Je, baba alitutesa au alitufundisha maisha?

Hahaaaaaaa, baba akiwa askari watoto mnapata tabu sana. Umenikumbusha mbali sana, si tulilima usiku tukitumia taa ya chemli. Ila alitufundisha maisha ambayo unaishi popote na unaishi na yoyote. Hakuwa anatudekeza, alikuwa anatukazia na sasa tunaona Matunda yake. R.I.P Swai
 
Duuuh, mkuu nimesoma hii story yaani nikama ni mimi niehadithia maana inarandana kabisa na mzee wangu kanali mstaafu. Tifauti tu ni kwamba yeye alikuwa kanali ila sio kmaeneo ya kusini mwa Tanzania bali hapahapa dar.

Ukali na adhabu zilizopitoliza, aliogopwa mpaka na majirani zake wanajeshi pale kota za maofisa.

Tulipohamia uraiani majirani pia walimwogopa sana.

Enzi hizo mzee ukikosea hakuna kuulizana zaidi ya adhabu na viboko kama mwizi.

Akifuatwa na gari kwenda kazini, gari yake hupandi wakati huo unakwenda shule hata kama gari inapita jirani na shule yako na usafiri ni shida, na akikukuta barabarani anakupita kama hakujui .

Kitu kimoja tofauti ni kuwa mshua huyu pamoja na ukali wake alikuwa anatupatia pesa mingi za matumizi bunafsi kiasi kwamba kwa upande wa bata hakuwa mgumu. Nikiwa ps nilikuwa napewa pesa nyingi za shuleni.

Nyumbani pombe zilikuwa hazikosi, makreti ya bia konyagi. Hakuwa mlevi alikuwa anakunywa kwa nidhamu sana.

Akiwa barabarani na gari yake hata polisi waliisoma namba kwake.


Familia hatukuwa na amani ndani, watoto tulimwogopa sana. Yaani mpaka leo ilituathiri kisaikolojia, tumeshakuwa watu waazima bado hatuwezi kujiachia nae japo una mwona kwa sasa anatamani tuwe karibu ila inashindikana.

Wajukuu zake ndio wako nae karibu kuliko wanae, tunapiga story sana ila huwa tuko strait kwenye stori tunaogopa kuingiza utani kwenye stori japo yeye anatamani tutaniane walau ila ndio hivyo tena too late hakutulea hivyo tuwe karibu.

Maisha yale yamenifanya niwapende sana wanangu na niwe nao karibu, niwasikilize na kushea nao maoni yao.

Kiufupi maisha yale yalinifanya leo hii niweze kuishi mazingira yoyote na niweze kuishi na kila mtu.
 
Nyie mnaolea watoto legs lege ndio mnasababisha wawe mashoga
Kama kawaida unaleta shombo za logical non sequitur za kawaida kwa wabongo.

Wapi nimesema nalea watoto lege lege? Unajua kusoma kwa ufahamu wewe ngumbaru mtovu wa nidhamu?

Hujajua hata kama nina mtoto ushanipa malezi tayari.

Wewe ushoga lazima utakuwa unaupenda kisirisiri, ndiyo maana kila kitu wazo la kwanza ushoga.

Ujinga mtupu.
 
Hayo ndo maisha ya wajeda from kambini to nyumban.....doso oyeeee

Sent from my Infinix X653 using JamiiForums mobile app
 
Mchaka mchaka wa familia [emoji23][emoji23][emoji23]

Sent from my Infinix X653 using JamiiForums mobile app
 
Ni umasikini na stress ndio zilizokuwa zinamsumbua mzee wenu.
Mtoto wa darasa la sita hauwezi kumbebesha tofali 100 tena umbali wa mita 250..mzee wenu alikuwa hana pesa ya kuwalipa watu wabebe tofali akaona awatumie nyinyi.
Tambua kazi zinaendana na umri ukimpa mtoto kazi ngumu lazima mtoto atadumaa.
Hata sisi baba yetu alikuwa major general lakini hajawahi kutuendesha kama punda
 
Kiuchumi home tuko vizuri mpaka Leo sio sababu etu umasikini Ila mzee alitaka kutufundisha maisha Japo kwa upande mwingine tuliteseka lkn kila nyumba Kuna malezi yake na Sheria zake
 
Mkuu ukweri mtupu wazee walitufundisha ili tupambane na dunia ya Sasa respect nyingi Sana kwao
 
Mshukuru Mungu hukawa shoga,umelelewa vyema malezi mabovu huharubu watoto
 
Mkuu walitufundisha ili tupambane na dunia ya Sasa unaishi kwenye mazingira yeyote ata ukiwa ugenini unaheshimu taratibu za pale
R.I.P our father swai
 
Kweli mkuu mapapai yamekuwa mengi
 
Angalia maisha yako ya sasa, yameathiriwa vibaya au vizuri na namna mzee alivyowalea.

