Jasusi Honda ndani ya mpango wa Congo

Jasusi Honda ndani ya mpango wa Congo

Nimemkumbuka sana Kasuku (Remmy) na Mtega nyoka. Natarajia sehemu inayofuata tutarudishwa Mwanza


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
RIWAYA: MPANGO WA CONGO

SEHEMU YA 19


Remi alipotoka kituo cha polisi alihitaji sana kuonana na Mwasu lakini pia alihitaji kupumzika walau saa kadhaa baada ya kuwa kwenye heka heka kwa siku kadhaa.

Akajipekua kwenye sidiria aliokuwa amevaa na kutoa kikaratasi kilichokuwa na namba za simu za Malima mtu aliesemekana kuwa na mahusiano na Mwasu.


Kwa msaada wa vijana waliokuwa wamesimama karibu yake,walifanikiwa kupata simu ambayo walimpa Remi.

Remi akampigia Malima.

****

Malima alikuwa ndani kwake akiwa ameshika kiuno huku akitikisa kichwa kushoto kwenda kulia na kulia kwenda kushoto.

Alichanganyikiwa!!

Alikuwa ametumia zaidi ya saa tatu akitafuta nyaraka fulani zilikokuwa kwenye mkoba wake wa kazini bila mafanikio.

Alipekuwa kila pahali bila kupata jawabu la wapi alipoziweka.
Mwanzo alidhani aliziacha ofisini lakini kumbukumbu zake zilimwambia hajawahi kuacha hizo nyaraka kila alipokwenda.

Na alikumbuka vyema kabisa ya kuwa hata wakati yupo msibani,nyaraka zile zilikuwa ndani ya gari hadi wakati aliporuhusu gari limpeleke Mwasu mgahawani kwake Igoma.

Kila alipofikiria ni nani hasa anaeza kuwa amezichukua kati ya dereva na Mwasu; hakupata jibu.

Hakuona kama Mwasu anaeza kuwa amezichukua nyaraka zile muhimu wakati ule ama dereva wake ambae amemwamini zaidi ya miaka mitatu.

Zipo wapi? Hakujua.

Alirudi tena kwenye mkoba na kutazama,alikuta nyaraka zingine zipo kama kawaida isipokuwa zile nyaraka tu.

Akaingiwa na wasiwasi.

Akatamani kumpigia mkubwa wake wa kazi ambae ndie aliempa kazi ya kuzimilisha nyaraka zile baada ya zile za mwanzo kuonekana zinahitaji marekebisho kadhaa.

Mbali ya yote ni kuwa mkubwa wake wa kusanifu majengo alikuwa amemwambia kazi ile ina pesa nyingi sana na pia ni sifa kwa kampuni yao kupata kazi ile ya serikali.

Alichanganyikiwa zaidi baada ya kugundua umuhimu wa kazi ile.

Wakati akiwa amekata tamaa ya kuzipata nyaraka zile ni wakati aliposikia simu yake ikiita kwa fujo.

Akasonya huku akienda kuipokea.

Alikutana na namba ngeni!!

Akapokea!!

"Habari!!" Ikasabahi sauti kavu ya kike.

Malima akasita kujibu huku akijaribu kubahatisha sauti itakuwa ya nani bila kupata majibu.


"Nzuri" akajibu Malima kwa sauti ya kukwaruza.

"Naongea na Malima!!" ikahoji sauti upande wa pili.

"Ndio,nawe nani?" akahoji Malima.

"Naitwa Remi!!" ikajibu sauti upande wa pili.

"Nikusaidie nini usiku huu" akauliza Malima.

"Naomba nielekeze au nipe namba za Mwasu tafadhali!!" akasema Remi.

"Mwasu!!" akashangaa Malima.

Ukapita ukimya wa nusu dakika.

"umepata vipi namba yangu!!" akauliza Malima baada ya kutilia mashaka mtu aliempigia.

"Samahani ndugu mi ni mdogo wake Mwasu; kupata namba nitakweleza siku nyingine ndugu!" akaeleza Remi.

Malima akakaa kimya kidogo kisha akauliza.

"Upo wapi!!?"

"Nipo hapa Soko la Mwendesha!!" akajibu Remi huku akimtizama kijana aliempa simu ambae alitikisa kichwa kuafiki ni sahihi alipotaja.

"Subiri kidogo!!" Malima akasema na kukata simu kisha akampigia Mwasu.


"Nambie mpenzi!!" ilisema sauti ya Mwasu baada ya kupokea simu.

"Samahani kwa kukusumbua usiku!!" alijitetea Malima.

