi ??

ya Mormon , KJV, QJV, AV , Mormon Bible au maelfu ya biblia tofauti ??

Kwa kukuongezea kama unaelewa kiengereza msikilize huyu anayefantya kazi sehemu ya kuhifadhia hizo bible za zamani anasema nini



 
Kinacho ni shangaza ni kuona watoto 12 wa Yakobo(Israel)wametokana na wanawake wanne na sheria hizo hizo za kiyahudi zinawatukuza.Ila pia kumbuka Ibrahim aliishi miaka mingi sana kabla ya kuwepo uyahudi.
 
Bro kama ukiwa na mtoto kabla ya kuoa na baadae ukaoa ukapata watoto unafikiri ni nani atabeba jukumu la kuwa mkubwa kwenye familia? Aliyepatikana Kwa agano au zao la uzinzi?
Pia ahadi ya Mungu ilikua ni kumpa uzao kupitia mke wake halali Sara. Jina la ukoo haliendelezwi na mzaliwa wa nje na ndo maana hata Waislamu wenyewe huwa wanasema mtoto wa nje ni wa mama yao. Iweje Ishmael awe tofauti?
Mtoto wa mjakazi atabaki kuwa wa hadhi ya chini kuliko wa mke wako wa ndoa. Siku unagawa urithi watoto wa ndoa unawarithisha ila wa mchepuko unampa zawadi. Kuna tofauti kubwa kati ya kurithi na kuzawadiwa.
Kinacho ni shangaza ni kuona watoto 12 wa Yakobo(Israel)wametokana na wanawake wanne na sheria hizo hizo za kiyahudi zinawatukuza.Ila pia kumbuka Ibrahim aliishi miaka mingi sana kabla ya kuwepo uyahudi.
 
Kumbuka Ibrahim hakuwa mgumba?

Ungeanza kuuliza tamaduni na sheria za Kale za kiebrània zilikuwa zinasemaje.

Mtoto wa kijakazi nd Suria hahesabiki kama mtoto wa pekee yaani astahiliye urithi.
Mtoto wa mke halali wa ndoa ndiye mtoto anayetambulika


Alafu waislamu haohao sio kwamba hawajui hi,o sheria kwa sababu wanazitumia mpaka hivi leo.
Mtoto haramu haitwi kwa jina la Baba na wala hastahili urithi

Hizo ni sheria za zamani huko mashariki ya kati
Kinacho ni shangaza ni kuona watoto 12 wa Yakobo(Israel)wametokana na wanawake wanne na sheria hizo hizo za kiyahudi(kiebrania)zinawatukuza.Ila pia kumbuka Ibrahim aliishi miaka mingi sana kabla ya kuwepo kwa sheria za kiyahudi.
 
Ujuwe tu kuwa Quran ina miaka 1400 wakati Bibilia ina miaka zaidi ya 2000. Hapo utagundua ni nani kakopi kwa nani?

Halafu kuna watu wanadanganywa eti Mtume wao aliteremshiwa kitabu. Uwongo mtupu
Biblia ina edition ngapi??? Mpaka sasa Qur'an kuna edition ngapi mpaka sasa???
 
Suria upo wa aina mbili katika mazingira ya zamani.
1. Suria aliyechaguliwa ña Mke halali
Sarah alimchagua Hajiri.
Lea ma Rahel wakachagua vijakazi wao kuwa masuria.
2. Suria aliyechaguliwa na Mume.
Suleiman anaingia katika kundi hili.

Suria anabaki kuwa Suria na hawezi kuwa kwenye hadhi sawa ya Mke.
Biblia inaposema Suleiman alikuwa na Wake mia saba na masuria Miatatu inamaana kubwa kisheria.

Mke yupo kisheri na anapatikana kisheria kulingana na mila na tamaduni za Kale kama vile Kutoa mahari n.k.
Suria au hawara hatambuliki kisheria za kizamani,

Torati ambayo ni sheria ya Kiyahudi haitambui kitu kitu kinaitwa Suria
Inatambua Mke.

Tukija kwenye m/Watoto.

Mtoto wa kwanza kisheria za dini ni yule aliyezaliwa ndani ya ndoa. Kwa mke halali.

Kidini hasa za Ibrahim au kimila hata hapa Afrika mtoto wa kwanza ni yule ambaye umezaa ndani ya ndoa.
Bahati nzuri sheria za kiislamu zinaeleza hilo.

Tukirudi kwenye mfano uliotoa kuwa mbona Watoto wa masuria wa Yakobo walihesabika na kupewa urithi

Walihesabika kwa sababu walijua kula na kipofu.
Waliwaheshimu Wake wa Yakobo ambao ndio waliowateua kuwa masuria.

Hii ni tofauti na Hajiri ambaye alileta ujeuri na kiburi akataka ligi na mke halali wa ndoa akasahau mke huyo ndiye aliyechagua amsaidie baadhi ya majukumu na ndiye mwenye mamlaka ya kumfukuza.

Ibrahim akamwambia Mkewe Sarah kuwa huyo kijakazi wake yupo chini yake(wala sio chini ya Ibrahim) hivyo yeye ndiye mwenye maamuzi ya kumfukuza au kumbakiza.

Pascal Mayalla uliona wapi Suria mwenye hadhi sawa na mke mamlaka ya kumfukuza ikawa kwa mke mkubwa?

Tuzingatie, vijakazi wote zamani walikuwa wanakuja na Wanawake wanaoolewa tokea huko kwao au wanatafuta wenyewe na sio kAzi y mume kutafuta kijakazi wa kumsaidia mke.

