Je, dakika yake ya mwisho duniani alisemaje? Ilikuwaje?

Je, dakika yake ya mwisho duniani alisemaje? Ilikuwaje?

Wakati mgumu mno ni ule wakati uhai unatoka - usiombe kitu hicho kikukute. Ukitaka kujua namna utakavyohangaika jaribu kuziba pumzi yako wa dakika kama 3 hivi... au jaribu kujinyonga na kisha ukijitundika mwambie nduguyo awepo hapo ili kabla hujakata roho aikate kamba - then uje utushuhudie uchungu wake.

Kwa kweli kifo ni kitu kichungu mno, na kibaya zaidi ukishazaliwa tu lazima ushuhudie maumivu hayo na baada ya kukata roho hutajua upo wapi, kama ulizaliwa duniani ama laah.

Kifo ni fumbo.
Wengine hufa kwa Amani kabisa, wakiwa usingizini. Kwamba ni viungo muhimu kama ini, figo na hatimaye moyo, huacha kufanya kazi, mhusika anajihisi kuchoka au usingizi. Hivyo hapati shida ya kusema siwezi kupumua n.k. hana maumivu kwani kupooza kunakuwa kumempata, na inaishia hivyo.
 
Dahhhh, ilikuwa jumamisi ya 13/11/2018 Mzee wangu alianguka tu ghafla baada ya kumaliza kusali Jumuia nyumbani kwake. Alimwambia Mama "Mke wangu, usisumbuke kunipeleka hospitali kwani nimeshakufa, nimeuona Yesu na kaniambia nimeshakufa. Kisha akasema, Mungu wangu unisamehe kwa yote niliyotenda nikiwa duniani" Akafunga Macho na mdomo ndio moja kwa moja.
Jinsi nzuri ya kufa!
 
more milk more milk...
maneno ya mwisho ya wacko jacko
Hakumaanisha maziwa, bali madawa ya kumfanya alale, hapo alikuja akimwambia daktari wake maalum aliyeshitakiwa kwa kumuua kwa madawa.
 
Tukiwa kwenye harakati za kumuuguza mke wangu mpendwa,Mama alikuwa msaada mkubwa kwangu na kwa mke wangu,siku hiyo nimetoka hospitali kumuona mke wangu,nafika nyumbani nikaambiwa mama ananiita kwake,nikaenda na kumkuta ana huzuni sana,akaniuliza tu mgonjwa anaendeleaje?nikamwambia anaendelea vizuri sana,akaniambia "moyo wangu unaniuma sana nimeshindwa kwenda kumuona,miguu yangu haifanyi kazi kabisa,ila naamini tu Mungu ATANIKUTANISHA naye siku moja" niliondooka kwake saa tano usiku,tukaagana,akaenda kulala na mimi nikaenda kwangu,siyo mbali sana! Usiku wa kama saa nane nikapigiwa simu na mtu aliyekuwa hospitali alipokuwa amelazwa mke wangu!akaniambia hali ya mke wangu imekuwa mbaya ghafla,hivyo kama nitaweza niende asubuhi,hospitali yenyewe ilikuwa mkoa mwingine, nikakosa amani kabisa! Kufika saa kumi hivi usiku nikapigiwa simu tena! Roho ikapasuka paah!! Kuicheki ni mdogo wangu anayeishi na mama,nikapokea,akawa analia huku akiniambia "njoo nyumbani haraka" nikatoka mbio,nikafika na kumkuta mdogo wangu nje ana haha na kulia,nika muuliza kuna nini?akanikumbatia huku akilia na kuniambia niingie ndani,nikaingia mbio,nikaenda haraka chumbani kwa mama! Nikamkuta amelala huku anakoroma kwa sauti ya chini kabisa nikajaribu kkumwamsha kwa kumtikisa! Hakujibu,wala hakuamka,Akaondoka hivyo!! Tukaandaa mazishi na kumzika hapo hapo nyumbani huku mke wangu akiwa bado hospitali na akiwa na hali mbaya,siku tumezika mmke wangu ni kama alipata nafuu ghafla na kuongea na dokta aniambie nimpe mama simu aongee naye,nikamwambia mama ametoka kidoogo,akasisitiza sana,maana siku mama yangu anazikwa mimi nilienda hospitali asubuhi na mke wangu akawa anaongea kwa tabu akinilaumu kwa kumnyima kuongea na mama,akasema kuna kitu anataka amwambie mama ili mmama aniambie mimi,akasema "mimi nakufa,ila kuna jambo nataka nimwambie mama kwa ajili yako, basi tukamzika mama!! Mke wangu hakujua kuwa mama amefariki hadi siku moja alipoambiwa na mgonjwa mwingine aliyefika hospitalini akkitokea huku tunakoishi siku hiyo mke wangu alilia sana,akaniita,nikaenda,akalalamika kwa nini Mungu amemchukua Mama aliyekuwa mzima na mwenye aliyempenda sana na kumuacha yeye akiteseka kitandani kwa miaka!! Nimekuwa na wakati mgumu toka hapo ndugu zangu! Wiki mbili baada ya kumzika mama mke wangu mpenzi naye akafariki!! Lile neno alillotaka kumwambia mama aliniambia mimi mwishoni,nikamzika nyumbani pembeni ya mama aliyependa na waliopendana sana!! Mimi bado nipo kwenye msiba mzito!! Ni wiki tatu tu zimepita tangu nimzike mke wangu,mke wangu aliugua saratani ya ziwa(breast cancer) naandika huku machozi yananimwagika.
 