"usiwe na shaka upo huru kunipigia muda wowote ule unaojisikia mpenzi." Mwasu alimtoa wasiwasi Malima.

"Ok! Nimepigiwa simu hapa na binti anaitwa Remi...!" hakumaliza alichotaka kusema akasikia mshituko alioupata Mwasu.

"Wewe unasema nani vile!!" aliuliza Mwasu huku akinyanyuka kitandani alipokuwa amejilaza huku kanga ikimdondoka na kubaki uchi.

Hakujali wala!!


"Remi!!" alijibu Malima na kuzisikia pumzi za Mwasu alizopandisha na kuzishusha kwa mkupuo.

"Kasema yuko wapi saivi!!" aliuliza Mwasu.

"Soko la Mwendesha" alijibu.


"Naomba umwambie anisubiri hapo hapo asitoke lakini pia mwambie namna ya kunipata!" alisema Mwasu huku akikita simu.

Malima akabaki akiitazama simu yake bila kufanya lolote.

Yalimchanganya mambo.

Akabinua mabega yake kuashiria hayamhusu.

Akampigia tena Remi.

Simu ikapokelewa.

"Kanambia umsubiri hapo hapo atakuja kukufuata ila akikawia shuka chini kutoka hapo ulipo ulizia kanisa la wokovu, na ukifika hapo ulizia kwa Bibi Tuku. Sawa!!" akaelekeza Malima.

"sawa" akajibu Remi na Malima akakata Simu.

Malima akakaa kwenye sofa huku akirudi kuwaza zilipo nyaraka za ofisi.

Hakupata usingizi.

*****

Ilikuwa saa, ikatimia hadi lisaa la pili bila kumuona Mwasu ama dalili ya kutokea Mwasu na kutoka pale alipokuwa tayari watu walianza kupungua baada ya usiku kuanza kuwa mkubwa.

Remi alitamani kuondoka pale alipokuwa ili aelekee huko kanisani kumtafuta Mwasu ila akajionya huenda kufanya hivyo kungempelekea Mwasu kumkosa.


Akavuta zaidi subira.

Kwake subira haikuwa heri,muda ulienda bila Mwasu kutokea.

Remi alikuwa amekaa kwenye kibalaza cha duka la kuuza filamu na mbele yake pia kulikuwa na duka lingine la kuuza filamu kifupi eneo lile lilizungukwa na maduka mengi ya kurudufu filamu na muziki.

Duka la tatu kutoka alipokuwa Remi kulikuwa na vijana wawili waliokuwa wamesimama kama hawafahamiani huku mara kwa mara wakimtizima kwa kuibia.

Remi hakutaka kuwatilia mashaka na aina ya utazamaji wao ila wasiwasi wake ulizidi pale ambapo mwenye duka alifunga na wale vijana wakabaki wakiwa wamesimama bila kuonesha jitihada zozote za kuondoka.

Remi aliishi kwa mashaka siku zote hivyo hakutaka kuendelea kukaa pale wakati roho yake haitaki.

Akanyanyuka huku akiwatizama vijana wale ambao nao walinyanyuka na kuanza kumfuata.


Remi aliongeza hatua za miguu yake,vijana nao wakaongeza hatua.

Remi akaingia katikati ya soko pweke lililogubikwa na kiza kizito.

Alipokelewa na kelele za mapaka shume yaliokuwa yanagombania mabaki ya chakula sokoni pale.

Akapiga hatua akiwa na lengo la kupotelea gizani ili kuwapoteza vijana wao ambao alijua dhamira yao.

Hakufika mbali akasikia sauti ikiamuru nyuma yake.

"Simama hivyohivyo!" ilikuwa sauti ya watu iliojaa mamlaka.

Remi akasimama na akageuka na akashuhudia vijana wale wakija mkukumkuku wakiwa wamewasha taa za simu zao.

Lakini hakumuona alieamrisha asimame.

Remi matatani tena!!
 
MPANGO WA CONGO..

SEHEMU YA 20


Vijana wale walimsogelea Remi.

"Tafadhali binti tulia usifanye ujanja wowote!!" alionya mmoja wa vijana wale huku akimsogelea Remi akiwa na bastola mkononi.

Remi akili yake ilifanya kazi harakaharaka bila kupata la kufanya kutoka mikononi mwa vijana wale walioonesha hawana mzaha endapo akiwabugudhi.

Remi akabaki akijiuliza alipo mtu wa tatu ambae alimkoromea na kumfanya asimame na hapo ndipo akafanya akili yake ivute subira kufanya lolote mana hakujua alieamrisha ni upande gani yupo na yupo kwa niaba ipi.