Nikupe stori kuhusu (sisi)
Baba yetu alikuwa mdemokrasia sana. Nyumbani tulikuwa watoto wengi sana, mimi nilkuwa mdogo sana. Kaka zangu waliwekeana zamu ya kwenda kuchunga ng'ombe, lakini ilikuwa ikitokea mwenye zamu hajaenda baba alikuwa anaenda mwenyewe kuwachunga. Yeye ilikuwa ukiwa na shida na kitu ukimfuata atakwambia nenda kaombe ulikoshinda siku ambayo hukuenda kuchunga ng'ombe.

Tabia ya baba ya kuwa mdemokrasia sana ilifanya kaka zangu wengi waachie shule njiani. Maana ilikuwa kama hawajaenda shule atauliza "vipi mbona hujaenda shule ukijibu naumwa.. atakwambia tu, shauri yako utaumwa mpka uzeeni"

Yeye alikuwa mchapakazi sana, na alikuwa na mafanikio makubwa sana, ameacha mali nyingi sana ambazo sasa watoto wake wanagombaniana [emoji23]

Alipenda kufundisha kwa mifano sana, kwa mfano kipindi wakija watu wazima kuomba kazi ya kupalilia migomba au mahindi atakutuma ukamuoneshe shamba, ukirudi atakwambia "umeona yule mtu, alivyokuwa kama wewe alikuwa anacheza, usipokuwa makini utakuja nawe kuomba vibarua ukiwa mzee".

Na utu uzima huu, nimegundua maneno pekee hayatoshi kuleo mtoto, muda mwingine misimamo kama ya baba yako ndo inafanya mtoto awe kwenye njia flani nzuri, hata si ukatili. Malezi ya kubembelezana si maadili yetu, tumeiga tu ndo maana jamii sasa imepotoka maana hata mtoto akikosea eti inabidi uongee naye, umbembeleze (nani kasema) ujinga na upumbavu upo kwenye akili ya mtoto, anatakiwa anyooshwe hata kwa viboko.

Tumechukua tamaduni za watu, sasa hata namna ya kulea watoto wetu tunaita ukatili. Katili atanyima msosi, atakunyima pa kulala. Lakini adhabu ya kubeba tofali ukizingua ilikuwa si ukatili, alikuwa anakuandaa kukabili nyakati ngumu katika maisha, pia alikuwa anakuandaa kusimamia msimamo, ndo maana ilikuwa usipomwigilia miti hata saa nane ya usiku utaenda mwagilia. Hiyo ilikuwa na maana kuwa unakiwa kufanya wajibu wako kwa wakati sahihi.

Kwa upande wangu baba yako alikuwa sawa sana.
 
Mlikuwa mnafundishwa maisha.
 
Je baba alitutesa au alitufundisha maisha...sehemu ya 2

Tukio lingine nakumbuka kwenye michezo ya kitoto Niko na wezangu niliwahi kudondokaa Juu ya mti,mti ulikuwa mkubwa nikatua mpaka chini palepale nikapoteza fahamu mana nilidondoka vibaya nakuja kushtuka nipo nyumbani mguu unauma Sana pembeni Yuko mshua nikajisemea kimoyomoyo Leo nimeisha nakumbuka nilichezea kipigo na nikapewa adhabu ya kubeba mchanga hakuna mtu wa kunisaidia Ile siku ilikuwa noma Nina maumivu ya mguu afu nikawa nabeba mchanga nikikanyaga tu mguu chini nilikuwa najisikia maumivu makali Sana unatupa mfuko wa mchanga chini unayasikilizia maumivu Kwanza mshua yupo tu amekaa pembeni ananiangalia tu Kama mtuhumiwa hivi Ile siku nilieleza nilijuta kupanda kwenye miti....siku ya pili nilipelekwa hospital kwa matibabu

