Je, gari hii itaenda kuua soko la Kluger na Harrier Tanzania?

Je, gari hii itaenda kuua soko la Kluger na Harrier Tanzania?

Utam wake uwe na masafa ya mbali alafu gari liwe moya kidogo sisi tulitoka na breavs hapa dar hadi moshi masaa 5 kasori point ila usiku saa saba tulitoka dar
Hivi wazee wa kukesha hawapo usiku.... Traffic?!
 
Hio gari nimeiendesha juzi tu. Ni ya best yangu plate DSF. Kiukweli ni gari ambayo nje ina muonekano wa kibabe ila ndani full plastics. Dashboard haivutii kabisa halafu pia kiti chake kiko chini sana. Kiukweli sikufeel kama niko ndani ya suv. Japo inaitwa SUV.

The next day niliendesha Suzuki Sport Grand Vitara V6 2.7ltr toka beforward DSM to Moshi. Aisee gari lina pulling kinoma yani. Linatembea balaa yani full kukata upepo. Halafu ndani liko very spacious ukikaa unakuwa juu juu yani una feel umekalia SUV kabisa. Naona Suzuki iko comfortable kuliko hio Subaru.
Unajua hii ni cross breed ya SUV na WAGON. Sababu iliyotangulia ilikuwa chini kabisa yaani ni almost kama hizi carina kwa kimo. Then hii wakaadopt looks za gari kama rav 4 but haijaifikia rav 4 kwa kimo i think.

Kuhusu seat hii nimenotice ipo kwenye subaru sana. Siti yake ukiingia kwenye gari unakuwa kama umezama kwenye shimo of which me huwa sipendi maana inatoa ile hali ya kuhisi una control ya usukani.

Nimeona kwenye subaru forester zile model mbili za awali, pia kwenye subaru imprenza na hii pia ina hiyo kitu.
 
Kluger,Harrier,Premio,IST ndiyo magari yalioyopo hapa mji ninaoishi.
Wasukuma tunanunua gari kwa kuangalizia[emoji3][emoji3][emoji3]
 
Wanaboa wale machoko. Kuharibu stimu tu za kudrive.... Mtu unataka uendeshe gari wao wanataka uende kwa limit ya speed yao.
Hahahaaa wale wakikusimamisha kwwnye gari isishuke wee shusha kioo kidoogo waangalie alafu unawaambia "hali zenu poleni na kazi" wenyewe unasikia wanasema pita mkuu safari njema [emoji2][emoji2][emoji2] yaani wanajishtukiaga sana
 
Kwanzia 2009 ndo naona wametoka kwenye sport look na kuingia ushindan na kina rav4 .yan zimekuwa za kiutu uzima sana ila crossport ya 2008 ni kali sana ukiweka wa BOV yako map ya maana ni gari flan hivi unaeza chukua attention muda wowote
Mkuu Subaru Forester zenye attention ukiifanyia mapping ni matoleo ya 2005 kushuka chini hapo ndipo utaisikia Boxer engine ikikohoa.

Haya matoleo ya sasa hata ukifanya mapping usiiwekee dhamana sana, ukiishurutisha kidogo inaweza ikakufedhehesha.

Subaru kwenye mapping kitu kidogo kikizingua uwezi kuendelea na mchezo.Mapping tamu zitabaki kwa Toyota na Mitsubishi.
 
Unajua hii ni cross breed ya SUV na WAGON. Sababu iliyotangulia ilikuwa chini kabisa yaani ni almost kama hizi carina kwa kimo. Then hii wakaadopt looks za gari kama rav 4 but haijaifikia rav 4 kwa kimo i think...
Nadhani design wao wana tabia za ki sports maana sports car nyingi unazama kwenye seat ila nilitabili bila kukosea naona Subaru imeanza kuwa hot
 
Back
Top Bottom