"Huwezi kutukimbia Remi yani wajisumbua tu" alisema kijana mwingine huku akifanya jitihada kuikwepa meza moja ya matunda iliokuwa imewatenganisha.

Remi akapiga hatua moja nyuma ili kujiweka mbali na watu wale lakini jamaa mmoja akamwonya ya kuwa asiendelee kusogea.

"Tulia hivyo hivyo,hatua nyingine nakupasua ubongo wako!!" alikoroma jamaa.

Remi akatulia!!

Jamaa mmoja akamkaribia zaidi huku akiweka simu sikioni kuashiria alihitaji kumpigia mtu wakati huo.

"Tupo nae...ndio..eeh!!" alisema jamaa huku Remi akishindwa kujua walichozungumza.

Punde yule jamaa akampa simu Remi.

Remi akaipokea na kuweka sikioni na kubaki kimya.

"Hatuna shida na wewe endapo ukiwapa hao vijana mzigo wetu na watakwacha uende zako" iliunguruma sauti iliojaa upole wa hali ya juu kana kwamba ni tabibu akisema na mgonjwa wake.

"Najua mtaniua nikiwapa ila.." alikatishwa Remi..

"Kukuua hata sasa vijana wangu wanaweza kukuua ila hatuna nia hiyo kabisa binti!!" ilisihi sauti ile ambayo Remi aliitambua vilivyo.

Remi alijuwa hawawezi kumwacha salama na usalama wake pekee ni kuendelea kuwa na alichonacho mana hata akiwapa bado alishuhudia mengi hivyo ni lazima azibwe mdomo.

Hata!!..

Remi alijakatilia nafsini mwake.

"Haiwezekani niueni tu!" alisema Remi.


Upande wa pili ulikaa kimya kwa muda bila kusema lolote.

"Una hakika unataka kufa Remi!!?" ilihoji sauti upande wa pili.

"Ndio!!" alijibu kimkato Remi.

"Wewe unakufa! Tabibu wako Santina je!?"


Eeh bana eeh!!

Remi alistuka manusura adondoshe simu.

Lilikuwa ni jambo jipya kwake hasa kutajiwa jina la tabibu Santina.

Ndipo alipoamini watu wale kweli wanamkono mrefu.

Akaamua kucheza pata potea!!


"Muueni nae, ila hautakuwa mwisho wa haya mambo" alisema Remi kwa sauti ya kitetemeshi.

Alicheka mtu wa upande wa pili,kisha akasema.

"Chaguo ni la..." sauti haikumalizia likatokea tukio la kustukiza ambapo mlinzi wa soko lile alitokea gafla na kuanza kuita kelele za mwizi huku akipiga filimbi na Remi hakutaka kuipoteza nafasi ile nae akairusha juu simu ile aliokuwa nayo.
Wakati jamaa mwingine akigeuka kumkabili mlinzi, jamaa aliekuwa karibu na Remi akatoa sauti ya hamaniko kwa kitendo kile alichokifanya Remi.

Akajitia mjuzi wa kutaka kuidaka simu yake mpya na ya garama, wakati yupo katikati ya jitihada zake hizo za kuokoa simu ndipo Remi akaachia kifuti kilichompata jamaa yule katikati ya kifua na kumbwaga chini yule jamaa ambae alibaki akitoa miguno kama kahaba aliedhulumiwa haki yake ya kifedhuli.

Jamaa mwingine akashindwa cha kufanya,iwapo amsaidie mwenzie ama amdhibiti mlinzi ambae bado alikuwa anapiga filimbi na kelele za mwizi.

Remi alimsoma vizuri bwana yule wakati anajinyanyua akiwa amepiga magoti.
Remi akamuwahi kwa teke safi lililoenda moja kwa moja kwenye shingo ya jamaa na kumrudisha chini asiamini kama ni Remi aliemtwanga teke lile.

Remi alijua yeye si mjuzi wa ngumi hivyo kuendelea kuwa pale ni kujiweka hatarini zaidi hivyo akaamua kuumwaga huku akijishangaa namna alivyoweza kumdhibiti yule jamaa.

Jamaa mwingine alipoona Remi ameumwaga akaamua nae kumaliza kelele za Mlinzi.
Ambapo alimtandika teke moja la kifua lililokata kelele zote na kumwacha mlinzi akibweka chini kama mbwa koko jalalani.

Akaenda kumnyanyua mwenzie aliekuwa amekaukwa na koo baada ya teke la Remi kumpata sawasawa.