Tukio lingine nakumbuka Kuna siku Niko na brother tulitumwa twende mahali tukachukue mahindi ni mbali kidogo na nyumbani mshua alikuwa na kawaida moja akinunua mahindi mkaa nk hakuna Cha usafiri mtabeba mgongoni mpaka nyumbani hata yakiwa magunia kumi mtamaliza tu Sasa Ile siku tulichelewa kwenda majira Kama ya saa 10 hivi tulianza Safari sehemu tunakoenda ni mbali tunatembea kwa miguu saa 11 kasoro tukawa tumefika kuja pale wenye nyumba hawapo wapo kanisani walikuwa ni walokole ikabidi tuwasubirie mpaka ibada iishe baada ya ibada kuisha majira saa12 jioni wanatukuta pale tumekaa tupo Mimi na brother walitushangaa jioni hii mnabeba mahindi si mngekuja ata kesho tukifiria mziki wa mshua afu tusirudi bila mahindi hapa ni msala ikabidi tukaze tupewe mahindi kila mtu akapimiwa abebe anayoweza tukaaga Safari ikaanza Giza linaanza kuingia brother akasema Kuna njia ya shortcut anaijua tutafika mapema nyumbani kumbe ni kosa Ile njia ilikuwa inapita pembezoni mwa mto ikabidi tupite njia hiyo baada ya kutembea kitambo kirefu tunapita porini tu kumbe njia tunayopita sio tumepotea ghafla kwa mbela tunakutana na Bibi kikongwe akatuuliza mnenda wapi wajukuu zangu ikabidi tutaje sehemu tunayoenda akasema huku hakuna njia ya kufika mnakoenda rudini mlipotoka aisee tulichoka, shingo kichwa kilishaanza kuchoka sababu ya uzito wa mzigo na Giza lishaingia ikabidi turudi na mizigo yetu kichwani baada kutembea kitambo kidogo tukatokea kwenye njia inayoenda maeneo ya nyumbani kufika nyumbani ni saa 3 na nusu usiku hapo tumechoka,tunanjaa kinoma kufika home geti limefungwa baada ya kupiga sana hodi akaja mama kufungua mlango alivyotuona Kwanza jinsi tulivyo na mizigo yetu alishangaa Sana nyie mda wote mlikuwa wapi na baba yenu karudi muda tu tukamjibu tulienda kuchukua mahindi ilibid tuingie ndani mshua katulia tu kwenye sofa anatuchora ana habari na sisi tupo na mizigo yetu tukamsalimia yupo kimya akatuangalia tu akasema tu hivi nyinyi tabia ya kurudi usiku na mizigo ya watu mmeanza lini ikabidi brother aanza kuelezea huku anatetemeka mkasa wote hadi tumechelewa kufika....
Ule ulikuwa usiku wa mateso tulifungwa Kama miguuni huku mizigo ipo kichwani afu akatuambia mtasimama hivyo mpaka asubuhi na mizigo yenu ole wako udondoke au utupe mzigo chini....Yani umesimama hivi mwili unatetemeka umechoka inabid ujikaze tu huku machozi yanakutoka unajiuliza hivi huyu baba angu kweri tulisimama tokea Ile saa 4 usiku mpaka saa 7 za usiku ndo anafika kutufungua kamba nakumbuka hatukulala ndani siku Ile tulifungiwa stoo mpaka asubuhi.

Nilichompendea mshua kila ikifika mwezi wa 12 likizo Ile anaweka kikao baada ya hotuba ndefu na 'siku hiyo mtapiga stori nyingi na kucheka' sas kila mtu alikuwa anapewa hela akanunue anachotaka kulingana na kuwajibika kwake nyumbani iwe kwenye kazi,usafi,heshima hadi kwenye masomo ukiwa na makosa mengi na hela yako inapunguzwa unakuta wew umepata elfu 80 mwezako kachukua laki 2 na zaidi hii kitu ilifanya tupambane Sana kuwajibika pale nyumbani na shuleni kwenye kila kitu ili mwisho wa mwaka uwe na kibunda Cha maana siunajua Xmas na mwaka mpya unavimba tu
Sio kwamba hela tulikuwa tunapewa mwezi wa 12 tu hapana Ile ilikuwa kamaa zawadi hela tulikuwa tunapewa kila mwezi ununue mahitaji ya shule na nguo.

Matukio ni mengi Sana tuliokutananae kwa mzee baba,mshua,dingi don Ila yalitufunza jinsi ya kupambana na maisha kwenye mazingira yeyote yale
 
Umefaidika aje na haya mateso? Pole kwa kufiwa na ndogo wako, natumaini hakufariki akiwa anapitia mateso ya mzazi wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…