Tena Baba Mkwe wa mwanamke ndiye humsaidia binti yake kumtafutia kijakazi binti yake.

Tukija kwenye urithi, baba anahaki ya kutoa urithi kwa watoto kulingana na vile awaonavyo.
Ni ngumu Mwanamke uliyetalakiana naye au kugombana naye ukatoa urithi kwa watoto wake ingawaje ni wako pia. Unaweza ukawapa lakini hawawezi kufikia donge nono kwa watoto ambao mama yao alikuwa anakufurahisha.

Tumeona Kwa Ibrahim jambo hilo lilifanyika. Kwa Yakobo tumeona Yusuphu na Yuda wakipendelewa.

Kwa Daudi tumeona Suleiman akipendelewa ilhali kuna Wakubwa zake.

Na kwa zama za leo tumeona Kesi ya Tajiri marehemu Mengi.
Pia tumeona Wake wadogo wakipendelewa au watoto wa mke mdogo wakipendelewa hii yote ni kutokana na uhusiano wa mume na wake zake.

Sio mume na masuria. Nop.

Pascal Mayalla hebu twende sawa kwanza tuone jinsi gani mikanganyiko ilivyo kwenye biblia kuhusiana na hii story ya Ismael na Isaka.


Je Hagar na mwanawe Ismael walipelekwa Jangwani kipindi Isaka hajazaliwa au baada ya kuzaliwa?

Kwa mujibu wa Biblia Ibrahim alimzaa Ismael akiwa na umri wa miaka 86 (mwanzo 16:16)

Na kwa mujibu wa biblia, Ibrahim alikuwa na miaka 100 pindi anapata mtoto wa pili ambaye ni Isaka (mwanzo 21:5)

Kwa maana Ismael tayari alikuwa na miaka 14.

Kwa mujibu wa Biblia tukio la Ismael na mama yake kutolewa na kuhamishiwa jangwani lilitokea mara baada ya Isaka kuacha ziwa (kunyonyeshwa) kwa maana ni kipindi Ibrahim ana miaka 103 hivi...huku Ismael akiwa na miaka 17 akiwa tayari kashabalehe.

Ila tukirejea katika biblia (mwanzo 21:14-19) tukio la Ismael kupelekwa jangwani halioneshi kuwa ni la kijana wa miaka 17 bali ni mtoto mchanga. Kwanini?
Ili swali ajibu Che mittoga
 
Hekima ya Mungu haichunguziki. Hata upumbavu wake ni mwema kuliko hekima yetu binadamu. Tumaini Leo, kesho tutajua zaidi kama yeye atujuliavyo zaidi. Hiyo ni ahadi tuliyopewa.
 
Habari stormryder
Japo sikuzungumzia kuhusu Ibrahimu Kufika Makka/Bakka ila ninaweza kuwa nina majibu ya Huenda alifika Makka au Bakka..

Kwanza nitadeclare Interest:- Mimi sio Muislamu,Muarabu wala Mkristo..
Ila ni Mtu wa kuchunguza na Kuweka Fact mezani...


Kwanza kabisa katika Mapito ya Ibrahimu Alizaliwa Ur of the Chaldeans (Uru wa Wakaldayo) ambayo ilipatikana Mesopotamia..Ambayo kwa sasa inaitwa modern town of Tell el-Muqayyar in southern Iraq..
So naweza kusema Kuwa Ibrahimu Alizaliwa Iraq ambapo Ni Uarabuni..


(Soma Mwanzo 11:31-32)

Tuendelee.. Abrahimu Aliishi Shuri (Ambayo kwa Sasa Huitwa saudi Arabia au Macca na medina)

Mwanzo 20:1
"Ibrahimu akaondoka huko kwenda nchi ya kusini, akakaa kati ya Kadeshi na Shuri, naye akatembea katika Gerari."



Na Je Hajari na Mwanaye walikimbilia Wapi?

Mwanzo 16:7
"Malaika wa BWANA akamwona kwenye chemchemi ya maji katika jangwa, chemchemi iliyoko katika njia ya kuendea Shuri"

Je Hiyo Shuri Iko wapi kwa Sasa?
Jaribu kusoma Historia Utajua..
Wote Tunafahamu kuwa Shuri Ipo karibu na Bahari ya Shamu Humo ndyo Mlima sinai ulipo..(Kutoka 15:22)

Sasa Mlima sinai Upo wapi?

Wagalatia 4:25

"Maana Hajiri ni kama mlima Sinai ulioko Arabuni, umelingana na Yerusalemu wa sasa; kwa kuwa anatumika pamoja na watoto."

Sasa kwakuwa Sasa Tunajua kuwa Ibrahimu alikaa Shuri yaani Uarabuni....

Kwanini Sasa Tutaje makka.. Nifuatishe hapa Chini..

Zaburi 84:6-8 (Psalms)

"As they pass through the Valley of Baca, they make it a place of springs; the autumn rains also cover it with pools.
They go from strength to strength, every one of them in Zion appeareth before God.

O LORD God of hosts, hear my prayer: give ear, O God of Jacob. Selah."

Umeona valley of Baca/Bakka/Makka?
Sasa hao wanaoenda Makka/Bakka ni kina nani?

Najua unaweza ukashangaa ila Jina Jingine la Maca ni baca..
View attachment 3021297

Kama una swali Unaweza kuniuliza nitakujibu
Asante
 
Back
Top Bottom