Ikazuka tafrani ndani ya soko huku panya na paka shume wakishindwa kujua Dunia yao imeingiliwa na nini.

Remi alitokomea kwa kupita Mashi hotel kisha akatokezea shule ya Nyakato na kushika njia ya machinjioni.

Kama alidhani vijana wale walimwacha alikosea bado walikuwa nyuma yake haihai.

Kila kichochoro alichopita Remi na wao walipita huku wakiwa makini asiwapotee.

Remi akiwa anakaribia kufikia kiwanda cha pamba mara mbele yake likatokea gari lililowasha taa kali na kummlika usoni.

Akainama chini ili asiumie macho yake na bila kusema lolote kwa kitendo kile japo alijua si salama kwake na alipogeuka nyuma bado vijana wale walikuwa wanamnyemelea huku wakionekana kutokujali kabisa uwepo wa gari lile liliwamulika makusudi.

Remi matatani tena!!
 
Safi sana mkuu nakuomba malizia moja mid mida
RIWAYA: MPANGO WA CONGO

SEHEMU YA 19


Remi alipotoka kituo cha polisi alihitaji sana kuonana na Mwasu lakini pia alihitaji kupumzika walau saa kadhaa baada ya kuwa kwenye heka heka kwa siku kadhaa.

Akajipekua kwenye sidiria aliokuwa amevaa na kutoa kikaratasi kilichokuwa na namba za simu za Malima mtu aliesemekana kuwa na mahusiano na Mwasu.


Kwa msaada wa vijana waliokuwa wamesimama karibu yake,walifanikiwa kupata simu ambayo walimpa Remi.

Remi akampigia Malima.

****

Malima alikuwa ndani kwake akiwa ameshika kiuno huku akitikisa kichwa kushoto kwenda kulia na kulia kwenda kushoto.

Alichanganyikiwa!!

Alikuwa ametumia zaidi ya saa tatu akitafuta nyaraka fulani zilikokuwa kwenye mkoba wake wa kazini bila mafanikio.

Alipekuwa kila pahali bila kupata jawabu la wapi alipoziweka.
Mwanzo alidhani aliziacha ofisini lakini kumbukumbu zake zilimwambia hajawahi kuacha hizo nyaraka kila alipokwenda.

Na alikumbuka vyema kabisa ya kuwa hata wakati yupo msibani,nyaraka zile zilikuwa ndani ya gari hadi wakati aliporuhusu gari limpeleke Mwasu mgahawani kwake Igoma.

Kila alipofikiria ni nani hasa anaeza kuwa amezichukua kati ya dereva na Mwasu; hakupata jibu.

Hakuona kama Mwasu anaeza kuwa amezichukua nyaraka zile muhimu wakati ule ama dereva wake ambae amemwamini zaidi ya miaka mitatu.

Zipo wapi? Hakujua.

Alirudi tena kwenye mkoba na kutazama,alikuta nyaraka zingine zipo kama kawaida isipokuwa zile nyaraka tu.

Akaingiwa na wasiwasi.

Akatamani kumpigia mkubwa wake wa kazi ambae ndie aliempa kazi ya kuzimilisha nyaraka zile baada ya zile za mwanzo kuonekana zinahitaji marekebisho kadhaa.

Mbali ya yote ni kuwa mkubwa wake wa kusanifu majengo alikuwa amemwambia kazi ile ina pesa nyingi sana na pia ni sifa kwa kampuni yao kupata kazi ile ya serikali.

Alichanganyikiwa zaidi baada ya kugundua umuhimu wa kazi ile.

Wakati akiwa amekata tamaa ya kuzipata nyaraka zile ni wakati aliposikia simu yake ikiita kwa fujo.

Akasonya huku akienda kuipokea.

Alikutana na namba ngeni!!

Akapokea!!

"Habari!!" Ikasabahi sauti kavu ya kike.

Malima akasita kujibu huku akijaribu kubahatisha sauti itakuwa ya nani bila kupata majibu.


"Nzuri" akajibu Malima kwa sauti ya kukwaruza.

"Naongea na Malima!!" ikahoji sauti upande wa pili.

"Ndio,nawe nani?" akahoji Malima.

"Naitwa Remi!!" ikajibu sauti upande wa pili.

"Nikusaidie nini usiku huu" akauliza Malima.

"Naomba nielekeze au nipe namba za Mwasu tafadhali!!" akasema Remi.

"Mwasu!!" akashangaa Malima.

Ukapita ukimya wa nusu dakika.

"umepata vipi namba yangu!!" akauliza Malima baada ya kutilia mashaka mtu aliempigia.