Mtateseka nikiwa nimekufa lakini siyo nikiwa hai, 12 hours before his death, then tukaenda mtoni doing our laundry with him, as he insisted that we must do it bse the next day we were about to embark a journey.

Usiku alisema twende tukakale mwanangu then he died.

I miss you mshua , I wish that heaven have visiting hours , so I could come by and ask your advice
Poleni sana mkuu
 
Kuna mtu huko juu amenishauri niandike kisa changu ilikuwa 2019 august asubuhi siku ya ijumaa kuamkia jmosi. Saa tisa alfajiri niliota mtoto wangu wa kiume alikuwa analia mgongoni kwa mama yake. Sasa mimi nikamfokea kidogo kwamba anyamaze nikamshika mguu wake kumtingisha nikamwambia J acha kulia usiku sahizi wakati huo mimi nipo ndani ya chandarua na wao wamesimama nje ya kitanda na mama yake wanabembelezana. Huwezi amini kitendo cha kumuambia mwanangu J acha kelele basi eti akamfia mama yake mgongoni.

Nikastuka usingizini kwa hii ndoto mbaya sasa nikawa najiuliza inamaana nimemuua mwanangu? Nikajiskia vibaya sana baada usingizi ukanipitia tena nikalala. Kwenye saa 12 asubuhi napokea simu njoo haraka nyumbani umpeleke baba hospital. Ni umbali wa km 90 toka ninapofanyia kazi mpaka kwa mzee. Asubuhi hiyo hiyo nikajiandaa fasta huku moto mzito sana hasa nikiwaza ile ndoto.

Nafika umbali wa kama mita mia naona geti la nyumbani limefunguliwa na kuna watu nje. Nikastuka sana .Mama mzazi alikuwa jasiri sana (ila pia walishatengana na mzee kitambo) mama mzazi akaniwahi getini akanishika mkono akaniambia jikaze. Nikajua nimeshampoteza baba. Kufika chumbani kwake nikamkuta baba amelala kimya. Na wamemfunika kanga. Katika maisha yangu juu ulikuwa wakati mgumu kuliko yote toka nizaliwe!

Kukidhi matakwa ya uzi huu. Nikwamba niliongea nae kwenye simu two days before! Had I known that could be the last moments talking to my father I could have recorded his voice! We Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema naomba uendelee kumpatia baba yangu mzazi pumziko lenye amani ya milele. Amin.
Pole sana
 
Alituita watoto wake wote wa 3 akatupa mikono kwa tabu Sana akatuambia vitu vyangu vyote mnavijua chochote watakacho watakachosema ni Chao waachieni.kisha akamwambia brother wasimamie wadogo zako huku machozi yanamtoka.tukatolewa nje mshua alikufa kifo Cha maumivu Sana Mana akijua anatuacha kwenye mikono ya wadharimu watu wabaya tukiwa Bado wadogo Sana.
Na kweli kwenye nyumba 9 alizoziacha tumebakiwa na mbili tu.
Kwenye hekari 22 vikindu 1994.tumebakiwa na eneo iliyopita njia kuu.
Kila kitu chake waligawana ndugu zake kwa kweli maneno yake yalitimia.mshua pumzika kwa amani ulitabili ukifa tutapata tabu Sana na kweli walitunyoosha pa moja na wema wako wote ule waliyotutendea tumemuachia MUNGU.tumesahau now tunafuraha Tuna maisha yetu tunakukumbuka daima....
Pole sana makilo,hao waliodhulumu hizo mali lazima ni makapuku mali ya dhuluma inawatesa
 
Ok,Km mngemuuliza akawajibu tungeweza kujua kuwa ni Malaika au lah!!!.
Mpaka leo najiuliza ni malaika watoa roho au ni ndugu zake waliotangulia walikuja kumkaribisha kwenye makazi mapya. Ajabu walivyoondoka wakamuacha alikuwa kama anasikitika kwanini wameondoka bila yeye..inanifikirishaga sana
 
Tukiwa kwenye harakati za kumuuguza mke wangu mpendwa,Mama alikuwa msaada mkubwa kwangu na kwa mke wangu,siku hiyo nimetoka hospitali kumuona mke wangu,nafika nyumbani nikaambiwa mama ananiita kwake,nikaenda na kumkuta ana huzuni sana,akaniuliza tu mgonjwa anaendeleaje?nikamwambia anaendelea vizuri sana,akaniambia "moyo wangu unaniuma sana nimeshindwa kwenda kumuona,miguu yangu haifanyi kazi kabisa,ila naamini tu Mungu ATANIKUTANISHA naye siku moja" niliondooka kwake saa tano usiku,tukaagana,akaenda kulala na mimi nikaenda kwangu,siyo mbali sana! Usiku wa kama saa nane nikapigiwa simu na mtu aliyekuwa hospitali alipokuwa amelazwa mke wangu!akaniambia hali ya mke wangu imekuwa mbaya ghafla,hivyo kama nitaweza niende asubuhi,hospitali yenyewe ilikuwa mkoa mwingine, nikakosa amani kabisa! Kufika saa kumi hivi usiku nikapigiwa simu tena! Roho ikapasuka paah!! Kuicheki ni mdogo wangu anayeishi na mama,nikapokea,akawa analia huku akiniambia "njoo nyumbani haraka" nikatoka mbio,nikafika na kumkuta mdogo wangu nje ana haha na kulia,nika muuliza kuna nini?akanikumbatia huku akilia na kuniambia niingie ndani,nikaingia mbio,nikaenda haraka chumbani kwa mama! Nikamkuta amelala huku anakoroma kwa sauti ya chini kabisa nikajaribu kkumwamsha kwa kumtikisa! Hakujibu,wala hakuamka,Akaondoka hivyo!! Tukaandaa mazishi na kumzika hapo hapo nyumbani huku mke wangu akiwa bado hospitali na akiwa na hali mbaya,siku tumezika mmke wangu ni kama alipata nafuu ghafla na kuongea na dokta aniambie nimpe mama simu aongee naye,nikamwambia mama ametoka kidoogo,akasisitiza sana,maana siku mama yangu anazikwa mimi nilienda hospitali asubuhi na mke wangu akawa anaongea kwa tabu akinilaumu kwa kumnyima kuongea na mama,akasema kuna kitu anataka amwambie mama ili mmama aniambie mimi,akasema "mimi nakufa,ila kuna jambo nataka nimwambie mama kwa ajili yako, basi tukamzika mama!! Mke wangu hakujua kuwa mama amefariki hadi siku moja alipoambiwa na mgonjwa mwingine aliyefika hospitalini akkitokea huku tunakoishi siku hiyo mke wangu alilia sana,akaniita,nikaenda,akalalamika kwa nini Mungu amemchukua Mama aliyekuwa mzima na mwenye aliyempenda sana na kumuacha yeye akiteseka kitandani kwa miaka!! Nimekuwa na wakati mgumu toka hapo ndugu zangu! Wiki mbili baada ya kumzika mama mke wangu mpenzi naye akafariki!! Lile neno alillotaka kumwambia mama aliniambia mimi mwishoni,nikamzika nyumbani pembeni ya mama aliyependa na waliopendana sana!! Mimi bado nipo kwenye msiba mzito!! Ni wiki tatu tu zimepita tangu nimzike mke wangu,mke wangu aliugua saratani ya ziwa(breast cancer) naandika huku machozi yananimwagika.
Kaka pole sana,mungu akufanyie wepesi
 
Mtu kama huyu nitafurahi kifo chake badala ya kulia, ni maisha ya ushuhuda sana sana
Bro hata mimi kwa jinsi ya kimwili niliumia sababu alikuwa ananishauri na kuniongoza ila kwa jinsi ya Roho nilikuwa na furaha. Ameshinda na kumaliza vizuri. Mimi natumika kanisani, siku aliyokufa niliota ndoto naenda nyumbani ila nikarudi kwangu bila mchele. Hii ni kwa sababu mara nyingi nilipokuwa naenda nyumbani na watoto wangu, mzee alikuwa ananikobolea gunia 1 la mpunga then narudi nao kwangu. Sasa siku hiyo nikaota narudi bila kitu. Huwa naamka saa 9 au 10 kwa ajili ya maombi. Nikaamka nikasali ila sikuwa najua maana ya ndoto hiyo. Saa 12 alfajiri nikarudi kitandani ikaja kwa namna nyingine. Nikaamka na kuingia kusali ila kuna Wimbo ukawa unatembea kichwani mwangu "Kwa Mji wa Mwangaza" baadae wananipigia simu he is no longer. Msiba ule wimbo mkubwa uliokuwa kichwani mwangu ni huo. Nikilala, nikiamka mchana na usiku moyo na mawazo yangu yana wimbo huo. Binafsi nikawa namuomba na kumsihi Mungu nijue mzee kaendaje. Sikupata maono wala ndoto kuhusu yeye ila baada ya maiba kuisha nami kurudi kwangu ndipo nilipata ndoto moja na ya mwisho kuhusu yeye. Akaniambia" Ndetefyose kwanini unanililia? Mimi nimeshamaliza mwendo, ililie nafsi yako. Sina deni na mtu na fulani unayezani namchukia simchukii ila sikuwa nataka nimuachie mji wangu.

Hakika tutaonana baadae mzee, hakika tutakutana patakatifu pale katika ibada ile ya harusi ya mwanakondoo tukiimba hossana hossana huku tukizunguka kiti cha enzi.
 
Tukiwa kwenye harakati za kumuuguza mke wangu mpendwa,Mama alikuwa msaada mkubwa kwangu na kwa mke wangu,siku hiyo nimetoka hospitali kumuona mke wangu,nafika nyumbani nikaambiwa mama ananiita kwake,nikaenda na kumkuta ana huzuni sana,akaniuliza tu mgonjwa anaendeleaje?nikamwambia anaendelea vizuri sana,akaniambia "moyo wangu unaniuma sana nimeshindwa kwenda kumuona,miguu yangu haifanyi kazi kabisa,ila naamini tu Mungu ATANIKUTANISHA naye siku moja" niliondooka kwake saa tano usiku,tukaagana,akaenda kulala na mimi nikaenda kwangu,siyo mbali sana! Usiku wa kama saa nane nikapigiwa simu na mtu aliyekuwa hospitali alipokuwa amelazwa mke wangu!akaniambia hali ya mke wangu imekuwa mbaya ghafla,hivyo kama nitaweza niende asubuhi,hospitali yenyewe ilikuwa mkoa mwingine, nikakosa amani kabisa! Kufika saa kumi hivi usiku nikapigiwa simu tena! Roho ikapasuka paah!! Kuicheki ni mdogo wangu anayeishi na mama,nikapokea,akawa analia huku akiniambia "njoo nyumbani haraka" nikatoka mbio,nikafika na kumkuta mdogo wangu nje ana haha na kulia,nika muuliza kuna nini?akanikumbatia huku akilia na kuniambia niingie ndani,nikaingia mbio,nikaenda haraka chumbani kwa mama! Nikamkuta amelala huku anakoroma kwa sauti ya chini kabisa nikajaribu kkumwamsha kwa kumtikisa! Hakujibu,wala hakuamka,Akaondoka hivyo!! Tukaandaa mazishi na kumzika hapo hapo nyumbani huku mke wangu akiwa bado hospitali na akiwa na hali mbaya,siku tumezika mmke wangu ni kama alipata nafuu ghafla na kuongea na dokta aniambie nimpe mama simu aongee naye,nikamwambia mama ametoka kidoogo,akasisitiza sana,maana siku mama yangu anazikwa mimi nilienda hospitali asubuhi na mke wangu akawa anaongea kwa tabu akinilaumu kwa kumnyima kuongea na mama,akasema kuna kitu anataka amwambie mama ili mmama aniambie mimi,akasema "mimi nakufa,ila kuna jambo nataka nimwambie mama kwa ajili yako, basi tukamzika mama!! Mke wangu hakujua kuwa mama amefariki hadi siku moja alipoambiwa na mgonjwa mwingine aliyefika hospitalini akkitokea huku tunakoishi siku hiyo mke wangu alilia sana,akaniita,nikaenda,akalalamika kwa nini Mungu amemchukua Mama aliyekuwa mzima na mwenye aliyempenda sana na kumuacha yeye akiteseka kitandani kwa miaka!! Nimekuwa na wakati mgumu toka hapo ndugu zangu! Wiki mbili baada ya kumzika mama mke wangu mpenzi naye akafariki!! Lile neno alillotaka kumwambia mama aliniambia mimi mwishoni,nikamzika nyumbani pembeni ya mama aliyependa na waliopendana sana!! Mimi bado nipo kwenye msiba mzito!! Ni wiki tatu tu zimepita tangu nimzike mke wangu,mke wangu aliugua saratani ya ziwa(breast cancer) naandika huku machozi yananimwagika.
Nakosa la kuandika!
Kuna watu wana mapito...tamar pole sana
 
Tukiwa kwenye harakati za kumuuguza mke wangu mpendwa,Mama alikuwa msaada mkubwa kwangu na kwa mke wangu,siku hiyo nimetoka hospitali kumuona mke wangu,nafika nyumbani nikaambiwa mama ananiita kwake,nikaenda na kumkuta ana huzuni sana,akaniuliza tu mgonjwa anaendeleaje?nikamwambia anaendelea vizuri sana,akaniambia "moyo wangu unaniuma sana nimeshindwa kwenda kumuona,miguu yangu haifanyi kazi kabisa,ila naamini tu Mungu ATANIKUTANISHA naye siku moja" niliondooka kwake saa tano usiku,tukaagana,akaenda kulala na mimi nikaenda kwangu,siyo mbali sana! Usiku wa kama saa nane nikapigiwa simu na mtu aliyekuwa hospitali alipokuwa amelazwa mke wangu!akaniambia hali ya mke wangu imekuwa mbaya ghafla,hivyo kama nitaweza niende asubuhi,hospitali yenyewe ilikuwa mkoa mwingine, nikakosa amani kabisa! Kufika saa kumi hivi usiku nikapigiwa simu tena! Roho ikapasuka paah!! Kuicheki ni mdogo wangu anayeishi na mama,nikapokea,akawa analia huku akiniambia "njoo nyumbani haraka" nikatoka mbio,nikafika na kumkuta mdogo wangu nje ana haha na kulia,nika muuliza kuna nini?akanikumbatia huku akilia na kuniambia niingie ndani,nikaingia mbio,nikaenda haraka chumbani kwa mama! Nikamkuta amelala huku anakoroma kwa sauti ya chini kabisa nikajaribu kkumwamsha kwa kumtikisa! Hakujibu,wala hakuamka,Akaondoka hivyo!! Tukaandaa mazishi na kumzika hapo hapo nyumbani huku mke wangu akiwa bado hospitali na akiwa na hali mbaya,siku tumezika mmke wangu ni kama alipata nafuu ghafla na kuongea na dokta aniambie nimpe mama simu aongee naye,nikamwambia mama ametoka kidoogo,akasisitiza sana,maana siku mama yangu anazikwa mimi nilienda hospitali asubuhi na mke wangu akawa anaongea kwa tabu akinilaumu kwa kumnyima kuongea na mama,akasema kuna kitu anataka amwambie mama ili mmama aniambie mimi,akasema "mimi nakufa,ila kuna jambo nataka nimwambie mama kwa ajili yako, basi tukamzika mama!! Mke wangu hakujua kuwa mama amefariki hadi siku moja alipoambiwa na mgonjwa mwingine aliyefika hospitalini akkitokea huku tunakoishi siku hiyo mke wangu alilia sana,akaniita,nikaenda,akalalamika kwa nini Mungu amemchukua Mama aliyekuwa mzima na mwenye aliyempenda sana na kumuacha yeye akiteseka kitandani kwa miaka!! Nimekuwa na wakati mgumu toka hapo ndugu zangu! Wiki mbili baada ya kumzika mama mke wangu mpenzi naye akafariki!! Lile neno alillotaka kumwambia mama aliniambia mimi mwishoni,nikamzika nyumbani pembeni ya mama aliyependa na waliopendana sana!! Mimi bado nipo kwenye msiba mzito!! Ni wiki tatu tu zimepita tangu nimzike mke wangu,mke wangu aliugua saratani ya ziwa(breast cancer) naandika huku machozi yananimwagika.
Pole sana kaka
 
Back
Top Bottom