"Samahani ndugu mi ni mdogo wake Mwasu; kupata namba nitakweleza siku nyingine ndugu!" akaeleza Remi.

Malima akakaa kimya kidogo kisha akauliza.

"Upo wapi!!?"

"Nipo hapa Soko la Mwendesha!!" akajibu Remi huku akimtizama kijana aliempa simu ambae alitikisa kichwa kuafiki ni sahihi alipotaja.

"Subiri kidogo!!" Malima akasema na kukata simu kisha akampigia Mwasu.


"Nambie mpenzi!!" ilisema sauti ya Mwasu baada ya kupokea simu.

"Samahani kwa kukusumbua usiku!!" alijitetea Malima.

"usiwe na shaka upo huru kunipigia muda wowote ule unaojisikia mpenzi." Mwasu alimtoa wasiwasi Malima.

"Ok! Nimepigiwa simu hapa na binti anaitwa Remi...!" hakumaliza alichotaka kusema akasikia mshituko alioupata Mwasu.

"Wewe unasema nani vile!!" aliuliza Mwasu huku akinyanyuka kitandani alipokuwa amejilaza huku kanga ikimdondoka na kubaki uchi.

Hakujali wala!!


"Remi!!" alijibu Malima na kuzisikia pumzi za Mwasu alizopandisha na kuzishusha kwa mkupuo.

"Kasema yuko wapi saivi!!" aliuliza Mwasu.

"Soko la Mwendesha" alijibu.


"Naomba umwambie anisubiri hapo hapo asitoke lakini pia mwambie namna ya kunipata!" alisema Mwasu huku akikita simu.

Malima akabaki akiitazama simu yake bila kufanya lolote.

Yalimchanganya mambo.

Akabinua mabega yake kuashiria hayamhusu.

Akampigia tena Remi.

Simu ikapokelewa.

"Kanambia umsubiri hapo hapo atakuja kukufuata ila akikawia shuka chini kutoka hapo ulipo ulizia kanisa la wokovu, na ukifika hapo ulizia kwa Bibi Tuku. Sawa!!" akaelekeza Malima.

"sawa" akajibu Remi na Malima akakata Simu.

Malima akakaa kwenye sofa huku akirudi kuwaza zilipo nyaraka za ofisi.

Hakupata usingizi.

*****

Ilikuwa saa, ikatimia hadi lisaa la pili bila kumuona Mwasu ama dalili ya kutokea Mwasu na kutoka pale alipokuwa tayari watu walianza kupungua baada ya usiku kuanza kuwa mkubwa.

Remi alitamani kuondoka pale alipokuwa ili aelekee huko kanisani kumtafuta Mwasu ila akajionya huenda kufanya hivyo kungempelekea Mwasu kumkosa.


Akavuta zaidi subira.

Kwake subira haikuwa heri,muda ulienda bila Mwasu kutokea.

Remi alikuwa amekaa kwenye kibalaza cha duka la kuuza filamu na mbele yake pia kulikuwa na duka lingine la kuuza filamu kifupi eneo lile lilizungukwa na maduka mengi ya kurudufu filamu na muziki.

Duka la tatu kutoka alipokuwa Remi kulikuwa na vijana wawili waliokuwa wamesimama kama hawafahamiani huku mara kwa mara wakimtizima kwa kuibia.

Remi hakutaka kuwatilia mashaka na aina ya utazamaji wao ila wasiwasi wake ulizidi pale ambapo mwenye duka alifunga na wale vijana wakabaki wakiwa wamesimama bila kuonesha jitihada zozote za kuondoka.

Remi aliishi kwa mashaka siku zote hivyo hakutaka kuendelea kukaa pale wakati roho yake haitaki.

Akanyanyuka huku akiwatizama vijana wale ambao nao walinyanyuka na kuanza kumfuata.


Remi aliongeza hatua za miguu yake,vijana nao wakaongeza hatua.

Remi akaingia katikati ya soko pweke lililogubikwa na kiza kizito.

Alipokelewa na kelele za mapaka shume yaliokuwa yanagombania mabaki ya chakula sokoni pale.

Akapiga hatua akiwa na lengo la kupotelea gizani ili kuwapoteza vijana wao ambao alijua dhamira yao.

Hakufika mbali akasikia sauti ikiamuru nyuma yake.

"Simama hivyohivyo!" ilikuwa sauti ya watu iliojaa mamlaka.

Remi akasimama na akageuka na akashuhudia vijana wale wakija mkukumkuku wakiwa wamewasha taa za simu zao.

Lakini hakumuona alieamrisha asimame.

Remi matatani tena!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom